Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

uongozi wote wa irani kuanzia kiongozi wao mkuu ayatola ambaye ni commander in chief wa jeshi kwa nchi nyingine ni kama raisi wa nchi, mkuu wa majeshi wote kuanzia waziri wa ulinzi, general mkuu wa jeshi na cream yote wameuliwa kirahisi kabisa bila ya kizuizi chochote kile halafu hapo hapo bado kuna watu wanasema kwamba irani anashinda? anashinda nini sasa? hana uwezo wowote ule wa kulinda air space yake anawezaje kushinda chochote?
Wanaoandika hayo ni Mashabiki tu.
 
Hoja kuu ya MALCOM LUMUMBA ambayo ninaiona inamashiko ni Wairan bado wengi wanamshikamano na serikali yao.
Hiyo ndio hoja kuu.

Kwamba Marekani na Israel vita hii itakuwa ngumu kwao kushinda au itachukua muda mrefu kushinda kwa sababu bado Iran inanguvu ya umoja baina yao.

Kwamba Wamerakani wameshindwa kuwagawanya wa Iran. Tofauti na Marekani alivyotarajia.

Hii itapelekea ugumu kwa Marekani kuvamia Iran kijeshi kwa kutumia Majeshi ya ardhini.
Na kama hakuna majeshi ya ardhini itamaanisha lengo la regime change halitafikiwa.
Naona hiyo ndio hoja yako kubwa.

Lakini mpaka sasa Iran yupo kujihami, anajitetea na Hana lengo na hawezi kushinda kwa kusema amuangamize adui yake.

Ukweli ni kuwa Marekani na Israel hii vita wanaitaka, na kwao ni muhimu kushinda. Na Hilo litatokea tuu.

Kwa vile Marekani na Israel nao ni watu kama watu wengine. Ikitokea Wameshindwa kufikia Malengo basi mambo mengi yatabadilika hapo Mashariki ya Kati lakini pia Mtazamo wa mataifa duniani kumhusu Mmarekani
Simple calculation

Hii vita Marekani na Israel wameshashindwa

1. Regime change imeshindikana
2. Military base za Marekani Middle East zimeharibiwa vibaya mno
3. Gulf Countries watajitenga na Marekani maana Hana msaada kwao ( Hili tayari limeanza na wameanza kulalamika)
4. Marekani atashuka kiuchumi sababu anapigwa sehemu nyeti za energy
5. Vita hii ni Allies wasionekana ambao ni China ,Urusi na NK ambao wako na Iran
6. South Africa member wa BRICS anaandaa ushawishi AU kuitwmbua Israel kama Terrorist state
7. Kama asemavyo MALCOM LUMUMBA hii ni vita ya Uchumi na Energy na kwenye hili wote tutembea kwa miguu kama Hali ikiendelea hivi na Strait of Hormuz ikiendelea hivi kwa kupitisha meli za Uchina tu hadi Sasa pipa Moja ni $97 hadi wiki ijayo itakuwa $150 na Iran lengo ni ifike $200 kiufupi target ya Vita hii ni ya Iran kumuondoa USA middle east , China kumshusha USA kiuchumi na Urusi kuwashusha Ulaya kiuchumi
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2022 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Huu uandishi wako wa leo umenikumbusha memba mmoja anaitwa Mathewson kama sikosei. Yeye alishaamua kutumia njia ya kufoka akisema wa Tanzania ukiwaeleza jambo kwa u pole hawasikii Wala hawaelewi.
Hahaa
 
Unachekesha wewe ambaye umeshindwa kusoma kwa ufahamu.

Japan kwa Uchina ni taifa dogo mno.

Japana kwa Uchina ni dogo kiuchumi, dogo kiukubwa, dogo kieneo, dogo kitamaduni na dogo kiumri.

Japan ni kubwa kwako wewe mtanganyika chogo a.k.a Bazazi Bin Dunya ila dogo kwa Uchina....
I always thought you are objective. Sasa mambo ya kuitana machogo mara dunya yanatokea wapi tena mwana diplomasia. At first niliona kawaida ila mbona hii siyo style ya diplomats
 
Mkuu changia hoja mbona kama uwezo wako imejaa kwenye Matusi tu kama hujui Geopolitics tulia usome tu ,

Acha kudhalilisha Ukoo wako
Wewe akili huna,ndo maana mtiani mlikuwa mnafeli,sasa mtu kaleta mada lakini records haziko sawa,mtu anakuambia Russia ilivamia Ukraine 2026,haoni hapo kabla ya kuchangia lazima uweke records sawa??
 
Hoja kuu ya MALCOM LUMUMBA ambayo ninaiona inamashiko ni Wairan bado wengi wanamshikamano na serikali yao.
Hiyo ndio hoja kuu.

Kwamba Marekani na Israel vita hii itakuwa ngumu kwao kushinda au itachukua muda mrefu kushinda kwa sababu bado Iran inanguvu ya umoja baina yao.

Kwamba Wamerakani wameshindwa kuwagawanya wa Iran. Tofauti na Marekani alivyotarajia.

Hii itapelekea ugumu kwa Marekani kuvamia Iran kijeshi kwa kutumia Majeshi ya ardhini.
Na kama hakuna majeshi ya ardhini itamaanisha lengo la regime change halitafikiwa.
Naona hiyo ndio hoja yako kubwa.

Lakini mpaka sasa Iran yupo kujihami, anajitetea na Hana lengo na hawezi kushinda kwa kusema amuangamize adui yake.

Ukweli ni kuwa Marekani na Israel hii vita wanaitaka, na kwao ni muhimu kushinda. Na Hilo litatokea tuu.

Kwa vile Marekani na Israel nao ni watu kama watu wengine. Ikitokea Wameshindwa kufikia Malengo basi mambo mengi yatabadilika hapo Mashariki ya Kati lakini pia Mtazamo wa mataifa duniani kumhusu Mmarekani
Unena ukweli bila ushabiki kinachoilinda ilani ni umoja wao Marekani alifikiri akimuua kiongozi wajuu basi nch itasambaratika hii vita itaishia kwenye mazungumzo
 
Wewe akili huna,ndo maana mtiani mlikuwa mnafeli,sasa mtu kaleta mada lakini records haziko sawa,mtu anakuambia Russia ilivamia Ukraine 2026,haoni hapo kabla ya kuchangia lazima uweke records sawa??
Sasa hiyo si ni minor issue kabisa ni February ndio lakini sio 2026 nini ambacho hukuelewa ? Unapenda kushadadia vitu vidogovidogo kama Kizimkazi
 
USA wenyewe kwa muhibu wa D.Trump atleast anakana kwamba wako vitani, anasema (Trump) wamechukua actions tu ku-bomb iran.
anyway, lkn jambo ambalo binafsi nashindwa kuelewa khs wanaoisifia islamic republic of iran, irani haina air defense kabisa ndege za USA na israel zinaingia na kutoka kwenye anga ya irani zinavyotaka, uongozi wote wa irani kuanzia kiongozi wao mkuu ayatola ambaye ni commander in chief wa jeshi kwa nchi nyingine ni kama raisi wa nchi, mkuu wa majeshi wote kuanzia waziri wa ulinzi, general mkuu wa jeshi na cream yote wameuliwa kirahisi kabisa bila ya kizuizi chochote kile halafu hapo hapo bado kuna watu wanasema kwamba irani anashinda? anashinda nini sasa? hana uwezo wowote ule wa kulinda air space yake anawezaje kushinda chochote?

kwa hali ya kawaida walipaswa (mullahs) kusalimu amri zamani sana kwani siyo mara ya kwanza mwezi juni mwaka jana 2025 USA waliiingia air space ya irani kirahisi kabisa na ku-bomb nuclears site bila ya kizuizi chochote kile hilo peke yake lilipaswa liwashtue kwa kushindwa kujilinda kwani hawana uwezo, wangesalimu amri kujipanga upya na kuanza maisha mapya lkn bado wanashupaza shingo wakati hawana uwezo wowote ule wa kujilinda dhidi ya adui ...
Kama hawana huwezi SI ndo ingekuwa
Raisi kumaliza vita
 
kwenye namba 5.
Nilitegemea ungetumia akili kidogo kufanya comparison ya kijiografia kati ya IRAN na USA kulinganisha RUSIA na UKRAINE..
Comparison kivipi,kwamba inashindikana ukiwa Tanzania na kuishambulia Marekani kwa missiles? Hapo ndio ujue Iran sio level ya Marekani maana tumeona Marekani anatuma ndege kutoka kwake directly kwenda kushambulia Iran ambapo Iran hawezi hili.
 
Ilitegemewa kwamba Iran lazima atajibu kwa nguvu tena alisema kabisa atakuwa anapiga kwenye kambi za USA zilizopo kwenye nchi za kiarabu na ilishatokea kwenye ile vita ya siku 12

Sasa Iran anakata moto kadri siku zinavyosogea! Awali alikuwa anarusha drones na makombora yapatayo 500 kila siku, leo anarusha chini ya 20 kwa siku.

Kwa sababu lounchers na maghala ya siraha yanawindwa na Myahudi na kuyalipua kila siku.
Imefika hatua marubani wa USA na Israel wanapiga hadi selfie wakiwa kwenye anga la Iran, aibu sana hii

Itafika hatua hututaona kombora hta moja ikitokea Iran ni suala muda tu
 
Ilitegemewa kwamba Iran lazima atajibu kwa nguvu tena alisema kabisa atakuwa anapiga kwenye kambi za USA zilizopo kwenye nchi za kiarabu na ilishatokea kwenye ile vita ya siku 12

Sasa Iran anakata moto kadri siku zinavyosogea! Awali alikuwa anarusha drones na makombora yapatayo 500 kila siku, leo anarusha chini ya 20 kwa siku.

Kwa sababu lounchers na maghala ya siraha yanawindwa na Myahudi na kuyalipua kila siku.
Imefika hatua marubani wa USA na Israel wanapiga hadi selfie wakiwa kwenye anga la Iran, aibu sana hii

Itafika hatua hututaona kombora hta moja ikitokea Iran ni suala muda tu
Sawa Mzee akivamiwa ukrein sisawa ila Kwa Irani ni sawa huo niuendawazimu na uchawa ulipitiliza
 
USA wamesema itawachukua 4-6 weeks kukamilisha objectives zao. Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu alitegemea hii vita iishe ndani ya wiki.
Na hadi sasa mwanga wa kukamilisha objectives zao unaonekana pa kubwa sana.
 
Simple calculation

Hii vita Marekani na Israel wameshashindwa

1. Regime change imeshindikana
2. Military base za Marekani Middle East zimeharibiwa vibaya mno
3. Gulf Countries watajitenga na Marekani maana Hana msaada kwao ( Hili tayari limeanza na wameanza kulalamika)
4. Marekani atashuka kiuchumi sababu anapigwa sehemu nyeti za energy
5. Vita hii ni Allies wasionekana ambao ni China ,Urusi na NK ambao wako na Iran
6. South Africa member wa BRICS anaandaa ushawishi AU kuitwmbua Israel kama Terrorist state
7. Kama asemavyo MALCOM LUMUMBA hii ni vita ya Uchumi na Energy na kwenye hili wote tutembea kwa miguu kama Hali ikiendelea hivi na Strait of Hormuz ikiendelea hivi kwa kupitisha meli za Uchina tu hadi Sasa pipa Moja ni $97 hadi wiki ijayo itakuwa $150 na Iran lengo ni ifike $200 kiufupi target ya Vita hii ni ya Iran kumuondoa USA middle east , China kumshusha USA kiuchumi na Urusi kuwashusha Ulaya kiuchumi

Vita bado mbichi kusema Marekani ammeshindwa ni mapema Sana.

Kwa ninavyoona jinsi Amerika alivyopania. Sioni kama atashindwa. Atatumia Kila mbinu kubadilisha utawala hapo Iran.

Watu Aina ya Trump sio watu WA kukubali kushindwa
 
Back
Top Bottom