Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Tukisema jamaa kapuyanga anatumind. Taifa dogo ambalo hata China mwenye alihofia??? Jamaa hapa kazingua.
Comrade Bazazi Bin Dunya hebu tulia.

Japan is a Chihuahua with a memory of a lion....

Japan aliweza kumuonea Uchina pale tu ambapo Uchina alikuwa chini ya utawala wa mataifa ya Ulaya.

Kihistoria Uchina na India ndiyo mataifa makongwe na yaliyowahi kuwa na nguvu sana Mashariki ya Mbali kwa miaka zaidi ya 5000. Kiufupi Uchina limewahi kuwa taifa tajiri zaidi duniani kwa vipindi vitatu tofauti ndani ya miaka 2000. Huyo Japan amenza kuwa na nguvu karne ya 19 baada ya Mapinduzi ya kisayansi ya Mfalme Meiji. Ila Japan aseme ajidanganye amvimbie Uchina, nakwambia itakula kwake. Taifa lenye watu zaidi ya Bilioni moja, tena majirani zako, utapambanaje nao labda ???
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.
Mkuu 'Malcom Lumumba', umeandika mengi; najuwa maandishi marefu ya aina hii huwa ni kikwazo kwa wengi humu JF

Nimejitahidi nikakusoma mzima. Mara zote huwa nipo upande unaoonewa, (underdog) na hasa kama anayeonewa hafanyiwi haki. Sikuwa upande wa Ukraine kwa sababu alikubali kuwa chambo cha kutumiwa na wakubwa.

Lakini hasa lililonifanya nirudi na kukusoma mada nzima, baada ya kukaribishwa kwenye mada yako hii, ni kuhusu swali lako hilo ulilowasilisha kama kichwa cha mada yako:

"---kwa nini Marekani ameshindwa kumaliza Iran haraka"

Kwani ulikuwa na matarajio ya Iran kumalizwa haraka katika muda gani?

Kumalizwa kwa Iran ulitegemea kuweje?

Kuna mifano yoyote ambayo nchi ilimalizwa haraka? Unaweza kusemalabda Venezuela ilimalizwa haraka?

Umetoa mfano wa Afghanistan kumalizwa haraka, jambo ambalo siyo kweli, kwa sababu sote tunajuwa walivyokimbia na kuacha silaha huko

Hakuna nchi hata moja iliyomalizwa haraka; mara zote wanaoshambuliwa wakiweka ngumu kazi ya kumalizwa huwa haipo; isipokuwa misukule kama tulivyo sisi sasa hivi.

Ningependa kuingia kwenye sababu za hawa wakubwa kuwa na tabia hizi za uonevu hasa kwa sasa. Bila ya kueleza kwa undani, nakurejesha tu kwenye shughuli iliyofanyika mwaka jana Uchina ikiwahusisha akina Putin, Xi Jinping, Kim Jong Un, na waziri mkuu wa India. 'Optics' hizo na yaliyozungumzwa hapo usifikiri yalienda bila kutiliwa maanani na hawa wakubwa.

Ngoja niishie hapa kwa sasa.
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2022 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Hapo kwa ndugu zetu katika imani🤣🤣
 
Comrade Bazazi Bin Dunya hebu tulia.

Japan is a Chihuahua with a memory of a lion....

Japan aliweza kumuonea Uchina pale tu ambapo Uchina alikuwa chini ya utawala wa mataifa ya Ulaya.

Kihistoria Uchina na India ndiyo mataifa makongwe na yaliyowahi kuwa na nguvu sana Mashariki ya Mbali kwa miaka zaidi ya 5000. Kiufupi Uchina limewahi kuwa taifa tajiri zaidi duniani kwa vipindi vitatu tofauti ndani ya miaka 2000. Huyo Japan amenza kuwa na nguvu karne ya 19 baada ya Mapinduzi ya kisayansi ya Mfalme Meiji. Ila Japan aseme ajidanganye amvimbie Uchina, nakwambia itakula kwake. Taifa lenye watu zaidi ya Bilioni moja, tena majirani zako, utapambanaje nao labda ???
EEEEnHEEEE!

Mwambie Waingereza wapeleke "opium war" wakati huu huko China!

Hii miamvuli wanayoitegemea akina Japan na wengineo imeanza kuwa na matundu ya kutisha sana.
 
Myahudi wa kibosho likimwaga madini kama lipo uwanja wa vita Iran kumbe pumbavu tu
Mkuu MALCOM LUMUMBA kwanza nikupe pole kwa maumivu ya kichwa unayopitia katika kipindi hiki cha vita. Nafikiri ulitegemea Iran iwe imelipua aircraft carrier ya Marekani huko Mediterania sea lakini mpaka sasa ni kipondo tu kinatembea. Kiuhalisia Iran inaona mambo ni magumu na baada ya wiki moja ya huu msako wananchi watajitoa mhanga kupambana na serikali ya kiimla ya Iran kwani mpaka sasa haina mkuu wa nchi na hata makamanda wakuu wa jeshi wameshakufa na kuna wasiwasi wa kuuawa kwa rais na wasaidizi wake wote. Kwa sasa Iran hata internet pia imezimwa siku ya sita leo na hili ni hatari kwa usalama wa taifa. Mkuu see you next
waga
 
Mkuu 'Malcom Lumumba', umeandika mengi; najuwa maandishi marefu ya aina hii huwa ni kikwazo kwa wengi humu JF

Nimejitahidi nikakusoma mzima. Mara zote huwa nipo upande unaoonewa, (underdog) na hasa kama anayeonewa hafanyiwi haki. Sikuwa upande wa Ukraine kwa sababu alikubali kuwa chambo cha kutumiwa na wakubwa.

Lakini hasa lililonifanya nirudi na kukusoma mada nzima, baada ya kukaribishwa kwenye mada yako hii, ni kuhusu swali lako hilo ulilowasilisha kama kichwa cha mada yako:

"---kwa nini Marekani ameshindwa kumaliza Iran haraka"

Kwani ulikuwa na matarajio ya Iran kumalizwa haraka katika muda gani?

Kumalizwa kwa Iran ulitegemea kuweje?

Kuna mifano yoyote ambayo nchi ilimalizwa haraka? Unaweza kusemalabda Venezuela ilimalizwa haraka?

Umetoa mfano wa Afghanistan kumalizwa haraka, jambo ambalo siyo kweli, kwa sababu sote tunajuwa walivyokimbia na kuacha silaha huko

Hakuna nchi hata moja iliyomalizwa haraka; mara zote wanaoshambuliwa wakiweka ngumu kazi ya kumalizwa huwa haipo; isipokuwa misukule kama tulivyo sisi sasa hivi.

Ningependa kuingia kwenye sababu za hawa wakubwa kuwa na tabia hizi za uonevu hasa kwa sasa. Bila ya kueleza kwa undani, nakurejesha tu kwenye shughuli iliyofanyika mwaka jana Uchina ikiwahusisha akina Putin, Xi Jinping, Kim Jong Un, na waziri mkuu wa India. 'Optics' hizo na yaliyozungumzwa hapo usifikiri yalienda bila kutiliwa maanani na hawa wakubwa.

Ngoja niishie hapa kwa sasa.
Mzee unaogopa kuwa na record mbaya kwa mafaili ya jamaa wa Msasani pale Mwai Kibaki?
Unaogopa kunyimwa ruhusa kujivinjari nchini kwao 😃
Mambo ya kugongewa muhuri kwenye mkoba au siyo?
 
CIA na MOSSAD zikae chini for years waje na suluhisho halafu mtu uje tu uone US na Israel zimekosea, HAPANA.
Katika vita ya siku 12 , PM Netanyahu alikiri kwamba MOSAD walikosea kwa kutoa data zisizosahihi kuhusu uwezo wa Iran kwa ku under estimate nguvu ya Iran. CIA wamekiri kukosea Libya na hata Syria ya leo

MALCOM LUMUMBA amerudia sana mfano wa Viet Nam . CIA ilifeli kama ilivyofeli kule Afghanistan
 
Sijui kwa nini Trump kawa mtumwa wa Netanyahu wakati Biden hakua ivyo
Hapana! Marekani ni watumwa wa Israel. Kuna lobbying group inaitwa AIPAC( America-Israel PUBLIC Affairs Committee)! imefanikiwa kuweka viongozi katika Congress na White house. Senators na Reps wanafadhiliwa na AIPAC inayoundwa na Wayahudi wenye pesa

Biden alisadia vita ya Gaza na kuzuia UN resolutions zote. In fact Biden ameburuzwa sana na Israel
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2022 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Ukishachagua TU upande
Uchambuzi wako unakosa mantiki na credibility

Unalinganisha vita ya Marekani aliyepigana chini ya wiki mbili na Urusi ambaye anapigana miaka mitatu Hadi sasa na taifa jirani hapo
 
Wewe nikikumbuka ulivyokuwa unatuaminisha mwanzoni mwa vita vya Urusi
Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.

Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.
Wewe jamaa tangu uandike uongo uongo kule kwenye uzi wa mgogoro wa Urusi na Ukraine, inahitaji kusoma mara mbili mbili unachoandika.
Kwa hiyo nyinyi mnafurahi taifa moja kuua political leadership ya taifa jingine kisa vita???Hiyo ni sign ya weakness sio nguvu.Nguvu inatambulika kwenye utiifu wa sheria za kimataifa, sio kulipua watu na nchi kisa una jeshi kubwa, nguvu kubwa etc.
Pili mlitaka Urus wamle kichwa Zelensky ili tu awafurahishe watu kama nyinyi et ndo nguvu hizo au sio???Umesahau Putin alimuhakikishia waziri mkuu wa Israel kipindi kile kuwa hatomgusa Zelensky???Uo ndo uongozi...
Vita sio betting, au Simba na Yanga, kwamba mna-prove ubishi wenu kwa kutembea na roho za watu.
Et Urusi hatawali anga, mosi hujui kuwa kuna vijeba vimejichimbia pale -NATO na air defenses za Kutosha, utalinganisha na Iran??
Pili Urusi anawezapiga popote kwa missiles akitokea kwake, kwa nini ahangaike kuweka rehani maisha ya airforce yake wakati ana alternative??Makombora tu na drones zinagusa kila kona..

US atashinda pambano pale Iran lakini hatshinda vita...BATTLES yes, atawatwanga kwelikweli lkn kushinda vita sio rahisi pale, nchi kubwa ile, milima na mapango kama yote
 
Back
Top Bottom