Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Tz nchi isiyoamini katika elimu.
Kwani tatizo ni viroba ama watu wenyewe? Wasipopata viroba wanakunywa gongo na kuvuta gundi/petrol
 
Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.

Kupunguza wafanyakazi ndiyo kufunga virago? Konyagi ni mali ya Tanzania kama ilivyo Waragi mali ya Uganda. Konyagi watafunga virago waende wapi?
 
Sisi sera yetu ni kujenga viwanda nyie mnafunga,hakika huu ni uchochezi dhidi ya mtukufu,zero fanya kazi yetu fasta.
 
boraaaa hata maana si kwa kutuharibia nguvu kazi ya vijana kwa kiasi hiki
 
serikali bila pombe haiendi wewe unasema taifa la kesho wakati ajira zinaondoka hivyo serikali yenyewe haiajiri,swala wala sio vijana kuharibikiwa swala ni la mazingira ndio limepelekea kusitishwa kwa biashara hiyo,sasa unaondoa kiroba sigara utasemaje sasa..!1tuanakurupuka karibia katika kila kitu
Nguvu kazi ya nini wakati hakuna ajira? Wacha waburudike walale usingizi.
 
The Spirit of the Nation?? sasa hatutakua na spirit tena??
 

Attachments

  • upload_2017-3-8_14-37-4.jpeg
    upload_2017-3-8_14-37-4.jpeg
    9.6 KB · Views: 36
Samahani kuna mwenye utafiti usio na shaka kuhusiana na % katibya wanaokufa kwa
1. Pombe
2. Malaria
3. Ukimwi
4. Ajali
 
Hiyo ni kutaka kulazimisha waendelee kuuza Viroba ili vijana na taifa la kesho liangamie...haiwezekani lazima watanzania Fujifunze kutofautisha biashara na afya za vijana wetu. Kwa hili waondoke tu!
Issue sio viroba pekee

Iwe ni pamoja na kila aina ya pombe yenye % ya kilevi inayoathiri afya ikiwemo bapa na baadhi ya wine. Na pia sigala na mengineyo.

Kwa hayo nadhani wananchi tutakuwa vzr
 
Kwani wamezuiliwa wasizalishe au kinachotakiwa ni kubadilisha vifungashio visiwe vile vi ji plastic?
 
Kama huo uchumi ulikuwa unakua kwa huku kung'oa roho za vijana wetu kwa viroba, basi ufe na utokomee kabisa!

Uchumi ungekuaje siku za usoni baada ya kua nguvu kazi ya siku usoni na viroba?Au unazungumzia uchumi wa namna na wakati gani?

Kasi ya ukuaji uchumi ni inatokana na increase in production, na viwanda ndo wahusika wakuu kwenye hilo.Sasa vikianza kufungwa mnategemea nini!

Halafu hii excuse ya kusema viroba ndo vinaua nguvu kazi ya taifa, siafikiani nayo kabisa.
Viroba ni pombe, kama ndo hivyo basi watunge sheria ili kunywa na kutengeneza pombe ya aina yoyote ile iwe illegal.
 
hahaha bado kweli halafu maisha yakitushinda tunaenda magogoni akatupe chakula kila mahali watu wanapunguzwa na serikali haiajiri ................... hili ni bomu kaka wa bashite anajiundia mwenyewe hakuna viwanda hakuna ajira hakuna pesa kuna siku tutamdai kama tunavyomdai daudi basshite vyeti nayeye aende sa ni hatari sana kampuni yetu iliyodumu tangu mwaka 56inaelekea omega na ina wafanyakazi zaidi ya 400 tz nzima hatari hatari hatari
Serikali haina shamba
 
Back
Top Bottom