Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

..kijana aliyekwenda chumbani kwa marehemu na kumfanyia fujo alitakiwa kufukuzwa chuo na kupelekwa mahakamani kujibu kesi ya jinai.

..viongozi wa chuo ambao hawakuchukua hatua walipaswa kuchukuliwa hatua za kiutawala na kinidhamu.

..kwenye nchi za wenzetu Makamu Mkuu wa Chuo angelazimishwa kujiuzulu kwa kushindwa kuwasimamia waliokuwa chini yake na kulea tabia mbaya ya unyanyasaji.

NB.

..sheria zetu zinasemaje?

..Je, hakuna uwezekano wa kumfungulia kesi ya jinai Omari Salota ambaye ametajwa kwamba alimvamia na kumjeruhi marehemu?
 
Hao Saloti na Victor sijui wanajisikiaje sasa!!?? Hivi familia haiwezi kufungua kesi ya madai Chuo Kikuu au against these people??
Ipo haja ya serikali ya JPM kuanzisha upya uchunguzi wa hili Jambo na wahusika wafikishwe mahakamani haki itendeke
 
Inasikitisha kwa waliokumbwa na dhahama za aina hii....
Punch ilikua nzuri kwenye siasa, nadhani hili la kudhalilisha halikua lengo lao la msingi...nadhani walitumia vibaya nia na uwezo wa punch!!!
Kwahiyo unawatetea au?
 
Niweke sawa kwenye huu uzi. Nimeangalia karibu comments zote. Naona wahandisi wengi waliokuwapo udsm wamekaa kimya.

Huyu mnaye mwita Omary Saloti hili jina si sahihi. Jina lake kamili llikuwa ni Omary Sarota. Mtu tokea mkoa wa Mara. Labda kabila ni mkurya, mwanafunzi mwaka wa pili Mechanical Engineering wakati huo.

Omary Sarota kwa sasa ni marehemu. Ilisemekana alifariki si muda mrefu baada ya Levina kufariki.

Kwa bahati mbaya kifo hiki cha kusikitisha cha Levina kilikuwa politicised ambapo nafasi ya kushutumiwa na wana jamii wa udsm wote ilipokwa. Bila shaka ilikuwa kutokana na ukweli huu ma nguli kama kina Prof. Shivji walitokea kama inavyoelezewa kujaribu kutenganisha 'vitivo na punch' na pia 'vitivo na uhalifu wa wanafunzi mmoja mmoja'.

Binafsi nilikuwa mlimani kipindi hiki, sikuwahi kumsikia Victor; wala Sarota; wala Levina kabla ya kifo cha kusikitisha cha Levina kutokea.

Kama tulivyokuwa wengi wengine, tuliona mengi yaki unfold baada ya kifo kile. Kwa hakika ilihitaji watu wenye busara haswa, kupisha maafa zaidi ambayo yangeweza kutokea. Katika watu hao Prof. Shivji naamini alikuwa mmoja wao.
 
Kuna nadharia kuwa 'PUNCH' walikuwa hawahawa 'WASIOJULIKANA' katika 'practicals' zao za 'propaganda warfare .....', na ndio maana dada yao akavunga kuizika 'PUNCH' rasmi!
NB: MARA BAADA YA MKASA WA LEVINA MUKASA, ULIFUATA MGOMO MKUBWA KUWAHI KUTOKEA CHUO KIKUU CHA MLIMANI!
"WACHAWI HUNGOJEA MTU AFE, ILI WACHEZE NGOMA YAO"
......... MWALIMU
 
Unyanyasaji upo kila kona kuanzia Ndani ya familia, sasa nini cha upekee cha huyu muhanga Miss Mukasa? Story ya 1990s!
Cha pekee nikipi kumuhusu huyu Dada?
Maana ma "punch"wapo kona kuanzia ndani ya familia zetu mpaka maofisini
Sidhani kama 1990.msichana aliyefanyiwa ukatili wa kijinsia ni huyu tu!!??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna chuo cha ualimu haya mambo yalikuwepo mpaka mwaka 2014,
 
JKT, wale ma-Coplo Magwegwa, Gumo, Wawa, Wera, Manyilizu, Mandevu, Chacha, Matron Makunyanzi nk kwa kweli walikuwa wanajua kutukana na kunyanyasa.
Mzee wa sikonge bila Shaka wewe ulikuwa 823KJ Taboraaa dadadeki! mzee wa ma Burn tumbaku, Igombe dam kwenye vitaru, Maisha ya jkt matamu sana hasa ukiwa mdogo!

Afande Wawa huyu bana sijui yuko wapi, au alisha kufa? huyo Seargent alinisurubu sana huyu jamaa! nilipo jaribu kutoroka gwaride
Magweiga wa chiguru bangi mtu!
Manyirizu peace sana yule mzee atakuwa amesha staff!

afande sipi je
Mohamed msomi huyu jamaa!
 
Samahani Kaka paschal Mayalla hujasoma Kirua Sec au Kuishi Maeneo ya Kirua Vunjo
No hapana sijasoma kabisa Moshi. Nimesoma Dar na Arusha.

Ila KV kunanihusu, mwaka 1991/92/93 nikiwa RTD, nilifanya vipindi vya redio shule za KV kuanzia Uparo, Keura, Mandangeni, Kirua Sec, Kisomachi, nikaenda mpaka kule juu Iwa.

Hivyo koo za KV kina Kundi, Kesi, Njau, Mlay, Kifai nazifahamu sana, na kwasababu fulani kila Krismasi time huwa nakuwa KV hata Krismasi hii nilikuwa huko. Tena this time nilipata shida hadi nikaitangaza humu.
P
 
No hapana sijasoma kabisa Moshi. Nimesoma Dar na Arusha.

Ila KV kunanihusu, mwaka 1991/92/93 nikiwa RTD, nilifanya vipindi vya redio shule za KV kuanzia Uparo, Keura, Mandangeni, Kirua Sec, Kisomachi, nikaenda mpaka kule juu Iwa.

Hivyo koo za KV kina Kundi, Kesi, Njau, Mlay, Kifai nazifahamu sana, na kwasababu fulani kila Krismasi time huwa nakuwa KV hata Krismasi hii nilikuwa huko. Tena this time nilipata shida hadi nikaitangaza humu.
P
Okey sawa nimesoma Mandangeni primary school na sisi ndiyo tuliifungua, pindi nilikuona nadhani itakuwa ulikuwa rafiki ya moja wa brother yangu kwenye hiyo familia ya Njau.

Hongera sana kwa kujumuika na wana KV mimi na familia tilikuwa huko pale uparo tarehe 24, 25,26 namalizia Arusha leo, kesho Dodoma jtano narudi jijini.
 
Pascal Mayalla, Natamani hii ndio iwe comment ya mwisho. Sababu umeandika kwa weledi na umakini wa hali ya juu. Pia umeweza kushade light katika hili swala la vandalism katika maeneo ya taasisi za kielimu.

Haya maswali si ya kuyatazama kijinsia au kihisia. Bali ni maswala ya kuyaelewa kiundani na kujua hawa victims na perpetrators wanafikiriaje.

Huwa nachukia sana inapotokea tatizo au mtafaruku katika ya mwanamke na mwanaume then mwanamke akadhurika wachangia mada wanakuwa very quick kujump into conclusion kuwa ni swala la unyanyasaji wa kijinsia of which is not always the case. Mostly huwa inakuwa ni two individuals with psychological issues kupambana.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okey sawa nimesoma Mandangeni primary school na sisi ndiyo tuliifungua, pindi nilikuona nadhani itakuwa ulikuwa rafiki ya moja wa brother yangu kwenye hiyo familia ya Njau.

Hongera sana kwa kujumuika na wana KV mimi na familia tilikuwa huko pale uparo tarehe 24, 25,26 namalizia Arusha leo, kesho Dodoma jtano narudi jijini.
Kuna kabinti fulani ka Njau kalikuwa kanasoma Kiraeni, nilikapendaga na ilikuwa nioe KV, tatizo likawa vitoto vya KV vimefunzwa mambo fulani ni mpaka baada ya ndoa, sisi watu wa mjini, unataka kufanya kwanza test drive ndipo, ulipende gari ndipo ulinunue, wenyewe wanataka ulitazame tuu ulinunue kwanza ndipo uliendesha, hakuna test drive, hiyo tukashindwana.
Kiukweli mabinti wa KV wa enzi hizo, ilikuwa ni bila bila mpaka kieleweka, hakuna test drive!.
P
 
Back
Top Bottom