JBourne59
JF-Expert Member
- Jan 17, 2020
- 941
- 8,547
UPDATE
Simulizi hii ina misimu mitatu (three seasons) na zote zitakuwepo kwenye uzi huu huu.
1st season ina episodes 4 tu japo ndefu ndefu kiasi.
2nd season ipo post #90 na episodes zake ni fupi fupi...
3rd season #237
UTANGULIZI
Maisha baada ya kustaafu huwa yana ‘stress’ nyingi. Kujaribu kupunguza stress hizo nilifungua ‘account’ hii JF ili kujiburudisha na kuburudishwa. Account zangu nyingine JF zina ‘personality’ tofauti kabisa.
Michengesho (decoys) zipo kama kawaida ili kulinda nukta kuunganishwa.
HEKAHEKA UZEENI
Sehemu ya kwanza – KUSTAAFU UTUMISHI WA UMMA SI JAMBO LA GHAFLA.
Katika kazi za utumishi wa umma, wapo wanao staafu wakiwa na miaka arobaini na mitano na kuendelea, mimi nilibahatika kufanya kazi hadi miaka sitini na kustaafu kwa mujibu wa sheria. Kujifunza ‘hakwishi’, kuna karaha zake baada ya kustaafu hususani wakati wa kufuatilia stahiki zako. Angalau siku hizi utaratibu ni mzuri sana usumbufu umepunguwa kwa kiasi kikubwa.
Kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla, yampasa mtumishi yeyote aliyeajiriwa kuajiandaa na maisha baada ya kustaafu. Tumeshuhudia wengi baada ya kustaafu kuendelea Kwenda eneo la kazi na kukaa kupiga soga nk, hii hutokana na ama kufuatilia mambo yake ama kukosa sehemu muafaka ya Kwenda kwakuwa labda hakujiandaa na mahali ya Kwenda baada ya kustaafu.
Miaka 45 ni mtu mwenye nguvu bado, hivyo anaweza kufanya Maisha yaendelee kwa mtindo mwingine bila kuathirika na kazi alizozioea kazini, vivyo hivyo kwa miaka 50 ama 55 ama 60 na hata 65 bado mtu anaweza kujishughulisha na mambo ambayo yatamfanya asiwe ‘bored’
Mara nyingi kwa watumishi wengi maisha yao baada ya kustaafu huwa ni ya upweke, ‘kupigwa mizinga’ kutoka kwa ndugu na jamaa na usipokuwa makini utajikuta unapata magonjwa ya kisukari na moyo pasipo kutarajia kutokana na mtindo wa maisha utakao kuwa nao.
“…hela ya mafao ya kustaau siyo ya kujengea kaka…!” aliwahi kuniambia mzee mwenzangu mmoja aliyetangulia kustaafu.
“…hiyo hela ni ya kukutunza wewe, ni ya kufurahia maisha yako ya uzeeni hadi siku Mwenyezi Mungu atakapo kuchukuwa…”
“…ndugu na jamaa wengi watakuletea shida zao, sisemi usiwasaidie, lakini saidia kwa kiasi tu ili usiharibu fungu lako wala uhusiano wako na ndugu na jamaa, ikiwezekana tangaza hali mbaya ya uchumi kabisa ili wasiweke dhana kwamba una hela, singizia chochote kuepusha usumbufu, mwenzako yamenikuta sana…” Ni maneno yamzee mwenzangu mwingine ambaye yeye alitangulia kustaafu pia.
Sentesi ya ‘hela ya kustaafu ni ya kufurahia maisha..’ ndiyo iliyonifanya nianze kuandika simulizi hii.
Kama nilivyoserma awali, kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla yapaswa kujiandaa kwa kuwa na miradi midogo midogo wakati ukiwa bado katika utumishi. Hii ni kwa wote, watumishi wa umma na wa sekta binafsi. Anzisha mradi wowote wenye kukuingizia kipato hata kama ni kidogo ili mradi kiweze kukidhi mshahara wa anayesimamia, kutunza mtaji, kukuza mtaji na kujipatia faida kidogo. Hapa nazungumzia wale ambao kima chao cha mshahara ni cha chini. Kwa wale wenye vima vya juu nawashauri wafikirie kufanya miradi mikubwa yenye kuleta ajira kwa vijana na kutopeleka hela nje ya nchi, wekezeni humu humu nchini hiyo miradi yenu mikubwa kwa maana mzunguko wa fedha hizo zitabaki ndani. Sisemi msiwekeze nje ya nchi lakini nasema msisahau kuwekeza ndani kuwasaidia hawa vijana wetu wanaomaliza masomo yao kila mwaka.
Hebu niache haya mambo ya ushauri-nasihi usio rasmi maana kila mtu anajipangia mambo yake mwenyewe, lakini usisahau pia kuishi na mkeo / mmeo vizuri maana ukitangulia kustaafu kabla ya mwenza wako na haukuwa unaishi naye katika mahaba tarajia ‘stress’ za vijimambo vidogovidogo tu ambapo sasa vitakusanyika na kuwa kero.
nijikite sasa kwenye hii sentesi …”..hela baada ya kustaafu ni za kufurahia Maisha…”
Wakati na mbwela-mbwela kusubiria ‘fuba’ la mkupuo si nikapata mkataba fulani hivi kusaidia mambo fulani nchini DRC!. Ulikuwa ni mchongo wa miezi mitatu. Namshukuru sana yule jamaa aliyeniunganisha maana alikuwa anajuwa uwezo wangu katika fani ile kuhusiana na mchongo huo.
‘Paapu’, nikaambiwa niripoti Goma – Kivu ya kaskazini DRC tarehe fulani. Nikajiangalia mfukoni nikaona kuchukuwa flight hakunifai.
“…bora nipande basi kwa kuwahi wiki moja kabla ya tarehe husika…” nilijisemea moyoni.
Wakati huo Stendi ya Mbezi, “Magufuli Bus Terminal” ilikuwa bado haijaanza kutumika, hivyo nikatinga Ubungo bus terminal kuangalia usafiri maridhawa. Nilikuta kuna basi mbili za kampuni moja ambayo niliambiwa ni wazuri kwenye huduma ambazo zote zilikuwa zinaenda Kigali. Nikakata tiketi ya basi kubwa kama walivyokuwa wakiita wenyewe.
Kwakuwa huwa napenda kuona mbele ya basi kwenye lami, nilichaguwa siti ya nyuma ya dereva siyo upande wa dirishani lakini ingawaje palikuwa bado hapajachukuliwa. Sababu nyingine iliyonifanya kuchukuwa nafasi hiyo nili ile nafasi kati ya dereva na siti nyuma yake ni kubwa pa kuweza kunyoosha miguu na pia kuna kama meza fulani hivi mbele (fridge) hivyo kufanya paonekane ni sehemu muafaka kwangu kwa safari ndefu kama ile.
Siku ya safari nikafika mapema sana Ubungo bus terminal, moja kwa moja kwenye eneo ambalo basi husika lilikuwa linapakilia abiria, nilikuta baadhi ya abiria wakiwa tayari ndani ya basi ingawaje nilifika takribani nusu saa hivi kabla ya safari. Sikuwa na mizigo bali backpack Fulani hivi kubwa kiasi ambayo iliweza kubeba laptop yangu pamoja na nguo zangu chache ambazo nilidhani kwa kazi ya siku 90 ningeweza ‘kupiganisha’ bila kuhisi sina nguo za kubadilisha.
Kampuni ya basi ilikuwa inaitwa ‘utatu mtakatifu’, kwa kweli basi nililopanda walijitahidi sana kufanya liwe na hadhi yake mle ndani, viti vyenye vitambaa vya ngozi (synthentic leather), nafasi kubwa kati ya siti na siti, ila kwenye lugha za kuhudumia wateja walikuwa wanafeli sana, sijui ni kwa sababu ya kutojuwa Kiswahili vizuri ama nini. Hakika kwenye hili walikuwa wanafeli, siku hiyo kulikuwa na madereva wawili, mmoja Mtanzania na wa pili ni Mnyarwanda, na mhudumu tuliye safiri naye mmoja mwanume na mwingine ambaye alishukia njiani alikuwa ni wakala wao, akisindikiza gari.
Nilitulia kwenye kiti vizuri huku basi likiwa limekaribia kujaa kabisa abiria lakini kwenye kiti changu bado hapakuwa na abiria aliyekuja. Shingo nikiwa nimeinua juu kidogo kuangalia kwaya walizoweka kwenye runinga ya basi pale mbele mara nikasikia sauti ikiniambia…
“Excuse me, let me pass that is my seat..” alikuwa ni binti mrembo na kwa sura ile moja kwa moja nikajuwa huyu ni Mnyarwanda.
Nikampisha bila kusema neno, na alipokuwa ameketi sasa ikanibidi siti nibonyeze sehemu ili kuongeza nafasi ili tuenee vizuri maana si kwa ma ‘hips’ yale.
“Hujambo?” nilimsalimia na akaitikia kwa kichwa huku akiendelea na mambo yake mara kashika hiki mara kashika kile ili mradi alikuwa hatulii kama ana wasiwasi fulani hivi kama vile kuna jambo halijakamilika.
Macho nikarudisha kwenye runinga kuendelea kuburudika na kwaya za kisabato, ‘what a beautiful melody!’
Punde si punde mlango wa basi ukafungwa na tukawa kwenye foleni ya kutoka nje ya bus terminal. Ajabu ni kwamba vurugu za mabasi kugombania kutoka nje ya geti zilikuwepo licha ya utaratibu mzuri ambao uliwekwa na uongozi wa kituo na kusimamiwa na askari.
Baada ya chekecha chekecha ya hapa na pale hatimaye tukawa kwenye mstari ulionyooka sasa wa kutoka nje. Nikageuza shingo kuangalia nyuma, hakika basi lilikuwa limejaa na hakukuwa na mtu aliyesimama zaidi ya mhudumu mmoja na Yule msindikizaji ambao wote walisimama pale mlangoni, wakati huo tayari yule wakala msindikizaji alikuwa amesha maliza mambo ya ushuru wa getini nk.
===
Safari iliendelea hadi maeneo ya Mbezi Luis ambapo yule msindikizaji alikuwa ameshakamiliza zoezi lake la kukabidhi kila abiria tiketi ya mashine ingawaje tulikuwa na zile tiketi za karatasi. Tiketi hizi za mashine (POS) hazikuwa hizi zilizounganishwa na mifumo ya LATRA na TRA bali zilikuwa kwa ajili ya udhibiti wa kiofisi yao tu.
Niliangalia begi langu kwa mara nyingine, nikajiridhisha lipo salama haliwezi kumuangukia abiria wa jirani maana nililiweka kwenye kibebeo (carrier) cha upande wa kushoto wakati mimi nipo siti za upande wa kulia ili niweze kuliona muda wowote ninapotaka ingawaje watu wengine hupenda kuweka upande huo huo alipo kaa yeye tena juu sehemu aliyokaa.
Safari iliendelea, wakati huo video ilikuwa imezimwa na kufunguliwa radio (RFA) tukiendelea kupata habari. Kwenye hili la kelele za miziki, video za ndani ya basi walikuwa wamefanikiwa, maana hawakuwa wakifungulia kwa sauti za juu, ilikuwa sauti ya kadri tu ambapo hata ukiongea na simu kwa sauti ya chini bado mtasikilizana.
Basi lilitembea mwendo wa Serikali, ‘tatu bila, tano bila nane bila’ hadi tulivyofika Chalinze na misafara ya mabasi kuongozana na kukimbizana ikapungua na mabasi kuanza kumwaga moto. Kutoka Mbezi hadi Chalinze nadhani siku hiyo kulikuwa na fatiki kabambe ya ‘traffic police’ kwa maagizo ya kamanda wa wakati huo, maana kabla ya safari kulisikika tangazo pale Ubungo bus terminal kuwa madereva wote wakusanyike sehemu husika kwa ajili ya kuongea na Kamanda (alitajwa). Nadhani semina fupi ile iliwaingia hadi Chalinze tu, sijui madereva wa mabasi wana matatizo gani, kha!
Basi lilikuwa ni YUTONG, sijui namba ngapi ngapi lakini wenyewe wanasema ndio kubwa katika mfululizo wa wakati huo. Huko mbele ya safari ndio nikajuwa maana niliona ilivyokuwa inafunguka. Licha ya kuchezewa vts lakini pia nahisi ‘limiter’ ya spidi pia ilichezewa, si kwa mwendo ule baada ya kuvuka Rusumo border.
Chalinze hadi Moro basi lilitembea lakini ile kibongo bongo, minara ilikuwa inafanya kazi maana yule mhudumu muda wote alikuwa na simu sikioni na mkono mmoja ameweka juu ya dashboard, mara anapiga dashboard mara anainua kama vile anaita yani alikuwa anapata taarifa nje ya basi na yeye alifikisha ujumbe kwa dereva kwa kupiga dashboard, kuinua kiganja na kuita kwa kiganja.
Mwendo haukuwa hatarishi kiasi cha kuripoti kwa askari waliokuwa akiuliza sehemu za ukaguzi na dereva wala hakuwa mchafuzi wa overtake za ‘kubeti’ ila kwenye mwendokasi sehemu za hamsini hadi tulivyofika mbele kidogo ya Singida. Huko ilikuwa muda mwingi ni over 90kph.
Kabla ya kufika Morogoro, jirani yangu ambaye katika simulizi hii nitampa jina la Janeth, alikuwa ametulia, maana muda wote tangia Dar alikuwa kwenye simu akiongea mara akiandika jumbe za simu. Nikaanza kumsemesha sasa kwa Kiswahili ili kujuwa uwezo wake katika lugha hii adhimu, alikuwa anajibu kwa tabu sana ingawaje alifinyanga finyanga tukawa tunaelewana.
Kwa haraka haraka kutokana na maongezi ndani ya basi, nikajuwa mle ndani kuna Wabongo, Wanyarwanda, Warundi, Wakongo, wa Uganda na Wakenya. Pia kulikuwa kuna watu weupe wawili mmoja akiwa mwanamme, sijui ni Wazungu au Wamarekani lakini hawakuwa Waasia.
Janeth hakuwa mweupe wa rangi, bali maji ya kunde na aling’aa vyema kama ngozi yake ilivyokuwa ikionesha, alivaa ‘tracksuit’ na raba kama vile alikuwa ametoka kufanya mazoezi, nywele alisokota rasta bila kuunganisha nywele za bandia. Hakunizidi urefu, mana pale Chalinze tulipokuwa tunakunywa chai tuliteremka pamoja na kutembea pamoja kabla hatujaachana njia mimi nikielekea maliwatoni upande wa wanaume.
Kwakuwa mimi ni mpenda chai ya maziwa yenye kahawa, basi nilienda upade ule kwenye huduma hiyo na yeye Janeth wa sikumuona tena alipoelekea.
Kwenye jambo hili la kuwapa muda wa kutosha abiria wakati wa chakula, hawa jamaa nao walifaulu vizuri, maana mhudumu alipotangaza alisema tutatumia nusu saa kuchimba dawa pamoja na kupata chochote, tuzingatie namba ya basi maana yalikuwa mawili, baadaye sana ndio nikajuwa kuwa moja litaelekea Uganda na lile tulilopanda ndio litaelekea Kigali.
Kwakuwa siti yangu ilikuwa jirani na sikuwa nakaa dirishani, niliingia wa mwisho mwisho kwenye basi na kumkuta Janeth akiendelea kula nyama za kuchoma alizofungiwa kwenye bahasha fulani hivi ya khaki.
“Welcome nyama choma…” alinikaribisha huku akimaanisha nichukuwe msongo mmoja niendelee nao…
“Aaah, ahsante sana, unaitwa nani?” nilijibu huku moyoni nikikataa kuchukuwa nyama kwa ishara ya kuonesha nimetosheka (nimeshiba)
“Yaleyale ya kupewa chakula na usiyemjuwa wala kuona chakula kilipotoka mwisho wa siku unajikuta umeshaibiwa…” niliwaza.
Nikatoa ‘chewing gum’ za ‘mint’ na kuanza kutafuna ili kuweka kinywa changu katika hali ya kuanzisha maongezi ya kisafari safari.
“Karibu bublish…” nilinyoosha mkono na kumpatia kadhaa na akapokea kimya kimya na kuzihifadhi kwenye kimfuko kidogo kilichopo kwenye lile friji mbele ya siti zetu huku akiendelea kutafuna minofu ya mishikaki ya ng’ombe.
Safari ikaanza tena tukiitafuta mizani ya Mikese, mwendo mzuri, nane bila na uchafuzi wa speed kiasi maana dashboard nilikuwa naiona lakini ilikuwa haizidi 89kph. Pila nilikuwa na Garmin Drive 52 iliyoipata katika harakati za kutafuta ugali ambapo katika safari hii nilitarajia itanisaidia kule niendako ambako sikuwa na uhakika wa coverage ya internet.
Kelele za king’amuzi (vts) kilikuwa almost muda wote alipokuwa zaidi ya 85kph kinasikika kwa mbali sana, sijui waliweka kitu gani wale jamaa, maana kama sio mjuzi wala huwezi kuelewa ni kitu gani kinaendelea, dereva huyu Mtanzania alikuwa na nidhamu ya michoro ya makatazo ya kuovateki ila alikuwa ana ‘maintain maximum’ ya Latra muda mwingi, hii ilifanya tusiwe nje ya muda wa ratiba ya gari.
Janeth mkononi alikuwa amevaa kitu mama shanga hivi maarufu kama “culture” lakini ilikuwa na bendera ya Kenya.
“Wewe ni mkenya?” nilimuuliza huku nikiutolea macho mkono wake wa kushoto ambao ndio alikuwa amevaa hiyo shanga.
“No, Mnyrwanda” alijibu huku akitabasamu.
Nikachukuwa smartphone yangu, nikafungua playstore ili nidownload dictionary ya English – Kinyarwanda lakini haikunisaidia sana maana wakati huo bado haikuwa na maneno mengi.
“Do you speak English” nilimuuliza tena ili kama vipi tuhamier kwenye Kiingereza maana Kiswahili chake kilikuwa hakieleweki.
“Kidogo…” alijibu kisha akaendelea … “French and Kinyarwanda okay...”
Katika harakati za maisha sikubahatika kujifunza Kifaransa, bali niliyajuwa maneno machache sana maana rafiki yangu wa zamani sana, mototo wa Kihindi aitwaye Raani alinipatia kamusi ya Kifaransa kwa kiingereza lakini wala sikuwa na mzuka. Raani binti yule wa Kihindi urafiki wetu haukudumu kwa sababu ya Sue mototo wa Kispaniola ambaye naye pia wala hatukufika mbali, maana baada ya chuo tu miezi ishirini hivi baadaye mawasiliano yalikatika.
Alivyojibu kuwa kwenye Kifaransa na Kinyarwanda ndio yuko vizuri, basi sikuwa na chaguo lingine zaidi ya kuvumilia Kiswahili chake na kiingereza chake ingawaje kwenye kiingereza alikuwa yuko vizuri zaidi kuliko Kiswahili.
Hili ni jambo lingine la kushangaza, yani ukitoka Bongo kwenda Rwanda, hapo Rwanda wenyeji wanazungumza kilugha chao tu na Kifaransa, siyo wengi wazungumzao kiigereza. Ila ukivuka Rwanda kwenda Congo DR huko utakutana na Kiswahili cha aina yake, lakini angalau watu wanaelewana.
Kigali haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, lakini huko Goma ndiyo ilikuwa ‘fisrt time’. Niliuchangamkia huo mchongo ingawaje Hamida alinikataza nisiende kwa kuhofia hatari iliyopo ya vita baina ya majeshi ya Serikali na watu wanaojiita waasi.
“The first time when I saw you, I knew for sure you are Mnyarwanda…” nilisema.
“Why?” aliniuliza.
Hapo ndipo nikafunguka kuhusu jinsi sisi Wabongo tunavyowaona Wanyarwada. Nilimwambia kuhusu maumbile yao ya urefu, sura nyembamba, urembo wa asili, nyama za kutosha sehemu ambazo huwafanya wanaume wageuke nyuma kuangalia ili kuburudisha macho, nikaeleza weee mwishoe naye akaniambia kuwa hiyo dhani si asilimia mia sahihi, siyo Wanyarwanda wote warembo kama nilivyowapamba…
Eeee ni kweli nilimpamba sana ‘mixer’ ukweli na chumvi ili kuwasifia kama ilivyo kawaida ya wanaume.
Kwakuwa Rwanda haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, nilikuwa najuwa hawa warembo tunaowaona kwenye mitandao ni wachache tu, wanawake wa Kinyarwanda wapo kwa maumbile mbalimbali na sura tofauti wengi ni wa kawaida sana na tofauti kabisa na tunao waona hawa wa kwenye mitandao. Hata hivyo haiondoi ukweli kwamba wapo wanawake warembo wa sura na maumbile huko Rwanda. Tabia zao tu ndio zina ukakasi kiasi fulani juu ya kujiona wapo matawi ya juu sana, kuwa na ukatili uliojificha labda kutokana na historia yao nk.
“…Lakini sasa mbona umevaa bendera ya Kenya?” nilidadisi.
Hapa akafunguka kuwa yeye ni mfanyabiashara, ana duka la nguo za wanawake kwao Kigali na kabla hajajuwa machimbo ya Tanzania alikuwa akifungia mizigo yake Uganda na Kenya, na hiyo ‘bracelet’ aliyovaa aliipatia Kenya…
Mazungumzo ya kawaida yaliendelea kama ilivyo kawaida kwa abiria na abiria. Safari nayo ilisonga salama kabisa hadi tukafika Dodoma pale jirani na panapoitwa ‘four ways’, tukawa na ‘short break’ ya dakika kumi ya ajili ya kuchimba dawa kisha safari iliendelea hadi Singida baada ya mizani mbelembele kidogo gari ikaingia sehemu fulani kuna hoteli ambapo napo tulipata dakika ishirini za kuchimba dawa na kupata chochote kisha safari ikaendelea. Tulipokaribika Igunga giza fulani hivi lilianza kuingia, hadi tunapita mzunguko wa Nzega pale tayari dereva yuleyule tuliyetokanaye Dar akiwa anaendesha hadi muda huo aliwasha taa hafifu zilizowaka kwenye sakafu ya basi pembeni pembeni na kufanya mandhari kuwa nzuri sana ndani ya basi.
Awali nilidhani basi litanyoosha moja kwa moja hadi border ya Rusumo lakini kumbe hayapitilizi bali wanalala Kahama kisha asubuhi na mapema safari huendelea hadi boda.
“Have you made your reservation to pass your night at Kahama…” Janeth aliniuliza wakati gari ikiwa inakunja Tinde kuelekea Isaka.
Nilimjibu kuwa sijafanya chochote, si nitalala ndani ya basi!
“Please don’t sleep in the bus, you will get tired, and you won’t enjoy your looong journet from there to Kigali, its tiresome…” alisema Janeth na alikuwa anamaanisha. Nilijua hivyo siku ya pili baada ya kufika Rusumo.
“I don’t have enough cash with me…” nilitaka kujitetea akanikatisha…
“Don’t worry, I will pay for you and you will refund me when we reach border or Kigali…”
Sikumwambia kuwa mie pale mpita njia tu naelekea DRC. Nadhani alidhani namie ni mmoja wa wanaoelekea kwenye “sabasaba yao” (trade fair) maana tarehe hizo kulikuwa na maonesho ya kibiashara hapo Kigali iliyoanza kama siku mbili zilizopita na inayotarajiwa kuwepo kwa siku kadhaa zijazo.
“Why spend a lot of money! We can share the room…” nilichombeza huku nikiwa simaanishi.
“…Really!?” alihoji
“Why not!” nikajikuta tu neno limenitoka.
Mazungumzo yaliendelea na akaniambia yeye hufikia Gaprena Hotel. Nikatafuta review ya hotel hiyo harakaharaka kwenye simu nikaona ni zile wanazoita hotel kumbe ni lodge tu iliyochangamka. Anyway, ni Hotel. Sifa kuu aliniambia kuwa pako salama na ni karibu na stendi kuu pia gharama ni ndogo kulinganisha na hadhi ya hoteli yenyewe. Mimi wakati huo nimeshasoma review kadhaa na kupata picha halisi ya sehemu anayotarajia kufikia.
Tukaingia mizani Kahama na baada ya kutoka hapo mhudumu alitutangazia ratiba ya gari na kutupatia elimu maelekezo na tahadhari. Moja ya maelekezo aliyotoa ni kwamba basi halitoendelea na safri hadi kesho saa kumi na mbili asubuhi, hivyo anashauri abiria watafute lodge za kupumzika kwa watakaopenda kufanya hizo, na wale watakao amua kulala ndani ya basi wawe makini na mizigo yao ya ndani ya basi maana ulinzi wa mali iliyo ndani ya basi ni wa abiria husika.
“Muwe makini na mutu mugeni yanakuja ndani ya basi, hakuna abiria naingia usiku huu…” alimalizia yule mhudumu na Kiswahili chake kibovu.
Gari ikakunja kulia moja kwa moja hadi stendi kuu. Stendi ilikuwa imechangamka sana na ilikuwa ni majira ya saa tatu hivi usiku. Watu wengi, wauza vyakula mama lishe wengi huku wakikaribisha wateja, wapiga debe wa lodge pia wengi wakijitahidi kutafuta wateja, hakika Kahama palikuwa pamechangamka sana.
Wahudumu wa basi tulikuwa nao safarini wote waliondoka akaja wakala mkazi wa hapo ambaye alikuwa akisimamia ‘shoo’ bila shaka na walinzi wao pia walikuwepo ingawaje sikuwaona mara moja.
Abiria walikuwa wanajivuta sana kushuka mimi na Janeth tukiwemo. Nusu saa baadaye tuliamua kutembea kuelekea hoteli ambayo abiria mwenzangu alikuwa ameweka nafasi. Bajaj, tax na bodaboda zilikuwepo, lakini tuliamua kunyoosha miguu baada ya safari ndefu.
Tulivyofika pale mapokezi tulikaribishwa kwa bashasha lakini ‘walinikata maini’ nilipoulizia kama kuna chumba…
“Ishi, kwani hampo pamoja!...” aling’aka yule mhudumu
“Vyumba vyote vimejaa, basi ngoja nikupeleke hoteli ya jirani na hapa, pale unaweza kupata ila bei ipo juu kidogo…” aliongea yule mhudumu kwa lafudhi ya kisukuma.
Janeth akaingilia kati…
“Lets share as you said, no problem… are you going to swallow me!?”
Yani hapa angalau kwenye uandishi inabidi nikinyooshe kidogo hivi vilugha vya watu maana jinsi alivyokuwa akiongea Janeth unaweza ukawa unacheka tu kila mara.
“Well, its okay, lets share the room and I promise will not swallow you…” tukawa tunacheka huku tukielekea chumba husika maana mwenzangu pale inaonekana ni mwenyeji.
======
INAENDELEA…
Simulizi hii ina misimu mitatu (three seasons) na zote zitakuwepo kwenye uzi huu huu.
1st season ina episodes 4 tu japo ndefu ndefu kiasi.
2nd season ipo post #90 na episodes zake ni fupi fupi...
3rd season #237
UTANGULIZI
Maisha baada ya kustaafu huwa yana ‘stress’ nyingi. Kujaribu kupunguza stress hizo nilifungua ‘account’ hii JF ili kujiburudisha na kuburudishwa. Account zangu nyingine JF zina ‘personality’ tofauti kabisa.
Michengesho (decoys) zipo kama kawaida ili kulinda nukta kuunganishwa.
HEKAHEKA UZEENI
Sehemu ya kwanza – KUSTAAFU UTUMISHI WA UMMA SI JAMBO LA GHAFLA.
Katika kazi za utumishi wa umma, wapo wanao staafu wakiwa na miaka arobaini na mitano na kuendelea, mimi nilibahatika kufanya kazi hadi miaka sitini na kustaafu kwa mujibu wa sheria. Kujifunza ‘hakwishi’, kuna karaha zake baada ya kustaafu hususani wakati wa kufuatilia stahiki zako. Angalau siku hizi utaratibu ni mzuri sana usumbufu umepunguwa kwa kiasi kikubwa.
Kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla, yampasa mtumishi yeyote aliyeajiriwa kuajiandaa na maisha baada ya kustaafu. Tumeshuhudia wengi baada ya kustaafu kuendelea Kwenda eneo la kazi na kukaa kupiga soga nk, hii hutokana na ama kufuatilia mambo yake ama kukosa sehemu muafaka ya Kwenda kwakuwa labda hakujiandaa na mahali ya Kwenda baada ya kustaafu.
Miaka 45 ni mtu mwenye nguvu bado, hivyo anaweza kufanya Maisha yaendelee kwa mtindo mwingine bila kuathirika na kazi alizozioea kazini, vivyo hivyo kwa miaka 50 ama 55 ama 60 na hata 65 bado mtu anaweza kujishughulisha na mambo ambayo yatamfanya asiwe ‘bored’
Mara nyingi kwa watumishi wengi maisha yao baada ya kustaafu huwa ni ya upweke, ‘kupigwa mizinga’ kutoka kwa ndugu na jamaa na usipokuwa makini utajikuta unapata magonjwa ya kisukari na moyo pasipo kutarajia kutokana na mtindo wa maisha utakao kuwa nao.
“…hela ya mafao ya kustaau siyo ya kujengea kaka…!” aliwahi kuniambia mzee mwenzangu mmoja aliyetangulia kustaafu.
“…hiyo hela ni ya kukutunza wewe, ni ya kufurahia maisha yako ya uzeeni hadi siku Mwenyezi Mungu atakapo kuchukuwa…”
“…ndugu na jamaa wengi watakuletea shida zao, sisemi usiwasaidie, lakini saidia kwa kiasi tu ili usiharibu fungu lako wala uhusiano wako na ndugu na jamaa, ikiwezekana tangaza hali mbaya ya uchumi kabisa ili wasiweke dhana kwamba una hela, singizia chochote kuepusha usumbufu, mwenzako yamenikuta sana…” Ni maneno yamzee mwenzangu mwingine ambaye yeye alitangulia kustaafu pia.
Sentesi ya ‘hela ya kustaafu ni ya kufurahia maisha..’ ndiyo iliyonifanya nianze kuandika simulizi hii.
Kama nilivyoserma awali, kwakuwa kustaafu ‘hakukuji’ ghafla yapaswa kujiandaa kwa kuwa na miradi midogo midogo wakati ukiwa bado katika utumishi. Hii ni kwa wote, watumishi wa umma na wa sekta binafsi. Anzisha mradi wowote wenye kukuingizia kipato hata kama ni kidogo ili mradi kiweze kukidhi mshahara wa anayesimamia, kutunza mtaji, kukuza mtaji na kujipatia faida kidogo. Hapa nazungumzia wale ambao kima chao cha mshahara ni cha chini. Kwa wale wenye vima vya juu nawashauri wafikirie kufanya miradi mikubwa yenye kuleta ajira kwa vijana na kutopeleka hela nje ya nchi, wekezeni humu humu nchini hiyo miradi yenu mikubwa kwa maana mzunguko wa fedha hizo zitabaki ndani. Sisemi msiwekeze nje ya nchi lakini nasema msisahau kuwekeza ndani kuwasaidia hawa vijana wetu wanaomaliza masomo yao kila mwaka.
Hebu niache haya mambo ya ushauri-nasihi usio rasmi maana kila mtu anajipangia mambo yake mwenyewe, lakini usisahau pia kuishi na mkeo / mmeo vizuri maana ukitangulia kustaafu kabla ya mwenza wako na haukuwa unaishi naye katika mahaba tarajia ‘stress’ za vijimambo vidogovidogo tu ambapo sasa vitakusanyika na kuwa kero.
nijikite sasa kwenye hii sentesi …”..hela baada ya kustaafu ni za kufurahia Maisha…”
Wakati na mbwela-mbwela kusubiria ‘fuba’ la mkupuo si nikapata mkataba fulani hivi kusaidia mambo fulani nchini DRC!. Ulikuwa ni mchongo wa miezi mitatu. Namshukuru sana yule jamaa aliyeniunganisha maana alikuwa anajuwa uwezo wangu katika fani ile kuhusiana na mchongo huo.
‘Paapu’, nikaambiwa niripoti Goma – Kivu ya kaskazini DRC tarehe fulani. Nikajiangalia mfukoni nikaona kuchukuwa flight hakunifai.
“…bora nipande basi kwa kuwahi wiki moja kabla ya tarehe husika…” nilijisemea moyoni.
Wakati huo Stendi ya Mbezi, “Magufuli Bus Terminal” ilikuwa bado haijaanza kutumika, hivyo nikatinga Ubungo bus terminal kuangalia usafiri maridhawa. Nilikuta kuna basi mbili za kampuni moja ambayo niliambiwa ni wazuri kwenye huduma ambazo zote zilikuwa zinaenda Kigali. Nikakata tiketi ya basi kubwa kama walivyokuwa wakiita wenyewe.
Kwakuwa huwa napenda kuona mbele ya basi kwenye lami, nilichaguwa siti ya nyuma ya dereva siyo upande wa dirishani lakini ingawaje palikuwa bado hapajachukuliwa. Sababu nyingine iliyonifanya kuchukuwa nafasi hiyo nili ile nafasi kati ya dereva na siti nyuma yake ni kubwa pa kuweza kunyoosha miguu na pia kuna kama meza fulani hivi mbele (fridge) hivyo kufanya paonekane ni sehemu muafaka kwangu kwa safari ndefu kama ile.
Siku ya safari nikafika mapema sana Ubungo bus terminal, moja kwa moja kwenye eneo ambalo basi husika lilikuwa linapakilia abiria, nilikuta baadhi ya abiria wakiwa tayari ndani ya basi ingawaje nilifika takribani nusu saa hivi kabla ya safari. Sikuwa na mizigo bali backpack Fulani hivi kubwa kiasi ambayo iliweza kubeba laptop yangu pamoja na nguo zangu chache ambazo nilidhani kwa kazi ya siku 90 ningeweza ‘kupiganisha’ bila kuhisi sina nguo za kubadilisha.
Kampuni ya basi ilikuwa inaitwa ‘utatu mtakatifu’, kwa kweli basi nililopanda walijitahidi sana kufanya liwe na hadhi yake mle ndani, viti vyenye vitambaa vya ngozi (synthentic leather), nafasi kubwa kati ya siti na siti, ila kwenye lugha za kuhudumia wateja walikuwa wanafeli sana, sijui ni kwa sababu ya kutojuwa Kiswahili vizuri ama nini. Hakika kwenye hili walikuwa wanafeli, siku hiyo kulikuwa na madereva wawili, mmoja Mtanzania na wa pili ni Mnyarwanda, na mhudumu tuliye safiri naye mmoja mwanume na mwingine ambaye alishukia njiani alikuwa ni wakala wao, akisindikiza gari.
Nilitulia kwenye kiti vizuri huku basi likiwa limekaribia kujaa kabisa abiria lakini kwenye kiti changu bado hapakuwa na abiria aliyekuja. Shingo nikiwa nimeinua juu kidogo kuangalia kwaya walizoweka kwenye runinga ya basi pale mbele mara nikasikia sauti ikiniambia…
“Excuse me, let me pass that is my seat..” alikuwa ni binti mrembo na kwa sura ile moja kwa moja nikajuwa huyu ni Mnyarwanda.
Nikampisha bila kusema neno, na alipokuwa ameketi sasa ikanibidi siti nibonyeze sehemu ili kuongeza nafasi ili tuenee vizuri maana si kwa ma ‘hips’ yale.
“Hujambo?” nilimsalimia na akaitikia kwa kichwa huku akiendelea na mambo yake mara kashika hiki mara kashika kile ili mradi alikuwa hatulii kama ana wasiwasi fulani hivi kama vile kuna jambo halijakamilika.
Macho nikarudisha kwenye runinga kuendelea kuburudika na kwaya za kisabato, ‘what a beautiful melody!’
Punde si punde mlango wa basi ukafungwa na tukawa kwenye foleni ya kutoka nje ya bus terminal. Ajabu ni kwamba vurugu za mabasi kugombania kutoka nje ya geti zilikuwepo licha ya utaratibu mzuri ambao uliwekwa na uongozi wa kituo na kusimamiwa na askari.
Baada ya chekecha chekecha ya hapa na pale hatimaye tukawa kwenye mstari ulionyooka sasa wa kutoka nje. Nikageuza shingo kuangalia nyuma, hakika basi lilikuwa limejaa na hakukuwa na mtu aliyesimama zaidi ya mhudumu mmoja na Yule msindikizaji ambao wote walisimama pale mlangoni, wakati huo tayari yule wakala msindikizaji alikuwa amesha maliza mambo ya ushuru wa getini nk.
===
Safari iliendelea hadi maeneo ya Mbezi Luis ambapo yule msindikizaji alikuwa ameshakamiliza zoezi lake la kukabidhi kila abiria tiketi ya mashine ingawaje tulikuwa na zile tiketi za karatasi. Tiketi hizi za mashine (POS) hazikuwa hizi zilizounganishwa na mifumo ya LATRA na TRA bali zilikuwa kwa ajili ya udhibiti wa kiofisi yao tu.
Niliangalia begi langu kwa mara nyingine, nikajiridhisha lipo salama haliwezi kumuangukia abiria wa jirani maana nililiweka kwenye kibebeo (carrier) cha upande wa kushoto wakati mimi nipo siti za upande wa kulia ili niweze kuliona muda wowote ninapotaka ingawaje watu wengine hupenda kuweka upande huo huo alipo kaa yeye tena juu sehemu aliyokaa.
Safari iliendelea, wakati huo video ilikuwa imezimwa na kufunguliwa radio (RFA) tukiendelea kupata habari. Kwenye hili la kelele za miziki, video za ndani ya basi walikuwa wamefanikiwa, maana hawakuwa wakifungulia kwa sauti za juu, ilikuwa sauti ya kadri tu ambapo hata ukiongea na simu kwa sauti ya chini bado mtasikilizana.
Basi lilitembea mwendo wa Serikali, ‘tatu bila, tano bila nane bila’ hadi tulivyofika Chalinze na misafara ya mabasi kuongozana na kukimbizana ikapungua na mabasi kuanza kumwaga moto. Kutoka Mbezi hadi Chalinze nadhani siku hiyo kulikuwa na fatiki kabambe ya ‘traffic police’ kwa maagizo ya kamanda wa wakati huo, maana kabla ya safari kulisikika tangazo pale Ubungo bus terminal kuwa madereva wote wakusanyike sehemu husika kwa ajili ya kuongea na Kamanda (alitajwa). Nadhani semina fupi ile iliwaingia hadi Chalinze tu, sijui madereva wa mabasi wana matatizo gani, kha!
Basi lilikuwa ni YUTONG, sijui namba ngapi ngapi lakini wenyewe wanasema ndio kubwa katika mfululizo wa wakati huo. Huko mbele ya safari ndio nikajuwa maana niliona ilivyokuwa inafunguka. Licha ya kuchezewa vts lakini pia nahisi ‘limiter’ ya spidi pia ilichezewa, si kwa mwendo ule baada ya kuvuka Rusumo border.
Chalinze hadi Moro basi lilitembea lakini ile kibongo bongo, minara ilikuwa inafanya kazi maana yule mhudumu muda wote alikuwa na simu sikioni na mkono mmoja ameweka juu ya dashboard, mara anapiga dashboard mara anainua kama vile anaita yani alikuwa anapata taarifa nje ya basi na yeye alifikisha ujumbe kwa dereva kwa kupiga dashboard, kuinua kiganja na kuita kwa kiganja.
Mwendo haukuwa hatarishi kiasi cha kuripoti kwa askari waliokuwa akiuliza sehemu za ukaguzi na dereva wala hakuwa mchafuzi wa overtake za ‘kubeti’ ila kwenye mwendokasi sehemu za hamsini hadi tulivyofika mbele kidogo ya Singida. Huko ilikuwa muda mwingi ni over 90kph.
Kabla ya kufika Morogoro, jirani yangu ambaye katika simulizi hii nitampa jina la Janeth, alikuwa ametulia, maana muda wote tangia Dar alikuwa kwenye simu akiongea mara akiandika jumbe za simu. Nikaanza kumsemesha sasa kwa Kiswahili ili kujuwa uwezo wake katika lugha hii adhimu, alikuwa anajibu kwa tabu sana ingawaje alifinyanga finyanga tukawa tunaelewana.
Kwa haraka haraka kutokana na maongezi ndani ya basi, nikajuwa mle ndani kuna Wabongo, Wanyarwanda, Warundi, Wakongo, wa Uganda na Wakenya. Pia kulikuwa kuna watu weupe wawili mmoja akiwa mwanamme, sijui ni Wazungu au Wamarekani lakini hawakuwa Waasia.
Janeth hakuwa mweupe wa rangi, bali maji ya kunde na aling’aa vyema kama ngozi yake ilivyokuwa ikionesha, alivaa ‘tracksuit’ na raba kama vile alikuwa ametoka kufanya mazoezi, nywele alisokota rasta bila kuunganisha nywele za bandia. Hakunizidi urefu, mana pale Chalinze tulipokuwa tunakunywa chai tuliteremka pamoja na kutembea pamoja kabla hatujaachana njia mimi nikielekea maliwatoni upande wa wanaume.
Kwakuwa mimi ni mpenda chai ya maziwa yenye kahawa, basi nilienda upade ule kwenye huduma hiyo na yeye Janeth wa sikumuona tena alipoelekea.
Kwenye jambo hili la kuwapa muda wa kutosha abiria wakati wa chakula, hawa jamaa nao walifaulu vizuri, maana mhudumu alipotangaza alisema tutatumia nusu saa kuchimba dawa pamoja na kupata chochote, tuzingatie namba ya basi maana yalikuwa mawili, baadaye sana ndio nikajuwa kuwa moja litaelekea Uganda na lile tulilopanda ndio litaelekea Kigali.
Kwakuwa siti yangu ilikuwa jirani na sikuwa nakaa dirishani, niliingia wa mwisho mwisho kwenye basi na kumkuta Janeth akiendelea kula nyama za kuchoma alizofungiwa kwenye bahasha fulani hivi ya khaki.
“Welcome nyama choma…” alinikaribisha huku akimaanisha nichukuwe msongo mmoja niendelee nao…
“Aaah, ahsante sana, unaitwa nani?” nilijibu huku moyoni nikikataa kuchukuwa nyama kwa ishara ya kuonesha nimetosheka (nimeshiba)
“Yaleyale ya kupewa chakula na usiyemjuwa wala kuona chakula kilipotoka mwisho wa siku unajikuta umeshaibiwa…” niliwaza.
Nikatoa ‘chewing gum’ za ‘mint’ na kuanza kutafuna ili kuweka kinywa changu katika hali ya kuanzisha maongezi ya kisafari safari.
“Karibu bublish…” nilinyoosha mkono na kumpatia kadhaa na akapokea kimya kimya na kuzihifadhi kwenye kimfuko kidogo kilichopo kwenye lile friji mbele ya siti zetu huku akiendelea kutafuna minofu ya mishikaki ya ng’ombe.
Safari ikaanza tena tukiitafuta mizani ya Mikese, mwendo mzuri, nane bila na uchafuzi wa speed kiasi maana dashboard nilikuwa naiona lakini ilikuwa haizidi 89kph. Pila nilikuwa na Garmin Drive 52 iliyoipata katika harakati za kutafuta ugali ambapo katika safari hii nilitarajia itanisaidia kule niendako ambako sikuwa na uhakika wa coverage ya internet.
Kelele za king’amuzi (vts) kilikuwa almost muda wote alipokuwa zaidi ya 85kph kinasikika kwa mbali sana, sijui waliweka kitu gani wale jamaa, maana kama sio mjuzi wala huwezi kuelewa ni kitu gani kinaendelea, dereva huyu Mtanzania alikuwa na nidhamu ya michoro ya makatazo ya kuovateki ila alikuwa ana ‘maintain maximum’ ya Latra muda mwingi, hii ilifanya tusiwe nje ya muda wa ratiba ya gari.
Janeth mkononi alikuwa amevaa kitu mama shanga hivi maarufu kama “culture” lakini ilikuwa na bendera ya Kenya.
“Wewe ni mkenya?” nilimuuliza huku nikiutolea macho mkono wake wa kushoto ambao ndio alikuwa amevaa hiyo shanga.
“No, Mnyrwanda” alijibu huku akitabasamu.
Nikachukuwa smartphone yangu, nikafungua playstore ili nidownload dictionary ya English – Kinyarwanda lakini haikunisaidia sana maana wakati huo bado haikuwa na maneno mengi.
“Do you speak English” nilimuuliza tena ili kama vipi tuhamier kwenye Kiingereza maana Kiswahili chake kilikuwa hakieleweki.
“Kidogo…” alijibu kisha akaendelea … “French and Kinyarwanda okay...”
Katika harakati za maisha sikubahatika kujifunza Kifaransa, bali niliyajuwa maneno machache sana maana rafiki yangu wa zamani sana, mototo wa Kihindi aitwaye Raani alinipatia kamusi ya Kifaransa kwa kiingereza lakini wala sikuwa na mzuka. Raani binti yule wa Kihindi urafiki wetu haukudumu kwa sababu ya Sue mototo wa Kispaniola ambaye naye pia wala hatukufika mbali, maana baada ya chuo tu miezi ishirini hivi baadaye mawasiliano yalikatika.
Alivyojibu kuwa kwenye Kifaransa na Kinyarwanda ndio yuko vizuri, basi sikuwa na chaguo lingine zaidi ya kuvumilia Kiswahili chake na kiingereza chake ingawaje kwenye kiingereza alikuwa yuko vizuri zaidi kuliko Kiswahili.
Hili ni jambo lingine la kushangaza, yani ukitoka Bongo kwenda Rwanda, hapo Rwanda wenyeji wanazungumza kilugha chao tu na Kifaransa, siyo wengi wazungumzao kiigereza. Ila ukivuka Rwanda kwenda Congo DR huko utakutana na Kiswahili cha aina yake, lakini angalau watu wanaelewana.
Kigali haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, lakini huko Goma ndiyo ilikuwa ‘fisrt time’. Niliuchangamkia huo mchongo ingawaje Hamida alinikataza nisiende kwa kuhofia hatari iliyopo ya vita baina ya majeshi ya Serikali na watu wanaojiita waasi.
“The first time when I saw you, I knew for sure you are Mnyarwanda…” nilisema.
“Why?” aliniuliza.
Hapo ndipo nikafunguka kuhusu jinsi sisi Wabongo tunavyowaona Wanyarwada. Nilimwambia kuhusu maumbile yao ya urefu, sura nyembamba, urembo wa asili, nyama za kutosha sehemu ambazo huwafanya wanaume wageuke nyuma kuangalia ili kuburudisha macho, nikaeleza weee mwishoe naye akaniambia kuwa hiyo dhani si asilimia mia sahihi, siyo Wanyarwanda wote warembo kama nilivyowapamba…
Eeee ni kweli nilimpamba sana ‘mixer’ ukweli na chumvi ili kuwasifia kama ilivyo kawaida ya wanaume.
Kwakuwa Rwanda haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda, nilikuwa najuwa hawa warembo tunaowaona kwenye mitandao ni wachache tu, wanawake wa Kinyarwanda wapo kwa maumbile mbalimbali na sura tofauti wengi ni wa kawaida sana na tofauti kabisa na tunao waona hawa wa kwenye mitandao. Hata hivyo haiondoi ukweli kwamba wapo wanawake warembo wa sura na maumbile huko Rwanda. Tabia zao tu ndio zina ukakasi kiasi fulani juu ya kujiona wapo matawi ya juu sana, kuwa na ukatili uliojificha labda kutokana na historia yao nk.
“…Lakini sasa mbona umevaa bendera ya Kenya?” nilidadisi.
Hapa akafunguka kuwa yeye ni mfanyabiashara, ana duka la nguo za wanawake kwao Kigali na kabla hajajuwa machimbo ya Tanzania alikuwa akifungia mizigo yake Uganda na Kenya, na hiyo ‘bracelet’ aliyovaa aliipatia Kenya…
Mazungumzo ya kawaida yaliendelea kama ilivyo kawaida kwa abiria na abiria. Safari nayo ilisonga salama kabisa hadi tukafika Dodoma pale jirani na panapoitwa ‘four ways’, tukawa na ‘short break’ ya dakika kumi ya ajili ya kuchimba dawa kisha safari iliendelea hadi Singida baada ya mizani mbelembele kidogo gari ikaingia sehemu fulani kuna hoteli ambapo napo tulipata dakika ishirini za kuchimba dawa na kupata chochote kisha safari ikaendelea. Tulipokaribika Igunga giza fulani hivi lilianza kuingia, hadi tunapita mzunguko wa Nzega pale tayari dereva yuleyule tuliyetokanaye Dar akiwa anaendesha hadi muda huo aliwasha taa hafifu zilizowaka kwenye sakafu ya basi pembeni pembeni na kufanya mandhari kuwa nzuri sana ndani ya basi.
Awali nilidhani basi litanyoosha moja kwa moja hadi border ya Rusumo lakini kumbe hayapitilizi bali wanalala Kahama kisha asubuhi na mapema safari huendelea hadi boda.
“Have you made your reservation to pass your night at Kahama…” Janeth aliniuliza wakati gari ikiwa inakunja Tinde kuelekea Isaka.
Nilimjibu kuwa sijafanya chochote, si nitalala ndani ya basi!
“Please don’t sleep in the bus, you will get tired, and you won’t enjoy your looong journet from there to Kigali, its tiresome…” alisema Janeth na alikuwa anamaanisha. Nilijua hivyo siku ya pili baada ya kufika Rusumo.
“I don’t have enough cash with me…” nilitaka kujitetea akanikatisha…
“Don’t worry, I will pay for you and you will refund me when we reach border or Kigali…”
Sikumwambia kuwa mie pale mpita njia tu naelekea DRC. Nadhani alidhani namie ni mmoja wa wanaoelekea kwenye “sabasaba yao” (trade fair) maana tarehe hizo kulikuwa na maonesho ya kibiashara hapo Kigali iliyoanza kama siku mbili zilizopita na inayotarajiwa kuwepo kwa siku kadhaa zijazo.
“Why spend a lot of money! We can share the room…” nilichombeza huku nikiwa simaanishi.
“…Really!?” alihoji
“Why not!” nikajikuta tu neno limenitoka.
Mazungumzo yaliendelea na akaniambia yeye hufikia Gaprena Hotel. Nikatafuta review ya hotel hiyo harakaharaka kwenye simu nikaona ni zile wanazoita hotel kumbe ni lodge tu iliyochangamka. Anyway, ni Hotel. Sifa kuu aliniambia kuwa pako salama na ni karibu na stendi kuu pia gharama ni ndogo kulinganisha na hadhi ya hoteli yenyewe. Mimi wakati huo nimeshasoma review kadhaa na kupata picha halisi ya sehemu anayotarajia kufikia.
Tukaingia mizani Kahama na baada ya kutoka hapo mhudumu alitutangazia ratiba ya gari na kutupatia elimu maelekezo na tahadhari. Moja ya maelekezo aliyotoa ni kwamba basi halitoendelea na safri hadi kesho saa kumi na mbili asubuhi, hivyo anashauri abiria watafute lodge za kupumzika kwa watakaopenda kufanya hizo, na wale watakao amua kulala ndani ya basi wawe makini na mizigo yao ya ndani ya basi maana ulinzi wa mali iliyo ndani ya basi ni wa abiria husika.
“Muwe makini na mutu mugeni yanakuja ndani ya basi, hakuna abiria naingia usiku huu…” alimalizia yule mhudumu na Kiswahili chake kibovu.
Gari ikakunja kulia moja kwa moja hadi stendi kuu. Stendi ilikuwa imechangamka sana na ilikuwa ni majira ya saa tatu hivi usiku. Watu wengi, wauza vyakula mama lishe wengi huku wakikaribisha wateja, wapiga debe wa lodge pia wengi wakijitahidi kutafuta wateja, hakika Kahama palikuwa pamechangamka sana.
Wahudumu wa basi tulikuwa nao safarini wote waliondoka akaja wakala mkazi wa hapo ambaye alikuwa akisimamia ‘shoo’ bila shaka na walinzi wao pia walikuwepo ingawaje sikuwaona mara moja.
Abiria walikuwa wanajivuta sana kushuka mimi na Janeth tukiwemo. Nusu saa baadaye tuliamua kutembea kuelekea hoteli ambayo abiria mwenzangu alikuwa ameweka nafasi. Bajaj, tax na bodaboda zilikuwepo, lakini tuliamua kunyoosha miguu baada ya safari ndefu.
Tulivyofika pale mapokezi tulikaribishwa kwa bashasha lakini ‘walinikata maini’ nilipoulizia kama kuna chumba…
“Ishi, kwani hampo pamoja!...” aling’aka yule mhudumu
“Vyumba vyote vimejaa, basi ngoja nikupeleke hoteli ya jirani na hapa, pale unaweza kupata ila bei ipo juu kidogo…” aliongea yule mhudumu kwa lafudhi ya kisukuma.
Janeth akaingilia kati…
“Lets share as you said, no problem… are you going to swallow me!?”
Yani hapa angalau kwenye uandishi inabidi nikinyooshe kidogo hivi vilugha vya watu maana jinsi alivyokuwa akiongea Janeth unaweza ukawa unacheka tu kila mara.
“Well, its okay, lets share the room and I promise will not swallow you…” tukawa tunacheka huku tukielekea chumba husika maana mwenzangu pale inaonekana ni mwenyeji.
======
INAENDELEA…