Umenikumbusha mbali sana Mkuu.
Huyu dada moja ya sababu iliyofanya ajiuwe inasemekana ni kukosa uvumilivu kulikochangiwa na kutokwenda JKT.
Wengi wanasema kama angelikwenda JKT, basi matusi ya PUNCH yasingelimtisha kabisa maana JKT, wale ma-Coplo Magwegwa, Gumo, Wawa, Wera, Manyilizu, Mandevu, Chacha, Matron Makunyanzi nk kwa kweli walikuwa wanajua kutukana na kunyanyasa.
Kuna Madada wawili sikumbuki walisoma miaka gani, ambao nasikia Mzee Punch alishindwa kabisa kuwanyoosha. Walikuwa wakiwahi kula kama Wanaume na kuvaa suruali, tabia ambayo Punch hawakuipenda. Basi wakaanza kuwashughulikia. Na wao wakaanza ukorofi wa kwenda mapema Cafeteria kuangalia wamechorwa na nguo gani, basi wanarudi chumbani na kuvaa kama walivyochorwa ili kila mtu awafahamu.
Walisumbuana na Punch hadi mwisho jamaa hawa wakakosa nguvu na kuwaacha. Walipowaacha na wao kweli ndipo wakatulia kabisa na kuacha ukorofi wao. Ila hii kama sikosei inaweza kuwa ilitokea miaka ya 70 kwa sababu zote ni story ambazo mie nilisikia na kwa bahati mbaya, sikusoma UDSM.
Halafu kweli dunia imebadilika Bandugu. Siku hizi wanafunzi wanajibandika wenyewe picha za uchi wa Mnyama na siyo za kuchorwa tena. Wengine walienda kabisa na kuanza kujieleza "nimebakwa Meen" na bila wasiwasi wowote huku TV Camera na Radio zinawarekodi. Mzee Puch angelikuwepo basi watu wangelilipa ili wawekwe pale na wajiongezee umaarufu.
Kufa kwa Punch ilikuwa ni lazima hata kama Levina asingelijiuwa. RIP LEVINA.