Kuna kazi wanaozifanya sijawahi kuelewa huwa wanaishi vipi

Kuna kazi wanaozifanya sijawahi kuelewa huwa wanaishi vipi

Unajua hizi hearsay za kusimuliwa tu, hazina uthibitisho.

Hakuna anayeleta experience yake mwenyewe ya hizi biashara.

Kila mtu analeta stori za kuambiwa na kusimuliwa tu.

Mara, Kuna jamaa anauza tikiti tu, katoboa, kuna jamaa anauza ice cream tu, kuna jamaa anatembeza nguo tu.

Sasa hizi ni stori za kusimuliwa tu, inabidi mtu ambaye ametajirika na mwenye experience ya biashara hizi ndio aeleze mchanganuo mzima ulivyoenda.

Maana mtu aki kuhadithia tu, anauza ice cream au tikiti, utahakikisha vipi kwamba ni kweli na hana biashara nyingine inayo msapoti?
Halafu ukiangalia kuna wengine tunafanya zaidi ya hapo na hatuoni mbele kabisa😬
 
Yes, Hapa kkoo kuna watu wanapata hayo matunda, sahani buku wanawekwa kwenye vifungashio vya take away na vijiti vya meno.

1. Uchafu wao wanajaza mapipa matatu ama zaidi, siku wasipopita watu wa takataka mtaa haupitiki.

2. Matunda wanauza sahani kwa mamia kama sio maelfu, MTU kufunga faida laki kadhaa kwa siku Jambo la kawaida kabisa.

3. Nenda mwenyewe Kariakoo pita Mitaa kama Swahili na mchikichi ama Swahili na Agrey wamejaa kibao kaa kama nusu saa hesabu wameuza plate ngapi, then Rudi jukwaani ubishe tena.
Labda upate hela ya kula na kusogeza siku.

Ila hela ya kushusha mjengo mkali, labda ufanye hiyo biashara kwa kipindi kirefu sana, ukifanya savings za hatari kabisa.
 
Makuli kushusha gunia la kiaz buku semi ina gunia 300 wanakuwa wanne kwa siku wanapiga had semitrael 2 jion kila mmoja anarud na ka 70 mtaji nguvu vp wewe wa mshahara laki 8 unaeza mfikia sema wanamatumiz makubwa hasa ya starehe
Mwenye mshahara wa laki 8 ana bima ya afya na NSSF,
Mtu anayeshusha gunia 70 za kilo mia mia kwa siku ana tofauti gani na wale manamba au watumwa wa wakoloni? Anaishi miaka mingapi huyu?
 
Mwenye mshahara wa laki 8 ana bima ya afya na NSSF,
Mtu anayeshusha gunia 70 za kilo mia mia kwa siku ana tofauti gani na wale manamba au watumwa wa wakoloni? Anaishi miaka mingapi huyu?
Huwa wanakufa upesi, na wengi hawana maisha hasa Hawa wa mbeya wanaobeba magunia ya mipunga, pia Hela zao nyingi zinaishia kwenye kula
 
Wamachinga watembezi bidhaa barabarani, bar n.k.
Wapiga debe,
Wauza ice cream,
Wabeba mizigo(makuli),
Wachuuzi stendi,

Sijawahi kuelewa mtu anayefanya hizi kazi anawezaje kukidhi mahitaji yake ya chakula, mavazi, makazi na kuhudumia familia bila kukata tamaa ya maisha.

Ni kazi za kusikitisha sana.
Labda wapiga debe. Hao wengine hela ya mahitaji ya muhimu wanapata
 
Huwa wanakufa upesi, na wengi hawana maisha hasa Hawa wa mbeya wanaobeba magunia ya mipunga, pia Hela zao nyingi zinaishia kwenye kula
Inasikitisha sana, yani mtu anageuka kuwa kama mashine ya mafuta au umeme kabisa.
 
Wamachinga watembezi bidhaa barabarani
Hawa watu ukikutana nao kama kuna siri unazijua weka super glue mdomoni kwako wengi wao siyo hao kama unavyowaona kwa jicho la umachinga.

Pia wapiga debe wengi ni vitengo au mamluki chunguza kwa makini utakuja kunishukuru
 
Mkuu, wapiga debe wanapata pesa, tena hutaamini ila mtu kufunga 30k-50k per day ni kawaida.
Hawa wa stendi wanaorushiwa 200 na kondakta au unaamnisha wale madalali wa kukatisha tiketi stend za mabasi ya mabasi ya mikoani.

Hawa wa kurushiwa 200 na kondakta wengi wao huwa nawaona wamechoka. 30k per day hali zao za kiafya na uchumi zingeakisi hicho kipato
 
Hawa wa stendi wanaorushiwa 200 na kondakta au unaamnisha wale madalali wa kukatisha tiketi stend za mabasi ya mabasi ya mikoani.

Hawa wa kurushiwa 200 na kondakta wengi wao huwa nawaona wamechoka. 30k per day hali zao za kiafya na uchumi zingeakisi hicho kipato
Ninaowaona hasa hapo Mbezi stand ndogo wapo safi kabisa, tena baadhi yao ni wale makonda na madereva ambao hawana magari kwa kipindi hicho. Kila gari ni 1000.
 
Hawa watu ukikutana nao kama kuna siri unazijua weka super glue mdomoni kwako wengi wao siyo hao kama unavyowaona kwa jicho la umachinga.

Pia wapiga debe wengi ni vitengo au mamluki chunguza kwa makini utakuja kunishukuru
Toka hapa mpuuzi wa mbogamboga.
 
Back
Top Bottom