Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Nipelekeeni salamu sigara zimeniathiri sana nimekua teja nina uhakika mapafu yangu yameshakua na rangi ya tairi naomba muheshimiwa kama unanisikia ukataze sigara na vile viwanda vifungwe muheshimiwa siko peke yangu waathirika wa sigara tupo wengi muheshimiwa "inawezekana" tukawazidi waathirika wa viroba muheshimiwa
 
Hiyo ni kutaka kulazimisha waendelee kuuza Viroba ili vijana na taifa la kesho liangamie...haiwezekani lazima watanzania Fujifunze kutofautisha biashara na afya za vijana wetu. Kwa hili waondoke tu!
Ni ukweli mtupu. Nifikishie salamu pia kuhusu sigara. Kwanini hawaziongelei wakati zina madhara makubwa tena ya mmoja kwa moja
 
Bora uchumi ufe lakini raia wabaki na afya salama ya mwili na akili tofauti na sasa ambapo vijana wamebadilishwa kuwa wagonjwa na vichaa sababu ya hayo maroba . Waende tutakunjwa bia
 
Kasi ya ukuaji uchumi ni inatokana na increase in production, na viwanda ndo wahusika wakuu kwenye hilo.Sasa vikianza kufungwa mnategemea nini!

Halafu hii excuse ya kusema viroba ndo vinaua nguvu kazi ya taifa, siafikiani nayo kabisa.
Viroba ni pombe, kama ndo hivyo basi watunge sheria ili kunywa na kutengeneza pombe ya aina yoyote ile iwe illegal.
Uko sahihi kabisa, ukuaji wa uchumi unatokana na kuongezeka kwa tija katika uzalishaji. Suala hapa ni, tunazalisha nini na kwa namna gani na pia tunamlenga nani!?

Pombe ni dawa za kulevya zilizofanyiwa utafiti kitaalam na kupimwa kiwango cha ulevi ulioruhusiwa kisheria kutumika kwa kundi maalum katika jamii(Watu wazima).
Ili kuzuia au kupunguza kundi lisiloruhusiwa (kisheria) kunywa kilevi(watoto chini ya miaka 18). Namna nzuri na ya pekee inayoweza kutumika ni kuongeza ujazo wa vifungashio ambayo moja kwa moja itaongeza bei, jambo ambalo hili kundi lengwa litashindwa kumudu kirahisi. Kuza uchumi ila OKOA VIJANA.

Ninaishi karibu na shule fulani ya sekondari imepakana na mto, ninayoyaona yanayofanyika na jinsi waalimu wanavyohangaika na hawa vijana..! Wewe ongelea nadharia tu ila hali halisi kwa hawa vijana wetu ilishakuwa mbaya sana.
 
Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.
Viroba ni sumu,viroba vinaharibu nguvu kazi viroba havipashwi kuchekewa tuache siasa ktk mambo ya msingi.
 
Kama hujui kuishi kishetani ndio kunaamza rasmi sasa! Na ukishindwa kuendana na hali hiyo unaweza ukaishi kama msukule.
 
Viroba vilisaidia kukuza uchumi, kama tatizo ni vijana kuharibika kwanini vijana hawa wasipewe somo juu ya madhara ya pombe na kuhakikisha mnunuaji ana kitambulisho awe na umri Zaidi ya miaka 21 au zaidi?
Wewe ndio umeandika hapa kweli... Nooo bhn utakua umeandikiwa
 
Hiyo ni kutaka kulazimisha waendelee kuuza Viroba ili vijana na taifa la kesho liangamie...haiwezekani lazima watanzania Fujifunze kutofautisha biashara na afya za vijana wetu. Kwa hili waondoke tu!

Hivyo viroba vinagaiwa bure? Wazazi kushindwa kulea watoto wao katika maadili mema ndio yanafanya vijana watumie viroba.
Wamezuia viroba,sasa hivi wanakunywa gongo na kutumia ugoro.
Wazazi tulee watoto wetu katika maadili mema na wao hawataweza kuangamizwa na pombe.
 
hahaha bado kweli halafu maisha yakitushinda tunaenda magogoni akatupe chakula kila mahali watu wanapunguzwa na serikali haiajiri ................... hili ni bomu kaka wa bashite anajiundia mwenyewe hakuna viwanda hakuna ajira hakuna pesa kuna siku tutamdai kama tunavyomdai daudi basshite vyeti nayeye aende sa ni hatari sana kampuni yetu iliyodumu tangu mwaka 56inaelekea omega na ina wafanyakazi zaidi ya 400 tz nzima hatari hatari hatari
Afya za watanzania na ajira nini bora?Arachuga wataathirika sana huko kwa kukosa hii kitu
 
Back
Top Bottom