Heshima na Uthibitisho: Kwanini Tunajionyesha?

Heshima na Uthibitisho: Kwanini Tunajionyesha?

bless on

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2026
Posts
743
Reaction score
1,733
Unajua kwamba watu waliodharauliwa sana katika nyakati fulani za maisha, hubaki na kumbukumbu inayowafanya watafute heshima na kuthaminika kwa namna yoyote. Hujawahi kuona watu waliozaliwa kwenye familia zenye nguvu ya pesa, ni watulivu sana, hawajioneshi na siyo rahisi kujua kama ni watoto wa kishua. Lakini kuna wale ikitokea baba kapata unafuu kidogo, ni lazima dunia nzima ijue. Hii ni kawaida kwa watu waliotamani heshima kwa muda mrefu.

Waliozaliwa na kukulia kwenye 'mkate na cheese' hawajawahi kukosa heshima, kwa hiyo hawahangaiki kuitafuta wala kujipa uthibitisho sababu wanajua wao wenyewe ndiyo heshima wala hawahitaji kukuonesha chochote ili uwaheshimu. Wale rachirachi mara nyingi hawana uhakika kama wanaheshimiwa, wana tatizo la inferiority complex, ni lazima watafute uthibitisho wa heshima na kukubalika.

Utajuaje kama una hilo tatizo, ukiona unapokuwa na hali nzuri kidogo, hutulii mpaka watu wajue, basi tambua wewe ni mhanga. Wengine akishapokea kimshahara ni lazima aanzie bar na kuzungusha raundi kwa walevi kadhaa. Hii yote ni sababu ndani yake anahisi anahitaji uthibitisho wa heshima au thamani ambayo anadhani hakuwahi kuwa nayo.

Kuna wengine hubeba mabegi ili kwenda kupiga picha viwanja vya ndege na kupost mitandaoni. Ukweli ni kwamba, waliozoea kupanda ndege tangu utotoni huwa hawahangaiki na shughuli hizo. Kuna watu humu mitandaoni wanasafiri kila siku na wanakula maisha kisawasawa lakini hawakumbuki kabisa ku post. Ni kwa sababu hayo ni maisha yao, hawaoni ajabu kwa lolote na wanadhani watu wote wanaishi hivyo.

Mtoto aliyezaliwa na kukulia kwenye familia ya viongozi, huwa anaenda ikulu kucheza na anamuona rais au waziri mkuu kama mjomba au ndugu, hawezi kuhangaika kuuonesha ulimwengu kuwa anajuana nao. Lakini kina ngwapangu wakipiga picha na mkuu wa wilaya ni lazima apost mitandao yote na maneno "God did"🤣🤣

Anyway sina lengo la kukandia mtu ila najaribu kukuonesha jinsi ambavyo akili zetu haziwezi kuficha upungufu fulani tulionao.
 

Attachments

  • FB_IMG_1779182661347.jpg
    FB_IMG_1779182661347.jpg
    69.6 KB · Views: 9
Unajua kwamba watu waliodharauliwa sana katika nyakati fulani za maisha, hubaki na kumbukumbu inayowafanya watafute heshima na kuthaminika kwa namna yoyote. Hujawahi kuona watu waliozaliwa kwenye familia zenye nguvu ya pesa, ni watulivu sana, hawajioneshi na siyo rahisi kujua kama ni watoto wa kishua. Lakini kuna wale ikitokea baba kapata unafuu kidogo, ni lazima dunia nzima ijue. Hii ni kawaida kwa watu waliotamani heshima kwa muda mrefu.

Waliozaliwa na kukulia kwenye 'mkate na cheese' hawajawahi kukosa heshima, kwa hiyo hawahangaiki kuitafuta wala kujipa uthibitisho sababu wanajua wao wenyewe ndiyo heshima wala hawahitaji kukuonesha chochote ili uwaheshimu. Wale rachirachi mara nyingi hawana uhakika kama wanaheshimiwa, wana tatizo la inferiority complex, ni lazima watafute uthibitisho wa heshima na kukubalika.

Utajuaje kama una hilo tatizo, ukiona unapokuwa na hali nzuri kidogo, hutulii mpaka watu wajue, basi tambua wewe ni mhanga. Wengine akishapokea kimshahara ni lazima aanzie bar na kuzungusha raundi kwa walevi kadhaa. Hii yote ni sababu ndani yake anahisi anahitaji uthibitisho wa heshima au thamani ambayo anadhani hakuwahi kuwa nayo.

Kuna wengine hubeba mabegi ili kwenda kupiga picha viwanja vya ndege na kupost mitandaoni. Ukweli ni kwamba, waliozoea kupanda ndege tangu utotoni huwa hawahangaiki na shughuli hizo. Kuna watu humu mitandaoni wanasafiri kila siku na wanakula maisha kisawasawa lakini hawakumbuki kabisa ku post. Ni kwa sababu hayo ni maisha yao, hawaoni ajabu kwa lolote na wanadhani watu wote wanaishi hivyo.

Mtoto aliyezaliwa na kukulia kwenye familia ya viongozi, huwa anaenda ikulu kucheza na anamuona rais au waziri mkuu kama mjomba au ndugu, hawezi kuhangaika kuuonesha ulimwengu kuwa anajuana nao. Lakini kina ngwapangu wakipiga picha na mkuu wa wilaya ni lazima apost mitandao yote na maneno "God did"🤣🤣

Anyway sina lengo la kukandia mtu ila najaribu kukuonesha jinsi ambavyo akili zetu haziwezi kuficha upungufu fulani tulionao.
Una point ila hio picha ya kusindikiza sio flex ni mtu mwenye stress anaweza gumia hio kitu hivo
 
Saikolojia ipo hivi; mtu aliefanikiwa/alienacho hana haja ya kuthibitisha hilo kwa yeyote.
Angalia tuu ukipanda ndege na mtu ambaye amekua anazisikia tuu ndege maisha yake yote; Anakuwa na wenge, mara akupe simu umpige picha, mara aguse kile na hiki, akishuka anaomba umpige picha. Atapiga video calls kibao kwa ndugu, jamaa na marafiki. 😊

Mtu aliekulia pesa/ushuani, pesa haimuwashi wala haimpi mchecheto, kashaizowea, ni mazingira yake hayampi mchecheto.

Kuna mshikaji wangu mmoja, alipata kibarua kizuri akanunua gari, nakumbuka siku za kwanza kwanza zile, hakulala, alikuwa anachungulia gari nje dirishani; alikuwa akipaki sehemu akirudi analipukuta vumbi na matambala ya maji, usafi mwingi sana kumbe ndio analichafua. Wenge lile likaisha kadiri anavyozowea magari. 😊

Kama una kitu, fedha, mali na mafanikio kisaikolojia hutakuwa na mawazo ya kuthibitisha hilo, na sababu ni ndogo tuu, tayari unavyo vitu hivyo. Jamii itafahamu kuwa unavyo pasipo wewe kusema au kuonyesha lolote, jamii ina macho. Watu wenyewe tuu ndo utasikia wanasema, na wewe utaanza kujiuliza wamejuaje. 😊
 
Back
Top Bottom