Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Kwanini Levina Mukasa alijiua UDSM?

Prof . shivji huyu huyu ninayemheshimu aliongea kauli dhaifu kama hiyo? Au alikuwa anamaanisha nini kuhusu saga hiyo labda sikuelewa??!!

R.I.P. Levina.

P, kwenye PhD, inamaanisha Philosophy. Falsafa, kwa Kiswahili. Vyuoni ndiko mahali ambako mijadala ya kifalsafa hujadiliwa zaidi. Falsafa maana yake ni "kupenda ufahamu". Kujadili kifalsafa, hisia huwekwa pembeni, na tafakuri ndio hutumika. Mijadala ya falsafa haiachi kitu salama. Hakuna mada iliyo takatifu au tukufu mno mpaka isiweze kujadiliwa. Kwa sababu mijadala ndio moja ya njia ya kupata ufahamu kuhusu vitu mbalimbali. Kwa hiyo, Prof. Shivji, ambaye pia nami namuheshimu sana, alijadili hoja ya Mheshimiwa Waziri kwa misingi ya kifalsafa.

Hivyo, kama Prof. Shivji alisema hayo yaliyonukuliwa, basi heshima yake inaongezeka, kwa vile aliitendea haki P yake ya kwenye PhD, kuweza kutoa mada ya kifalsafa, wakati makundi ya watu yanajadili mada kwa kutumia hisia.


Hawa Punch hawakuwa na adabu kabisa. Nakumbuka waliwahi kumpanchi hata mkuu wa nchi mwaka wa 1995. "It was so embarrassing!" :embarassed2:

Yalivyoandikwa kwenye OP utaweza kudhani Mzee Punch ilikuwa na kazi ya kuandama female students only, na kwamba male students, na watu nje ya chuo hawakuwa wakipanchiwa. Loss of life is tragic. It should not, however be used to revise history.


Kwa hiyo Prof Shivji naye alikuwa ana entertain huo uhuni wa PUNCH!

No wonder Prof Kabudi kapaita pale UDSM kuwa ni jalalani.

Mijadala ya kifalsafa ni shida kuwepo pale hisia zinapokuwa kubwa kuliko tafakuri. Kwa Profesa Shivji kujadili kifalsafa suala la ndugu waziri (hivi wakati ule tayari walishapitisha utaratibu wa kuitwa Waheshimiwa?) hakusemi lolote kuhusu yeye kuunga mkono au hata kupinga kuwepo kwa Mzee Punch. Kunasema tu kwamba Profesa Shivji ni msomi, ambaye aliweza kutumia usomi wake kujadili suala la ufahamu, linalohitaji tafakuri na siyo hisia.


Mada hii iko frontpage ya JF. Inatakiwa kujadili kwa tafakuri pia, na siyo hisia pekee.
 
Papa1,
Tukuulize wewe na hao marafiki zako, huyo saroti nae bado yupo? Na Huyo Victor nini kilimua?
 
Mlenge,
Maelezo mengi lakini porojo tu.

Are you Shivji's lapdog? Nukuu iko clear kabisa alikuwa anapingana na Mongela cha ajabu unaibuka na blah blah kibao na utetezi dhaifu kabisa.
 
Una cheti changu cha kuzaliwa ama?
Usisahau wengine hawajui asili ya daladala,chai maharage, hata matriculation tuliyofanya udsm wanaisikia tu,wananifanya sometimes nakosa nyuzi za kusoma wanaandika chips mayai tu.

Nakumbuka nilisoma shule moja ina genge la wahuni, bweni lao hata walimu wahaingii, hawa wahuni hawaogi, chakula wanabebea ndoo, na bangi ni kama chai, hawa wana harassments za ajabu. Wkt ule ukiangalia mikoa ya kaskazini walikuwa hivyo, kusini, nyanda za juu, kila shule ilikuwa na tabia hizi. Tambaza kilichonishinda ni genge la wahuni wale.

Watoto wengi wa 2000 wahajui haya madude. Hata Punch walimchora Nani siasa za wakati ule hawajui.

Kuna makundi mtaani yalijulikana kwa majina ya kibabe, kama Komando Yosso nk
 
Usisahau wengine hawajui asili ya daladala,chai maharage, hata matriculation tuliyofanya udsm wanaisikia tu,wananifanya sometimes nakosa nyuzi za kisoma wanaandika chips mayai tu.

Nakumbuka nilisoma shule moja ina genge la wahuni, bweni lao hata walimu wahaingii, hawa wahuni hawaogi, chakula wanabebea ndoo, na bangi ni kama chai, hawa wana harassments za ajabu. Wkt ule ukiangalia mikoa ya kaskazini walikuwa hivyo, kusini, nyanda za juu, kila shule ilikuwa na tabia hizi. Tambaza kilichonishinda ni genge la wahuni wale.

Watoto wengi wa 2000 hawajui haya madude. Hata Punch walimchora Nani siasa za wakati ule hawajui.
Kila masika na mbuu wake mkuu! Hizo zama 'primitive era' zimeshapita.
 
miaka flani nikiwa mkoa wa Mara kimasomo katika moja ya shule za kiseminary kulikuwa na makundi ya type ya PUNCH ila wao tofauti ni kwamba hawakuishia kunyanyasa wanawake tu,ilikuwa wana iba kwa nguvu,wanabaka wanawake na mambo mengine ya kihalifu,Jamaica mockers ni moja ya kundi la hao washenzi,rip levina
 
Wale wahandisi waliokuwa wanafanya haya wako wapi? Lazima wawe na matatizo makubwa sana. Kufanya haya ni kukosa utu. Kuna baadhi ya dhambi ukishazifanya, Huwezi kubaki salama.
RIP Levina
Mkuu

Unaweza kukuta wengine ni viongozi wetu leo

Kumbuka punch ilikua na vijana wa system Wengi Tu
 
Maelezo mengi lakini porojo tu.

Are you Shivji's lapdog? Nukuu iko clear kabisa alikuwa anapingana na Mongela cha ajabu unaibuka na blah blah kibao na utetezi dhaifu kabisa.

Kiongozi Karne, Nukuu ni hii hapa: Maneno ya kwenye mjadala ni yaliyokolezewa wino:

Namkumbuka sana huyu dada yangu, Levina Mukasa. Alikuwa Mtanzania kutoka maeneo ya Kyaka, Misenyi. Alikuwa anachukua shahada ya Ualmu. Alikuwa mtulivu sana kwa aiba na kwa matendo.

Nakumbuka siku aliyofika Getruda Mongela akahutubia akiwa amesimama juu ya HIGH TABLE, meza iliyokuwa katika cafeteria ya Manzese, na ilioyotumiwa exclusively na wanafunzi wa Engineering mwaka wa nne. Mama Mongela alisema kuwa alikuwa amekuja kuizika PUNCH.

Jioni yake Profesa Shivji aliweka mdahalo usiokuwa rasmi nje ya cafeteria ya Manzese na kupinga kauli ya Getruda na kumbeza kwamba " You can't declare resolution of what you didn't establish"
Wiki iliyofuata PUNCH akatoa toleo lingine likimtukana Getruda matusi yote.

Ndipo baada ya hapo serikali ikatangaza kitita cha Sh Mil 10 kwa yeyote atakayempata mshirika yeyote wa PUNCH. Baada ya hapo ilitoka makala ndogo ya PUNCH iliyotundikwa Hall One. Kisha PUNCH ikafifia kabisa.

EMT umenikumbusha mbali sana.

Kumbe, Mama Mongela alitoa hotuba [isiyo rasmi, pengine], aliyosema amekuja kuizika punch. Kisha Profesa Shivji naye aliitisha mjadala usio rasmi, akitoa motion kwamba you can't declare resolution of what you didn't establish. Kwa hiyo Karne unaweza kuona premises za mjadala: inawezekana kuzika kitu usichokianzisha? Mama Mongela hajulikani kwa kuanzisha PUNCH. Kwa hiyo Prof. Shivji alianzisha mjadala wa hoja ya iwapo Mama Mongela anaweza kuizika Punch asiyoianzisha. Hoja ni kwamba inawezekana au haiwezekani.

Tofauti na baadhi ya watu wasiozoea kujadili hoja kama hoja, vyuoni hutegemewa kuwepo kwa mijadala isiyojali wala kutegemea hisia, isipokuwa sababu (reason). Kwamba Prof. Shivji aliweza kutoa mada hiyo na kujadili wakati walio wengi walitumia hisia tu kutoa maoni yao, hii inaonyesha upeo mkubwa alionao Profesa na anastahili pongezi zaidi. Inawezekana kuzika kitu usichokianzisha?

Vyuo vikuu si echo chambers za hisia zitokanazo na tukio du jour, bali ni mahali ambapo hutarajiwa fikra-tunduizi hulelewa na kukomazwa. Kumbuka, mwanasheria nguli Prof. Shivji alikuwa ni mhadhiri mwenye kuandaa wanafunzi watakaohitimu kuwa wanasheria. Uanasheria ni miongoni mwa fani ambazo wataalamu hutegemewa kutumia weledi wa fikra yakinifu pasipo kutegemea hisia walizonazo wakati huo.

Karne, Watu wasio na uwezo wa kujadili hoja kwa kutumia fikra, huwa wepesi wa kuhamisha mjadala kutoka kwenye hoja jadiliwa kwenda kwa mtu binafsi. Maneno yawatokayo kifalsafa huitwa fallacious. Swali lako la iwapo mimi ni lapdog wa Prof. Shivji ni mfano mzuri wa fallacy iitwayo ignoratio elenchi: halina maana. Yaani nikiwa lapdog wa Prof. Shivji au nisipokuwa lapdog wake, haisemi chochote juu ya usahihi wa hoja nilizotoa. (angalia: Irrelevant conclusion - Wikipedia). Kadhalika, ni fallacy nyingine ya Ad hominem -- kumshambulia mtoa hoja badala ya kujibu hoja. Kuchangia mada humu si lazima uwe lapdog wa mtu -- vinginevyo ingenilazimu kutafuta na wewe ni lapdog wa nani -- au hata pengine ingesababisha kutumia Wembe wa Hanlon (Hanlon's razor - RationalWiki) kwamba, Never attribute to malice that which can be adequately explained by stupidity.
 
EMT,
Mpaka mtu anakufa mnaangalia tyu na hao punch ilikua sio kutangaza ni kufatilia chinichini na mkijiridhisha mnatia kiberit mmoja mmoja tyu mbna ingesambaa hiyo punch
 
Back
Top Bottom