Kuelekea mkutano mkuu wa CCM Aprili 01, nini maana ya mkutano mkuu wa CCM na nguvu yake?

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Na Bwanku M Bwanku.

Jumamosi Machi 12, 2022 Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka alitangaza Uamuzi wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kujadili pendekezo la kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa CCM lililotolewa kwenye Kikao chake cha Desemba 18, 2021 na hivyo kutangaza Ijumaa Aprili 01, 2022 kuwa ni siku ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Jijini Dodoma kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre.

Sasa nini maana ya Mkutano Mkuu wa CCM, Chama kinachoongoza Taifa letu?

Kwa Mujibu wa Katiba ya CCM ya Mwaka 1977, Toleo la Mwaka 2017, Fungu la 7, Ibara ya 99 (2) imeeleza wazi kwamba Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa utakuwa ndio Kikao Kikuu cha CCM kupita vyote na ndicho kitakachokuwa na madaraka ya mwisho. CCM ina jumla ya Vikao 7 kuanzia Vikao vya chini kabisa vya Shina, halafu vikao vya Tawi, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na vya juu kabisa, Vikao vya Taifa. Kwahiyo katika Vikao hivyo 7 vya CCM, Mkutano Mkuu wa CCM ndicho Kikao cha juu kabisa, chenye nguvu kubwa na chenye madaraka ya mwisho.

Kwa lugha rahisi, Mkutano Mkuu wa CCM ndicho Chombo Kikuu cha maamuzi yoyote makubwa yanayoathiri Chama kizima Kitaifa na Ibara ya 100 kuanzia sura ndogo (1) hadi (7) imeeleza vyema kazi za Mkutano Mkuu wa CCM kuwa ni pamoja na kusimamia siasa nzima ya CCM Taifa na kupanga na kusimamia Utekelezaji wa shughuli zote za CCM, kubadili sehemu yoyote ya Katiba yake ya Chama ili kujiimarisha, kuchagua na kuthibitisha Jina la Mwanachama mmoja wa Kugombea Urais wa Tanzania na Zanzibar pamoja na shughuli zingine nyingi za kuongeza ufanisi wa Chama chote.

Ibara ya 99 (7) ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 inaeleza pia kwamba Kikao hiki cha juu kabisa ndani ya CCM na chenye nguvu kubwa kuliko Kikao chochote kile kitaongozwa na Mwenyekiti wa CCM- Taifa ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu ama asipohudhuria basi mmoja wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa awe wa Bara au Visiwani basi ataongoza Kikao hicho na ikitokea wote watatu hawapo ama hawawezi kuhudhuria basi Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itamchagua Mjumbe mwingine miongoni mwao kuwa Mwenyekiti wa muda wa kuongoza Mkutano Mkuu.

Mkutano Mkuu wa CCM unajumuisha Wajumbe zaidi ya elfu 2 kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani (Zanzibar) na Mkutano Mkuu huu wa mwaka huu wa Ijumaa Aprili 01, 2022 pamoja na mambo mengine utajadili mapendekezo ya marekebisho ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2020, marekebisho yenye lengo la kuongeza kasi na ufanisi wa Chama kwenye maeneo mbalimbali.

Leo ni takribani bado siku 4 tu kuelekea kwenye Kikao ama Mkutano huo mkubwa kabisa wa CCM pale Jijini Dodoma.

Hizo ndizo dondoo chache na fupi kuhusu Mkutano Mkuu wa CCM, Kikao chenye nguvu zaidi ndani ya CCM na chenye maamuzi makubwa yenye maslahi kwa Watanzania na Taifa zima.

Tutege sikio kusikia Mkutano Mkuu huu wa CCM Aprili 01, Mkutano Mkuu Maalum utakaokuwa na agenda maalum ya marekebisho ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 toleo la mwaka 2020.

Bwanku M Bwanku
bwanku55@gmail.com

IMG-20220327-WA0008.jpg


IMG-20220327-WA0009.jpg

IMG-20220327-WA0027.jpg

IMG-20220327-WA0025.jpg

IMG-20220327-WA0029.jpg

IMG-20220327-WA0026.jpg

IMG-20220327-WA0028.jpg

IMG-20220327-WA0030.jpg

IMG-20220327-WA0032.jpg

IMG-20220327-WA0031.jpg
 

Attachments

  • VID-20220326-WA0024.mp4
    9.1 MB
Tunapoelekea karne toka nchi imepata Uhuru na nusu karne toka CCM imezaliwa bado Taifa lina kumbukumbu isiyofutika ya uzuri wa CCM.

CCM kikiwa ndicho chama pekee chenye itikadi isiyokufa ya Uafrika na Utanzania nayo ni Ujamaa kimefanikiwa kutuvusha kwenye nyakati za raha na tabu.
 
KUELEKEA MKUTANO MKUU WA CCM APRILI 01, NINI MAANA YA MKUTANO MKUU WA CCM NA NGUVU YAKE?.

Na Bwanku M Bwanku.

Jumamosi Machi 12, 2022 Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka alitangaza Uamuzi wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kujadili pendekezo la kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa CCM lililotolewa kwenye Kikao chake cha Desemba 18, 2021 na hivyo kutangaza Ijumaa Aprili 01, 2022 kuwa ni siku ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Jijini Dodoma kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre.

Sasa nini maana ya Mkutano Mkuu wa CCM, Chama kinachoongoza Taifa letu?

Kwa Mujibu wa Katiba ya CCM ya Mwaka 1977, Toleo la Mwaka 2017, Fungu la 7, Ibara ya 99 (2) imeeleza wazi kwamba Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa utakuwa ndio Kikao Kikuu cha CCM kupita vyote na ndicho kitakachokuwa na madaraka ya mwisho. CCM ina jumla ya Vikao 7 kuanzia Vikao vya chini kabisa vya Shina, halafu vikao vya Tawi, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na vya juu kabisa, Vikao vya Taifa. Kwahiyo katika Vikao hivyo 7 vya CCM, Mkutano Mkuu wa CCM ndicho Kikao cha juu kabisa, chenye nguvu kubwa na chenye madaraka ya mwisho.

Kwa lugha rahisi, Mkutano Mkuu wa CCM ndicho Chombo Kikuu cha maamuzi yoyote makubwa yanayoathiri Chama kizima Kitaifa na Ibara ya 100 kuanzia sura ndogo (1) hadi (7) imeeleza vyema kazi za Mkutano Mkuu wa CCM kuwa ni pamoja na kusimamia siasa nzima ya CCM Taifa na kupanga na kusimamia Utekelezaji wa shughuli zote za CCM, kubadili sehemu yoyote ya Katiba yake ya Chama ili kujiimarisha, kuchagua na kuthibitisha Jina la Mwanachama mmoja wa Kugombea Urais wa Tanzania na Zanzibar pamoja na shughuli zingine nyingi za kuongeza ufanisi wa Chama chote.

Ibara ya 99 (7) ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 inaeleza pia kwamba Kikao hiki cha juu kabisa ndani ya CCM na chenye nguvu kubwa kuliko Kikao chochote kile kitaongozwa na Mwenyekiti wa CCM- Taifa ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu ama asipohudhuria basi mmoja wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa awe wa Bara au Visiwani basi ataongoza Kikao hicho na ikitokea wote watatu hawapo ama hawawezi kuhudhuria basi Halmashauri Kuu ya CCM Taifa itamchagua Mjumbe mwingine miongoni mwao kuwa Mwenyekiti wa muda wa kuongoza Mkutano Mkuu.

Mkutano Mkuu wa CCM unajumuisha Wajumbe zaidi ya elfu 2 kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani (Zanzibar) na Mkutano Mkuu huu wa mwaka huu wa Ijumaa Aprili 01, 2022 pamoja na mambo mengine utajadili mapendekezo ya marekebisho ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2020, marekebisho yenye lengo la kuongeza kasi na ufanisi wa Chama kwenye maeneo mbalimbali.

Leo ni takribani bado siku 3 tu kuelekea kwenye Kikao ama Mkutano huo mkubwa kabisa wa CCM pale Jijini Dodoma.

Hizo ndizo dondoo chache na fupi kuhusu Mkutano Mkuu wa CCM, Kikao chenye nguvu zaidi ndani ya CCM na chenye maamuzi makubwa yenye maslahi kwa Watanzania na Taifa zima. Tutege sikio kusikia Mkutano Mkuu huu wa CCM Aprili 01, Mkutano Mkuu Maalum utakaokuwa na agenda maalum ya marekebisho ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 toleo la mwaka 2020.

Bwanku M Bwanku
bwanku55@gmail.com

IMG-20220327-WA0009.jpg


IMG-20220327-WA0032.jpg


IMG-20220327-WA0031.jpg


IMG-20220327-WA0030.jpg


IMG-20220327-WA0028.jpg


IMG-20220327-WA0026.jpg


IMG-20220327-WA0029.jpg


IMG-20220327-WA0027.jpg


IMG-20220327-WA0025.jpg
 

Attachments

  • VID-20220326-WA0024.mp4
    9.1 MB
Mwenyekiti wa CCM ana wajibishwa vipi na chama Au huwa hakosei? Nimesikia Wanachama wengine/Wabunge wakitwa kujieleza kwenye kamati za kinidhamu za chama.
There are only two office rules ! Rule no. 1 The boss is always wright ! Rule no. 2 When he is wrong follow rule no. 1 !! Ndivyo ilivyo kwenye Ofisi yeyote ile !! Au siyo ??
 
There are only two office rules ! Rule no. 1 The boss is always wright ! Rule no. 2 When he is wrong follow rule no. 1 !! Ndivyo ilivyo kwenye Ofisi yeyote ile !! Au siyo ??

Huyu jamaa hakuweka iko kwenye Ibara ipi ya Katiba ya CCM.
 
Kila 01/04 kila mwaka ni siku ya wajinga. Ila 01/04/2022 ni siku maalum ya wajinga maalumu ambao kutamka ndio au hapana inaamuliwa na mtu mmoja.

Siku hiyo watakusanyika katikati kwa lengo la kusema ndioooooo......... Kwa kila kitakachosemwa
 
Ukikubali upande mmoja lazima ukubali na upande mwingine wa shilingi !! Lakini pia sio lazima ukaamini hivyo !!

Serikali na kubali kwa vile Bunge linaweza ingawa ni utaratibu mgumu pengine usio wezekana kumpigia kura ya kutokuwa na Imani na Rais.

Katika vyama huo utaratibu hauko na matokeo yake karibia vyama vyote vya Kisiasa Tanzania kasoro CCM tu, vina Wenyeviti wa maisha .
 
Kuna mtu anaenda kukabidhiwa kadi yake inayokisiwa aliny'ang'anywa japo bado anayo ila kupitia mkutano huo ni kum_boost awe na nguvu mpya.

Tunza hii reply.
 
Back
Top Bottom