Unakiri kua ndoa ikivunjika mwanamke ndiye anayeangaliwa,umewahijiuliza mke na mume wakichepuka yupi huleta aibu sana kwenye familia na jamii kwa ujumla.. acheni kuchepuka sio vuzuri,ukiona vipi achana na mwanaume uende ukaishi peke yako ufanye unavyotaka,kama mume anachepuka jaribu kumrekebisha vile unavyoweza nasio wewe kuanza kuchepuka kwasababu unakua unajishalilisha nakuleta fedheha kwa watoto na ndugu zako pamoja na jamaa unaoheshimiana nao,usijione wewe tu angalia na jamii itakuonaje,fanya kitu ambacho unaweza kuongea mbele ya watu ukaeleweka.
Tatizo lenu ni moja. Wanawake wawe na maadili nyie mfanye upuuzi isionekane hamna maadili. Mnawafundisha nini watoto wenu wa kike na wa kiume?
.
.
Kwanini tusiungane pamoja kurekebisha maadili ya jamii yote kwa ujumla? Jiangalia jinsi ulivyo...je ungependa mtoto wako wa kike aje kupata mume mwenye tabia kama zako? Uko proud na tabia zako na huna shaka mwanao akipata wa kufanana na wewe?
Tusiongee tu ili mradi tunaongea..tusikariri misemo ambayo kiuhalisia haitekelezeki.
.
aliyekuambia mwanamke akichepuka ni aibu kwa jamii. Jamii ipi? Hiyo aibu nani anaona? Mchepukaji au jamii?
.
.
Na je wewe mwanaume unayechepuka jamii inakuonaje? Rijali ama? Tuache kukandamiza upande mmoja..tuhubiri maadili both sides na hapo ndio tutafanikiwa. Jamii itaelimika vipi km maadili atekeleze mwanamke peke yake? Elimu itusaidie jamani.
.
.
Mnasomesha watoto wenu wa kike mnategemea mawazo yake yaendane na ya mwaka 47? Dunia haipo hivyo..kila kitu kinabadilika.
.
.
Mume na mke wapendane, waheshimiane na michepuko iwe mwiko! Ukichepuka nami unanipa mzuka wa kufanya umayofanya..tena natamani haswa yaaani. Unanipa vishawishi mwenyewe bila kujijua.
Na muache kutuambia habari ya nature yenu wanaume maana imeprove wrong! Kwa maisha ya sasa nawasihi muache kuchepuka maana mnawafundisha wake zenu tabia mbaya!
.
.
Hiyo aibu kwa jamii ifafanue vizuri. Kama muhusika haoni aibu inamuathiri nini? Watu hawana aibu wanafanya kwa kukusudia. Aibu ni pale unapofumaniwa...i
otherwise ni raha tu.
.
.
BILA KICHWA CHA NYUMBA KUBADILIKA MENGINE HAYATAENDA SAWA. Badilikeni nyie mnaojiita vichwa! sisi tunafuata muongozo wenu. Nyie ni madereva wa malori sisi ni makondakta. Msije mkawa kama yule anayejitapa dereva wa lori kumbe lori lenyewe limekongoroka na service hafanyi!