SoC01 Kuboresha kijiji kimoja nchini kuwa na Makazi bora na mfano wa Tanzania ya siku zijazo

Stories of Change - 2021 Competition

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Ninaamini nyumba bora huboresha afya ya mwili na akili. Mahitaji ya msingi ya binadamu ni hewa safi na kuishi sehemu isiyosababisha maradhi mfano baridi na unyevu unyevu. Nyumba bora huleta fahari kwa mwenye nyumba hata kukaribisha wageni na humjengea heshima katika jamii.

Watanzania wengi wanaishi kwenye nyumba za udongo na nyasi. Baadhi ya nyumba hizi zina ubora duni kiasi cha kwamba mvua zikinyesha wakazi wananyeshewa na maji kuingia ndani na kuleta hali ya unyevu nyevu. Pia nyingi hazina madirisha makubwa ya kuingiza hewa ya kutosha.

JamiiForums kama jumuiya ya jamii inaweza kuanzisha mchakato wa kujenga kijiji cha mfano. Wengine watakaopenda muundo wa kijiji hiki wataiga. Kijiji kichaguliwe katika Tanzania. Wanakijiji washirikishwe katika mpango na kama wakiridhia mchakato uendelee.

Ipatikane idadi ya wanakijiji, wenye uwezo wa kufanya kazi, vipato vyao nk. Wenye vipato wawe tayari kuchangia gharama za ujenzi. Wazee na walemavu wapatiwe msaada kutokana na michango ya jamii ikiwemo diaspora.

Wapatikane wabunifu watakao buni ramani ya kijiji na majengo. Majengo ya vyumba viwili na sebule pia vyumba vitatu na sebule kutokana na ukubwa wa familia. Nyumba ziwe sa saruji na kuwezekwa kwa mabati. Kuwe ná ceiling board pamoja na madirisha yanayoingiza hewa ya kutosha.

Vyoo viwe vya shimo vyenye sahani ya Indian toilet. Kila nyumba iwe na gutters za kuvunia maji pia kuwe na simtank.

Wanakijiji wanaweza kupatiwa majiko ya gesi pia kuhamasishwa kupanda miti. Hii ni katika harakati za kuokoa matumizi ya misitu na kuepuka jangwa siku zijazo.

Haya yakifanikiwa tuiombe serikali kujenga shule, zahanati, soko na ikiwezekana kituo cha polisi kijijini.

Katika kuchagua kijiji kiwe wapi ni lazima kuwe na vigezo vitakavyo washawishi wachangiaji kuchangia.
 
Awesome idea, kuna documentary inaitwa " grand designs: the street " walifanya experiment ya namna hiyo ambapo washiriki walijenga myumba za makazi kulingana na uhitaji na uwezo, kwa kufuata taratibu zilizowekwa.
 
Mbona Moshi walishatoa mfano siku nyingi. Nakumbuka 2013 tulikua na wazo Kama Hilo tukatipitia household survey reports vipo vijiji Moshi Kuna nyumba Bora za makazi, vyoo, maji tiririka, mpango wa makazi na kilimo, huduma nyingine za jamii hospital/zahanati.

Ila kasori kubwa ni sehemu za maziko vituo vya polisi kulikua hkauna pamoja na kuwa na miundo mbinu mibaya ya masoko/gulio na ujenzi holela wa makanisa naframe za maduka
 
Mbona Moshi walishatoa mfano siku nyingi. Nakumbuka 2013 tulikua na wazo Kama Hilo tukatipitia household survey reports vipo vijiji Moshi Kuna nyumba Bora za makazi, vyoo, maji tiririka, mpango wa makazi na kilimo, huduma nyingine za jamii hospital/zahanati.

Ila kasori kubwa ni sehemu za maziko vituo vya polisi kulikua hkauna pamoja na kuwa na miundo mbinu mibaya ya masoko/gulio na ujenzi holela wa makanisa naframe za maduka
Hiki kijiji safari hii kiwe mkoa mwingine Kilimanjaro walisha jaribu. Tujifunze kutoka Kilimanjaro tuwe na eneo la kuzikia na eneo la nyumba za ibada.
 
Mbona Moshi walishatoa mfano siku nyingi. Nakumbuka 2013 tulikua na wazo Kama Hilo tukatipitia household survey reports vipo vijiji Moshi Kuna nyumba Bora za makazi, vyoo, maji tiririka, mpango wa makazi na kilimo, huduma nyingine za jamii hospital/zahanati.

Ila kasori kubwa ni sehemu za maziko vituo vya polisi kulikua hkauna pamoja na kuwa na miundo mbinu mibaya ya masoko/gulio na ujenzi holela wa makanisa naframe za maduka
Moshi vijiji ni vichache sana sehemu nyingi zimekuwa miji
 
Wazo zuri sana. Nitakuwa nachungulia hapa. Pa kuanzia yaweza kuwa sehemu ambayo walipata majanga yawe ya asili au yaliyosababishwa na watu kama wale waliochomewaga nyumba na waasi wa Msumbiji kule.
 
Hili wazo halitekelezeki kwa nchi kama Tanzania na umasikini wake

hao unataka pesa za wanajf zipigwe pia hakuna kijiji kinachoweza kuyaiga hayo bila pesa
Kila anaetuma pesa aweke risiti wazi na pesa zote zijumlishwe na wahusika watoe maelezo ya matumizi.
 
Nilivyoona heading nikajua ni wazo la kujenga Nyumba za asili za kitanzania (Kama zile za wamasai vijijini) au kama Nyumba za pale Makumbusho Kijitonyama Dar,

Yaani kijengwe kijiji ambacho kitakua na Nyumba za asili ila zenye ubora zaidi but kwa kutumia zana/materials ya asili kama vile miti,udongo na nyasi ambazo zitakua ni enviromentally friendly,

Anyway hata idea yako sio mbaya,

Good luck.
 
Back
Top Bottom