Kula tunda kimasihara kunavyoigarimu ndoa yangu

Kula tunda kimasihara kunavyoigarimu ndoa yangu

Mkuu hapa itaonekana kama ukatili lakini ni bora ukamlee mtoto wa single mama aliefikisha mwaka mmoja kuliko huyo mtoto wa chini ya mwaka wa shemeji yako.

Ngoja nikuulize umezaa watoto na huyo mkeo?
Mjamwepesi now
 
Mjamwepesi now
Mkeo kama huyo mtarajiwa ndio mtoto wa kwanza hajui kiuhalisia mzigo anao ubeba wa kulea kichanga.
Tena vichanga viwili.
Ukikubali huo mzigo ambao sio wa lazima ni starehe au uzembe wa shemejio utatukumbuka tunao kuonya sasa kuto kubali huo mzigo.
Najua nitaonekana katili hapa, lakini huo muziki unakuja kuathiri hadi malezi ya mtoto wako mchanga ajae.
Ukifanya masiala hili sakata lako utavuruga familia yako au unakuja kumtesa mtoto wako na kuja kupoteza wasaa wako na mkeo sababu ya kuwa busy na malezi ya mtoto ambae si wako na wazazi wake wote wapo hai na sio walemavu.
 
Mwambie mkeo na ndugu zake huyo mtoto wako wewe ndio baba yake, na huyo mtoto wa shemeji yako ana baba yake hai na mama yake hai.
Shule ingekuwa kipaumbele chake hasingeshika mimba wakati kuna njia kibao za kuzuwia mimba.
Mwambie kulea mtoto wake ni muhimu na hakuna kuhairisha lakini kusoma unaweza kuhairisha hadi mwaka au miaka mingine.
 
bro uko sahihi kabisa....ila ulikosea kumpiga....hapo tuuu....kwanza wewe ni jasiri....ulimweleza mkeo kuhusu mchepuko....ukaamua kumleta kwako,,,,...wanawake siku zote wana kisasi......na hasa akigundua ulichepuka....wewe ulimdhibitishia hilo......linapokuja suala la shemeji yako kuacha kichanga........fukuza mbali......huyo mie ningemfukuza toka akiwa mjamzito......mwanaume lazima uwe wa KIUME......pambafu zake...wacha akae kwao akili mpya ziote......fanya kazi kwa bidii.....kuwa karibu sana na huyo dogo uliyempata kwa zinaa....maana mkeo hapo ndipo atapalenga....pambana...umeshasajili line....????
 
Kifupi tu wamekuonea na wataendelea kukuonea kama hutachukua tahadhari mapema. Kuachiwa mtoto wa mwezi mmoja ni upuuzi wa kiwango cha lami!! Nakushauri ndugu yangu kataa huyo mtoto, shemeji aende shule na mwanae kwani wakati anamzaa hakujua? Nimeshikwa na hasira ghafla aiseeeeee!

Kwani humu hakuna wale kinamama wenye watoto wa kuime tuunde chama chetu tutetee watoto wetu? 😡😡😡😡😡😡😡
 
Kuna mtoto wa mdogo wangu wa kike nilikuwa nalea vizuri sana na sikuwahi mjua baba yake hata kidogo, lakini Mungu si athumani siku moja nipo kilwa road pub na wanangu nashangaa dogo anamkimbilia jamaa flani ana bonge la tumbo huku akiita baba baba baba, nilishangaa sana ikabidi nimfate yule mtoto nikijua ananitia aibu sasa ile nimefika kwenye meza namchukua naona jamaa alivyofanana na kale ka-anko aiseee fotokopi kabisa.
Jamaa akanisalimia, habari yako bwana shemeji karibu tukae wote hapa mimi leo sina kampani. Aisee nikamkabidhi mwanae palepale tena bila hata kumpigia mama yake(dada yangu).
Iliniuma sana kuona mateso niliyoyapata mimi na mke wangu kumlea yule mtoto huku wanangu nikiwapunguzia haki zao za kusoma shule nzuri ili wawe sambamba na ndugu yao(binamu yao) kumbe baba wa mtoto yupo na anajiweza kiuchumi kunizidi hata mimi na isiishie hapo kumbe mtoto huwa anapelekwa kwa baba yake na mama yake kwa kujiiba dooooh!

Sent using mazonge yamezidi
 
Aishi haina shida, umuone mkeo atakavyofanya wewe usijiguse, mwanao mlete kwangu au mpeleke kwa shangazi yake yaani dada yako
 
G.Jacob,
Duu hii nayo kali.
Dada zetu wakati mwingine wanatuumiza hasa wakijua kuna mtu atawabebea mzigo wao.
 
Vichapo vingi wanavyopata wake zetu hutokana na mdomo! Mwanamke akiona anapokukwaza kwa maneno hukwaziki, huongeza ukali wa maneno na kuongeza sauti ili udharirike... Hapo ndo mikono ya mwanaume hunyanyuka yenyewe na kufanya kazi yake ya kichapo bila kutumwa na ubongo. Ndo maana baada ya kichapo wanaume wengi hujutia kuwapiga wenzi wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi kumbe wanawake wengi wapo hivi me nilidhani niwangu2 ndio anatabia zakuniletea mdomomdomo. Bahati yake kumbe wengi wao wapo hivi nilikuwa nafikiria kumuacha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom