Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,483
- 40,498
Wapo watu wanajivunia kuwa na mawazo ya biashara ila hawana mitaji; ukiomba wakushirikishe wazo lao, wanakataa wakihisi unaweza kuchukua wazo lao na kulifanyia kazi.
Unakuta miaka nenda rudi, mpaka anakuwa mzee bado yuko na wazo lake tu, na hataki kushirikisha watu ili lifanyiwe utekelezaji.
Katika mazingira ya kibiashara, tunasema hayo ni mawazo mfu, yanakuwa hayana tofauti na ndoto za usiku; ukiamka asubuhi unajikuta uko pale pale.
Kushirikisha wazo lako kwa jamii, kunakusaidia kulishepu vizuri hilo wazo lako, pamoja na kugundua changamoto iliyopo, ambayo ulikuwa ujaitazamia.
Kwa hiyo, kuficha wazo la biashara huku huna mtaji sio ufahari; bali ni kuendeleza umasikini uliopo.
Kwa hiyo, tuzidi kufunguka zaidi kwa kuweka mawazo ya kibiashara ili kuboresha maisha yetu.
Nb: Hakuna wazo jipya la kibiashara ambalo halijawahi kufanyika.
Unakuta miaka nenda rudi, mpaka anakuwa mzee bado yuko na wazo lake tu, na hataki kushirikisha watu ili lifanyiwe utekelezaji.
Katika mazingira ya kibiashara, tunasema hayo ni mawazo mfu, yanakuwa hayana tofauti na ndoto za usiku; ukiamka asubuhi unajikuta uko pale pale.
Kushirikisha wazo lako kwa jamii, kunakusaidia kulishepu vizuri hilo wazo lako, pamoja na kugundua changamoto iliyopo, ambayo ulikuwa ujaitazamia.
Kwa hiyo, kuficha wazo la biashara huku huna mtaji sio ufahari; bali ni kuendeleza umasikini uliopo.
Kwa hiyo, tuzidi kufunguka zaidi kwa kuweka mawazo ya kibiashara ili kuboresha maisha yetu.
Nb: Hakuna wazo jipya la kibiashara ambalo halijawahi kufanyika.