Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Wanaajiri vijana 20 , lakini product Yao inawaangamiza na kuuwa MAELFU NA MAELFU ya vijana. Kiwanda chao Hawkins faida kwa watanzania Bali ni wauwaji baridi, wafunge NA waende zao.
 
Kwani ubaya uko wapi, hiyo pesa waliyokuwa wananywea Konyagi watu wataenda kunywea maziwa ya Azam, kwahiyo ajira zitahamia tu Azam, wakaombe ajira huko. Kwa style hii tutakuwa tumeboresha afya na kupunguza walevi na wagonjwa.
 
Kama huo uchumi ulikuwa unakua kwa huku kung'oa roho za vijana wetu kwa viroba, basi ufe na utokomee kabisa!

Kwani walikuwa wanalazimishwa au wananunua wenyewe ?????
Na jee kama viroba hakuna hawatanunua pombe nyingine ????

Kwani mtengenezaji and a viroba alimlenga nani kama mteja jee ni hao watoto wenu ????

Mwenye kosa ni nani ???

Muuzaji au mnunuaji au mnywaji ???????
 
Potelea mbali athari za viroba ni kubwa kuliko faida.
 
Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.

That's good news
 
the main issue here is why the young people are the major consumers of viroba?

Bibie, young ones walipata kirahisi kutokana na uholela. Viliuzwa hadi viduka vya mangi. Imagine na mamlaka zikawa zinafumba tu macho. Na kanuni na sheria za pombe zinajulikana.

Mbona enzi za Totapak haikua hivi?
 
Bibie, young ones walipata kirahisi kutokana na uholela. Viliuzwa hadi viduka vya mangi. Imagine na mamlaka zikawa zinafumba tu macho. Na kanuni na sheria za pombe zinajulikana.

Mbona enzi za Totapak haikua hivi?
Mimi ninaona ni kwasababu vijana hawana shughuli zinazoipa chenga akili yao, hii inatokana na boredom.
 
Si kufunga tu ila wahame kabisa, kazi yenye kuangamiza Taifa ni ushetani sawa na ule wa Gwajima
 
Mbona kuzuia viroba ni juzi tu hapa?wamejuaje kua uzalishaaji utakua ni mgumu?kama wanywa viroba watahamia kwenye konyagi wanajuaje?
 
Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.
Waondoke tu kwa kweli wametuongezea mazebe wengi sana nchini
 
Mimi ninaona ni kwasababu vijana hawana shughuli zinazoipa chenga akili yao, hii inatokana na boredom.

Lakini mimi nimeshuhudia madereva bodaboda na hiace wakinywa huto tudude tena asubuhi na mapema wakiwa kazini. Na kazi zao si rahisi kihivyo.

Urahisi na uholela wa viroba ulichangia sana.
 
hahaha bado kweli halafu maisha yakitushinda tunaenda magogoni akatupe chakula kila mahali watu wanapunguzwa na serikali haiajiri ................... hili ni bomu kaka wa bashite anajiundia mwenyewe hakuna viwanda hakuna ajira hakuna pesa kuna siku tutamdai kama tunavyomdai daudi basshite vyeti nayeye aende sa ni hatari sana kampuni yetu iliyodumu tangu mwaka 56inaelekea omega na ina wafanyakazi zaidi ya 400 tz nzima hatari hatari hatari
Tufike sehemu tujielewe vijana, hapa unaona ni bora vijana wafe na nguvu kazi ya taifa liishe kwa issue ya kiwanda. Ningekuwa rais hawa ningewatimua haraka sana. Ifike sehemu maslahi ya taifa liwekwe mbele, kiwanda chake kinatusaidia nini sisi kama wateja wake ambao ni nguvu kazi ya taifa wanakufa kwa viroba. Serikali fungeni viwanda vyote vinavyizalisha haya madude kisha mje kwenye viwanda vya mifuko ya plastiki. Mabadiliko lazima yaje na maumivu.
 
Inaelekea hivi viroba vina sumu kali ya kuua na hivyo haviwezi kuachwa vikaisha taratibu baada ya uzalishaji kusitishwa! bora watu wajinyonge tu baada ya kupata hasara
 
Watakuwa sio wafanyabiashara kwakuwa konyagi haijafutwa,bali kifungashio.Pia hii habari haina chanzo rasmi cha wenye kiwanda.Hivi inaweza kuwa ni uzushi tu
 
hahaha bado kweli halafu maisha yakitushinda tunaenda magogoni akatupe chakula kila mahali watu wanapunguzwa na serikali haiajiri ................... hili ni bomu kaka wa bashite anajiundia mwenyewe hakuna viwanda hakuna ajira hakuna pesa kuna siku tutamdai kama tunavyomdai daudi basshite vyeti nayeye aende sa ni hatari sana kampuni yetu iliyodumu tangu mwaka 56inaelekea omega na ina wafanyakazi zaidi ya 400 tz nzima hatari hatari hatari
Viwanda 27 vya mifuko ya kijamii vinakuja ajira watu 1000000 na vingine vingi vinajengwa na kufufuliwa. Kiwanda cha konyagi kilianza na pombe za chupa baadae vikaja viroba vidogo havikupata soko wakasimamisha wakaendelea na chupa kisha wakaanzisha viroba vikubwa kidogo vikapata soko la landslide lkn za chupa ziliendelea kuzalishwa. Sasa kama hawataki kuimarisha pombe za chupa badala ya viroba waende tu. Afya na nguvu kazi ya vijana kwanza.
 
Viroba vilisaidia kukuza uchumi, kama tatizo ni vijana kuharibika kwanini vijana hawa wasipewe somo juu ya madhara ya pombe na kuhakikisha mnunuaji ana kitambulisho awe na umri Zaidi ya miaka 21 au zaidi?
Uchumi ulikuzwa kwa kiasi gani na viroba? Na utapungua kwa kiasi gani? Je huo uliopungua utalingana na afya na nguvu kazi ya vijana inayoathiriwa na viroba? Watanzania wangapi wana vitambulisho vya kuonyesha kabla ya kuuziwa viroba? Think twice.
 
Back
Top Bottom