Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kwa maoni yangu ni kejeli kubwa na ni tusi kwa kudai kuwa tatizo letu la mikataba ni tatizo la watu kukosa elimu. Hivi tunaweza kusema tatizo la sekta ya afya ni watu kukosa elimu ya udaktari? au tatizo la elimu watu kukosa elimu ya ualimu? Tanzania imekuwa na wanasheria mahiri wengi tu napo wengi tu ambao wamespecialize katika international contracts na sheria hizi za mikataba. Ni kweli Tanzania haina watu wenye elimu hiyo?
Au wanaposema tatizo ni elimu wana maana kuwa wasomi wetu (wanasheria na wengine) wanapokaa na hawa wageni kwenye meza moja wasomi wetu hawana upeo au uwezo wa kujadiliana kisomi? Kama hili ni kweli kundi lililopelekwa kujadiliana na wa Malawi lenye kuhusisha wasomi lina matumaini gani? Hivi juzi MWakyembe na wataalamu toka Wizarani wameenda Ujerumani na huko wana/wamekutana na wadau mbalimbali wa sekta ya anga na usafirishaji. Sasa waje kuingia mkataba halafu baadaye tuseme hatuna wataalamu wenye ujuzi wa mambo ya anga na usafirishaji?
It is fallacious kudai kuwa tatizo letu la mikataba ni tatizo linalotokana na elimu? Kivipi.. hatuna wasomi, vyuo vyetu havijui kufundisha mambo ya mikataba? wanafunzi wetu ni wagumu kuelewa? au ni nini hasa? Maana hata Kikwete aliwahi kusema alipokuwa Sweden?? kuwa tatizo la nchi kuingia mikataba mibovu ni kwa sababu wanasheria wetu hawana ujuzi sana! Na hakuna aliyebisha na hivyo kufanya iaminike kuwa tatizo ni elimu.
Sasa kama tatizo ni elimu na kuwa hatuna wasomi wa kuingia mikataba mizuri hiki kimbelembele cha kuendelea kuingia mikataba mingine kinatoka wapi? Kama kweli hatuna wasomi wenye kuweza kutuletea deals nzuri kwenye mikataba ni kitu gani kinatufanya tukubali kuingia mikataba mingine tukitarajia kuwa itakuwa tofauti? Si imewahi kusemwa kuwa the classical definition of insanity is doing the same thing, the same way, every time expecting different results? Kila ukipanda michongoma unakaa pembeni na kuombea mpunga uote? na ukiota mchongoma unalaumu udongo?
Au wanaposema tatizo ni elimu wana maana kuwa wasomi wetu (wanasheria na wengine) wanapokaa na hawa wageni kwenye meza moja wasomi wetu hawana upeo au uwezo wa kujadiliana kisomi? Kama hili ni kweli kundi lililopelekwa kujadiliana na wa Malawi lenye kuhusisha wasomi lina matumaini gani? Hivi juzi MWakyembe na wataalamu toka Wizarani wameenda Ujerumani na huko wana/wamekutana na wadau mbalimbali wa sekta ya anga na usafirishaji. Sasa waje kuingia mkataba halafu baadaye tuseme hatuna wataalamu wenye ujuzi wa mambo ya anga na usafirishaji?
It is fallacious kudai kuwa tatizo letu la mikataba ni tatizo linalotokana na elimu? Kivipi.. hatuna wasomi, vyuo vyetu havijui kufundisha mambo ya mikataba? wanafunzi wetu ni wagumu kuelewa? au ni nini hasa? Maana hata Kikwete aliwahi kusema alipokuwa Sweden?? kuwa tatizo la nchi kuingia mikataba mibovu ni kwa sababu wanasheria wetu hawana ujuzi sana! Na hakuna aliyebisha na hivyo kufanya iaminike kuwa tatizo ni elimu.
Sasa kama tatizo ni elimu na kuwa hatuna wasomi wa kuingia mikataba mizuri hiki kimbelembele cha kuendelea kuingia mikataba mingine kinatoka wapi? Kama kweli hatuna wasomi wenye kuweza kutuletea deals nzuri kwenye mikataba ni kitu gani kinatufanya tukubali kuingia mikataba mingine tukitarajia kuwa itakuwa tofauti? Si imewahi kusemwa kuwa the classical definition of insanity is doing the same thing, the same way, every time expecting different results? Kila ukipanda michongoma unakaa pembeni na kuombea mpunga uote? na ukiota mchongoma unalaumu udongo?