🤣 nyingi tu mkuu, we wasikilize atheist in their perspective utanielewa
Niliona unajadiliana na mtu kuhusu Huruma,.. kwamba kwanini matatizo yapo ikiwa Mungu ana huruma?
Mimi naona tunashindwa kuelewa kwasababu hatutaki kusoma na ku push akili zetu kuelewa zaidi,.... ngoja nijaribu kuelezea kama utanielewa:
Kwa mfano ishu ya huruma & kwanini mabaya yanatokea wakati Mungu ana huruma,.... Mfano kwenye Qur'an kuna aya inasema "....
Mungu habadilishi hali za Jamii/watu husika mpaka wao watakapoamua kubadilika......" sasa hapa tumepewa nyenzo kubwa ambayo ni "Akili" kupitia akili ndiyo utajua kwamba Mungu ametuhurumia sana.,, akili inatufanya tujue kipi kina madhara tuepuke na kipi kina faida tukifanye,.. ukiangalia kuna mateso mengi binadamu tunapitia kutokana na jinsi sisi wenyewe tulivyoamua kuendesha maisha yetu,. tukiamua kubadilisha tabia zetu tukaishi kwa kuthaminiana na kujaliana kwenye hali tofauti regardless ya rangi wala mitazamo asilimia kubwa ya mateso hayatokuepo,..
Lakini pia kwenye kusoma kuhusu Mungu anavyofanya huruma zake kuna sehem anasema....
" Wala usidhani Mwenyezi Mungu amepuuzia wanayoyatenda madhalimu. Anawaakhirishia tu mpaka siku ambayo macho yatakodoka yakibaki yametazama kwa kutetemeka.”
Hiyo inajibu kwamba Kuna mambo Mungu anayaachia yatokee haijalishi sisi tutayaona ni mabaya kiasi gani, Yeye ameshayapangia muda wa kuyahukumia,.....
Pia miongoni mwa changamoto ninayoiona kwa atheist ni mtazamo wao juu ya kifo& uhai,.. atheist wengi wanaona Uhai ni kitu bora na kifo ni kitu kibaya au kuangamia, (Sasa huo mtazamo kwa uelewa wangu sio sahihi,.. What if kwa Mungu uhai na kifo ni vitu vya kawaida sana kwake? huenda sisi tunathamini uhai kwakuwa hatujui kuna nini nyuma ya kifo,. what if kifo ni utulivu usio na purukushani za uhai... kuna uwezekano ukijua yaliyo nyuma ya kifo ukabadili mtazamo).
Nimejaribu kufafanua sikulazimishi kukubaliana na mimi ila nadhani kuna concept umepata..., kama kuna sehem hujaelewa unaweza kuuliza.