YouTube haiwezi kuwa zaidi ya shule hata siku moja ndugu yangu. Hizo contents unazo ziona ndio zimekusaidia kuliko mkufunzi wako chuo kuuu, zimewekwa na mtu aliye kwenda shule na kufahamu kama mwanafunzi anatakiwa afanye nini.
Hivyo mnavyovisifia havijajiweka YouTube, vimewekwa na binadamu mwenye maumbile na ubongo kama wako tofauti ni kwamba yeye alijua anapaswa kufanya nini zaidi ya pale anapoishia mwalimu wakati wewe ulipokuwa chuo alipokuwa anaishia mwalimu wewe uliishia nyuma yake kidogo.
Hivi unadhani Mmilikiwa Facebook alifundishwa chuoni namna ya kutengeneza facebook? ama muanzilishi wa YouTube alifundishwa darasani namna ya kutengeneza hicho unachokiona ni bora!