Kwanini Ma IT bongo sio matajiri?

Kwanini Ma IT bongo sio matajiri?

Ma-IT watanzania wako wengi. Check github ujionee mwenyewe kuwa wabongo wako wengi. Ila kwa kifupi shida ni moja; kama wewe ni software developer mzuri, hauna sababu ya kubaki bongo. Nchi kibao duniani zitakupigania na kukupa visa karibu bure.

Nikupe mfano. Nilirudi bongo baada ya kusoma nje kwa muda mrefu. Nilitaka kuanzisha kampuni ya software na kujitegemea. Nilianzisha kampuni na kuanza kuzunguka mtaani kuuza solution yangu. Tatizo kubwa nililiona ni kuwa wabongo hatuna uwezo wa kuona solution mpaka inapofika too late (hii ni shida kubwa duniani kote ila bongo nimeliona zaidi). Kwa maana nyingine, mpaka tuone wengine wanatumia kitu ndio tunaanza kudandia. Idea zetu za software ni za kizamani sana. Na software development ni eneo ambalo linakuwa na kubadilika haraka. Mfano ni baadhi ya kampuni na sekta kibao serikalini zinang'ang'ania kuwa na server kwenye ofisi zao. Mambo ya kuwa na cloud computing ni kitu kigeni. Wengi wanabaki kuhofia security ya cloud computing. Ukijaribu kuwaelewesha kuwa security ni balaa zaidi unapokuwa na server zako mwenyewe, wanabaki kufikiri kuwa mradi unaiona server kila siku basi hiyo ndio security (kana kwamba server ikiibiwa ndio security imefeli). Baada ya kusota miaka kadhaa kujaribu biashara bongo bila mafanikio nikaamua kupiga kazi na kampuni za nje ya nchi kama consultant nikiwa bado bongo (remote working). Mshahara wangu wa kwanza ulikuwa $3000 kwa mwezi. Kipindi nasota na wabongo, nikipata $800 kwa mwezi nilikuwa najiona mjanja. Huo mshahara wa kampuni za nje hata sikupigania na tayari nilikuwa napiga hela mara nne ya nilichozoea. Nilikuwa single, sina demu wala mtoto. Naomba niwaulizeni, utabaki kujaribu kupiga dili na wabongo baada ya hapo? Baada ya kama mwaka hivi nikaanza kudai hela ambayo ni halali kwa experience yangu. Bila mabishano mshahara ulipanda hadi $4800 kwa mwezi ($30/hr).

Unauliza ni kwanini hakuna matajiri wa IT bongo? Jibu hilo hapo juu 😀 Mpaka siku bongo tutapoanza kuona umuhimu wa IT, vijana wote wanaoweza hizi kazi tutabaki kupiga biashara na nchi ambazo zinafadhili kazi zetu.
 
Shida kubwa ni kutokuwa na ile kiu ya kutaka mafanikio.
Kukata tamaa kwa haraka na wengine kutaka shortcut kwa kupata pesa ya haraka.
Ujuzi unahitajika sana ili uwe vizuri kwenye IT halafu mengine yanafuata.
 
Silicon valley sio wabunifu kama mnavyofikiri, ila wana access kubwa sana ya hela.
Fikiria kampuni kama Uber ambayo haijawahi kupata faida inaweza kupata wawekezaji waliowapa $8 billion!

WhatsApp kabla haijanunuliwa walipewa $60 million na wawekezaji kujikuza, wabongo tukianzisha hizo kampuni hakuna hata wa kutupa senti, mwisho wa mwezi hatuwezi hata kulipia servers.
 
Kuna tatizo upande wa mamlaka ya mawasiliano na hawa watu kwa mfano TCRA walijaribu kuzifungia simu feki lakini kuna kijana mmoja alijaribu kuibadilishia imei number ikafanya kazi, walichokifanya TCRA ni kumkamata na kumpeleka mahakamani. Badala ya kujiuliza wao wamewekaje imei lock kwenye simu yenye serial number na product code na bado ikavalishwa imei number na kufanya kazi. Matokeo yake walimpiga faini ya milioni 5 (5,000,000/=).. sasa tujiulize na wenzetu wa mataifa mengine walifikaje huko ?
Unamkamata kama huyo aliefanya hivyo aweze kuwaonyesha mmekosea wapi ili muweze kujizatiti zaidi kwa mpango wenu endelevu.
 
Silicon valley sio wabunifu kama mnavyofikiri, ila wana access kubwa sana ya hela.
Fikiria kampuni kama Uber ambayo haijawahi kupata faida inaweza kupata wawekezaji waliowapa $8 billion!

WhatsApp kabla haijanunuliwa walipewa $60 million na wawekezaji kujikuza, wabongo tukianzisha hizo kampuni hakuna hata wa kutupa senti, mwisho wa mwezi hatuwezi hata kulipia servers.

Inawezekana bongo hapa. Your network determines your networth. Edwin Bruno Smart Code deal ya M-paper alipigwa kama Million 900 hivi na vodacom. Nakumbuka alivuta Range mpyaaa 0km hadi mzee mengi aliongea. Ahah big up kwake edwin. Ishu ni kujipanga mzee proffessionally and unatoboa. Sio una andaa mzigo hafu ujanja ujanja tu bila kuandaa proper presentation kutoboa inakua ngumu sana. Pia muhimu kushirikisha watu sio coder wewe, graphics wewe, marketing wewe yani kila kitu unajikuta juajua hapa you r likely to fail.
 
Tatizo bongo hakuna investors ukuiangalia kampuni kubwa za tech zimekua kwasababu kuna watu walifanya ivestemestment.
Tatizo si kwa watu wa IT tu pia Investors hawajaona fursa katika...Naamini kuna watu wana ideo tena nzuri tu ......
 
Wanajua kubadilisha ram, hdd, CD Rom windows ikiwa na shida utengenezaji wao nikuipiga chini na kufuta kila kitu
 
Inawezekana bongo hapa. Your network determines your networth. Edwin Bruno Smart Code deal ya M-paper alipigwa kama Million 900 hivi na vodacom. Nakumbuka alivuta Range mpyaaa 0km hadi mzee mengi aliongea. Ahah big up kwake edwin. Ishu ni kujipanga mzee proffessionally and unatoboa. Sio una andaa mzigo hafu ujanja ujanja tu bila kuandaa proper presentation kutoboa inakua ngumu sana. Pia muhimu kushirikisha watu sio coder wewe, graphics wewe, marketing wewe yani kila kitu unajikuta juajua hapa you r likely to fail.
Hongera zake ila hiyo ni $400,000 before taxes, developer aliyeajiriwa Sillicon Valley anaitenegeneza hiyo ndani ya miaka kama miwili/mitatu bila kujisumbua kuendesha biashara. Of coz sisemi kuwa hakuna atakayetoka bongo ila sio kwa rate na viwango wa SV na tusijifananishe kabisa.
 
We hadi mtu awe tajiri unahitaji awe anaingiza how much?
Nafahamu watu kama wanne wa karibu ambao washavuka Tshs. bilioni moja, na wengine wanaochezea kwenye milioni mia na. Na wapo kwenye hii hii sector na wanaishi Tanzania. Situation ni ileile tu dunia nzima, wachache unakuta wamewin sana, wengine unakuta wa katikati na wengine hawajui kabisa wanachofanya wamefulia.
Hawa wa bongo sema tu sio watu wa kelele, huwezi kujua kama wapo unless upo karibu nao.
 
Hongera zake ila hiyo ni $400,000 before taxes, developer aliyeajiriwa Sillicon Valley anaitenegeneza hiyo ndani ya miaka kama miwili/mitatu bila kujisumbua kuendesha biashara. Of coz sisemi kuwa hakuna atakayetoka bongo ila sio kwa rate na viwango wa SV na tusijifananishe kabisa.

Ila Silicon Valley kodi ya nyumba ni kuanzia $4000/mwezi. Kikombe cha kahawa ni $8. Bongo kwa hiyo hela unaishi kama mfalme.
 
Just being curious...kwani watanzania wa fields zingine ni matajiri mpaka uwaone hao IT sio matajiri?
By the way nadhani tqnzania yote ni nchi masikini pamoja na hao kina bakhresa mengi manji rostam dewji....ila bado ni nchi masikini dunia ya 3
 
Ndugu wanajukwaa, nimefuta mafaili niliyokuwa nimehifadhi ndani ya simu ya Samsung J1 ACE kwa bahati mbaya, inaniuma sana! Naomba mtu mwenye maujanja ya ku-RECOVER files hizi anisidie tafadhali.
 
Tatizo hata serikali haitumia IT ndio tatizo linaanzia hapo, ukiona serikali imetangaza nafasi za IT ujue hao wanaenda kuwa kama ma-typist tu wa ofisini, Serikali ikiamua kutumia teknolojia utaona jinsi hali itakavyokuwa nzuri.
Mfano tu nenda kwenye zahanati hata hospitali za serikali za wilaya/mkoa uangalie kuna kompyuta ngapi..!?
Pia nenda shule za serikali kuanzia msingi hadi high schools hesabu kuna kompyuta ngapi..!?
Nenda mahakamani Je hata ofisini tu kwa hakimu kuna kompyuta..!?
Nenda kwenye vituo vya polisi Je hata MKUU wa kituo/Ocd/RPC anakompyuta..!?
Ukizikuta labda mfanyabiashara au mwana siasa alijitolea tu..
Kwa hiyo ili sekta yoyote ikue lazima uwepo na mkono wa serikali utiari wake.
Chukulia mfano tu hata kwenye bongofleva Diomond wa kipindi kile anapelekwa na mh.kikwete Marekani anakutanishwa na wadau wa mziki kule na Diamond wa sasa nazani kuna tofauti kubwa sana..!
Mimi ni IT mzuri tu na ninajua customers servics vizuri na ndo inayonipa ugali hapa mjini lakini sifanyi kazi ya IT kwa sana...!!
 
Kuna Ma it au Mafundi tu Tanzania... it anaimba kazi ati kha!
 
Matajiri sapo hats ha pa bongo. Tatizo wengi wanataka networking ma sip software development. Ukiwana innovation utapata Pesa tu. Ma sip kukopi ah kurekebisha vilivyopo.
 
Ma-IT watanzania wako wengi. Check github ujionee mwenyewe kuwa wabongo wako wengi. Ila kwa kifupi shida ni moja; kama wewe ni software developer mzuri, hauna sababu ya kubaki bongo. Nchi kibao duniani zitakupigania na kukupa visa karibu bure.

Nikupe mfano. Nilirudi bongo baada ya kusoma nje kwa muda mrefu. Nilitaka kuanzisha kampuni ya software na kujitegemea. Nilianzisha kampuni na kuanza kuzunguka mtaani kuuza solution yangu. Tatizo kubwa nililiona ni kuwa wabongo hatuna uwezo wa kuona solution mpaka inapofika too late (hii ni shida kubwa duniani kote ila bongo nimeliona zaidi). Kwa maana nyingine, mpaka tuone wengine wanatumia kitu ndio tunaanza kudandia. Idea zetu za software ni za kizamani sana. Na software development ni eneo ambalo linakuwa na kubadilika haraka. Mfano ni baadhi ya kampuni na sekta kibao serikalini zinang'ang'ania kuwa na server kwenye ofisi zao. Mambo ya kuwa na cloud computing ni kitu kigeni. Wengi wanabaki kuhofia security ya cloud computing. Ukijaribu kuwaelewesha kuwa security ni balaa zaidi unapokuwa na server zako mwenyewe, wanabaki kufikiri kuwa mradi unaiona server kila siku basi hiyo ndio security (kana kwamba server ikiibiwa ndio security imefeli). Baada ya kusota miaka kadhaa kujaribu biashara bongo bila mafanikio nikaamua kupiga kazi na kampuni za nje ya nchi kama consultant nikiwa bado bongo (remote working). Mshahara wangu wa kwanza ulikuwa $3000 kwa mwezi. Kipindi nasota na wabongo, nikipata $800 kwa mwezi nilikuwa najiona mjanja. Huo mshahara wa kampuni za nje hata sikupigania na tayari nilikuwa napiga hela mara nne ya nilichozoea. Nilikuwa single, sina demu wala mtoto. Naomba niwaulizeni, utabaki kujaribu kupiga dili na wabongo baada ya hapo? Baada ya kama mwaka hivi nikaanza kudai hela ambayo ni halali kwa experience yangu. Bila mabishano mshahara ulipanda hadi $4800 kwa mwezi ($30/hr).
Unauliza ni kwanini hakuna matajiri wa IT bongo? Jibu hilo hapo juu 😀 Mpaka siku bongo tutapoanza kuona umuhimu wa IT, vijana wote wanaoweza hizi kazi tutabaki kupiga biashara na nchi ambazo zinafadhili kazi zetu.
mkuu ulikuwa na level gan ya elimu kufanya kazi kama consultant
na unaweza kutupa list ya makampuni uliyokuwa unayaconsult?
na unaweza toa list ya nchi ambazo zinatoa free visa kwa IT?
nje ulikaa kwa muda gan?
 
Kuna fursa kubwa sana yani pesa mingi ya duniani ipo katika sekta ya teknolojia. Fursa inazidi kukua kila siku but why jamaa zetu bongo hapa hawana mpunga yani kuunga unga kwingi.

Personally am not an IT but i love this profession. Nchi kama bongo ipo nyuma sana lakini yenye matamanio makubwa yakufahamu teknolojia then whats pulling us back.?!

Mi ishu nimeona kwenye management ya hawa talented stars pia na wengi wao kuto fahamu marketing and advertisement.

Costech wanafeli na hubs zingine the push is not that hard. Hebu tuimarishe huu mfumo vijana wapige hela. Mifumo user friendly ambayo kila mwananchi hata mwenye elimu ndogo ya teknolojia anaweza master. Kwa research nliyofanya tech is not that expensive nkimaanisha kuna softwares, systems and tools zinawwza patikana in a cheaper way ughaibuni kwa njia tofauti(kijanja).

Na madini yote haya tufungue cyber mall moja kubwa sana, wajae wabongo humo, wachina na warusi wa kutosha. [HASHTAG]#YouthWeCan[/HASHTAG]
Watu wa IT wenyewe tulishakimbia nchi.IT ni fani ambayo ina nafasi kubwa sana za kutanua kimataifa.

Wajanja tulishaona fursa zamani tukawahi kujichanganya viwanja vya kimataifa.

Bongo hakuna soko kubwa la watu wa ndani wanaotumia bidhaa za ndani za IT.

Mifumo mingi watu wa nje wamekinga.
 
Back
Top Bottom