Unaweza mshangaa, lakini kama mke anayejua wajibu wa kuwa mke hawez weka udhaifu wa mumewe hadharani, hawezi sema kuwa mume wangu ananisaliti
Sababu kakaa katika nafasi ya mke na anajua kuuficha udhaifu wa mumewe,
Tukiangalia abigail na nabal,
Nabali alikuwa mume mume mpumbavu lakini ona abigail alivyo mtetetea mume wake mbele ya Daudi,
Msamehe mume wangu kwani aliyatenda haya yote kwaajil ya upumbavu
Akasema msamehe, alibeba udhaifu wa mumewe na kumuombea msamaha kwa niaba na Daud akamsamehe hakumuua
Hakwenda mikono mitupu alienda na vitu vingi niviite zawad au sadaka ili mume asamehewe.
Mwanamke alikuwa mwerevu na mume mpumbavu lakin mke alijua ku cover upumbavu wa mumewe
Kama angekuwa mke asiyejua wajibu wake katika nafasi ya ulinz kwa kumuombea na yeye angekuwa mpumbavu angemwambia tu Daudi muue ni mpumbavu huyu, kanichosha na kwel angekufa
Lakin abigail alijua udhaifu wa mumewe na alijua kuubeba na kumtetea.
Hivyo usishangae kuona mwanamke anamtetea mume mbele za watu, ni wajibu wake
Ila akiwa ndani anajua jinsi ya kusolve.
Sitetei wanaume ila naelezea kuwa kama mke mlinzi juu ya ndoa yako.
In ua Presence Jesus is where I belong