Kuna ubaya mwanamke akikuzidi kiuchumi?

Kuna ubaya mwanamke akikuzidi kiuchumi?

Hiyo labda barani ulopa lakini huku Africa, ukizidiwa pato na mke andika umeumia. Utakuwa mtumwa we ndo utakuwa mpikaji na kutenga chakula mezani! Hawa wanawake wa kiafrika mwanaume unatakiwa ukaze buti tu umzidi kipato. Ndo mana hata wanawake ambao wamesoma sana na wako juu kiuchumi most of mens wanawaogopa kuwaoa. Ukichunguza kwa undani wanaume wanaogopa kuzidiwa kipato na wanawake kwenye maisha yao,

Si kwamba tunaogopa kuwaoa ila HAWAOLEKI
 
Safi sana ila kaa ukijua kuwa hekima za masikini hazisikilizwi

Muhammad Salla Lllahu Aleyhi Wasalaam na Yesu Aleyhi Salaam hawakuwa matajiri na mpaka leo wanasikilizwa miaka zaidi ya 1,000?

Hayo mawazo ya "kuwa hekima za masikini hazisikilizwi" ni mfu.

Hakuna masikini kama hakuna tajiri na hakuna tajiri kama hakuna masikini. Kumbuka hilo.
 
Biblia inasenasema alikuwa tajiri wa moyo. Hakuwa tajiri wa dunia hii.
Angalizo. Nani walimsikilliza zaidi? Mafarisayo na viongoz wa serikali au fukara kwa wingi wao? FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Biblia inasenasema alikuwa tajiri wa moyo. Hakuwa tajiri wa dunia hii.
Angalizo. Nani walimsikilliza zaidi? Mafarisayo na viongoz wa serikali au fukara kwa wingi wao? FaizaFoxy

Yeyote aliyemsikiliza kamsikiliza. Mpaka leo wapo wanaomsoma lakini hawamuelewi.
 
Ni kweli. Na sio rahisi kumwelewa. Ndio maana wengine wanatajirika kupitia jina lake
 
Kwa wanawake wetu hawa wa JF, facebook, IG na twitter hapo ni tatizo. Ipo siku tu utaona her true color.

upo sahihi mkuu. Ila me naamini kwamba kuna watu wamebahatika kupata 'wife material' kwenye hii hii mitandao ya kijamii, japo mmmh ni wachache mno, one in hundred!!!
 
upo sahihi mkuu. Ila me naamini kwamba kuna watu wamebahatika kupata 'wife material' kwenye hii hii mitandao ya kijamii, japo mmmh ni wachache mno, one in hundred!!!

Wife material is just the mind set. Tunachoona Leo ni mwendelezo wa yale ya kale
 
Mwanamke akikuzidi kipato ni noma nyumbani hapakaliki panageuka Jahanamu......kejeli, matusi na dharau vitakuwa ni sehemu ya maisha yako ya kila siku......kwa hiyo inabidi uzoee....alafu inabidi uende kwa dokta akautoe mshipa wa hasira.........
 
Kwa dunia ya sasa hakuna ubaya wowote mke kumzidi kipato/pesa mume. Hata vitu vingine vingine kama elimu na umri mi naona poa tu ili mradi malavidavi na heshima ndani ya nyumba ipo pale paleeeee
 
Heshima itatoka wapi na Wewe umezidiwa? WABALLA Inc
 
Last edited by a moderator:
Akiwa anajitambua kuwa hata awe trillionea bado atabaki kuwa mke na wewe mme, heshima itakuwepo tu mkuu!!
 
Ni mpaka.... Kujitambua si mchezo
 
Huwa hakuna tatizo kabisa muhimu Ni kuheshimiana na inategemea ndoa yenu imejengwa au ilianza kwenye misingi ipi yaani Ni hela,vitu au upendo.Kama Ni upendo ndoa utakuwa na hofu ya Mungu.From my own experience,mume amenisaidia na kunisapport niweze kufanya vizuri na hata kujiongezea kisomo ili niweze kupanda cheo nipate mshahara nzuri.Hata akiina kazi nzuri inatangazwa uwa ananiletea gazeti ananiambia na kunicoach na Nina cheo kikubwa Tu na mshahara kumzidi na tunaeshimiana Sana hapo hiccup za dos zipo
 
Huwa hakuna tatizo kabisa muhimu Ni kuheshimiana na inategemea ndoa yenu imejengwa au ilianza kwenye misingi ipi yaani Ni hela,vitu au upendo.Kama Ni upendo ndoa utakuwa na hofu ya Mungu.From my own experience,mume amenisaidia na kunisapport niweze kufanya vizuri na hata kujiongezea kisomo ili niweze kupanda cheo nipate mshahara nzuri.Hata akiina kazi nzuri inatangazwa uwa ananiletea gazeti ananiambia na kunicoach na Nina cheo kikubwa Tu na mshahara kumzidi na tunaeshimiana Sana hapo hiccup za dos zipo

Hongera kuendeleza heshima. Una muda gani tangu umeanza kumzidi kipato?
 
mmmh! hapo penyewe maana nina mchumba ananizidi kipato ila ananiheshimu sana na kuniogopa pia,ila nikimwambia hata aniongeze elfu 50 ili nifanikishe miradi yangu hataki...pesa yake anawatumia marafiki zake (wa kike) tu aliosoma nao nairobi eti anawapa mitaji coz ajira kwao ni ngumu....ninamaswali mia kidogo....tutajenga familia kweli ? anasema lazima nimuoe tena mwaka kesho tu.
 
hapo hakuna jibu la moja kwa moja bali ni namna mweza wako alivo, hata mm nina mchumba wangu ananizidi kipato kidogo na mwakan nitamuoa kama mwenye uhai wetu atataka.... shida ni kwamba chake chake tu na ndugu zake,mi nakomaa na miradi yangu lakin hata yeye kujiongeza ili to move haraka naona inakua shida...hela yake iko kwenya akaunti za benki tu.... akiendelea hivi..atakua sio halali kwa ndoa mwakani.
 
mmmh! hapo penyewe maana nina mchumba ananizidi kipato ila ananiheshimu sana na kuniogopa pia,ila nikimwambia hata aniongeze elfu 50 ili nifanikishe miradi yangu hataki...pesa yake anawatumia marafiki zake (wa kike) tu aliosoma nao nairobi eti anawapa mitaji coz ajira kwao ni ngumu....ninamaswali mia kidogo....tutajenga familia kweli ? anasema lazima nimuoe tena mwaka kesho tu.

Pole sana mkuu... Hapo anahofu ya kukupa na ukakimbia au ukamisiyuzi.
Ukimuoa anaweza kukupa.

Au anakuzowesha kuwa Wewe unawajibika kwa familia yako ijayo na sio yeye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom