Kwanini hivi jamani...

Kwanini hivi jamani...

Siku nyingi kweli my dear, ukisikia naanzisha uzi baadaye wa talaka usishangae naona wanaume tumebadilishana nao jinsia siku hizi.
wee...ukae huko huko hakuna kuachika

vita dhidi ya wanaume haijawahi kutuacha salama...we komaa tu kulala wazi

sent from motorola bapa and nokia jeneza
 
Wamezidi tabia. Mhenga tukiwapata wanaume wa hivi Mara moja moja mbona wataacha umbea tuu.
Waliowahi kum private massage wajiandaa kuja kuvuliwa nguo hadharani .
Midume minafiki hii ndiyo dawa yao lazima uwachane direct.
Ndiooo
 
Unajikuta mchambuzi mzuri poyeeeeeeee. Huu ni ubuyu anakula kila mtu ndiyo maana uliweka Uzi public.
Nilifuatilia vizuri ile skendo usinione wa kuja.
Baada ya wewe kusema cute alikufuata pm watu pale ndiyo wakaanza kuuliza ahaaa kumbe cute dem wa mshikaji.
Watu usiojuana nao hata pm? Ulitaka kila unayegombana naye aje pm ujuane nae kwanza?
Jipaaaangeee Leo ni ubuyu tuu mwanaume kashikwa umbea

Waliowahi kuprivate? Unajua wapo wangapi?

Watu sampuli yenu ndiyo mtaongea juu yangu haya maana tunaqoutiana Humu tu hamnijui japo 20%.

Na wanakusoma hapa wanakushangaa. Endeleeni kujimwaya mwaya na shoga ako.....
Sema ujue dunia ni sehemu ya ajabu sana, mnaweza mkaishia kuja kuwa wapenzi ninyi
 
Salaam jf members

Hivi inakuaje watu wazima wenye familia zao,wanakua wanashindwa kua na busara,hekima na uvumilivu?

Hivi jf hapa ni kama nyumbani kwetu sisi ni wanafamilia moja au majirani tunaoishi pamoja kama ndugu.

Sasa nashangaaa na kupatwa na bumbuazi haswaa nikiona wanajamii moja tunashindwa kustiriana kama ndugu au marafiki wa dhati kwa kweli inaumiza sana na kustaajabisha.

Yaani humu sisi sote ni watu wazima,wasomi na wasio wasomi,lakini leo hii watu wa humu wengine tuna mambo ya ajabu ajabu mpaka yanatia aibu

Kutongozana ni jambo la kawaida sana katika jamii kama hii,lakini sasa humu mwingine akimla 'nyama'msichana basi ndo anajutaa atamtangaza mpaka ajutee..unabaki kua topic tena miaka mia
Mdada nae akitongozwa basi anakuja kumlipua mwanaume wa watu loohh...!!!
Wengine mnawateta watu PM siku mkilipuana mnaumbuana yoootee..

Wengine mnakutana PM,mnapena contacts mnakutana hukoo baadae mnaanza kuwacompare na kuwacontrast kama bidhaa vile

Na wengine msiojijua na kujielewa sasa yaani nyie ndo shida tupu!!ninyi ndo vichaa nashindwa hata kuwaweka kundi lipi...
Unapewa picha ya mtu 'either PM or whasaap'then unaexpose kwa wengine wasiomjua yule mtu..na kuwaambia yule ni nani...!!


Wengine tena wakiwa na mahaba tunajua jf nziima siku wakiachana wanatoleana ya moyoniii yooote looo ...

Kuna wengine ni waongo balaaa yaani kusambaza umbea tu usiomhusu na unaomuhusu...

Jamani tuweni na hekima na busara binadamu ni kiumbe mwenye mapungufu lakini sasa yakizidi ni shidaa...

Tuheshimiane sana tukilana,kukimbiana gesti,kukopana tuuchune tu jamani kibingwa kwani shilingi ngapi...hata tukikataliwa pia tujifunze kupiga kimyaa tu...!!

Hata kama ninyi ni wapenzi msijipambanue saana vile maana dah!mkiachana mwingine akapata"goma"lingine humu mnatupa shida sana kunnua bando la kusoma umbea .

Ni hayo tu kwa leo!!!Mengine mtaongezea


sent from motorola bapa and nokia jeneza
Naona Geni leo umeamua.... Ha ha ha ha ha....... Tatizo moja tu... UTOTO.
 
Watu wengine wanatafuta cheap popularity. Hayo mambo ya kutangazana ni utoto wa miaka kadhaa iliyopita. Lazima utambue kila binadamu ana mapungufu yake. Vijana wa miaka ya sasa umama umewazid. Inasikitisha sana
dc4a88c5833b8e113cc0c6e838ef3035.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza mvujisha taarifa na mvujishwaaji wa hizo taarifa wanatakiwa wajitathimini wote. Wengi wao huwa ni matahira wote.

Mtu mwenye busara atatongoza mwenye busara. Asiye na busara mara nyingi atatongoza matahira wenzake.

Wewe mwanamke/mwanamme unashindwa kumsoma mtu hata kwenye chatting. Basi za jukwaani umeshindwa je za pm. Au ukishafika pm haraka haraka mnapeana location na namba mambo yamekwisha.
Ha ha ha ha ha ha ha... Mzee mwenzangu tatizo moja tu.... UTOTO. Mtu mzima na akili zake anatangaza mambo kama hayo ili iweje?
 
Back
Top Bottom