Points 10 za ujenzi: Joto ndani ya jengo

greater than

JF-Expert Member
Sep 22, 2018
781
1,211
MAKALA YA 2
Karibuni tena katika Makala yenye kutoa elimu juu ya mambo muhimu kwenye ujenzi wa Majengo (madogo) I.e. Nyumba, Maduka, Darasa, Zahanati n.k

Leo tunatazamia katika Halijoto ndani ya jengo.Hili suala linawasumbua wakazi wa mikoa ya ukanda wa Pwani, Longido, Loliondo, Simanjiro, Mwanza n.k

1. Halijoto ni moja katika kitu kinachofanya mtu uone Jengo uone ni zuri pindi unapokuwa ndani.
Nje ya jengo, joto ni 30⁰C lakini ukiingia ndani joto linakuwa 36⁰C,hauwezi ukasema hilo jengo ni zuri.

Kwa upana wa Wilaya au Mji,joto usababishwa na;
I)Ukaribu wa Mji na Bahari,Ziwa au Bwawa
ii)altitude ya mji
iii)Mpango mji mbovu
iv)Ukosefu wa Uoto na mvua

2. Kuna miji ambayo ina halijoto kavu,yani inajoto kali lakini kiwango cha unyevu katika hewa ni chini ya 50%
Mfano;Longido,Loliondo,Simanjiro,Dodoma na Same.
Kwenye hii miji ,joto kali lakini jasho kidogo
Kuna miji ambayo ina halijoto lenye unyevu,yaani ina joto halafu na unyevu kwenye hewa unazidi 50%.
Kwa mfano;Dar,Tanga mjini,Zanzibar,Mtwara na Bagamoyo na Mwanza.
Kwenye hii miji joto kali na jasho la kutosha

3. Mambo yanayosababisha joto ndani ya Jengo.(Kabla ya ujenzi)

I) Umbo la Jengo : Kwa mikoa iliyo na joto ,inashauriwa jengo liwe na umbo la mstatili kuliko mraba. Umbo hili linaipa uraisi upepo kuingia na kutoka ndani ya jengo ukiwa bado una kasi.
Mfano.Majengo ya wakoloni mkoani Dar I.e. ikulu
II) Uelekeo wa jengo: Mapana ya jengo yanatakiwa yaelekee mstari wa jua kuliko marefu yake.
Mf.Kota za polisi Oysterbay

III) Nafasi kati ya jengo na jengo:Angalau kuwe na kuwa na nafasi isiyopungua mita 3,ili kuruhusu mzunguko wa upepo.

4. Visababishi vya joto (kipindi cha Ujenzi )
I) Urefu kati ya Sakafu na Dari;joto huwa ni hewa nyepesi kwahiyo itakaa karibia na dari. Hakikisha urefu wa Dari katika Chumba chenye makutano ya watu wengi kinazidi mita 2.5
II)Idadi ya Madirisha pale itakapowezekana hakikisha kila chumba kuna madirisha mawili

III)Ukubwa wa madirisha: Kadri dirisha linavyokuwa kubwa ndipo unaporuhusu upepo mwingi kuingia

iv) Madirisha yawekwe uelekeo wa upepo
Na
Panapowekwa dirisha:Madirisha ambapo hewa huingia yaanzie angalau 0.8m kutokea kwenye sakafu,hewa baridi huwa nzito so huwa chini.

V ) Ukubwa wa vyumba : watu hutaka kujaza vyumba vingi kwenye Majengo Yao na nafasi ikiwa ndogo, hutaka vyumba vipunguzwe vipimo .

VI) Milango mingi : kutoka jikoni kwenda sebreni mlango, kutoka sebreni kwenda korido ya chumbani kuna mlango,kwenda sehemu ya kula mlango:hewa haizunguki hapo.
 
5.Visababishi vya joto (Ukiwa unamalizia ujenzi/Finishing)
I) Matilio :Chumba kinachowekwa tiles/Marumaru ukutani,joto huongezeka.
Mfano:vyooni.
II) Rangi : Usipake chumba /jengo rangi nyeusi.
Vyumba vyenye kupigwa sana jua epuka kupaka rangi kali mfano Nyekundu/Orange
III)Ukuta kuachwa mtupu bila plasta
IV) Ukosefu wa Dari :Joto lite huingia ndani ya jengo.
V) Vioo : haya matilio huwa hayaruhusu joto kutoka.

6.Visababishi vya Joto (Jengo likianza kutumika)
I) Vifaa vya umeme : vifaa hivi huzalisha joto mfano:taa,Kompyuta,Friji,mashine
II) Samani/Furniture : Chumba kikiwa na furniture nyingi na vitu kama nguo, joto huongezeka.
III) Idadi watu :watu wakiwa wengi ndani joto huongezeka.
IV) Matumizi ya jengo: Shughuli kama ya kupika huongeza joto

7.Visababishi vya nje ya Nyumba
I) Miti mirefu/mikubwa kuwa karibu na nyumba
II) Kutoweka Nyasi/Maua kuzunguka nyumba
III) Pavements: Yan eneo kubwa la kiwanja kuwa na pavers

8.Joto huweza kupunguzwa ndani ya jengo kwa njia kuu mbili, Njia za Asili na za umeme.
Njia za umeme
I) kutumia Feni
II) Kutumia kiyoyozi
Njia hizi nategemea umeme katika kufanikisha hilo,lakini ni gharama na kwa wengine si nzuri kiafya

9.Njia za Asili.
I)Kuwa na Ramani iliyosanifiwa kitaalam:Usichukue ramani mtandaoni
Mfano:Nyumba nyingi za Marekani,Canada na Ulaya majiko huwa mbele ili upepo ukivuma, joto la jikoni liende sebreni,

II) Kuzingatia matumizi bora ya kiwanja
I.e usijenge zaidi ya 70% ya kiwanja
Sehemu kubwa ya nje izungwe na Uoto kuliko pavements.

III) Kuacha wazi madirisha hasa usiku: ukuta Huanza kutoa joto ambalo ilihifadhi mchana kutwa
IV) Kutumia vifaa vya umeme vya kisasa.
V) Kutumia matilio yenye kuendana na halijoto ya mji husika.
Mfano.madirisha ya vioo ni mazuri kwa mikoa yenye ubaridi.

VI) Kufuata ushauri wa wataalam.
VII) Kuweka Swimming pool au water fountain katika upande ambao upepo uvuma kuelekea kwenye jengo : Maji yatapunguza joto la hewa kabla ya kuingia ndani.
VIII) Kuweka tiles/Marumaru za ukutani nje ya jengo, hii ni miji yenye joto kavu pekee.
IX) Ila kama unapenda madirisha ya vioo, heri yale ya kufunguka nje au kuna vioo maalum vyenye low-e,kwa bongo bado sijapata viona hata kwa waturuki madukani

10.Uzruri wa jengo ni muonekano lakini utamu wa jengo ni halijoto nzuri.


Nakaribisha maoni na maswali.
Pendekezeni mada mtakazopenda zijadiliwe huko mbeleni (mni PM)
 
Karibuni tena katika Makala yenye kutoa elimu juu ya mambo muhimu kwenye ujenzi wa Majengo (madogo) I.e. Nyumba,Maduka,Darasa,Zahanati n.k

Leo tunatazamia katika Halijoto ndani ya jengo.Hili suala linawasumbua wakazi wa mikoa ya ukanda wa Pwani,Longido,Loliondo,Simanjiro ,Mwanza n.k

1.Halijoto ni moja katika kitu kinachofanya mtu uone Jengo uone ni zuri pindi unapokuwa ndani.
Nje ya jengo,joto ni 30⁰C lakini ukiingia ndani joto linakuwa 36⁰C,hauwezi ukasema hilo jengo ni zuri.

Kwa upana wa Wilaya au Mji,joto usababishwa na;
I)Ukaribu wa Mji na Bahari,Ziwa au Bwawa
ii)altitude ya mji
iii)Mpango mji mbovu
iv)Ukosefu wa Uoto na mvua

2.Kuna miji ambayo ina halijoto kavu,yani inajoto kali lakini kiwango cha unyevu katika hewa ni chini ya 50%
Mfano;Longido,Loliondo,Simanjiro,Dodoma na Same.
Kwenye hii miji ,joto kali lakini jasho kidogo
Kuna miji ambayo ina halijoto lenye unyevu,yaani ina joto halafu na unyevu kwenye hewa unazidi 50%.
Kwa mfano;Dar,Tanga mjini,Zanzibar,Mtwara na Bagamoyo na Mwanza.
Kwenye hii miji joto kali na jasho la kutosha

3.Mambo yanayosababisha joto ndani ya Jengo.(Kabla ya ujenzi)

I) Umbo la Jengo : Kwa mikoa iliyo na joto ,inashauriwa jengo liwe na umbo la mstatili kuliko mraba. Umbo hili linaipa uraisi upepo kuingia na kutoka ndani ya jengo ukiwa bado una kasi.
Mfano.Majengo ya wakoloni mkoani Dar I.e. ikulu
II) Uelekeo wa jengo: Mapana ya jengo yanatakiwa yaelekee mstari wa jua kuliko marefu yake.
Mf.Kota za polisi Oysterbay

III) Nafasi kati ya jengo na jengo:Angalau kuwe na kuwa na nafasi isiyopungua mita 3,ili kuruhusu mzunguko wa upepo.

4.Visababishi vya joto (kipindi cha Ujenzi )
I) Urefu kati ya Sakafu na Dari;joto huwa ni hewa nyepesi kwahiyo itakaa karibia na dari. Hakikisha urefu wa Dari katika Chumba chenye makutano ya watu wengi kinazidi mita 2.5
II)Idadi ya Madirisha pale itakapowezekana hakikisha kila chumba kuna madirisha mawili

III)Ukubwa wa madirisha: Kadri dirisha linavyokuwa kubwa ndipo unaporuhusu upepo mwingi kuingia

iv) Madirisha yawekwe uelekeo wa upepo
Na
Panapowekwa dirisha:Madirisha ambapo hewa huingia yaanzie angalau 0.8m kutokea kwenye sakafu,hewa baridi huwa nzito so huwa chini.

V ) Ukubwa wa vyumba : watu hutaka kujaza vyumba vingi kwenye Majengo Yao na nafasi ikiwa ndogo, hutaka vyumba vipunguzwe vipimo .

VI) Milango mingi : kutoka jikoni kwenda sebreni mlango, kutoka sebreni kwenda korido ya chumbani kuna mlango,kwenda sehemu ya kula mlango:hewa haizunguki hapo.
Number V (5) sijakuelewa
 
Number V (5) sijakuelewa
Hapo nimelenga juu ya ukubwa wa Vyumba katika Jengo...
Huwa kuna viwango maalum vya vyumba ambapo hutofautiana kati ya mji na mji. Vyumba vya miji ya joto vinatakiwa viwe vikubwa kuliko miji ya baridi.
Ukubwa huo huruhusu watu kutobanana au kutakuwa karibu na vifaa vyenye joto..
Vyumba vya kulala angalau viwe vya mita 3.2 kwa mita 3.2
 
Duh! Nilitegemea labda ungesema kwa walioweka aluminium waweke sliding vent ambazo wanaweza acha wazi.
1.Aluminium ni metal yenye kupitisha joto kwa uharaka kuliko chuma, nayo ni kichagizi cha joto...
2.Kwenye zile Frem huwa kuna mikanda ya Mpira, ambayo mieusi, huchagiza pia katika kuingiza joto.
3.Dirisha za ku-slide na vent zake,ni nusu ya dirisha ndiyo hufanya kazi. Dirisha la 1.4m,nusu ndiyo huwa wazi...
 
1.Aluminium ni metal yenye kupitisha joto kwa uharaka kuliko chuma, nayo ni kichagizi cha joto...
2.Kwenye zile Frem huwa kuna mikanda ya Mpira, ambayo mieusi, huchagiza pia katika kuingiza joto.
3.Dirisha za ku-slide na vent zake,ni nusu ya dirisha ndiyo hufanya kazi. Dirisha la 1.4m,nusu ndiyo huwa wazi...
Nadhani hujaelewa, nazungumzia vent ambazo zinafunguka. Hizo ndio unaweza acha wazi na sio kama unavyoshauri hapa ni kwa ajili ya usalama zaidi.
 
Mwezi wa 4 naingia likizo
Kwa mwenye kuhitaji kutembelewa katika eneo lake, kukagua na kutoa ushauri juu ya tatizo lolote, kuwa huru kunijuza.

Gharama : Huduma hii ni bure
Usafiri : ndiyo pekee utagharamia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom