BinSalum7
JF-Expert Member
- Jan 26, 2019
- 1,678
- 3,732
Inawezekana ndio hitaji lake la kwanza hilo.Kuna siku nliambiwa nina nuksi sana na ndio maana kila mtu anakupakazia ww ofisini. Hivyo nikaenda kwa Tawile. Baada ya kueleza kwa kina na ulinganifu tawile kwa umakini akaniambia "Pole sana mwanangu,hii dunia ina mambo mengi sana na nyie vijana mnapuuziaga. Ww umetupiwa jini wa chuki na mkata nyota hivyo itabidi ulete Kuku jogoo mwekundu na hela elf 30 kwa ajiri ya kutengeneza dawa" mwanaume niliondoka huku nikijisemea sasa wabaya wangu wataisoma namba.
Siku ya siku kwa kweli kuku mwekundu pure mlishindwa kumpata na nikaona bora nirejee tena kwa tawile ili nimwambie ili nimlete mwenye rangi nyekundu ila sickle zake ni nyeusi. Nilipofika nikakuta kuna wamama wawili na mabinti watatu wapo nje na ndani kuna mtu anahudumiwa. Palikuwa na tambara jeupe lenye maandishi mekundu na lilitutenganisha cc na mganga. Walichokuwa wanaongea niliweza kusikia na maelezo yaleyale niliyopewa mm yaani jini na alete kuku mwekundu na elf 30.
Katika ile foleni hadi mtu wa nne maelezo na maelekezo yaleyale. Hahaha nikajifanya kama naenda nje kuongea na simu ila nilipotoka nje nikarudi jumla home.
Ni usanii tu na siri hii naitoa hapa na sikuwahi kumwambia hata tetea wangu.
Sijawahi kuamini waganga tokea hapo na hawa kuku hawa watatushitakia kwa Mungu maana ndio wanaongoza kupelekwa kwa mganga.
NB: kuku akipelekwa kwa mganga hafugwi.