Kwa waliotunga sheria Hii; Kama Rais ni mzalendo na muadilifu ni sababu gani ikawepo kinga ya kutoshtakiwa?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
KWA WALIOTUNGA SHERIA HII; KAMA RAIS NI MZALENDO NA MUADILIFU NI SABABU GANI IKAWEPO KINGA YA KUTOSHTAKIWA?

Anaandika, Robert Heriel

Moja ya sheria inayonifanya nione nchi yetu bado hatuko serious ni sheria inayomkingia Kifua Rais KUTOSHTAKIWA. Kwa kweli sheria Hii sio tuu ni ya ajabu Bali ni sheria iliyolenga kumfanya Rais aabudiwe, awe mungu mtakatifu, Wakati kimsingi sivyo.

Hakuna sababu hata Moja yenye mashiko inayoifanya sheria hiyo iwe ya maana. Ati Mimi Robert Heriel kitendo tuu cha kuwa Rais basi sitashtakiwa. Huo sio uungwana. Hiyo sio sheria za kiungwana.

Rais kama binadamu wengine anaweza kufanya Makosa na uhalifu kama wanavyofanya wengine. Ni muhimu sheria Hii ikaondolewa.
Hatutaki kuchagua Rais ambaye atakuwa na kinga akifanya uhalifu au Makosa. Hilo hatutaki. Ninapotumia wingi ninamaanisha Watu wote wenye fikra na mtazamo kama wangu.

Kitendo cha Sheria hiyo kumkinga Rais asistakiwe automatically kinawakinga na vipenzi wa Rais husika. Ikiwa Rais ambaye ni Kiongozi wa nchi sheria inamlinda basi kimantiki ni kuwa sheria hiyo itawalinda na vipenzi wa Rais.
Sheria hiyo pia inawapa ugumu Mahakimu na majaji kufanya kazi Yao vizuri hasa katika kudili na kesi Kwa baadhi ya Watu hasa vipenzi wa Rais. Hii itafanya Na kuwaingiza Mahakimu na majaji katika Wakati mgumu katika kutoa Haki pindi wafanyapo kazi zao.

Sheria hii sio nzuri Kabisa. Kwamba, ili Rais awe comfortable akiongoza bila kuhofia Jambo lolote. Kwa nini hiyo comfortable inayotafutwa na sheria hiyo iwe katika kumlinda Rais endapo atageuka kuwa Mhalifu?

Sheria hiyo tufanye Mpango ifutwe. Rais au kiongozi atakayekuwa madarakani ambaye ataifuta sheria hiyo basi kuna kila sababu ya kumuita kiongozi huyo ni MZALENDO na MUADILIFU.
Uadilifu ni pamoja na kuwajibika pale unapofanya Makosa.
Ikiwa Rais atakuwa tayari kushtakiwa endapo atafanya uhalifu na Makosa na akabadilisha hiyo sheria basi huyo Rais atakuwa anamaanisha Uzalendo halisi.

Kumtenga Rais na Mkono wa sheria ni kuihujumu nchi na taifa. Ni kuligawa taifa na kuweka kundi la Watawala na watawaliwa. Watawala kamwe hawatafungwa Kwa sababu watalindwa na Rais. Hiyo itafanya kila kiongozi kujipendekeza Kwa Rais hata kama Rais anapuyanga. Kwani kujipendekeza Kwa Rais NI kujiwekea na wewe kinga ya KUTOSHTAKIWA.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
KWA WALIOTUNGA SHERIA HII; KAMA RAIS NI MZALENDO NA MUADILIFU NI SABABU GANI IKAWEPO KINGA YA KUTOSHTAKIWA?

Anaandika, Robert Heriel


Kwa sasa Dar es salaam
Hakuna mzalendo tangu 1995! Tulipinga humu awamu ile kujinasibu ni wazalendo wenye uchungu na Nchi lkn kibaya zaid awamu hiyo ikapitisha sheria bungeni ya kuwaongezea kinga mihimili mingine. Hapo ndipo niliona hakuna nia njema dhidi ya kupambana na wabadhirifu na mafisad!!!
 
Hiyo ni akili ya ma ccm ya kulindana, na ndio inayotuletea hawa machawa wa sasa!.
 
KWA WALIOTUNGA SHERIA HII; KAMA RAIS NI MZALENDO NA MUADILIFU NI SABABU GANI IKAWEPO KINGA YA KUTOSHTAKIWA?

Anaandika, Robert Heriel

Moja ya sheria inayonifanya nione nchi yetu bado hatuko serious ni sheria inayomkingia Kifua Rais KUTOSHTAKIWA. Kwa kweli sheria Hii sio tuu ni ya ajabu Bali ni sheria iliyolenga kumfanya Rais aabudiwe, awe mungu mtakatifu, Wakati kimsingi sivyo.
KATIBA hii ya Jamuhuri ya muungano wa Tz, na CCM ndio jinamizi la watanzania kutopata maendeleo ya haraka,Kumbuka Marais wa Afrika kuwa wachafu ni lazima ndio maana KATIBA haziwagusi asikudanyanye mtu.
 
Hakuna mzalendo tangu 1995! Tulipinga humu awamu ile kujinasibu ni wazalendo wenye uchungu na Nchi lkn kibaya zaid awamu hiyo ikapitisha sheria bungeni ya kuwaongezea kinga mihimili mingine. Hapo ndipo niliona hakuna nia njema dhidi ya kupambana na wabadhirifu na mafisad!!!

Ni kweli Kabisa.
Kwenye nchi na jamii yenye Haki na uungwana hakuna aliyejuu ya sheria. Kwamba huyu anaweza kupelekwa Mahakamani, lakini Yule hawezi kisa anacheo Fulani. Lakini kosa kafanya. Hivi hizi Akili huwa zinatokaga wapi? Ni Akili za ajabu
 
Rais kama binadamu wengine anaweza kufanya Makosa na uhalifu kama wanavyofanya wengine. Ni muhimu sheria Hii ikaondolewa.
Hatutaki kuchagua Rais ambaye atakuwa na kinga akifanya uhalifu au Makosa. Hilo hatutaki. Ninapotumia wingi ninamaanisha Watu wote wenye fikra na mtazamo kama wangu.

Kitendo cha Sheria hiyo kumkinga Rais asistakiwe automatically kinawakinga na vipenzi wa Rais husika. Ikiwa Rais ambaye ni Kiongozi wa nchi sheria inamlinda basi kimantiki ni kuwa sheria hiyo itawalinda na vipenzi wa Rais.
Sheria hiyo pia inawapa ugumu Mahakimu na majaji kufanya kazi Yao vizuri hasa katika kudili na kesi Kwa baadhi ya Watu hasa vipenzi wa Rais. Hii itafanya Na kuwaingiza Mahakimu na majaji katika Wakati mgumu katika kutoa Haki pindi wafanyapo kazi zao.
Kuna chawa fulani wachache ndiyo waliipenyeza kwa manufaa yao binafsi, wakimpotosha Rais akaharibu linakuwa lake na kwakuwa sheria inamlinda basi na yeye Rais anajibanza hapo
 
Hiyo ni akili ya ma ccm ya kulindana, na ndio inayotuletea hawa machawa wa sasa!.

Hiyo sheria ikifutwa itachangia uwajibikaji na uadilifu. Alafu automatically kutakuwa na separation of powers ndani ya serikali. Lakini uwepo wake sio ajabu mhimili mmoja ukawa kibaraka WA mhimili mwingine
 
Ni kweli Kabisa.
Kwenye nchi na jamii yenye Haki na uungwana hakuna aliyejuu ya sheria. Kwamba huyu anaweza kupelekwa Mahakamani, lakini Yule hawezi kisa anacheo Fulani. Lakini kosa kafanya. Hivi hizi Akili huwa zinatokaga wapi? Ni Akili za ajabu
Washachoka kifikra maan dunia ya sasa sio ile ya 5-2-1977!!
 
Bahati mbaya Rais anaweza kuwa mzembe asiyetaka kushughulisha kichwa chake, akaenda kuwatumbukiza shimoni watanganyika kwasababu ya uvivu wake wa kujisomea, bahati mbaya anakuja kulindwa na sheria.
 
Kuna chawa fulani wachache ndiyo waliipenyeza kwa manufaa yao binafsi, wakimpotosha Rais akaharibu linakuwa lake na kwakuwa sheria inamlinda basi na yeye Rais anajibanza hapo

Nafikiri hao machawa walilenga kujitajirisha kupitia Cheo cha Urais.
Waibe Mali za nchi kupitia Cheo cha Urais
Wawe Mafisadi kupitia kinga ya Urais,
Ikiwezekana wakamate na kuteka wapinzani na mahasimu wao na kuwafanyia kinyume cha sheria kupitia kinga ya Urais.
Ni mambo ya kusikitikisha
 
Bahati mbaya Rais anaweza kuwa mzembe asiyetaka kushughulisha kichwa chake, akaenda kuwatumbukiza shimoni watanganyika kwasababu ya uvivu wake wa kujisomea, bahati mbaya anakuja kulindwa na sheria.

Mbali na hayo.
Sheria hiyo inatoa upendeleo WA wazi Kwa MTU yeyote akiwa Rais awe mzembe na asiyehofia uzembe na uhalifu atakaoufanya kwani hakutakuwa na matokeo hasi dhidi yake.

Shria hiyo pia imepanua uwanja kuwa MTU yeyote anaweza kuwa Rais,
 
Na imeongezeka kinga ya wana TISS...

Unganisha dots

Hiyo ilikuwa ni swala la muda.
Kesho na kesho kutwa utasikia Waziri Mkuu yumo, Wakuu wa mikoa na wateule wa Rais ndani.
Kimantiki, ukishamuwekea Kiongozi Mkuu wa nchi kinga ya kushtakiwa tayari hata wale anaowatuma automatically hakuna wa kuwashtaki. Mbona hiyo haihitaji Rocket science kuelewa
 
Back
Top Bottom