Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Sheria hii inaweka masharti ya kusimamia uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, kufuta Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, 1985 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, 1979 na kuweka masharti mengine yanayohusiana na hayo.

Kwa mujibu wa Sheria hii, Mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na nane na ambaye hajapoteza sifa chini ya Sheria hii au sheria nyingine yoyote, atastahili kuandikishwa kuwa mpiga kura chini ya masharti ya Sheria hii.

Kila unapofanyika uchaguzi wa Rais, kila chama cha siasa kilichosajiliwa na kinachokusudia kushiriki katika uchaguzi wa Rais kitawasilisha kwa Tume jina la mgombea wa kiti cha Rais na jina la mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa chama hicho, atapaswa kudhaminiwa kwa maandishi na wadhamini walioandikishwa kuwa wapiga kura kwa madhumuni ya uchaguzi chini ya Sheria hii wasiopungua mia mbili kwa kila mkoa, angalau kwa mikoa kumi ya Jamhuri ya Muungano, kati ya hiyo angalau mikoa miwili kutoka Tanzania Zanzibar.

Endapo kutakuwa na mgombea mmoja halali wa kiti cha Rais aliyeteuliwa, Tume itamtangaza mgombea huyo kuwa mgombea pekee wa kiti cha Rais. Mgombea wa kiti cha Rais aliyetangazwa chini ya kifungu kidogo cha (1) atapigiwa kura ya ndio au hapana na atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa Rais endapo atapata kura nyingi zaidi ya kura zote halali zilizopigwa.

Endapo mgombea pekee wa kiti cha Rais atashindwa kupata kura nyingi zaidi kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), Tume itatangaza siku nyingine ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Rais kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali.
 

Attachments

  • SHERIA_YA_UCHAGUZI_WA_RAIS,_WABUNGE_NA_MADIWANI_YA_MWAKA_2024.pdf
    1 MB · Views: 6
Uchaguzi ni matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kila awamu tunapoteza fedha nyingi kwenye chaguzi ambazo mshindi anafahamika hata kabla ya zoezi la kupiga kura.

Mfumo uliopo humwezeshi mpinzani kutangazwa hata kama amepata 99.99% ya kura zote.
 
Maigizo yao wanayajua wenyewe washatuona manyani basi wanatuendesha na kwakua wabongo ni wavumilivu tutavumilia tena na tena ila mwisho wa watawala utafika
 
Mgombea wa kiti cha Rais aliyetangazwa chini ya kifungu kidogo cha (1) atapigiwa kura ya ndio au hapana na atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa Rais endapo atapata kura nyingi zaidi ya kura zote halali zilizopigwa.

Endapo mgombea pekee wa kiti cha Rais atashindwa kupata kura nyingi zaidi kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2), Tume itatangaza siku nyingine ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Rais kwa notisi itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali

Hapo wangerahisisha iwe asilimia 50 ya kura halali jumlisha kura moja (50% + kura 1),.

Kwanini wanaficha ficha kutamka asilimia ya kura zote halali au mgombea urais anaweza kushinda hata akipata kura 20% ya kura zote halali mradi tu amewashinda wagombea wa urais wote?

Ina maana Tanzania mtu anaweza kushinda urais kwa kupata kura milioni 3 !

Ni bora wabadilishe iwe chama kilichopata wabunge wengi ndiyo kitamteua rais wa Jamhuri ya Muungano badala ya kupoteza pesa kupiga kura ya urais.

Uchaguzi wetu ngazi ya urais wa Jamhuri ya Muungano uwe kama uchaguzi wa kumpata waziri mkuu wa India, Australia, Canada, South Africa n.k ambapo chama kinachopata wabunge wengi ndiyo kinatoa waziri mkuu ambaye hajapigiwa kura moja kwa moja na wananchi.

Mfano wakijitokeza walioandikishwa kupiga kura ni 18,000,000 halafu mshindi akaongoza kwa asilimia 20 yaani 18,000,000 × 20% = kura 3,600,000 za watanzani zimuingize mgombea Ikulu itakuwa kura hizi hazina uzito wa kidemokrasia.

Bora warahishishe mambo cha kitachoshinda wabunge wengi watuchagulie rais badala ya kiini macho hiki cha wananchi wachache kumuingiza Ikulu rais.

Tukifanya hivi kuwa demokrasia iwe katika chama kama South Africa ambapo rais anaweza kuondolewa na chama wakati wowote wanapoona hawamtaki ni demokrasia nzuri badala ya hii rais kutumia mgongo wa wapiga kura kubaki Ikulu.

1711527344883.png

Picha : Rais Cyril Ramaphosa akiapa mbele ya Bunge la Afrika ya Kusini baada ya chama cha ANC kilichopata wabunge wengi kumpendekeza na kumteua awe Rais.

Afrika ya Kusini chama kinaweza kukuondoa ktk madaraka ya urais ikiwa chama kitaona hautoshi. Hiyo imemtokea Thabo Mbeki, imemkuba Jacob Zuma kupitia demokrasia yenye nguvu ndani ya chama ambapo Halmashauri Kuu ya Chama na mkutano mkuu wa chama unaweza kumuondoa kutoka nafasi ya urais wa nchi mwanachama au kiongozi pale kinapoina hatoshi kutumikia nafasi.


South African legislators elected Cyril Ramaphosa president on Wednesday and he promised to create jobs and work for the interests of all citizens, not just members of the majority African National Congress (ANC).

The ANC won South Africa‘s May 8 general election, enabling the party to pick the country’s president, but its share of the vote fell to a post-apartheid low – reflecting anger at corruption and cronyism under Ramaphosa’s predecessor Jacob Zuma.
 
TANZANIA

Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024
46
Tume, taarifa ya matokeo ya awali ya uchaguzi wa
Rais katika jimbo
.
(5) Msimamizi wa uchaguzi atathibitisha na
kutoa nakala ya taarifa ya matokeo kwa kila wakala au
wagombea wa kiti cha Rais, kama wapo.
(6) Tume inaweza kuelekeza kwamba,
msimamizi wa uchaguzi, baada ya kuandaa taarifa ya
matokeo chini ya kifungu kidogo cha (3), abandike
nakala ya taarifa hiyo katika sehemu ya wazi
inayoonekana.
(7) Endapo kuna shaka yoyote kuhusu usahihi
katika kujumlisha kura za Rais katika jimbo lolote,
Tume inaweza kuelekeza kurudiwa kujumlishwa kwa
idadi ya kura za matokeo ya awali kutoka baadhi au
vituo vyote vya kupigia kura katika jimbo.
(8) Baada ya kupokea matokeo
yaliyowasilishwa chini ya kifungu kidogo cha (4),
Tume itatangaza matokeo ya uchaguzi wa Rais kwa
jimbo husika.
(9) Kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (3),
Tume, baada ya kujumlisha kura zote zilizowasilishwa
na kila msimamizi wa uchaguzi kwa mujibu wa
kifungu kidogo cha (4), itatangaza matokeo ya
uchaguzi wa Rais ya nchi nzima.

(10) Mgombea yeyote wa kiti cha Rais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa Rais iwapo
amepata kura halali nyingi zaidi kuliko mgombea
mwingine yeyote.
Marudio ya upigaji

kura

46.-(1) Endapo katika upigaji kura wa awali
hakuna mgombea wa kiti cha Rais aliyepata kura
nyingi zaidi kati ya kura halali zilizopigwa, Tume, kwa
notisi katika Gazeti la Serikali, itapanga siku nyingine
itakayofaa isiyozidi siku arobaini baada ya siku ya
uchaguzi, kwa ajili ya marudio ya upigaji kura katika
uchaguzi wa Rais.
(2) Endapo kutatokea kufungana kwa kura za
wagombea waliopata kura nyingi zaidi, wagombea wa
kiti cha Rais waliofungana ndio watakuwa wagombea
pekee katika uchaguzi wa marudio.
 
TANZANIA

Na. 1 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2024
42
endapo Msajili wa Vyama vya Siasa ataweka
pingamizi chini ya kifungu kidogo cha (3), pingamizi
hilo litawasilishwa ndani ya siku kumi na nne baada ya
siku ya uteuzi.

Mgombea pekee
wa kiti cha Rais

38.-(1) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja

halali wa kiti cha Rais aliyeteuliwa, Tume itamtangaza
mgombea huyo kuwa mgombea pekee wa kiti cha

Rais.
(2) Mgombea wa kiti cha Rais aliyetangazwa
chini ya kifungu kidogo cha (1) atapigiwa kura ya ndio
au hapana na atakuwa amechaguliwa kihalali kuwa
Rais endapo atapata kura nyingi zaidi ya kura zote
halali zilizopigwa.
(3) Endapo mgombea pekee wa kiti cha Rais
atashindwa kupata kura nyingi zaidi kwa mujibu wa
kifungu kidogo cha (2), Tume itatangaza siku nyingine
ya uteuzi kwa ajili ya uchaguzi wa Rais kwa notisi
itakayochapishwa katika Gazeti la Serikali.
Kujitoa ugombea 39.-(1) Mgombea wa kiti cha Rais anaweza
kujitoa ugombea kwa kutoa taarifa ya maandishi
aliyoisaini na kuiwasilisha yeye mwenyewe Tume na
nakala kwa Katibu Mkuu wa chama kilichomdhamini
kabla ya saa kumi kamili alasiri siku ya uteuzi.
(2) Kila taarifa ya kujitoa chini ya kifungu
kidogo cha (1) itaambatishwa na tamko katika fomu
itakayoainishwa, ambalo litajazwa na kusainiwa na
mgombea mbele ya Jaji.
(3) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1),
endapo mgombea atajitoa kugombea baada ya saa
kumi kamili alasiri ya siku ya uteuzi, chama chake
hakitaruhusiwa kuweka mgombea mwingine mbadala
na dhamana iliyotolewa na mgombea itataifishwa.
Kifo au
kukosekana kwa
wagombea
40.-(1) Endapo-
(a) baada ya saa kumi kamili alasiri ya siku ya
uteuzi hakuna mgombea halali aliyeteuliwa,
Tume, mapema iwezekanavyo kupitia notisi
katika Gazeti la Serikali, it
 
1711529040446.png

1711530013770.png

1711530092049.png

Kinamama viongozi ambao baadhi yao ni wakuu wa mikoa, Tabora mheshimiwa Dkt Batilda Buriani (kushoto) akifuatiwa na mkuu wa mkoa wa Kagera mheshimiwa Hajati Fatma Abubakari Mwasa na mama kigogo mwingine wachangia fedha kwa ajili ya fomu moja ya mgombea wa CCM kuelekea uchaguzi wa 2024 / 2025, harambee iliyoshuhudiwa na mheshimiwa waziri mkuu.
 
Sheria hii imetungwa kuweka Mazingira wezeshi kwa chama tawala kwa sasa yaani muda huu tulionao 2024 /2025 , haikuangalia maslahi mapana bila kujali vyama vya siasa wala miaka 200 mbele ya Tanzania wanayoitaka wananchi .
 
Ili kupunguza gharama za Uchaguzi ingefaa kama Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ungefanyika Kila baada ya miaka 7.

Iwapo Rais/Mbunge/Diwani aliyechaguliwa ikitokea amefariki Dunia ama amejiuzuru nafasi yake, basi aliyemfatia Kwa Wingi wa Kura atangazwe kuchukua nafasi yake.

Mfano ilipotokea Kifo cha JPM, basi mrithi wake angefaa awe Edward Lowassa badala ya ilivyo sasa.
 
TOKA MAKTABA :

Demokrasia ndani ya CCM Zanzibar walochukua fomu kutia nia wachaguliwe na chama chao CCM nafasi ya urais .

30 Juni 2020
Afisi ya Kisiwandui Unguja
Makao Makuu ya CCM
Zanzibar

UCHAGUZI WA URAIS 2020, WALIOCHUKUA FOMU CCM ZANZIBAR

1711531141801.png
 
27 ,MARCH 2024

🅻🅸🆅🅴 :WACHAMBUZI WA SIASA WANYUKANA VIKALI TATHIMINI YA MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA​


DKT. DENNIS A. MUCHUNGUZI : WATU HAWANA HAMU NA SIASA, WAMEKATA TAMAA...


View: https://m.youtube.com/watch?v=JCXc76BeMdA

Dr. Dennis A. Muchunguzi aongeza Siasa ni Maisha hivyo hali ya sasa watu kuwa wamepoteza hamu kufuatilia masuala ya kisiasa inahitaji kurekebishwa haraka.

Mchambuzi huyo anasema serikali ijenge mazingira ya vyama vya siasa viwe na vuguvugu la kuamsha siasa badala ya sasa kuna utitiri wa vyama legelege ktk kufanya siasa hadi vimebaki vyama viwili vya ..... huku vingine havishiriki moja kwa moja ktk shughuli za kisiasa .....

Dkt. Dennis A. Muchunguzi ameigeukia suala la Tume Huru ya Uchaguzi ..... msukumo wa katiba mpya iliyoasisiwa na kusimamiwa na Jakaya Kikwete ufufuliwe ...

Dorothy Semu kiongozi wa ACT Wazalendo amesema chaguzi 18 dogo za marudio za madiwani ambapo ACT Wazalendo wameshiriki, wameona bayana kabisa zile 4R anazochagiza Rais Samia Hassan kitaifa, lakini ngazi za chini hizo 4R zimepuuzwa ktk chaguzi dogo za juzi hivyo kutia shaka kama 2024 / 2025 kutakuwa na mabadiliko tofauti na yale ya 2020

Mwandishi wa habari nguli Jesse Kwayu naye auliza kwanini hizi 4R za Rais kitaifa, viongozi wenye dhamana huko mikoani, wilayani, majimboni na kata hawazitekelezi kama ambavyo mheshimiwa rais anavyosisitiza 4R

Prof. Samwel Wangwe naye ... uchumi urudi katika mikono ya sekta binafsi / private sector.... ni sehemu ya 4R Reconciliation kuhusisha serikali na sekta binafsi katika miradi ya ubia....
 
WALIOANDAMANA MIAKA YA 1990 WASIMULIA:

MARCH 2024

KWA MARA YA KWANZA NILIANDAMANA MWAKA 1990,UELEKEA WIKI YA MAANDAMANO NJOMBE ASEMA ONDOENI UOGA


View: https://m.youtube.com/watch?v=7KZa3sfpDUQ

Mzee wa CHADEMA asimulia namna ya juu ya ujasiri wao miaka ya 1990 na kutoa ushuhuda jinsi walivyotumia haki yao ya kuandamana miaka 1990 na kushangaa sasa maandamano ya hayana vikwazo vyovyote lakini waTanzania wanajifungia ndani wanashindwa kudai haki zao ...
 
Back
Top Bottom