Mkuu kwani sheria zinatungwa na nani?..Sheria zinatungwa na watu sisi wenyewe ndio tunatakiwa kuzitunga ili mwanasheria apate kuzitafsiri ktk mikataba yetu, sasa inapofika sisi hatuna sheria isipokuwa ile iloandikwa Ulaya kwa minajiri ya mwekezaji utamlalamikiaje mwanasheria ambaye kazi yake ni kutafsiri tu sheria na sio kuisimamisha. Hata huyo Muhongo siwezi kumlaumu maana sheria ya Ubinafsishaji ilikuwepo na viongozi wakaondolewa vizuizi vya kumiliki mali.. Muhongo angeweza vipi kumzuia Mkapa kununua Kiwila na kwa sheria gani ikiwa sio haramu imepitishwa bungeni.mimi sina taaluma ya sheria lakini kuna mikataba nikisoma kurasa chache naona hatari iliyopo mbeleni. Tatizo ni kukosa uzalendo kwa taifa na ndio maana serikali imejiwekea record nzuri ya kushindwa kesi mahakamani.
Nadhani tuwe na mijadala huru kupitia radio na TV ili watu wajadili namna ya kuhandle rasilimali zetu mfano 'sera ya gas na mafuta' badala ya kuitisha makongamano ya siasa kama yale kigoda cha mwalimu. Naamini wapo watanzania wengi sana wanaoweza kutoa points za maana kupitia mijadala hii
Vita yetu kubwa ni UFISADI ambao umetokana na viongozi wetu watunga sheria na wapitishaji wa sera. Kama hawa wamelala na wamepitisha vitu pasipo kuzama undani wake wakajua mazuri na mabaya utaweza vipi kuwalaumu watendaji ambao wanafungwa na sheria butu. Hivyo natanguliza kupeleka lawama zangu kwa SERIKALI na BUNGE (lenye wabunge zaidi ya 230 wa CCM) ambao ndio ktk kundi la SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Kama huko tumechemsha kupitisha vitu ktk SERA na sheria mbovu, mwanasheria hana budi pia kuchemsha anapotetea.