Utaratibu wa kutoa majina ya watumishi waliokidhi vigezo vya kuhama kwenye tovuti ya TAMISEMI kila mwezi wa Juni na Desemba umeshakufa. Kwa sasa barua zimerudikana pale idarani kurugenzi ya serikali za mitaa Mitumba.
Barua za watumishi waliokamilisha tàratibu za kuhama zote baada ya kupitishwa na ma-DED anakotaka kuhamia na anakotoka na baadae RAS wa mkoa anaotoka na kufikishwa wizarani pale zinapakiwa na haitashughulukiwa mpaka utakapoenda kuwaona.
Watumishi kadhaa waliofika pale kulalamika wapo ambao wamesubiria zaidi ya miaka 2. Mtumishi mmoja ambaye jina linahifadhiwa aliomba uhamisho kutoka Mtwara Mkindani na kufikishwa TAMISEMI mwaka jana alitakiwa kuona jina lake Desemba 2019 au Juni 2020, amedai wizara haijawahi kutoa majina tovutini hata moja katika kipindi hicho lakini tumekuwa tukishuhudia watumishi wakihama kimyakimya.
Mtumishi mwingine niliyekutana nae akitokea Singida licha kugoma kutaja Halmashauri anayotoka na anakotaka kuhamia amedai kuwa aliambiwa na mwenzake kuwa alihamia halmashauri yao baada ya kutoa rushwa ya laki 3, amefika akiwa na pesa hiyo baada ya kufanikiwa kumpata dalali hapo wizarani anadai atoe laki 6.
Inadaiwa afisa husika anachukua laki 3 na watumishi wote tunajua hivyo lakini kumpata muhusika mwenyewe ni shida mpaka upitie kwa madalali ambo huongeza cha juu. Mtumishi mwingine mfanyakazi katika idara nyungine pale wizarani alidai kuwa mambo ya hovyo yamejirudia kama enzi za Katibu Mkuu Sajini aliyewahi kutumbuliwa na Mhe. Rais.
Aliendelea kueleza enzi za Sajini kupata u-DED au ukuu was idara kwenye halmashauri ulilazimika kutoa rushwa ya milioni 5. Tunaomba mamlaka husika kuondoa kero hii. Kwani kila anayekubaliwa kuhama tena kwa kujihamisha ili mpaka kukubaliwa ulikotoka na unakohamia wamezingatia sababu za msingi watumishi hawa walizotoa.
Barua za watumishi waliokamilisha tàratibu za kuhama zote baada ya kupitishwa na ma-DED anakotaka kuhamia na anakotoka na baadae RAS wa mkoa anaotoka na kufikishwa wizarani pale zinapakiwa na haitashughulukiwa mpaka utakapoenda kuwaona.
Watumishi kadhaa waliofika pale kulalamika wapo ambao wamesubiria zaidi ya miaka 2. Mtumishi mmoja ambaye jina linahifadhiwa aliomba uhamisho kutoka Mtwara Mkindani na kufikishwa TAMISEMI mwaka jana alitakiwa kuona jina lake Desemba 2019 au Juni 2020, amedai wizara haijawahi kutoa majina tovutini hata moja katika kipindi hicho lakini tumekuwa tukishuhudia watumishi wakihama kimyakimya.
Mtumishi mwingine niliyekutana nae akitokea Singida licha kugoma kutaja Halmashauri anayotoka na anakotaka kuhamia amedai kuwa aliambiwa na mwenzake kuwa alihamia halmashauri yao baada ya kutoa rushwa ya laki 3, amefika akiwa na pesa hiyo baada ya kufanikiwa kumpata dalali hapo wizarani anadai atoe laki 6.
Inadaiwa afisa husika anachukua laki 3 na watumishi wote tunajua hivyo lakini kumpata muhusika mwenyewe ni shida mpaka upitie kwa madalali ambo huongeza cha juu. Mtumishi mwingine mfanyakazi katika idara nyungine pale wizarani alidai kuwa mambo ya hovyo yamejirudia kama enzi za Katibu Mkuu Sajini aliyewahi kutumbuliwa na Mhe. Rais.
Aliendelea kueleza enzi za Sajini kupata u-DED au ukuu was idara kwenye halmashauri ulilazimika kutoa rushwa ya milioni 5. Tunaomba mamlaka husika kuondoa kero hii. Kwani kila anayekubaliwa kuhama tena kwa kujihamisha ili mpaka kukubaliwa ulikotoka na unakohamia wamezingatia sababu za msingi watumishi hawa walizotoa.