Kuna ubaya mwanamke akikuzidi kiuchumi?

Kuna ubaya mwanamke akikuzidi kiuchumi?

Payer

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2014
Posts
824
Reaction score
189
Habari wana JamiiForums.

Natumai Jumatatu imeanza vyema tukiwa wenye siha njema.Kama sivyo nawaombea Mungu wote wasio katika ubora wao basi wairejee hali yao ya kawaida.

Nina moja tu la kutaka tushirikishane mawazo: " Ni sahihi mume kuzidiwa pato na mkewe?" Kuna faida au madhara gani iwapo mke atamzidi pato mumewe?

Karibuni tujadili kwa staha bila masihara mengi wala kutoka kwenye mada.
 
Sioni shida mke kumzidi mke kipato, lakini kwa dunia ya leo inaleta udhaifu sana kwa mwanaume maana saana nyingine mke anajisahau na kejeli zinaingia kwenye ndoa.

Kama mimi sioni shida lakini kuna tofauti ya mume kuzidiwa kupato na mwanamke kulea mwaaume, which I am against it.
 
Mkiheshimiana hakuna tatizo kabisa ila zikianza nyodo hapo ndio shida inapoanza
 
Nani ni mwepesi kuanzisha nyodo? MankaM
 
Last edited by a moderator:
Mimj naamini ktk biblia na kitabu cha mwanzo 3:16 kinajieleza. Vp wanawake Leo mtake kuwa juu?
 
Mwanamke akiwa ni mcha mungu mzuri na aliyeshiba imani na mapenzi. Kisha awe aliyepata malezi mazuri toka kwa wazazi wake hakuna shida kabisa. .hali inaweza kuwa mbaya kama ni yule mwenye ulimbukeni wa maisha na pia kazishika ukubwani. Usisahau hata wanaume wa namna hiyo wapo.
 
Mmmh.... Majukumu kama yepi? domitila
 
Last edited by a moderator:
Inategemea na mwanamke mwenyewe, level yake ya kuelewa mambo na kuikubali hali ile. Japo inawezekana mwanaume akawa chanzo maana atakuwa hajiamini na hamuamini mkewe. Mfano mke atatumia muda mwingi kwenye shughuli zake za kumuingizia kipato, kumbuka, ki asili ukiwa na mafanikio, muda mwingi sana utautenga kwa hayo mafanikio yako, kama ni mfanyabiashara atakuwa na safari nyingi za kibiashara, atakutana na watu ( hata wanaume) waliofanikiwa zaidi na kuwa na vikao nao sana, hii itasababisha inferiority complex kwa mume kufanya ianze misuguano ya hapa na pale.
 
Mwanamke akiwa ni mcha mungu mzuri na aliyeshiba imani na mapenzi. Kisha awe aliyepata malezi mazuri toka kwa wazazi wake hakuna shida kabisa. .hali inaweza kuwa mbaya kama ni yule mwenye ulimbukeni wa maisha na pia kazishika ukubwani. Usisahau hata wanaume wa namna hiyo wapo.

Kumpata sasa....
Hata wanaume wapuuzi wapo.
 
Inategemea na mwanamke mwenyewe, level yake ya kuelewa mambo na kuikubali hali ile. Japo inawezekana mwanaume akawa chanzo maana atakuwa hajiamini na hamuamini mkewe. Mfano mke atatumia muda mwingi kwenye shughuli zake za kumuingizia kipato, kumbuka, ki asili ukiwa na mafanikio, muda mwingi sana utautenga kwa hayo mafanikio yako, kama ni mfanyabiashara atakuwa na safari nyingi za kibiashara, atakutana na watu ( hata wanaume) waliofanikiwa zaidi na kuwa na vikao nao sana, hii itasababisha inferiority complex kwa mume kufanya ianze misuguano ya hapa na pale.

Msimamo wako ni nn ktk hili? Unapenda mkeo akupige gepu kiuchumi?
 
Mbona kawaida sana,mume akiwa muelewa mta enjoy maisha,lakini umpate yule mume mmekwazana kidogo anaanza eeh huomshahara wako ndio unaokutia kuburi eeh,kumbe akili yako haiko huko kabisa nimawazo yake mgando tuu..lakini as long as mna pendana hakuna tatizo kabisa na maisha hua matamu....
 
Msimamo wako ni nn ktk hili? Unapenda mkeo akupige gepu kiuchumi?


Mkuu Payer hayo ni matokeo tu. Ni juhudi na kuwa na vision katika maisha. Ninachofanya ni kufanya yale niyafanyayo kwa ufasihi zaidi, na kumuelewa. Mke akifanikiwa na nikijua chanzo cha mafanikio yake itanipa faraja sana na kumsaidia ki hali na mali afanikiwe.
 
Last edited by a moderator:
kwa wanawake wa hapa mjini ni shida akikuzidi kipato utakosa raha sana ila kwa mie naona ni challange maana kwenye utaftaji tumetofautiana kuna madada ni genius kwenye kusaka hela
 
kipimo cha tabia ya mtu niambapo amefanikiwa kimaisha ukikuta ni limbukeni wa maisha lazima unyanyasike vya kutosha na utakua huna thamani kwake ni wanawake wachache sana anaweza kukushinda kipato afu akakuheshim katika mia wakizidi sana watano au awe mchamungu na uchamungu wa wanawake huwa ni mdogo sana. Ukiona anaanza kukuzidi kipato anza kujiandaa kwa lolote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom