Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Ndugu Aangu Mshana Jr nakukubali hoja zako karibu ya zote, na hapo ulipoweka hii hoja haina uhusiano wa siasa kwa wale ambao wamebase kwenye siasa hii inamzungumzia maisha yake yote kwa ujumla Dr. Slaa.

Sasa napenda kukuuliza je mtu anawezaje kuviondosha viapo hivi ili visimsumbue? nimewahi kukutana na watu kama hivi ambao walitoa viapo na wengine unaweza kuwakuta wanakufa kiungo kimoja baada ya kimoja.

Kiapo cha kumtumikia Mungu hakitenguliwi hakitenguki alichofanya yeye ni kutengua kwa njia zake mwenyewe kiapo cha upadirisho
 
Ni kitu cha ajabu sana binadamu tena Mkristo kutamka hadharani kwamba yeye ni kipimo cha uadilifu katika jamii yake. Ndio maana hata Sumaye alimshangaa Kinana kuwa kama kweli anaweza kuongelea uadilifu basi yeye (Fredrick) ni Malaika!
Hebu jiulize hata Yesu mwenyewe aliyekuwa na kiwango cha juu kabisa alivyoongelea uadilifu aliikana hiyo stage na kusema aliye mkamilifu ni Mungu pekee aliye juu!!
Na kwa kukumbushana tu jamani kuna baadhi ya Maandiko Matakatifu yanayotukumbusha kuwa tusihukumu kabla ya kuhukumiwa na tuishi katika sala kwa kigezo kwamba kuna watu wameishi katika maisha ya kitakatifu lakini muda kidogo kabla ya kumalizia maisha yao wakamkana Mungu na hivyo kulaaniwa. Hivyo hivyo kuna watu wameishi katika dhambi maisha yao yote na karibia na mwisho wakatubu na kumrudia Muumba wao na wakasemehewa!

Maelezo marefu lakini yanaipanua hii picha ya Dr. Slaa kukutana na Dr. Mwakyembe na kisha kumuomba asaidie kuueleza ubaya wa Lowassa kana kwamba EL ni mtu asiyestahili kusamehewa hata pale atakapotubu dhambi zake! EL keshasema kuwa RICHMOND alielekezwa na wakubwa wake basi naye Dr. Slaa atueleze ni kwa nini anaitesa familia yake kwa mihogo na maharage huku akikodisha ukumbi kwa 80m kutushawishi tuichague ccm!
Uadilifu na utakatifu ni vitu viwili tofauti labda terminology hizi tuziweke kwenye kiingeleza, Integrity - Uadilifu na Holiness - Utakatifu kisha tafuta tafsiri zake. Baada ya kuzipata njoo tuangalie kwa pamoja kwa nini Dr. alimshambulia EL. mimi sihukumu kwa sheria za kidini uwenda sizifahamu sana. Lakini turudi kwa Dr. kwa maneno yake alimtaka EL auelezee umma kwamba yeye hausiki ni Richmond na muusika ni fulani....lakini EL hakufanya hivyo zaidi ya kusema hausiki, alijiuzuru, na kuna maagizo ya wakubwa. Kisha uangalie Dr. alimbana EL kwa Uadilifu au Utakatifu?

Mengine ni porojo tu siwezi kuyaongelea sana ili tubaki kwenye hoja ya msingi.
 
Hilo jicho lako la rohoni ni ukengeufu unaotokana na kutaka kutumia Neno la Mungu kuhalalisha matamanio yako. Kumtangazia laana Dr Slaa nikujitakia laana wewe mwenyewe. Sisi tunaoona kwa macho ya nyama hatuwezi kamwe kujikweza mpaka kiti cha hukumu cha Mungu.

Hebu chambua contents zake ukioanisha na hiyo laana inayomsumbua. Anzia pale alipojiunga na siasa mpaka kuijenga CHADEMA, mpaka hotuba yake ya kujitoa CHADEMA. Yapi katika aliyoyaamini yanaashiria amelaaniwa? Naomba ufanye hivyo ili tuone hujakariri. Oanisha contents na biblical curse

Kwani hii laana ya kiroho imekuwa triggered na nini? Tofauti yake na CHADEMA au nini? Alipokuwa nasi alikuwa mbarikiwa, alipoturudi alikuwa mlaaniwa! Mwacheni Mungu awe mkweli na wanadamu wote waongo.

Mshana Jr

Hongera, ulichosema ni kwa sababu uko upande Fulani kwa hiyo kila utachosema kitaelemea huko. Bahati mbaya nchi yetu haina Wachambuzi Huru wote wameelemea upande fulani.

Dr Slaa analaumiwa kwa kinachotokea Sasa ktk Siasa za Tz, kwa nini kwa sababu kaamua kusema ukweli ambao Mh Mbowe hakuusema, alitudanganya kwamba wamekubaliana na Dr Slaa apumzike atajiunga nao mbele ya safari!

Kwako MshanaJr, wewe ulikua wapi kusema haya uliyoyasema sasa mpaka baada ya Dr Slaa kuamua kufunguka.

Hoja ya CDM ilikua UFISADI ndicho Dr alichosema Je? ktk Kampeni zenu hilo lipo kama halipo kwa nini?

Ilikua bora kumpotezea Dr, kwa jinsi alivyofunguka kuliko kupambana naye tena kwa kumtusi elewa kwamba unatoa nafasi nyingine ya Dr kurudi Hewani jambo ambalo litakua Bomu la kuimaliza CDM

Lowasa ni Mgombea dhaifu kuwahi kutokea ktk CDM hawezi kujitetea kwa kombora lolote litakalo rushwa kwake ana sifa ya kupata Pesa toka kwa marafiki zake kama alivyosema mwenyewe, hawezi na hana maneno ya kuzidi dk 10. Jana Sumbawanga kaongea dk 5 leo Namanyere kaongea dk 5 hii inatosha kumfanya aende lkulu? Kumbuka watu wanakwenda ktk viwanja vya Kampeni kumsikiliza Mgombea, mpiga Kura amekaa uwanjani zaidi ya saa 3 Lowasa anaongea dk 5 hii ni sawa?

Usimtafute mchawi kosa ni lenu wenyewe mmewapa CCM ujasiri ambao hawakua nao kabla poleni kwa sababu kazi iliyokua ifanywe nao mnaifanya nyinyi kujibu Makombora.

Kama Uchaguzi Serikali za mitaa uliibeba CDM kwa Ajenda ya Escrow account basi Uchaguzi huu CCM itabebwa na Ajenda ya Lowasa

Naomba mnielewe tena na tena alichoongea Dr na maudhui yote ya mkutano ule ndio kilichonisukuma kuandika post hii... Hebu rudieni kusoma tena heading
Pale aliyeongea sio Slaa Yule mtheologia mwenye cheo cha daraja la upadri, sio yule Slaa wa TEC, sio Slaa wa CCBRT, sio Slaa mwenye mlolongo wa mambo mema na mazuri sio Slaa Yule lulu ya upinzani... Aliyeongea pale ni slaa ambaye ndio kwanza anafahamika kwa hasira uongo visasi vinyongo husuda nk
Aliyeongea pale ni slaa wa siasa za majitaka na kujikweza Sana.. Nilipatwa na mshtuko mkubwa... Sikutegemea na mamilioni hawakutegemea alichoongea pale HAVIFANANI NA SLAA TUNAYEMFAHAMU na kumheshimu na kumpenda sana
Nikatafakari kivyangu.. Post zilikuwa nyingi sana lakini mwishowe nikaamua nami nitie neno sikukurupuka
 
Kiapo cha kumtumikia Mungu hakitenguliwi hakitenguki alichofanya yeye ni kutengua kwa njia zake mwenyewe kiapo cha upadirisho
Kaka naona umeamua kubaki kwenye mahaba nipofushe... nilipokuwa mdogo kunawakati nilitamani watu wote wawe na fikra na mawazo kama yangu kwa hivyo nilitumia muda mwingi kuwashangaa walioshindwa kukubaliana nami. Baadae nikajifunza kwamba mitazamo maoni na maamuzi yetu ni tofauti ila sote niwabinafsi. Sifa tuliyo rithishwa toka uumbaji.

kwa hivyo tunatumia nguvu kubwa kuridhisha mioyo yetu hata yale ambayo sio sitahili yetu ilimradi tu yashibishe matarajio bila kujali ni sahihi au sio sahihi. Ndio maana nikauliza kumtumikia Mungu ni mpaka uwe padri?
 
Kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.

Pili yote anayoyafanya Kwasasa Slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .

Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo Nimeishi maisha ya viapo lakini SIKUAPA. viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.

Slaa Aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na Mungu na kukamilisha wito.

Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.

Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na Siasa haiongozwi na roho mtakatifu.

Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye Ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.

Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu Kwenye siasa amekosa Kuacha Heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.

Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .

Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea Dr na hii ni kanuni ya kidunia katika Ulimwengu wa roho.

Umeongea kitu kimenigusa sana.mimi babaangu nae kapita huko huu ninaoutoa ni ushuhuda wa kweli baba alipata upadre seminari kuu peramiho baati mbaya akaanguka na kukacha upadre hadi leo mungu tu ndo anajua kinacho endelea.
 
Aliyeongea pale ni slaa wa siasa za majitaka na kujikweza Sana.. Nilipatwa na mshtuko mkubwa... Sikutegemea na mamilioni hawakutegemea alichoongea pale HAVIFANANI NA SLAA TUNAYEMFAHAMU na kumheshimu na kumpenda sana
Nikatafakari kivyangu.. Post zilikuwa nyingi sana lakini mwishowe nikaamua nami nitie neno sikukurupuka

Toa Boriti ktk Jicho lako kwanza......
 
Kaka naona umeamua kubaki kwenye mahaba nipofushe... nilipokuwa mdogo kunawakati nilitamani watu wote wawe na fikra na mawazo kama yangu kwa hivyo nilitumia muda mwingi kuwashangaa walioshindwa kukubaliana nami. Baadae nikajifunza kwamba mitazamo maoni na maamuzi yetu ni tofauti ila sote niwabinafsi. Sifa tuliyo rithishwa toka uumbaji.

kwa hivyo tunatumia nguvu kubwa kuridhisha mioyo yetu hata yale ambayo sio sitahili yetu ilimradi tu yashibishe matarajio bila kujali ni sahihi au sio sahihi. Ndio maana nikauliza kumtumikia Mungu ni mpaka uwe padri?

Usilitumie hili neno la NATUMIA NGUVU kubwa tafadhali hapa ni jukwaani kumtumikia Mungu kuna vipawa vingi na si Lazima uwe padre. Lakini unapoamua kwa dhati ya Moyo wako kusomea upadri hicho ndio kipawa chako ulichochagua
Na kuonyesha kuwa ni jambo kubwa ndio maana mapadri hupikwa kwa muda mrefu kabla ya kupata daraja la upadirisho....na hili daraja hulipati kama cheo au cheti cha shule bali kwa ibada maalum ambayo ni nadra na ni ya kipekee mno
Kuna post niljkupa link kadhaa ukazisome naona hujafanya hivyo
Kile padre anachotamka pale madhabahuni ndio mkataba ambao hatakiwi kuuvunja.. Kuna kupotoka na kuanguka kwa hapa na pale lakini si mara zote na moja kwa moja.. Utafanya mengi mazuri na ya mafanikio tupu lakini mwishoni kila kitu hugeuka kuwa ubatili mtupu
 
Kiapo cha kumtumikia Mungu hakitenguliwi hakitenguki alichofanya yeye ni kutengua kwa njia zake mwenyewe kiapo cha upadirisho
Kuna vitu vingi nakupinga lakini hili la leo lina ukweli wake. Siajwahi kumwona mtu aliyeacha upadri akaishi maisha yasiyo ya kutangatanga. Nina mifano kama mitano ya watu ninaowafahamu. Waliacha upadri lakini mmoja alifariki kwa ajali, kuna aliyepata kichaa baada ya mke wake kumkomba kila kitu na kutokomea na bwana mwingine...
 
This is a very important thread, Slaa anaitafsiri siasa tofauti na siasa yenyewe
 
Mleta hoja hajadili ya jana mrudie tena umsome

Anajadili ya jana kwa kile anachokiita jicho la rohoni. Isingelikuwa kwa Dr Slaa kuisasambua CHADEMA, hoja kama hizi zisingalizaliwa. Yote haya ni matokeo ya Slaa kuwashambulia "taifa teule" CHADEMA. Hamuwezi kukwepa ukweli huu. Siku zote Dr Slaa amekuwa shujaa, leo kwa nini tumuone kalaaniwa? Wacheni habari zenu hizo.
 
Naomba mnielewe tena na tena alichoongea Dr na maudhui yote ya mkutano ule ndio kilichonisukuma kuandika post hii... Hebu rudieni kusoma tena heading
Pale aliyeongea sio Slaa Yule mtheologia mwenye cheo cha daraja la upadri, sio yule Slaa wa TEC, sio Slaa wa CCBRT, sio Slaa mwenye mlolongo wa mambo mema na mazuri sio Slaa Yule lulu ya upinzani... Aliyeongea pale ni slaa ambaye ndio kwanza anafahamika kwa hasira uongo visasi vinyongo husuda nk
Aliyeongea pale ni slaa wa siasa za majitaka na kujikweza Sana.. Nilipatwa na mshtuko mkubwa... Sikutegemea na mamilioni hawakutegemea alichoongea pale HAVIFANANI NA SLAA TUNAYEMFAHAMU na kumheshimu na kumpenda sana
Nikatafakari kivyangu.. Post zilikuwa nyingi sana lakini mwishowe nikaamua nami nitie neno sikukurupuka

Kwa maana hiyo angeongea kusapoti CHADEMA na UKAWA angekuwa "yule tunayemjua!?" Badala ya kujadili ni nini kilichopelekea hii u turn, tunakimbilia laana, a typical African way of reasoning. Nakushauri ujaribu kutazama matukio yaliyopelekea Dr Slaa kureact namna ile
 
Kwa maana hiyo angeongea kusapoti CHADEMA na UKAWA angekuwa "yule tunayemjua!?" Badala ya kujadili ni nini kilichopelekea hii u turn, tunakimbilia laana, a typical African way of reasoning. Nakushauri ujaribu kutazama matukio yaliyopelekea Dr Slaa kureact namna ile

Nafikiri Nyenyere una shida ya kuchambua mambo hebu tulia usome tena kwa hatua nilichokujibu tusichoshane kwa malumbano yasiyo na tija
 
Last edited by a moderator:
Usilitumie hili neno la NATUMIA NGUVU kubwa tafadhali hapa ni jukwaani kumtumikia Mungu kuna vipawa vingi na si Lazima uwe padre. Lakini unapoamua kwa dhati ya Moyo wako kusomea upadri hicho ndio kipawa chako ulichochagua
Na kuonyesha kuwa ni jambo kubwa ndio maana mapadri hupikwa kwa muda mrefu kabla ya kupata daraja la upadirisho....na hili daraja hulipati kama cheo au cheti cha shule bali kwa ibada maalum ambayo ni nadra na ni ya kipekee mno
Kuna post niljkupa link kadhaa ukazisome naona hujafanya hivyo
Kile padre anachotamka pale madhabahuni ndio mkataba ambao hatakiwi kuuvunja.. Kuna kupotoka na kuanguka kwa hapa na pale lakini si mara zote na moja kwa moja.. Utafanya mengi mazuri na ya mafanikio tupu lakini mwishoni kila kitu hugeuka kuwa ubatili mtupu
mshana jr Ooh hivi kumbe kwenye jukwaa tunazuiwa matumizi ya neno "NATUMIA NGUVU kubwa" samahani mkuu ikiwa limekukela ingawa nasikitika kwamba uzuiaji huu unanirudisha kwenye kuamini unalazimisha hoja ya laana kwa Dr.

Upotoshaji hautaisha na waliopotoshwa wakashindwa kujikwamua watabaki kuwa waliopotoka. Tatizo unacheza na akili yako mwenyewe unaamini padri hawezi kutoka katika upadri na akawa salama, wakati unashindwa kuelewa hata Pope alijiuzuru. Sijui yeye atakuwaje maana daraja lake huwa ni mpaka moshi mweupe toka kwa Mungu utoke ndio anasimikwa. Ukiwa mweusi maana yake Mungu hakupenda matokeo ya cardinals.

hoja yangu toka awali nilitamani sana uje na fact za laana ya Dr. lakini unarukaruka tu. CDM plus EL hakuna yeyote aliye jibu tuhuma za Dr. Maana tuhuma lazima zijibiwe ili kuupata ukweli. Iwe Dr aliongea na kada yeyote wa CCM bado haitoshi kwamba alichokisema ni tofauti alichohubiri sikuzote kabla ya kujitoa CDM.

Zaidi aliongeza mshangao wake kwa alie muita mshenga jinsi alivyo kuwa akijisifu kwa rushwa aliyotapanya....nimesikiliza majibu yao bado sijashawishika kuwa wamekuwa wakweli.

Kutumia dini kumshambulia Dr kisiasa kwenye jukwaa la siasa ni kosa. Angalia imani yako, na uombe modes wauhamishe uzi huu, uende kule kwenye dini.
 
Last edited by a moderator:
mshana jr Ooh hivi kumbe kwenye jukwaa tunazuiwa matumizi ya neno "NATUMIA NGUVU kubwa" samahani mkuu ikiwa limekukela ingawa nasikitika kwamba uzuiaji huu unanirudisha kwenye kuamini unalazimisha hoja ya laana kwa Dr.

Upotoshaji hautaisha na waliopotoshwa wakashindwa kujikwamua watabaki kuwa waliopotoka. Tatizo unacheza na akili yako mwenyewe unaamini padri hawezi kutoka katika upadri na akawa salama, wakati unashindwa kuelewa hata Pope alijiuzuru. Sijui yeye atakuwaje maana daraja lake huwa ni mpaka moshi mweupe toka kwa Mungu utoke ndio anasimikwa. Ukiwa mweusi maana yake Mungu hakupenda matokeo ya cardinals.

hoja yangu toka awali nilitamani sana uje na fact za laana ya Dr. lakini unarukaruka tu. CDM plus EL hakuna yeyote aliye jibu tuhuma za Dr. Maana tuhuma lazima zijibiwe ili kuupata ukweli. Iwe Dr aliongea na kada yeyote wa CCM bado haitoshi kwamba alichokisema ni tofauti alichohubiri sikuzote kabla ya kujitoa CDM.

Zaidi aliongeza mshangao wake kwa alie muita mshenga jinsi alivyo kuwa akijisifu kwa rushwa aliyotapanya....nimesikiliza majibu yao bado sijashawishika kuwa wamekuwa wakweli.

Kutumia dini kumshambulia Dr kisiasa kwenye jukwaa la siasa ni kosa. Angalia imani yako, na uombe modes wauhamishe uzi huu, uende kule kwenye dini.

Naona uko kimipasho zaidi fanya hivi tukubaliane kutokubaliana ili tuweze kufanya mengine
 
Last edited by a moderator:
Mimi nilikuwa mshabiki wa Dr Slaa lakini safari hii amecheza kete kilevi kabisa! Hakutazama mbele hata kidogo!
 
jamani mbavu zangu. nawaambieni hivi. hamna rangi atakayoacha kuiona slaa humu mitandaoni. kila aina ya jina baya atalipata. yalikuwa kwa zitto, kisha lipumba sasa ni zamu yake.


Kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.

Pili yote anayoyafanya Kwasasa Slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .

Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo Nimeishi maisha ya viapo lakini SIKUAPA. viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.

Slaa Aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na Mungu na kukamilisha wito.

Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.

Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na Siasa haiongozwi na roho mtakatifu.

Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye Ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.

Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu Kwenye siasa amekosa Kuacha Heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.

Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .

Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea Dr na hii ni kanuni ya kidunia katika Ulimwengu wa roho.
 
Katika hali inayoonyesha chama hiki hakina uongozi wenye busara na hekima viongozi wake na baraza lao la vijana wanamshambulia na kumtukana Dr Slaa bila breki. Bila shaka yoyote uongozi wa M,kiti wa chama hiki amekosa busara kwani kila linapotokea tatizo Mbowe hatumii busara kulitatua zaidi kutumia nguvu kubwa kwa kutumia wapambe wake ama kumfukuza asiyeelewana naye ama ajiondoe mwenyewe. Uwezo wa huyu M,kiti kupambana na challenge ndani ya chama na kulimaliza bila kuwa na tafrani ndani yake hana,tupia macho Chacha Wenga,zitto na sasa Slaa. Nyie Makanjanja na nyumbu mfahamu kuwa kuendelea kumtukana na kumshambulia Dr Slaa kwa ajili ya huyo askari wa kukodi iko siku itawatokea puani. Ingetosha kutumia busara kuliko kuendelea kumtusi na kumshambulia Dr Slaa mngetoa statement moja iliyojaa busara na hekima ikawa baas na kuachana naye. Lakini hii kitu "Busara" imekosekana kwa M,kiti na wapambe wake jambo ambalo litawagharimu baadaye mje kujuta. Tutaonana hapahapa Jf majuto ni mjukuu
 
Back
Top Bottom