Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

mshana jr

mshana jr katika ubora wako...
mimi nataka nimuapishe mpenzi wangu.. ili asiniache na kunisaliti...nafanyaje!?

Ooops kumbe ni jukwaa la siasa
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,
Tunasikia viongozi na wanasiasa wetu wakituambia kila siku kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa taifa letu sasa inakuwaje hatufanyi jitihada kukifufua?.Katika kipindi cha awamu ya tatu tumeona msisitizo ulikuwa kwenye sekta ya madini na imesaidia kidogo angalau kuongeza kodi.Lakini swala kubwa hapa ni kwamba sekta ya madini haiajiri wananchi wengi kama sekta ya kilimo.Swala ni hivi kwanini hatuweki nguvu nyingi kwenye kilimo kama tulivyowekeza kwenye madini? kama tungefanya hivyo miaka 10 hii ya Mkapa hii aibu ya njaa mnadhani ingetukumba?

View attachment 283230
 
Dr. Slaa katika hotuba yake alisema yeye ni Padre.
Padre na siasa wapi na wapi eeh! au padre na wachumba wapi wapi mzee?


Kwani kiapo cha upadre huwa kinakuaje?

Huwa kinaandamana na maapizo kama mtu aapaye akikiuka?

Mtu aliyeacha upadre na hataki kuendelea nao hakuna namna ya mtu huyo kutubishwa?
 
mshana jr

mkuu kwa kuongezea hapo kwenye viapo, hakuna dhambi mbaya nyingine kama kumtenda vibaya mke wa ujana wako. Ameishi na mrembo wa mwanzo akamtelekeza wakati analijua neno linavyosema!! Duu kazi kweli kweli
 
Last edited by a moderator:
Dr. Slaa katika hotuba yake alisema yeye ni Padre.
Padre na siasa wapi na wapi eeh! au padre na wachumba wapi wapi mzee?

Ni kuchanganya dunia tatu kwa pamoja... Kwa wakati mmoja Utaweza kumudu na kuhimili changamoto zake lakini sio marazote
 
Kwanini alijiita ( alisema yeye ni ) Padre katika mkutano wake na wwandishi wa habari kwenye ukumbi wa serena? Alisema mimi ni Padre


Acha kupotosha watu, kanisa katoriki lina sheria zake, ukiwa mtawa/Padre unaruhusiwa kuendelea na huduma maisha yako yote au unaruhusiwa kuomba kumpumzika na kuendelea maisha ya kawaida kama muumini mwingine wa kawaida. Dr Slaa aliomba kustaafu upadre kabla ya ujio wa Papa John II kuja tanzania miaka ya 1999 wakati huo akiwa na katibu wa TEC lkn kanisa lilimwomba asipumzike mpaka ziara ya PAPA ikamilike, kama ingekuwa ni dhambi basi kanisa lisinge mwomba kuendelea. baada ya ziara ya PAPA nchini Dr Slaa alikubaliwa na makao makuu kustaafu na kuagwa na kanisa kwa sherehe kubwa. Baada ya kustaafu Dr. Slaa alirudi kwao Karatu na kuanzisha miradi ya jamii, aliweza kupata wafadhiri mbalimbali hivyo kufanikiwa kuleta maendeleao Karatu. Baada ya wananchi kuona mafanikio yake, walimwomba agombee ubunge, na kweli akagombea kupitia CCM, CCM waliona kama ni mgeni katika siasa wakakata jina lake na kumpa mshindi wa tatu aliyekuwa mbunge wakati huo. Hivyo basi wananchi wakamshawishi kuhamia chama cha upinzani na kuwa wangempa kura, Dr Slaa akahamia CHADEMA wakati huo CHADEMA hakina umaarufu kama sasa, chama kilichikuwa maarufu kilikuwa ni NCCR mageuzi. Dr Slaa akashinda kwa kishindo na kuwa mbunge wa kwanza kutoka CHADEMA na Dr Warid Kabour kutoka jimbo la Kigoma mjini.

Kwa wasio jua Dr Slaa ndiye aliyeanziasha taasisi ya tiba ya CCBRT na ni mkurugenzi wa board. Nafikiri ni taasisi peke hapa nchini inayotoa tiba ya ulemavu wa viungo na macho kwa gharama nafuu.


In 1994: With the support of CBM, Dr. Willbrod Slaa, (still on the CCBRT Board) and Geert Vanneste founded CCBRT. Their mission was to contribute towards poverty alleviation by making rehabilitative services accessible and affordable to people with disabilities. In 1994, CCBRT was registered as a private Non-Governmental Tanzanian Society (NGO), under the Tanzanian Societies Act, No SO8261.
 
Mwalimu wako alipata taabu sana!
Tunajadili usaliti wa kiapo cha upadri kinachopelekea dr. slaa kutangatanga asijue pa kushika,
anatumia nguvu nyingi kujaribu kutuaminisha kuwa yeye ni mkweli sana kumbe hola!! usaliti wa kiapo unamtesa

anatumia nguvu nyingi kujaribu kutuaminisha kuwa ana akili nyingi kutuzidi (yeye ni doctor wa falsafa) yote ni katika kutangatanga kunakosababishwa na usaliti wa kiapo cha upadri.
kwa kifupi nikwambie hivii dr. slaa anajiona ana akili kama mungu.

Kiapo alichokisaliti cha upadri kinamhenyesha na hakitamuacha ng'o!!

Acha kujitoa ufahamu basi

Suala la uasi tushaliongelea kitambo kipindi iko ninyi chadema mulikua munamtetea leo hii mbona au ulikua bado mtoto?

Mimi nachomaanisha hapa ni kwamba ninyi wenyewe ni wanafiq kwa nini msiliongelee hili kipindi yupo chadema? Au tulete nyuzi hapa ya kuonyesha wayu waliyasema haya na mkamtetea sasa kama hili lilionekana kwa nini msiliseme kipindi yupo chadema iweje leo?
 
Kibliblia wote walio sariti au kwenda kinyume na maagizo tuliziona impact zake... 1. Yuda Iskariote 2. Mfalme Sauli 3. Anania na mkewe Safila.

Ukijua ukweli ina kuweka huru, ila kama uki ijua ukweli then ukaipindua hiyo kweli hiyo kweli ni lazima ikuondoe kwa maumivu makali sana kuliko uchungu wa mama mjazito ajifunguapo


Ni kuchanganya dunia tatu kwa pamoja... Kwa wakati mmoja Utaweza kumudu na kuhimili changamoto zake lakini sio marazote
 
Acha kupotosha watu, kanisa katoriki lina sheria zake, ukiwa mtawa/Padre unaruhusiwa kuendelea na huduma maisha yako yote au unaruhusiwa kuomba kumpumzika na kuendelea maisha ya kawaida kama muumini mwingine wa kawaida. Dr Slaa aliomba kustaafu upadre kabla ya ujio wa Papa John II kuja tanzania miaka ya 1999 wakati huo akiwa na katibu wa TEC lkn kanisa lilimwomba asipumzike mpaka ziara ya PAPA ikamilike, kama ingekuwa ni dhambi basi kanisa lisinge mwomba kuendelea. baada ya ziara ya PAPA nchini Dr Slaa alikubaliwa na makao makuu kustaafu na kuagwa na kanisa kwa sherehe kubwa. Baada ya kustaafu Dr. Slaa alirudi kwao Karatu na kuanzisha miradi ya jamii, aliweza kupata wafadhiri mbalimbali hivyo kufanikiwa kuleta maendeleao Karatu. Baada ya wananchi kuona mafanikio yake, walimwomba agombee ubunge, na kweli akagombea kupitia CCM, CCM waliona kama ni mgeni katika siasa wakakata jina lake na kumpa mshindi wa tatu aliyekuwa mbunge wakati huo. Hivyo basi wananchi wakamshawishi kuhamia chama cha upinzani na kuwa wangempa kura, Dr Slaa akahamia CHADEMA wakati huo CHADEMA hakina umaarufu kama sasa, chama kilichikuwa maarufu kilikuwa ni NCCR mageuzi. Dr Slaa akashinda kwa kishindo na kuwa mbunge wa kwanza kutoka CHADEMA na Dr Warid Kabour kutoka jimbo la Kigoma mjini.

Kwa wasio jua Dr Slaa ndiye aliyeanziasha taasisi ya tiba ya CCBRT na ni mkurugenzi wa board. Nafikiri ni taasisi peke hapa nchini inayotoa tiba ya ulemavu wa viungo na macho kwa gharama nafuu.


In 1994: With the support of CBM, Dr. Willbrod Slaa, (still on the CCBRT Board) and Geert Vanneste founded CCBRT. Their mission was to contribute towards poverty alleviation by making rehabilitative services accessible and affordable to people with disabilities. In 1994, CCBRT was registered as a private Non-Governmental Tanzanian Society (NGO), under the Tanzanian Societies Act, No SO8261.

Hakuna shida ukiondoka ndani ya kanisa kwasababu hayo ni maamuzi yako binafsi.
Ila mleta mada amekuambia Dr. Slaa ameondoka na viapo ambavyo havijatenguliwa.
Pamoja na kuagwa na kanisa kwa sherehe lakini kile kiapo bado yupo nacho.
 
Kwanini alijiita ( alisema yeye ni ) Padre katika mkutano wake na wwandishi wa habari kwenye ukumbi wa serena? Alisema mimi ni Padre

Ni kwakuwa ile roho ya kiapo chake bado iko live kabisa na alitamka bila kutegemea...kwa nje kajichanganya na dunia nje ya kiapo chake lakini wito aliouwekea nadhiri bado uko moyoni na hili ndio tatizo
 
Acha kujitoa ufahamu basi

Suala la uasi tushaliongelea kitambo kipindi iko ninyi chadema mulikua munamtetea leo hii mbona au ulikua bado mtoto?

Mimi nachomaanisha hapa ni kwamba ninyi wenyewe ni wanafiq kwa nini msiliongelee hili kipindi yupo chadema? Au tulete nyuzi hapa ya kuonyesha wayu waliyasema haya na mkamtetea sasa kama hili lilionekana kwa nini msiliseme kipindi yupo chadema iweje leo?

Halikusemwa kabla kwakuwa naye hakuyasema kabla.. Lakini wakati ulipotimia amesema nasi tumesema si kwa kutukana si kwa kukejeli bali kuainisha kwanini amesema sasa na hasahasa maudhui ya kile alichokisema
 
Asante mkuu mshana jr na kwa kuwa mada ina elements za kiroho nami kwa kurejea Biblia takatifu ninatoa onyo kuhusu viapo!
Matthew 5:33-37
Oaths
“Again, you have heard that it was said to the
people long ago, ‘Do not break your oath, but fulfill
to the Lord the vows you have made.’ But I tell
you, do not swear an oath at all: either by heaven,
for it is God’s throne; or by the earth, for it is his
footstool; or by Jerusalem, for it is the city of the
Great King. And do not swear by your head, for
you cannot make even one hair white or black.
All you need to say is simply ‘Yes’ or ‘No’;
anything beyond this comes from the evil one."
 
Last edited by a moderator:
Aina za viapo.
  1. kiapo Cha umaskini ....poverty
  2. Kiapo cha usafi wa moyo ... Chasitity
  3. Kiapo cha useja ....Celibacy
  4. Kiapo cha vitu .... materiali
  5. Kiapo cha upweke ..... Isolation

Kuna vingine kama vya ndoa, urafiki, (watu wawili wanachanjiana damu) vya kikatiba (viongozi) vya kutunza siri n.k Vilivyotajwa hapo juu ni vile vya mtu na Mungu. Vinaitwa pia oaths au maagano.
kimsingi kama alivyosema Mshana Jr kiapo hukaa ndani ya mwili na nafsi hadi kwenye DNA ya mtu. Hakitoki hadi utimize. Usipotimiza kivunje. Tatizo kubwa ni kutojua madhara ya maagano au viapo, na jinsi ya kuyavunja.
Slaa alikuwa na kiapo cha useja. Celibacy. Akaamua kuoa na hakuvunja kiapo hich au agano hilo. Kama anavyosema mwenyewe upadri hauishi, hata maagano yake hayaishi.

"
Vows are solemn and sacred and involve powerful heavenly realities that we should not mess with."
 
mshana jr huna haja ya kuhangaika na Dr Slaa.
Washashughulikiwa hawa na wote wenye kupanga hila za kutaka kuliangamiza taifa hili. Watapotea kwenye uso wa dunia kwa haraka sana na wala mali zao walizojilimbikizia kwa njia zisizo halali hazitawasaidia kamwe.
Malizia na AMINA kwenye huu uzi ili sala ikamilike.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom