Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Kuzuiwa viroba: Konyagi waanza kufunga virago?

Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.
Wafunge tu kabala ya viloba walikuwa hawazalishi
 
Niliwahi kuwepo pale kwa shifti kiwanda kinakua na wafanyakazi si chini ya 250
inawezekana wakapungua hadi kufikia 50
hawa 200 wanaenda wapi?
Kwani wao ni wa kwanza kupunguzwa kazini? Viwanda vingi vilikufa kama urafiki mwatex mutex morogoro shoes kiltex n.k walienda wapi?
 
Viroba vilisaidia kukuza uchumi, kama tatizo ni vijana kuharibika kwanini vijana hawa wasipewe somo juu ya madhara ya pombe na kuhakikisha mnunuaji ana kitambulisho awe na umri Zaidi ya miaka 21 au zaidi?
Elimu ndo dawa ya kudumu. Isije kuwa tumewapandisha daraja kwa sasa kunywea kwenye chupa badala ya nyloni! Naunga mkono pombe kali zipigwe vita, over 30%W/V zipigwe marufuku.
 
Wafunge tu mapombe kwanza mabaya hata mungu hapend...nawaza nkiwa rais wa nchi kisha nchi inauzwa mapombe
 
serikali bila pombe haiendi wewe unasema taifa la kesho wakati ajira zinaondoka hivyo serikali yenyewe haiajiri,swala wala sio vijana kuharibikiwa swala ni la mazingira ndio limepelekea kusitishwa kwa biashara hiyo,sasa unaondoa kiroba sigara utasemaje sasa..!1tuanakurupuka karibia katika kila kitu
Viroba vimezuiliwa kwa sab nyingi mojawapo ikiwa uharibifu wa mazingira. Athari ya sigara sio kubwa kama ya viroba. Kama serikali inakurupuka kuokoa vijana kiafya na madhara mengine wacha ikurupuke tu kwani kuna faida.
 
Tz nchi isiyoamini katika elimu.
Kwani tatizo ni viroba ama watu wenyewe? Wasipopata viroba wanakunywa gongo na kuvuta gundi/petrol
Hawanywi hadharani na kwa wingi kama viroba
 
Kwani walikuwa wanalazimishwa au wananunua wenyewe ?????
Na jee kama viroba hakuna hawatanunua pombe nyingine ????

Kwani mtengenezaji and a viroba alimlenga nani kama mteja jee ni hao watoto wenu ????

Mwenye kosa ni nani ???

Muuzaji au mnunuaji au mnywaji ???????
Kaisari, hao vijana ninaowazungumzia ni hawa wa umri usiozidi miaka18 ambao uwezo wao wa kujua baya na zuri ni mdogo. Umri ambao kwa msichana ukifanye naye ngono hata kama ni yeye amejipendekeza unahesabika umembaka. Kwa maana nyingine hawa vijana wadogo wananyweshwa viroba na walaku wa pesa

Hata kama watanunua ulevi mwingine baada ya viroba, hilo halihalalishi viroba kuendelea. Viroba viondolewe na kama kutakwepo na aina nyingine ya ulevi hatarishi, harakati zitahamia huko.
 
Kasi ya ukuaji uchumi ni inatokana na increase in production, na viwanda ndo wahusika wakuu kwenye hilo.Sasa vikianza kufungwa mnategemea nini!

Halafu hii excuse ya kusema viroba ndo vinaua nguvu kazi ya taifa, siafikiani nayo kabisa.
Viroba ni pombe, kama ndo hivyo basi watunge sheria ili kunywa na kutengeneza pombe ya aina yoyote ile iwe illegal.
Kwani usipokubaliana itasaidia viroba kurudi?
 
Kwani walikuwa wanalazimishwa au wananunua wenyewe ?????
Na jee kama viroba hakuna hawatanunua pombe nyingine ????

Kwani mtengenezaji and a viroba alimlenga nani kama mteja jee ni hao watoto wenu ????

Mwenye kosa ni nani ???

Muuzaji au mnunuaji au mnywaji ???????
Kaisari, hao vijana ninaowazungumzia ni hawa wa umri usiozidi miaka18 ambao uwezo wao wa kujua baya na zuri ni mdogo. Umri ambao kwa msichana ukifanye naye ngono hata kama ni yeye amejipendekeza unahesabika umembaka. Kwa maana nyingine hawa vijana wadogo wananyweshwa viroba na walaku wa pesa

Hata kama watanunua ulevi mwingine baada ya viroba, hilo halihalalishi viroba kuendelea. Viroba viondolewe na kama kutakwepo na aina nyingine ya ulevi hatarishi, harakati zitahamia huko.
 
Hiyo ni kutaka kulazimisha waendelee kuuza Viroba ili vijana na taifa la kesho liangamie...haiwezekani lazima watanzania Fujifunze kutofautisha biashara na afya za vijana wetu. Kwa hili waondoke tu!
Kuna tofauti yoyote kati ya viroba na konyagi, ukiacha packeging?
 
Hii ishu yote ya viroba ni muendelezo wa kutokua makini. Tatizo lilianza serikali ilipoamua kufumbia macho viroba kuuzwa kiholela.

Tulishauri sana vipigwe marufuku kungali mapema ila kwa kua labda walinufaika basi wakakaa kimya.

Sasa ni kuisoma namba kila mmoja. Atakaezidiwa atajua cha kufanya mbele ya safari. Maana hawa watu hawaeleweki.
Kwahiyo tatizo lako ni kutofungia viroba pale uliposhauri kwahiyo kufungia sasa ni kosa. Very funny.
 
Nipelekeeni salamu sigara zimeniathiri sana nimekua teja nina uhakika mapafu yangu yameshakua na rangi ya tairi naomba muheshimiwa kama unanisikia ukataze sigara na vile viwanda vifungwe muheshimiwa siko peke yangu waathirika wa sigara tupo wengi muheshimiwa "inawezekana" tukawazidi waathirika wa viroba muheshimiwa
Acha kuvuta sigara
 
Ee Mungu, tulikokosea TUSAMEHE, haya mambo sio ya kukurupuka, hivi rais anaona Tanzania inakoelekea ama!!!! Amevaa miwani ya mbao?
Haoni ni wewe pekee ndiye mwenye macho na uono wa kimungu.
 
Ee Mungu, tulikokosea TUSAMEHE, haya mambo sio ya kukurupuka, hivi rais anaona Tanzania inakoelekea ama!!!! Amevaa miwani ya mbao?
Haoni ni wewe pekee ndiye mwenye macho na uono wa kimungu.
 
aisee ile habari ya mfanyaiashara aliojiua Dodoma sio poa kabisa imagine mtu anafuata taratibu zote anashehena za billion moja halafu anakuja ny'ang'anywa dah...SAD...tujiangalie aisee ...maana hizi biashara ndo zinaongeza kutoa kodi yaani
Kodi nyingine inakuja tutaireplace tu usihofu mamia ya viwanda vinajengwa nchi nzima
 
Kutokana na agizo la serikali lililopiga marufuku uzwaji wa viroba hapa nchini Kiwanda cha TDL maarufu kama Kiwanda cha Konyagi kimeanza kufunga virago na kupunguza wafanyakazi, baada ya kuona wanapata hasara kubwa kwani wanazalisha lakini hawana Soko.

Wakizungumza baadhi ya viongozi wakubwa kiwanda hapo walisema kiwanda hicho kilikuwa kimesha uza mashine za kuzalisha Konyagi ya chupa na kuagiza mitambo ya kuzalisha viroba.

Jambo hilo limefanya waanze kupunguza wafanyakazi na kudai wataendelea kupunguza kwani mtambo mmoja wa kuzalishia Konyagi unaendesha na watu watatu tu kwahiyo wafanyakazi wengine wote waanze kutafuta sehemu ya kwenda.
Kweli kuna mdororo wa Biashara lakini kiwanda cha Konyagi hakiwezi kufungwa miaka ya hivi karibuni.

Konyagi wana Product nyingi sana ambazo zipo sokoni, nyingine hata hawazitengenezi wao zinatoka SOUTH AFRICA.
  1. Konyagi 12 x 750mls
  2. Konyagi 16 x 500mls
  3. Konyagi 35 x 200mls
  4. Valuer 12 x 750mls
  5. Valuer 35 x200mls
  6. Vladmir 12 x750mls
  7. Vladmir 35 x 200mls
  8. Regency Whisky 12 x 750mls
  9. Regency Whisky 35 x 200mls
  10. Zanzi Liquor 24 x 200mls
  11. Zanzi Liquor 12 x 750mls
  12. Viceroy 35 x 200mls
  13. Count Pushkin 35 x 200mls
etc..
Hizi ni Baadhi ya Pombe zinazozalishwa kwenye kiwanda chao Tanzania mpaka sasa hivi, kama ni hivyo wana haja gani ya kufunga kiwanda?

Achana na hizi zinazokuja kutoka S.A kama Drostdy hof wines, Amarula, Savanna, Chamdor champagne na kadhalika.

Tanzania Distilleries bado wana advantage ya kuendelea kukomaa sokoni kwa sababu wana Product nyingi sana ambazo hazimo kwenye katazo la serikali.

Kinachowasumbua Tanzania Distilleries ni stock ya viroba ambayo tayari walishaitengeneza, iliyoko kwao na ile iliyoko kwa wateja au mawakala wao, ni mabilioni ya shilingi.
 
Back
Top Bottom