Kudai kuwa chanzo cha mikataba mibovu ni kukosa elimu ni tusi na kejeli kwa wengi nchini!

MMK, performance inapokuwa mbaya unaweza kutukanwa kwa tusi lolote. Mimi siafiki kabisa kwamba tatizo letu watanzania (siyo waafrika) ni elimu japo in some cases ni kweli ufahamu mdogo wa mambo fulani unachangia. Tatizo letu kubwa ni kitu kinachoitwa kwa ujumla wake UBINAFSI. Mambo mengi yanayofanywa na viongozi wetu wawe ni wa kisiasa au watendaji ni UBINAFSI. Wengi wao kila walifanyalo wanaongozwa zaidi na UBIBAFSI. Wanapojadili mikataba baina ya nchi na nchi wanaangalia watapata nini wao kama wao na siyo nchi itapata nini. Mtu yupo radhi ajengewe nyumba na kununuliwa gari ya kisasa kwa milioni chache huku akitambua kuwa kwa kufanyiwa hivyo, anaikosesha nchi mabilioni ya fedha ambayo yangeinufaisha watanzania takriban wote.
Wala sio kununuliwa nyumba na gari ya kisasa bali aambiwe kuwa ananunuliwa gari hata Mark 11 kwa ajili ya kuwa linampeleka mke wake saloon au watoto tution na huu ndio ubinafsi wenyewe
 
Tanzania kama Tanzania hatusumbuliwi na suala la elimu katika mikataba. Tunasumbuliwa na majanga ya kitaifa ambayo ni Rushwa, Ufisadi na uongozi dgaifu wa serikali ya CCM ambapo tumeona mfano mdogo kiongozi mkuu ananunuliwa tai 5 na skuna anatoa Hotel.
 
japo mtani wangu Zitto Kabwe wengi wanamtilia mashaka siku hizi lakini anasema tatizo sio ukosefu wa elimu bali ukosefu wa uwazi!
Hapa ni sawa sana kwa sababu chukulia mkataba kama wa Richmond ambapo wasomi chungu nzima (Baraza la Mawaziri, makatibu wakuu na wataalamua wa Tanesco) mambo waliyoyaamua na kutoa ule mkataba hata mtu wa darasa la nne mwenye nia njema na nchi hii asingeliweza kufanya hayo.
 
Mimi naona tunazunguka sana, Tatizo ni CCM na TISS, maana maslahi ya nchi na watu wake yanalindwa na Serikali pamoja na TISS...
 
..Wakati mwingine interview nyingi za wanasiasa, wanatoaga majibu yao tuu ili swali lipite tuu kwa haraka..!
 
Mkuu wanasiasa ndio tatizo kubwa wakishalamba 10% wanapewa na draft ya mkataba huko huko sasa mwanasheria anakuwa redundant hana nafasi ya kushauri wala nini sana sanaataambiwa uweke sawa tayari kwa kusaini. ukiwabana watakueleza ukweli.

Mkuu ukiwa kama profession unakubali vipi kuweka sawa kwa ajili ya kusaini?
 
Kwa maoni yangu ni kejeli kubwa na ni tusi kwa kudai kuwa tatizo letu la mikataba ni tatizo la watu kukosa elimu. Hivi tunaweza kusema tatizo la sekta ya afya ni watu kukosa elimu ya udaktari? au tatizo la elimu watu kukosa elimu ya ualimu? Tanzania imekuwa na wanasheria mahiri wengi tu napo wengi tu ambao wamespecialize katika international contracts na sheria hizi za mikataba. Ni kweli Tanzania haina watu wenye elimu hiyo?

Au wanaposema tatizo ni elimu wana maana kuwa wasomi wetu (wanasheria na wengine) wanapokaa na hawa wageni kwenye meza moja wasomi wetu hawana upeo au uwezo wa kujadiliana kisomi? Kama hili ni kweli kundi lililopelekwa kujadiliana na wa Malawi lenye kuhusisha wasomi lina matumaini gani? Hivi juzi MWakyembe na wataalamu toka Wizarani wameenda Ujerumani na huko wana/wamekutana na wadau mbalimbali wa sekta ya anga na usafirishaji. Sasa waje kuingia mkataba halafu baadaye tuseme hatuna wataalamu wenye ujuzi wa mambo ya anga na usafirishaji?

It is fallacious kudai kuwa tatizo letu la mikataba ni tatizo linalotokana na elimu? Kivipi.. hatuna wasomi, vyuo vyetu havijui kufundisha mambo ya mikataba? wanafunzi wetu ni wagumu kuelewa? au ni nini hasa? Maana hata Kikwete aliwahi kusema alipokuwa Sweden?? kuwa tatizo la nchi kuingia mikataba mibovu ni kwa sababu wanasheria wetu hawana ujuzi sana! Na hakuna aliyebisha na hivyo kufanya iaminike kuwa tatizo ni elimu.

Sasa kama tatizo ni elimu na kuwa hatuna wasomi wa kuingia mikataba mizuri hiki kimbelembele cha kuendelea kuingia mikataba mingine kinatoka wapi? Kama kweli hatuna wasomi wenye kuweza kutuletea deals nzuri kwenye mikataba ni kitu gani kinatufanya tukubali kuingia mikataba mingine tukitarajia kuwa itakuwa tofauti? Si imewahi kusemwa kuwa the classical definition of insanity is doing the same thing, the same way, every time expecting different results? Kila ukipanda michongoma unakaa pembeni na kuombea mpunga uote? na ukiota mchongoma unalaumu udongo?
Mimi nadhani tunaposema tatizo ni elimu ina maana kwamba haiwezekani kabisa nchi kuanza kuingia mikataba ya gasi na madini wakati haina sera ya gasi na mafuta. ELIMU tunayosoma ni lazima itambue mazingira tuliyopo na sio kusoma elimu ya kimataifa kisha unakuja itumia nyumbani kama ilivyoandikwa..

Mwanakijiji inashangaza sana kuona shirika linakuja wekeza nchini wakati sisi hatua sheria inayolifunga shirika hilo kuingia Ubia, hakuna sheria kwa wote inayolazimisha shirika yote nchini kulipa corperate tax isipokuwa tuna sheria za kuunganisha. Mwananchi anatozwa kodi kuliko mgeni paispo mshama lakini mgeni anapewa miaka 10 ya msamaha wa mafuta na vifaa..USOMI ni uelemika hivyo unapoweka mkataba mbovu hakika elimu yako inatupa wasiwasi ikiwa hutazingatia Watu na Mazingira..

Hata yule mzee wa Kariakoo leo hii akiuza nyumba yake anataka akatiwe maghorofa yake ktk jengo litakalo jengwa. Sheria za usajili na mkataba wanakwenda kwa Lawyer lakini tayari mwenye nyumba kisha weka msimamo wake kwa kutazama na kujali maslahi yake na familia yake. Usomi wetu hautazami maslahi ya taifa isipokuwa maslahi ya wageni kwa kutumia sheria na vitabu vya wageni vilivvyo andikwa kwa ajili yao. Tumesoma lakini hatujaeleimika na hata kama iwe matusi lakini ndio ukweli. Tumesoma sana ili kumtumikia mzungu ambaye katunga sheria zinazoambatana na mazingira yake sio yetu, hii sio elimu bali kujazwa Ujinga zaidi..
 
No disrespect,kiwango chako cha elimu hakikupi nafasi ya kuelewa na kupambanua mambo mengi. But sio lazima ufike chuo kikuu ili uweze kuwa na busara na ufahamu. In this case with common sense, you could do much better than that!
kaka wewe pia ni part of the problem
Nakala ndefuuuuu wakati ukweli unaujua. Upuuzi huu ndio aliokwenda nao FREEMAN MBOWE huko DMV....kaja na filosofi ya ELIMU, ELIMU, ELIMU kisha LAW & ORDER

Richmond na EPA , kila kukicha mlitaka kutuaminisha kuwa mwenye makosa ni ROSTAM na LOWASSA lakini ukweli waliotuingiza hapo ni wanasheria wetu akina MKONO, akina MAAJAR & CO na wanasheria wengine ambao ni wasomi zaidi walioko Tanesco, wizarani, wizara ya sheria na kwingineko

Mie sina hiyo degree, kisomo changu ni form 6 lakini najua siku zote contracts zina pande 2 sasa iweje leo tunaaminishwa kuwa wahindi, wairan, akina mkono ndio wabaya wakai serikali hii ina mijitu ina degree 3 tutu?

mimi nakushairi. acha kutuletea hizo articles ndefu as if sisi ni wajinga na hatujui tatizo liko wapi. Lete article ya paragraph 2 max kisha waache hawa so called great thinkers waumize kichwa.

Mimi naona bora kama unapata ugali wako wewe endelea tuu lakini hii system imeoza, hao the so called wapinzani wameoza zaidi. Kila mmoja ale kwake

Eti LAW & ORDER...labda Law and order ya tv series na hata ile wahalifu wanakamatwa.

mimi nishachoka na naskia kichefu chefu nikisoma hizi habari eti kusoma kusoma sasa hao wasomi wametufikisha wapi?
 
MM Nitakuheshim siku zote, lakini ukiondoa elimu wazungu walitunga sheria ambazo tunaziita za kimataifa, mimi naziita za kinyonyaji, pia nilikuwa nachukia sana waafrika kuitwa nyani, lakini nalegea kwani kila mtu mweusi akikaa meza moja namzungu kuingia mkataba naamini kama mtumweusi atanyonywa tu, hata kama hao watu wana elim zinazolingana, kuna kila sababu ya wasomi wetu kukaa na kujadili kwa nini wazungu wanatuita nyani, naamini watu weusi tuna tatizo ambalo kama halitafanyiwa kazi tutaendelea kutawaliwa, nahisi KUTOJITHAMINI NA KUJIONA WATU KAMILI NDIO TATIZO LETU, kwani haiingii akilini wasomi wetu waendelee kutumia sheria za kimataifa ambazo sio tu zimetugwa na wazungu pekee pia ni kandamizi
 
Uko sahihi bro; tatizo sio elimu hata kidogo kwa sababu kama tatizo ni elimu kwa nini hatukutii maagizo ya mwalimu Nyerere ya awali kwamba kutokana na uelewa wetu mdogo kuhusu madini na raslimali kama hizo akaamua tuziache zibakli ardhini akizingatia kwamba haziozi!

Kama tatizo ni elimu na watawala wetu wanalijua Why on earth did they open up our natural resources for exploitation!!
Wizi mtupu, tatizo sio elimu bali wizi mtupu, umimi, ufisadi.
Mwalimu alitufundisha kwamba ili nchi iendelee tunahitaji vitu 4

1. Raslimali Watu (waadilifu, wachapa kazi na wazalendo)
2. Raslimali Ardhi (na vyote Mwenyezi Mungu alivyotujalia juu na chini ya ardhi yetu)
3. Siasa safi (read sera safi zinazotekelezeka)
4. Uongozi bora (unaotokana na raslimali watu ambao ni waadilifu, wachapa kazi, wazalendo, wacha Mungu na wenye mapenzi mema na nchi yao na wananchi wenzao)

Kwa bahati yetu mbaya mahitaji yote haya muhimu kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu yamekosekana; nathubutu kusema hivyo kwa sababu kila tukipata kiongozi mpya anaanza kazi vizuri sana tunasema eeh Mungu mjalie huyu, hamjakaa sawa kachemsha, anakuwa bubu, mara mnasikia kafanya ufisadi wa kutisha.

I am terribly disappointed with Professor Mhongo, Mtu mwenye akili timamu, mzalendo, mpembuzi yakinifu, anayejua kinachoendelea hapa nchini na duniani kote aliyesikia interview ya jana jioni kupitia BBC iliyomshirikisha Waziri Mhongo na Zitto kabwe atakuwa analia moyoni kimya kimya.
 
MM na wengine, sheria ni professional kama professional nyingine zote kuna pa kuanzia na kuna kubobea. Kwenye tasnia ya sheria LL.B ni basic tuu kama ilivyo MD kwa medicine.

Kuwa dakitari ni kitu kimoja lakini ili uweze kutibu baadhi ya magonjwa lazima uwe daktari bingwa. Ndio maana ili kuwa surgeon lazima kwanza uwe daktari halafu unaspecialize na upasuaji. Ili kuwa neorosurgeon lazima kwanza uwe dakitari, uspecialize kuwa surgeon ndipo uspecialize tena kuwa neurosurgeon!.

Tanzania tuna fundisha sheria na kuproduce wanasheria wengi tuu wa basic na ni wachache wana specialize ila hakuna chuo chochote kinafundisha specialization ya natural resources, madini, oil and gas hivyo mikataba yote ya madini iko drafted na mabingwa wao sisi tunaletewa tuu kupitia na kuisaini!.

Amini usiamini Watanzania kama Watanzania hatuna mwanasheria hata mmoja aliyespecialize kwenye Oil & Gas, niliandika hii mada kuwa tunaibiwa!.

Mkono and Co. ndio the most succesful solo law firm in Tanzania ukiangalia list ya wanasheria wake kwenye ile top cream ya 10 senior partners, 7 ni wazungu waliobobea na watatu ndio Watanzania wenzetu!. Consulancy fee yao ni US $ 5000 per hour!. Mkono as Mkono alimaliza UD na pass tuu lakini ameajiri ma profesa!. Sababu ni kwa nini aajiri wanasheria wazungu huku sisi tuna washeria kibao?!, ndipo unaambiwa hao jamaa wamespecialize kwenye fani maalum ambazo ni deal kwa Mkono!.

Madini yaligunduliwa siku nyingi tuu na Nyerere akagoma tusiyachimbe ili kwanza tuwajengee uwezo watu wetu ili tusiibiwe!.

Hili la Gas Mtwara, tunaibiwa mchana kweupe. Nimelifungulia thread humu na haikuchangiwa!, tukishaibiwa miaka 5 ijayo ndio nitakuja kukumbushia tulisema!.

Tunaibiwa kwa kukosa maarifa ambayo yanajumuisha elimu, uzalendo, ubinafsi, etc!. Gesi tunaibiwa mchana kweupe!.
kama una nafasi nisome hapa
https://www.jamiiforums.com/jamii-intelligence/298561-jf-exclusive-gesi-asili-is-it-day-light-robbery-watanzania-tunaibiwa-mchana-kweupe-2.html

Pasco.
 
Lakini utakuwa kuwa inakuwa assumed kuwa wasomi ndio wana 'common sense' ndio maana utaona watu wengi wanapenda sana kuuliza "CV"ya mtu na wakiona wanaamua kama mtu ni 'kichwa' au vipi. Wanakuwa impressed sana na CV kiasi kwamba mtu huyo anapoboronga watu wanashindwa kuelewa. Inanikumbusha mambo ya Prof. Peter Msola na Elimu ya Juu!

Yawezekana labda 'common sense is not that common after all'?

Rafiki yangu tatizo siyo wasomi katika nchi yetu hao wapo na mahiri kabisa. Kubwa ni ufisadi ambao ndani yake kukiwepo nepotism ya hali ya juu...Walio wataalamu mahiri hawajui siasa na wengi wamekata tamaa kwahiyo wako busy na chaki ama na biashara zingine zinazowapa return kubwa kuliko usomi wao. Ambao wameunga unga shule ndiyo wengi wanaobeba administration ya idara mbali mbali za vyuo na serikali nao kwakua ndiyo decision makers ndiyo wanjipa vyeo vya haraka haraka kwenda senior huku wakiwa hawajifunza vyakutosha ama kufanya kazi consistently katika field zao; hao ndiyo ambao sasa wanaonekana ni wasomi na wakipewa assignment ndiyo realities zinajionyesha kuwa ndivyo sivyo...

For God sake nchi hii isipopata kiongozi wakuipa vision na mission sahihi tutaendelea kutukana innocent people na kuchekwa kwenye kada za kimataifa kama ilivyofanya Israel publicly!

Nimewahi shuhudia kwa macho yangu university best students wakiachwa kuajiriwa kwakua tu hawana referees wenye nguvu lakini ufanyeje unabaki kuwaambia wasife moyo wajaribu kwingine! Na hata leo nikiambiwa nitoe evidence siwezi maana watakuja na reasons kibao na mm kuonekana mwongo na mbaya huku moyoni wakiwa na uhakika its morally and ethically wrong. Mbaya zaidi its for our own lose of gud welfare kama Taifa.

It is so sad and painful kwakweli but what do you do? Unaacha tu kama ilivyo miaka yako inaisha mnaendelea kuishi kimaskini bila sababu ya msingi. Lakini mm nimekata hii mambo am not helpless and can do something ndiyo maana nimeshika chekecheo kuondoa kila fisadi hadi wote watakapo isha ili tuijenge nchi tuipendayo in Jesus most high name!
 
Mimi nadhani tunaposema tatizo ni elimu ina maana kwamba haiwezekani kabisa nchi kuanza kuingia mikataba ya gasi na madini wakati haina sera ya fasi na mafuta. ELIMU tunayosoma ni lazima itambue mazingira tuliyopo na sio kusoka elimu ya kimataifa kisha unakuja itumia nyumbani kama ilivyoandikwa..

Mwanakijiji inashangaza sana kuona shirika linakuja wekeza nchini wakati sisi hatua sheria inayolifunga shirika hilo kuingia Ubia, hakuna sheria kwa wote inayolazimisha shirika yote nchini kulipa corperate taxisipokuwa tuna sheria za kuunganisha. Mwananchi anatozwa kodi kuliko mgeni paispo mshama lakini mgeni anapewa miaka 10 ya msamaha wa mafuta na vifaa..USOMI ni uelemika hivyo unapoweka mkataba mbovu hakika elimu yako inatupa wasiwasi ikiwa hutazingatia Watu na Mazingira..

Hata yule mzee wa Kariakoo leo hii akiuza nyumba yake anataka akatiwe maghorofa yake ktk jengo litakalo jengwa. Sheria za usajili na mkataba wanakwenda kwa Lawyer lakini tayari mwenye nyumba kisha weka msimamo wake kwa kutazama na kujali maslahi yake na familia yake. Usomi wetu hautazami maslahi ya taifa isipokuwa maslahi ya wageni kwa kutumia sheria na vitabu vya wageni vilivvyo andikwa kwa ajili yao. Tumesoma lakini hatujaeleimika na hata kama iwe matusi lakini ndio ukweli. Tumesoma sana ili kumtumikia mzungu ambaye katunga sheria zinazoambatana na mazingira yake sio yetu, hii sio elimu bali kujazwa Ujinga zaidi..

Wasomi hawa kwa mtazamo wangu ni wasomi kweli na wameelimika vya kutosha lakini wanachagua njia zinazoliangamiza Taifa wakiwa na uelewa kamili, hawajawa brain-washed na wazungu, wanaweza kuzifafanua vizuri kabisa sheria hizi za kizungu, ni suala la kuchagua tu, aidha kwa maslahi binafsi au kwa misukumo mbalimbali........tukitaka kutumia excuse ya kutoelimika ni kama tunawatoa mzigo wezi hawa kama si majambazi wa rasilimali za Taifa. Narudia kusema. WANAJUA WANACHOKIFANYA
 
MM na wengine, sheria ni professional kama professional nyingine. LL.B ni basic tuu kama ilivyo MD kwa medicine.

Kuwa dakitari ni kitu kimoja lakini uli uweze kutibu baadhi ya magonjwa lazima uwe daktari bingwa. Ndio maana ili kuwa surgeon lazima kwanza uwe daktari halafu unaspecialize na upasuaji. Ili kuwa neorosurgeon lazima kwanza uwe dakitari, ispecialize kuwa surgeon ndipo uspecialize tena kuwa neuro surgeon!.

Tanzania tuna fundisha sheria ma kuproduce wanasheria kibao na wengine wana specialize ila hakuna chuo chochote kinafundisha specialization ya natural resources, madini, oil and gas hivyo mikataba yote ya madini iko drafted na mabingwa wao sisi tunaletewa tuu kupitia na kuisaini!.

Amini usiamini Watanzania kama Watanzania hatuna mwanasheria hata mmoja aliyesoecialize kwenye Oil & Gas, niliandika hii mada kuwa tunaibiwa!.

Mkono and Co. ndio the most succesful solo law firm in Tanzania ukiangalia list ya wanasheria wake kwenye ile top cream ya 10 senior partners, 7 ni wazungu waliobobea na watatu ndio Watanzania. Consulancy fee yao ni US $ 5000 per hour!. Mkono as Mkono alimaliza UD na pass tuu lakini ameajiri ma profesa!. Sababu hao jamaa wamespecialize!.

Madini yaligunduliwa siku nyingi Nyerere akagoma tusiyachimbe ili kwanza tuwajengee uwezo watu wetu tusiibiwe!.

Hili la Gas Mtwara, tunaibiwa mchana kweupe. Nimelifungulia thread humu na haikuchangiwa!, tukishaibiwa miaka 5 ijayo ndio nitakuja kukumbushia tulisema!.

Tunaibiwa kwa kukosa maarifa ambayo yanajumuisha elimu, uzalendo, ubinafsi, etc!. Niko mobile nitaitafuta link niwawekee!. Gesi tunaibiwa mchana kweupe!.



Pasco nakubaliana na hizi sentensi zako za mwisho lakini zinginezo za juu hasa nilizozi bold na kataa katu katu...Kumbuka first degree ni basic knowledge katika decision making level na kila graduate wa degree ya kwanza (under normal circustance lakiniisiwe kupitia shule za kata) katika field yake anauwezo wa kutambua what and where something is wrong. Kwenye academics kuna kitu kinaitwa transfer of knowledge na managerial post ambazo zinafanya decision tu hazihitaji specialization ya hali ya juu bali ethics and negotiation skills...Huyo manager under good experience anawezajua specific problem inaweza kuwa solved na expert gani..

Ukija kwenye specialization siyo rahisi kupata specialist wa kila tatizo na field kwasababu life is so complex and diversed lakini kuna zile basics za specialization ambapo kwenye Identified world development sectors ambazo ni za Energy kwa maana ya ingines, Medicine, Plastic, iron and Agriculture kwa maana ya food sector ukiwa na mtu ambaye amespecialize katika hiyo area kwenye specific area basi lazima awe na basics za sector nzima na hivyo anauwezo ama wa ku-transfer knowledge ama kutafuta wenzake wanaoweza ku-share knowledge and experience ku-solve problems. So unachotaka kukileta ni zaidi siasa kuliko uhalisia. MMM amekwambia kuna watu mahiri katika sheria za contract so contract hata iwe ya wewe na mkeo ina basics fulani siyo lazima mtu awe specialist wa mambo ya ndoa japo inawezekana akawepo huyo specialist. Huo ni mfano tu..

Ombi tuache siasa katika kila jambo tuzingatie utaalamu kabla ya ku-decide na integration ya change in attitude and behaviour itleta welfare kwa kila mtanzania.
 
kaka wewe pia ni part of the problem
Nakala ndefuuuuu wakati ukweli unaujua. Upuuzi huu ndio aliokwenda nao FREEMAN MBOWE huko DMV....kaja na filosofi ya ELIMU, ELIMU, ELIMU kisha LAW & ORDER

Richmond na EPA , kila kukicha mlitaka kutuaminisha kuwa mwenye makosa ni ROSTAM na LOWASSA lakini ukweli waliotuingiza hapo ni wanasheria wetu akina MKONO, akina MAAJAR & CO na wanasheria wengine ambao ni wasomi zaidi walioko Tanesco, wizarani, wizara ya sheria na kwingineko

Mie sina hiyo degree, kisomo changu ni form 6 lakini najua siku zote contracts zina pande 2 sasa iweje leo tunaaminishwa kuwa wahindi, wairan, akina mkono ndio wabaya wakai serikali hii ina mijitu ina degree 3 tutu?

mimi nakushairi. acha kutuletea hizo articles ndefu as if sisi ni wajinga na hatujui tatizo liko wapi. Lete article ya paragraph 2 max kisha waache hawa so called great thinkers waumize kichwa.

Mimi naona bora kama unapata ugali wako wewe endelea tuu lakini hii system imeoza, hao the so called wapinzani wameoza zaidi. Kila mmoja ale kwake

Eti LAW & ORDER...labda Law and order ya tv series na hata ile wahalifu wanakamatwa.

mimi nishachoka na naskia kichefu chefu nikisoma hizi habari eti kusoma kusoma sasa hao wasomi wametufikisha wapi?
dah naona umejibu swali kama mwanafunzi ambae hata secondary hajafika. Kama hizo article zimekukera usizisome na kuandika maneno mengi yenye spelling mistake kibao eti form six hii ndo kitu gani?
 
Tumesoma lakini hatujaeleimika na hata kama iwe matusi lakini ndio ukweli. Tumesoma sana ili kumtumikia mzungu ambaye katunga sheria zinazoambatana na mazingira yake sio yetu, hii sio elimu bali kujazwa Ujinga zaidi..


ndio maana wakati mwingine nashangaa kama tatizo ni elimu au ni hawa waliopata elimu... inaonekana consensus hapa ni kuwa tuna tatizo na hawa waliopata elimu... maana unajua hawa hawa wakienda Namibia, Botswana, Russia, Uingereza au hata US.. wanakuwa ni nyota zinazong'ara...!!! Au wakipewa nafasi kwenye international organizations or companies.. ila ukiwaleta kwenye public service....
 
Kuna kusoma na kuelimika. Unaweza kuwa na kundi kubwa la wasomi nchi nzima lakini hawajaelimika. Hawana maarifa. Hawana uwezo wa kutumia elimu waliyoipata kwa faida ya jamii yao.
Elimu ni changamoto kubwa sana katika suala zima la mikataba kama ilivyo kwa uroho, tamaa, ulafi, wizi, uwongo, uzushi, kutokuwa makini, ulalamishi, ufisadi uliokithiri, kutotosheka nk.
Kuwa na rundo la wenye vyeti sio kuwa na wasomi. Wasomi ni wale wenye uwezo wa kutafsiri elimu zao walizopata ndani na nje ya Darasa kubadili maisha ya jamii zao.
Nitakupa mfano wa wasomi walioshindwa kutumia elimu zao na hivi sasa wanaonekana kama tumaini kwa serikali ya CCM. Prof. Muhongo - alikuwa mwenyekiti wa Bodi ya STAMICO mwaka 2005. Aliruhusu Kiwira kuuzwa kwa Mkapa, Yona na wenzake. Alikuwa mshauri mtaalamu kwa kampuni ya Sutton Resources ilipokuwa inauza mgodi wa Bulyanhulu kwa Barrick. Alikuwa kwenye timu iliyoandika sera ya madini ya mwaka 1997 na sheria ya madini ya mwaka 1998 ambayo ndio chanzo cha mikataba ya sasa ya madini ambayo imeligharimu sana Taifa.
Huyu ni msomi lakini at the hour of need hakusaidia jamii yake. Hata tulipokuwa tunahangaika (ukiwemo wewe MwanaKijiji) kuleta mabadiliko katika sekta ya madini hakupaza sauti yake. Hawa ndio wasomi wetu.

Ninapingana na hitimisho lako ambalo ndio ulianza nalo kwenye kichwa, mikataba mibovu inatokana na elimu mbovu. Elimu ambayo inaangalia maslahi binafsi badala ya maslahi ya Umma.
 
Wasomi hawa kwa mtazamo wangu ni wasomi kweli na wameelimika vya kutosha lakini wanachagua njia zinazoliangamiza Taifa wakiwa na uelewa kamili, hawajawa brain-washed na wazungu, wanaweza kuzifafanua vizuri kabisa sheria hizi za kizungu, ni suala la kuchagua tu, aidha kwa maslahi binafsi au kwa misukumo mbalimbali........tukitaka kutumia excuse ya kutoelimika ni kama tunawatoa mzigo wezi hawa kama si majambazi wa rasilimali za Taifa. Narudia kusema. WANAJUA WANACHOKIFANYA
Dada hawa wasomi wetu wameelimika ktk elimu ya vitabuni na hivyo sheria wanayoweza kuitumia ni ile inayowalinda wakoloni wawekezaji maana ndio ilokuwepo vitabuni. hakuna sheria ya kimataifa inayoandikwa kwa ajili yetu. Hata Marekani au Canada wana sera zao, hivyo kama hukusema ni lazima mwekezaji atoe share, asajili ktk soko letu DSE huyo mwanasheria ataweza vipi kutetea haki hiyo. Nini nafasi yetu ktk mikataba na kadhalika itakuwa kazi kubwa kupata utetezi wa haki..

Sheria za madini ni sawa na man's law, Ni sheria ya mfumo dume, inayotazama upande mmoja kumlinda mwekezaji zaidi ya sisi maskini na ndo maana vifo vingi ktk migodi ya madini huwezi kukuta shirika linahusishwa na mauaji. Mashirika ya madini wanalindwa na International law zaidi ya wananchi na nchi husika, hivyo mwanasheria msomi wetu ataitafsiri tu sheria iliyopo kuwalinda mabeberu na sii kutulinda sisi. Mgogoro wetu na Malawi tunatumia sheria ya mkataba wa Muingereza na Mjarumani tena karibu tunatoana macho lakini makubaliano na sheria yetu sisi ni ipi? Je, sisi wenyewe tumekubaliana vipi ama tuna sheria gani - hakuna! isipokuwa ile sheria ilitungwa karne 2 zilizopita kuwalinda wao na kwa maslahi yao lakini tunajiita wasomi.
 
mimi sina taaluma ya sheria lakini kuna mikataba nikisoma kurasa chache naona hatari iliyopo mbeleni. Tatizo ni kukosa uzalendo kwa taifa na ndio maana serikali imejiwekea record nzuri ya kushindwa kesi mahakamani.

Nadhani tuwe na mijadala huru kupitia radio na TV ili watu wajadili namna ya kuhandle rasilimali zetu mfano 'sera ya gas na mafuta' badala ya kuitisha makongamano ya siasa kama yale kigoda cha mwalimu. Naamini wapo watanzania wengi sana wanaoweza kutoa points za maana kupitia mijadala hii
 
Back
Top Bottom