Ngoda95
JF-Expert Member
- Sep 15, 2011
- 2,690
- 4,919
Mimi nilijifunza toka Jogoo halijachwa..Mnaanzishaga mada za kutuponda tunatulia tu kusikilizia maumivu maana mengine ni ya ukweli yanachoma kama pasi. Leo hili ni lenu. Na mjifunze kupitia huu uzi.
Kuna mambo hayahitaji ujuaji na ubishi ubishi usio wa lazima.
Kiburi na kupuuzana puuzana hakuna sababu, hakuna aliye malaika tukikosena tusameheane kwa yenye kustahili msamaha.
Tukizidisha makwazo "watagongwa tu" kwani kwa vigezo hivyo hivyo vilivyonivutia Mimi na mwingine vitamvutia ataombwa na kwa sababu ya stress wala hatagoma. Hakuna mshindi katika haya mambo anaweza kuliwa na wala usigundue kabisa.
Mimi kwa Kujiamini Kabisa Nimejifunza na kila uchwao najifunza na kubadilika ili kuboresha mahusiano na mke wangu. Once nikikengeuka sitajisahau, hakuna La maana sana huko michepukoni zaidi ni kujiongezea cost za maisha tu.