Mshana Jr
Hongera, ulichosema ni kwa sababu uko upande Fulani kwa hiyo kila utachosema kitaelemea huko. Bahati mbaya nchi yetu haina Wachambuzi Huru wote wameelemea upande fulani.
Dr Slaa analaumiwa kwa kinachotokea Sasa ktk Siasa za Tz, kwa nini kwa sababu kaamua kusema ukweli ambao Mh Mbowe hakuusema, alitudanganya kwamba wamekubaliana na Dr Slaa apumzike atajiunga nao mbele ya safari!
Kwako MshanaJr, wewe ulikua wapi kusema haya uliyoyasema sasa mpaka baada ya Dr Slaa kuamua kufunguka.
Hoja ya CDM ilikua UFISADI ndicho Dr alichosema Je? ktk Kampeni zenu hilo lipo kama halipo kwa nini?
Ilikua bora kumpotezea Dr, kwa jinsi alivyofunguka kuliko kupambana naye tena kwa kumtusi elewa kwamba unatoa nafasi nyingine ya Dr kurudi Hewani jambo ambalo litakua Bomu la kuimaliza CDM
Lowasa ni Mgombea dhaifu kuwahi kutokea ktk CDM hawezi kujitetea kwa kombora lolote litakalo rushwa kwake ana sifa ya kupata Pesa toka kwa marafiki zake kama alivyosema mwenyewe, hawezi na hana maneno ya kuzidi dk 10. Jana Sumbawanga kaongea dk 5 leo Namanyere kaongea dk 5 hii inatosha kumfanya aende lkulu? Kumbuka watu wanakwenda ktk viwanja vya Kampeni kumsikiliza Mgombea, mpiga Kura amekaa uwanjani zaidi ya saa 3 Lowasa anaongea dk 5 hii ni sawa?
Usimtafute mchawi kosa ni lenu wenyewe mmewapa CCM ujasiri ambao hawakua nao kabla poleni kwa sababu kazi iliyokua ifanywe nao mnaifanya nyinyi kujibu Makombora.
Kama Uchaguzi Serikali za mitaa uliibeba CDM kwa Ajenda ya Escrow account basi Uchaguzi huu CCM itabebwa na Ajenda ya Lowasa