Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Ni kweli kwamba post yako imeibua funzo kupitia pande mbili, husema kuupata mwisho rudi kwenye chanzo, historia ya Dr. mi huifananisha na mfugaji anaetafuta marisho kwa ajili ya mifugo yake, kwamba akiona malisho hapa yameisha anahama toka mahali fulani na kwenda sehemu nyingine. Kwa hivyo kuishi mahali fulani kwa kung'ang'ania ili tu ulinde muonekano wako kutaua mifugo yako.

Hivyo sina tatizo na kuondoka kwake toka sehemu fulani ili mradi tu anazo sababu za msingi kufanya hivyo. Rejelea Kuanzia upadri wake na aliyoyafanya huko...ukatibu, CCBRT, CCM, CDM, BUNGENI nk. kwa kufuata tu haki bila ushabiki niambie unaona tatizo wapi? Personal attack ni vitu vya kawaida kwenye siasa kama ulivyosema kwamba Siasa sio dini.

Turudi kwenye hoja ebu bomoa hoja alizozitoa Dr, kwenye PC yake bila ushabiki. tunahaja ya kukubali ukweli kwamba maamuzi bila tathimini hutugharimu sana. Mi pia nimechoshwa na mfumo mbaya wa iliyokuwa CCM ya kina EL na wenzake. Nilichoshwa kiasi cha kufikia maamuzi ya kuondoa watu wote wenye mfumo huo walio uishi. Lakini pahali sahihi kwangu kuidhibu CCM ilikuwa CDM niliwapa imani kwamba wangetusaidia kumfumua CCM.

Ghafla wakashindwa kusimamia imani niliyo wapa, nikaona sawa pamoja na dhamira yangu ya mageuzi kuna mambo ambayo ninaamini hayataweza kwenda sawa baada ya wale walezi wa mfumo kandamizi wengi wamekuja upande huu na wananguvu kuliko sisi.

Siwaamin CCM lakini walau naona ni nafuu kwa upande wa Rais abaki wa CCM kuliko huyu wetu. Sina chuki nae lakini sina imani nae. Mi ninautashi na naweza kupima maswala bila kufuata mob psychology.

Ni sahihi kabisa lakini ningependa tujikite kwenye hoja za kiroho zaidi kuliko kisiasa
 
Sio Mbowe kwa wenye kufikiri kwa makini. Slaa ni mkiristo mzuri kuliko wengi wakristo maana alifikia ngazi ya Upadri. Hivyo anaijua vizuri Biblia. Kutokana na Biblia kuna yafuatayo:
1. Upatapo hasira jua linachomoza usikae na hasira hiyo hadi jua likazama.
2. Dhambi hata iwe nyekundu kama damu ukitubu inakuwa nyeupe kama karatasi.
3. Sauli alikuwa mwiba mkali kwa wafuasi wa Yesu, aliua kupindukia baadae akageuka na kuwa mtume.
4. Mussa alikaa kwa faraho akiwatesa Waisrael lakini ndiye aliongoza msafara wao kuwapeleka kuelekea nchi ya ahadi japo hakuwafikisha.
5. Yapo mengi.

Umesema musa aliwatesa wa Israel?
 
Nisaidieni waungwana anapodai damu ya mkewe imemwagika kuokoa taifa

ukristo unaelekeza mke mmoja mume mmoja, kama ni mke alipaswa kuwa rose kamili.
Na mtu yeyote asemaye Dr. Slaa alistaafu upadre atakuwa hajatambua kuwa Slaa alichukua hatua mapema za kuudanganya umma dhidi ya dhambi yake ya UZINZI, ndio maana hata kwa Rose hakukaa, analitumikia Pepo la ngono.

Unasaafuje kumtumikia Mungu? unastafu kuhubiri kwani huwezi kuongea. Slaa ni mgoni na wale wote waliopiga kelele kabla yetu sasa ni wakati wa kuongeza sauti za wimbo huu.

"MPUUZENI SLAAA KWA MAANA NI MGONI"
chorus:-
amemdanganya Mungu itakuwa sisi wanadam x2
 
tunachotakiwa kujadili je ni alichosema ni kweli au uongo?? na km ni uongo jitokeze hadharani na ushahidi .... maandalizi ya mkutano ,ukumbi, na mazingira hayana tija..... je alichosema ni kweli au si kweli??
 
Sio Mbowe kwa wenye kufikiri kwa makini. Slaa ni mkiristo mzuri kuliko wengi wakristo maana alifikia ngazi ya Upadri. Hivyo anaijua vizuri Biblia. Kutokana na Biblia kuna yafuatayo:
1. Upatapo hasira jua linachomoza usikae na hasira hiyo hadi jua likazama.
2. Dhambi hata iwe nyekundu kama damu ukitubu inakuwa nyeupe kama karatasi.
3. Sauli alikuwa mwiba mkali kwa wafuasi wa Yesu, aliua kupindukia baadae akageuka na kuwa mtume.
4. Mussa alikaa kwa faraho akiwatesa Waisrael lakini ndiye aliongoza msafara wao kuwapeleka kuelekea nchi ya ahadi japo hakuwafikisha.
5. Yapo mengi.

Mmhh ni mambo ya kuyajua katika maisha ya mwanadamu.
 
Kama yeye anajua ni ukweli na anaanda press conference ya mamilioni kuusema ukweli, si angeenda tu mahakamani akafungue kesi?
Yakusemwa mdomoni tumeshayasikia mengi hatutaki porojo tena ,mwenye ushahidi akafungue kesi mahakamani FULLSTOP
 
Hakuna kitu kibaya kama kukariri usichoweza kukisimamia wala kukielezea

Mshana, tatizo watu hawajui...
>maagano ni nini na aina zake
~na kila agano lina mashart nyuma yake, whether it's written or not.
~madhara yake unapoamua kuvunja tena negative effects ni kubwa kuliko positive kwa agano lolote lile! Haijalishi ni aina gani ya agano

Pia agano lolote huwa lina wasimamizi either Mungu,au miungu(lucifer) ambao hawapo kimwili.

>Ulimwengu wa Roho ni nn~hii ni shida kubwa sn ht kwa wanaojiita wakristo na wanalijua neno, hawajui kuwa neno hatendi kazi bila roho.
 
Kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.

Pili yote anayoyafanya Kwasasa Slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .

Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo Nimeishi maisha ya viapo lakini SIKUAPA. viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.

Slaa Aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na Mungu na kukamilisha wito.

Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.

Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na Siasa haiongozwi na roho mtakatifu.

Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye Ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.

Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu Kwenye siasa amekosa Kuacha Heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.

Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .

Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea Dr na hii ni kanuni ya kidunia katika Ulimwengu wa roho.
mtu akifikiri kijuu juu hawezi kukuelewa
 
Umesema musa aliwatesa wa Israel?
kwa maana alipewa cheo kwenye utawala wa farao, alimuua mmisri pale alipowakuta wakipigana na myahudi, wakamfukia mchangani. siku nyingine yule myahudi akawa anagimbana na myahudi mwenzie, Musa alipotaka kuwaamua yule myahudi akamuuliza Musa ni nani amekuchagua uwe mwamuzi kati yetu? au unataka kuniua kama ulivyomuua mmisri?
Musa akaona ile siri sasa imejulikana na watu waliosikia pale.
akaamua kuikimbia misri akihofia farao akijua kuwa alimuua mmisri angeuliwa.
 
Ndugu Aangu Mshana Jr nakukubali hoja zako karibu ya zote, na hapo ulipoweka hii hoja haina uhusiano wa siasa kwa wale ambao wamebase kwenye siasa hii inamzungumzia maisha yake yote kwa ujumla Dr. Slaa.

Sasa napenda kukuuliza je mtu anawezaje kuviondosha viapo hivi ili visimsumbue? nimewahi kukutana na watu kama hivi ambao walitoa viapo na wengine unaweza kuwakuta wanakufa kiungo kimoja baada ya kimoja.
 
kwa maana alipewa cheo kwenye utawala wa farao, alimuua mmisri pale alipowakuta wakipigana na myahudi, wakamfukia mchangani. siku nyingine yule myahudi akawa anagimbana na myahudi mwenzie, Musa alipotaka kuwaamua yule myahudi akamuuliza Musa ni nani amekuchagua uwe mwamuzi kati yetu? au unataka kuniua kama ulivyomuua mmisri?
Musa akaona ile siri sasa imejulikana na watu waliosikia pale.
akaamua kuikimbia misri akihofia farao akijua kuwa alimuua mmisri angeuliwa.

Sasa kwa maelezo yako hapo musa amewatesaje
 
Duh...hivi na vile viapo wanavyoapaga viongozi wakiwa wanaanza kazi eg:Rais,wabunge, etc huku wameshikilia Biblia/Msahafu na kuinua mikono juu huwa vina nguvu ?

Tena vina nguvu sana, anaeapa inategemea na uzito wa suala analoliapia, kiapo kikiwa ni kikubwa kinaweza kukutesa wewe na familia yako yote, Mungu huwa hana haraka ya kujibu viapo tuwe makini sana.
 
Ndugu Aangu Mshana Jr nakukubali hoja zako karibu ya zote, na hapo ulipoweka hii hoja haina uhusiano wa siasa kwa wale ambao wamebase kwenye siasa hii inamzungumzia maisha yake yote kwa ujumla Dr. Slaa.

Sasa napenda kukuuliza je mtu anawezaje kuviondosha viapo hivi ili visimsumbue? nimewahi kukutana na watu kama hivi ambao walitoa viapo na wengine unaweza kuwakuta wanakufa kiungo kimoja baada ya kimoja.

Kwa uelewa wangu

Kwanza kabla ya kuvunja agano lolote lazima uingie kwenye TOBA! Toba hii si ya siku moja inachikua Muda mpka utakapojiridhisha moyoni mwako, hapa roho atakuongoza.

Then, unavunja sasa agano, hapa kwa siye wakristo tunatumia Damu ya Yesu tu, coz ndo yenye mamlaka ya kulipa fidia ya kilichofanyika kubatilisha, na kuondoa na kuvunja chochote kwa jina la Yesu!
 
ukristo unaelekeza mke mmoja mume mmoja, kama ni mke alipaswa kuwa rose kamili.
Na mtu yeyote asemaye Dr. Slaa alistaafu upadre atakuwa hajatambua kuwa Slaa alichukua hatua mapema za kuudanganya umma dhidi ya dhambi yake ya UZINZI, ndio maana hata kwa Rose hakukaa, analitumikia Pepo la ngono.

Unasaafuje kumtumikia Mungu? unastafu kuhubiri kwani huwezi kuongea. Slaa ni mgoni na wale wote waliopiga kelele kabla yetu sasa ni wakati wa kuongeza sauti za wimbo huu.

"MPUUZENI SLAAA KWA MAANA NI MGONI"
chorus:-
amemdanganya Mungu itakuwa sisi wanadam x2

Akili za kuazima zinajadili mtu badala ya contents. Aibu yenu kujaribu kuleta spinning kwenye hoja nzito na muhimu. Gwajima political kingmaker, kisa cha maaskofu 30, kufinyangwa demokrasia ndani ya CHADEMA, nk. Mambo ya uhusiano wake na Mungu hautuhusu, ufahamu wa Mungu na ufahamu wa wanadamu ni mbingu na nchi tofauti yake. Kina mshana jr na christine ibrahim mmejipa nafasi ya Mungu kuhukumu mambo ya rohoni.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom