Kuhusu kero za Muungano, Zanzibar wanapaswa kutumia nafasi ya uraisi wa Samia kuweka msukumo wa kupata Katiba mpya, la sivyo imekula kwao!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Yaani hapa wala sihitaji kuweka maelezo mengi. Tunapoongelea kero za Muungano, mara nyingi ni ndugu zetu wa Zanzibar wanaoona kuna mambo mengi yanahitaji kurekebishwa. Sasa basi, badala ya kufurahia baraka ndogo ndogo za uraisi wa Samia kwa Zanzibar kama kumtuma raisi wa Zanzibar kumwakilisha Raisi wa Tanzania kwenye mikutano, fursa ni hii ya kupata katiba mpya ya Tanzania katika kipindi ambacho Samia yupo madarakani. Zoezi hili linapaswa kuanza mara moja kwa kuwa hatujui litakalotokea mwaka 2025 au hata mwaka huu huu 2021.

Suala la Katiba mpya lisionwe kuwa ni la Mbowe, Zitto na vyama vyao vya Chadema na ACT, na wala lisionwe kama litatoa nafasi kwa CCM kuondolewa madarakani! Ni suala la Watanzania, lakini hasa Wazazibari kwa kuwa mara nyingi Watanganyika wanataja kero pale tu Wazanzibari wanapotaja kero za Muungano kupita kiasi!
 
Au kama vipi waandamane kumuomba Mzanzibar mwenzao kujitenga kabisa na Tanganyika! Halafu waone kama kuna chochote tutakacho pungukiwa baada ya kujitenga kwao.

Zaidi tu wataendelea kutudekea kika siku na kutupigia magoti ili waendelee kutunyonya kupitia huu Muungano kimeo.
 
Katiba mpya ni suala ambalo ccm hawataki kulisikia!
Ccm wapo tayari wakupe 0713 'mtandao pendwa' utifue tope mule lakini sio wakupe katiba mpya!
 
Kama kuwa na katiba mpya ni shida kwa chama tawala basi wapeleke petition bungeni ili muungano huu ufikie kikomo kisha kuwe na muungano wa East Afrika tu,muungano wa e/a unatoa fursa nyingi tu na hakutahitajika repatriation ya raia kuhamishwa popote ndani ya east Afrika
 
Back
Top Bottom