KUBENEA Vs LOWASSA

NI UHURU WANGU WA MAONI TU LAKINI PIMA MWENYEWE KAMA NI SAWA KWENYE ULIMWENGU WA SASA KWA MATOLEO SITA KUWA exPM FRONT PAGE! TENA KWA KURUDIA RUDIA KILE KILE.

Mzee usipandishe jazba, nadhani na wewe unatatizo na kuelewa mapema pia, repetition is one of the methodology to impart knowledge and understanding to dull scholars kama wewe mkuu labda na mimi na majorities hapa(pole I do wanna be offensive kwako) tujadili

Ushi
 
Ndugu Watanzani na msio Watanzani,
Ni fahari kwagu na kwenu kuwa na watu ambao tunawaita MASHUJAA WA NCHI HII. Kwa kipindi tunachoelekea hatutakuwa mbali sana na ukweli kuwa Kubenea ni mmoja wa mashujaa wa nchi. Nasema hivi kwa sababu ni wengi wanataarifa, wanajua na wanawaona mafisadi lakini kwao ni kama hawaoni wala hawasikii ingawa rohoni wanaumia. Ni jambo GUMU sana kwa mtu wa kawaida kabisa kumtaja mtu mwenye nguvu kama Edward mwenye kila uwezo hapa nchini kwenye ardhi hii (siyo mbinguni) kama afanyavyo ndugu yetu Kubenea. Tunakuombea ndugu yetu angalao uendelee na moyo huo huo wa kuwasema na wengine labda wataona HAYA kidogo lau kama si kuacha Ufisadi.
Wote tumeandika humu,,, lakini wasiwasi wangu ni kuwa kuna watu kama wachungaji wa kondoo,,, mzee wa Tanganyika,,,, anasema mengi kuwakemea mafisadi,, kuwa huyu kafanya hivi huyu kafanya vile,,, Mchezaji wa Maigizo,,, maigizo ya njaa,,,, labda atafanikiwa kumaliza kile kibanda chake! Njaa hii,,, njaa,,, njaa kali (lakini angepata wapi hizo 50M kama siyo maigizo yake). Eti anawaita waandishi wa habari kuzungumza nao. Jamani waandishi kuna mambo makubwa ya jamii ya kufanya na siyo kumsikiliza mwehu kama Mtikila,,, ndoyo Mtikila,,, anayejiita mchungaji sijui wa dhehebu gani,,,, Labda Rostam Azizi and E Lowasa Fool Church? Labda.
Watanzani tumezidi kuwa wapole na ndiyo jadi yetu,,, Lakini nawaambia kuwa WAKATI WAJA MTU MMOJA MWENYE ANGALAO UCHUNGU NA NCHI HII ATAKAPOSIMAMA NA KUSEMA SASA BASI YATOSHA!!!!!
Nimalizie kwa kuwakumbusha medani za kivita kwa wale angalao walipitia JKT. Vita ipiganwapo huwa tunamsaka Jemedari mkuu,,,, wote tuliona ama kusikia ya Uganda baada ya Amini kuikimbia nchi,,, ushindi ulikuwa wa wetu. Hali kadhalika EDWARD NGOYAI LOWASA (Na sijui kama huyu ni Mmasai kweli maana inasemekana mama yake alikuja na mimba baada ya kukataliwa na aliyempa mimba akalelewa kwa babu yake mzaa mama yake,,, akabatizwa kimasai,,, tutaona huko tuendako) AMBAYE NI JEMEDARI MKUU WA UFISADI TANGU AKIWA AICC NI LAZIMA JESHI HILI LIKIONGOZWA NA KUBENEA LIHAKIKISHE KUWA ANAKIMBIA KIKOSI CHAKE. Mr X PM EDWARD NGOYAI LOWASSA for the sake of Tanzania and your good wish to this nation, we ask you and your team to surrender all that belongs to Tanzanian.
No one will ever talk to you if you do so,,, Just surrender and go back to Monduli as you dont need that money to stay where you are now. Mwangalie mwenzako Pm aliyekutangulia Sumaye,,, nani anashughuli naye,,, aliondoka akaenda kijijini na ametulia ingawa naye alikuwa fisadi. maskini tuliokuwa Arusha kwenye Sullivan yeye na Mzee Msekwa wala hawakupitia VIP,,, tulipigana nao vikumbo.
jamani hii vita ndo inapamba moto,,, na kama tukiwa watoto wa Tanzania lazima tuseme na Kubenea anaendeleza mapambano,,, je tumwache mwenyewe?
Mungu mbariki Kubenea na team yake,,,
Mungu Ibariki Tanzania.
Mapambano yanaendelea.
 
Mwanahalisi la leo wanadai JK Kadanganya.

Sasa tuwangojee wataodai : Kubenea Vs JK
 
Oh! Niliandika bila kusoma maoni wa wengine. Naomba niseme hivi, sote tuna nia moja....Nadhani kuna wachache tu wenye nia mbaya na Taifa hili na haiyumkini tutwashinda. Ila jamani to be honest, kutoka kwenye mtima wa moyo wangu kabisa, uandishi wa jinsi hiyo sio wa karne ya sasa. Mimi naamini kubenea ana masikio na amesikia atajua yupi mwenye nia njema na yupi mwenye nia mbaya nae.

Narudia, hata kama wote tukaside kwa Kubea, ukweli utabaki palepale, SIO UANDISHI WA KISTAARABU.

Ndugu yangu Msongoru (sijui kama wewe ni msongoru kweli kwa tafsiri niijuayo ya kuwa UMETANGULIA,,, sijui. Labda nikuulize wewe ni uandishi gani unaousemea? Mwizi,, muuaji mfisadi unataka tuongee naye kistaarabu,,, tumwandike kwa kumremba? loh! Anza gazeti lako na uandike hayo unayoyaita USTAARABU. Na tena Unapozungumza ishu kama hii ujue unasema haki za baba yako, mama yako, watoto wako, mkeo na kila anayekuhusu. Ujambazi unafanyika mkeo anaathiriwa wewe unataka uwe mstaarabu kwa jambazi! mara nyingine tuangalie ya kuchangia,,,, Kama wewe ni mshirika wa EL basi kaa ukijua kuwa,,, hatutaacha kusema ya Lowasa hadi atakaporudisha na kujisafisha.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake
 
Mkuu hapo umepotoka nafikiri labda wewe umetumwa na huyo Lowassa uchokoze ili msikie watu watasema nini. Inawezekana sana makala nyingi zikawa zanamlenga Lowassa lkn ukiangalia kwa undani jamaa ndiyo centre ya ufisadi maana ndiyo mwana mtandao mkuu. Lakini pia Baba wa taifa alishasema kuwa jamaa mla rushwa hivyo wacha jamaa amuandike mimi nitamlaumu Kubenea iwapo tu ataandika uwongo juu ya jamaa. Na naamini kuwa yote ni kweli vinginevyo aende mahakani tuone. MIMI NITATOA MCHANGO KWA KUBENEA KUWEKA WAKILI.
 
Lowassa anaandikwa kwa sababu ana laana ya ufisadi toka wakali wa baba wa Taifa J.K. Nyerere. Ni kama Yuda Iscariot kwenye biblia. Amesaliti Tanzania hivyo ataandikwa daima na milele. Kajinyoge kama unampenda hivyo.

Byase
 
FDR.Jr,Kuhani,Mpita Njia,Sikonge,Nshunju,shedafa,Eeka,....

..Lowassa amekuwa akiyatumia magazeti kwa muda mrefu sana. alianza miaka ya 90 kipindi kile akitumia kura ya maoni ya kila juma ktk gazeti la majira.

..baada ya uchaguzi wa 1995 akaendesha kampeni ya miaka 10 kumsakama na kumuandika vibaya Waziri Mkuu Frederick Sumaye.

..mbinu chafu alizozitumia kuwashughulikia maadui wake wa kisiasa zinamrudia yeye mwenyewe sasa.
 
Kwa hiyo Joka Kuu unataka kuniambia kuwa hizo ni mbinu za Lowasa na Kubenea kujenga jina lake,,,, mimi hapo sielewi wadau,,,, jamani mnasemaje hapo?
 
Haya ni mawazo ya kifisadi nayo! Yaani Kubenea kuconcentrate na Lowasa ni tatizo!!!!! Kubenea kama anayoandika kuhusu Lowasa ni ya kweli mwache aendelee kuandika mpaka lowasa asuffocate au ayeyuke kabisa!! Maana hatuwezi kuwa tunashika habari hii kesho ile, si mafisadi watapumua sana! Kila mtu ashike mraba wake ikiwezekana. Kubenea na mraba wa lowasa wengine na wa EPA wengine wa vijisent, kiwira nk! Na wewe mtoa maada shika mraba wako mpaka tuuone ukiisha, sio kuanza tu halafu unaachia njiani!

umenikumbusha mbali, enzi za jeshini!!
miraba!
 
maane kuwa makini na nchi inavyokwenda.Kubenea kama alikuwa na demu Lowasa akamzidi ujuzi aseme,maana anachosa kama hana habari aseme,wimbo wa lowasa sasa ni zilipendwa zinazopigwa na uncle j radio one,toooooo much lowasa kwenye gazeti lake,kama anapata kitambi mpaka anashindwa kutafuta habari aanzae kufatilia ufisadi wa waganga wa kienyeji wanaomaliza maalbino!ndio ufisadi ulioshika chati kwa sasa,Lowasa alikuibia mfukoni kwako????????????????????????ufisadi anaoufanya Mkapa na Mkewe wakisaidiwa na Mramba yeye kubenea hauoni??????????au wamempa fungu lake lowasa akamnyima???au ndio CHUKI BINAFSI???
 
Ndugu yangu Msongoru (sijui kama wewe ni msongoru kweli kwa tafsiri niijuayo ya kuwa UMETANGULIA,,, sijui. Labda nikuulize wewe ni uandishi gani unaousemea? Mwizi,, muuaji mfisadi unataka tuongee naye kistaarabu,,, tumwandike kwa kumremba? loh! Anza gazeti lako na uandike hayo unayoyaita USTAARABU. Na tena Unapozungumza ishu kama hii ujue unasema haki za baba yako, mama yako, watoto wako, mkeo na kila anayekuhusu. Ujambazi unafanyika mkeo anaathiriwa wewe unataka uwe mstaarabu kwa jambazi! mara nyingine tuangalie ya kuchangia,,,, Kama wewe ni mshirika wa EL basi kaa ukijua kuwa,,, hatutaacha kusema ya Lowasa hadi atakaporudisha na kujisafisha.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake


Tafsiri iko sawa! Mimi ninachsema ni kwamba nina wasiwasi huwa hamsomi anachoandika Kubenea, ila mnaishia kwa heading zake tu! Hamna kitu mle naniii! Anarudi kile kile. Ok, lets say lowasa ni fisadi, je ni wa jengo la UVCCM tu? Humo kwenye jengo mie hata chembe ya mchanga hainihusu ukumbuke. SAS kama kweli Mungu ibariki Tanzania, tuwe wakweli kumsaidia ndugu yetu kubenea, hapa mnamdanganya!
 
Mzee usipandishe jazba, nadhani na wewe unatatizo na kuelewa mapema pia, repetition is one of the methodology to impart knowledge and understanding to dull scholars kama wewe mkuu labda na mimi na majorities hapa(pole I do wanna be offensive kwako) tujadili

Ushi

Ushi, hebu kasome kwanza anachoandika Kubenea, ndipo uje tujadili....
 
Ni wazi kubenea hana akili ya kutoa mawazo mapya kila siku anaandika yaleyale.gazeti lake lita kosa wasomaji muda si mrefu kutoka sasa.kwa kuwa watu wanapenda mawazo mapya
 
maane kuwa makini na nchi inavyokwenda.Kubenea kama alikuwa na demu Lowasa akamzidi ujuzi aseme,maana anachosa kama hana habari aseme,wimbo wa lowasa sasa ni zilipendwa zinazopigwa na uncle j radio one,toooooo much lowasa kwenye gazeti lake,kama anapata kitambi mpaka anashindwa kutafuta habari aanzae kufatilia ufisadi wa waganga wa kienyeji wanaomaliza maalbino!ndio ufisadi ulioshika chati kwa sasa,Lowasa alikuibia mfukoni kwako????????????????????????ufisadi anaoufanya Mkapa na Mkewe wakisaidiwa na Mramba yeye kubenea hauoni??????????au wamempa fungu lake lowasa akamnyima???au ndio CHUKI BINAFSI???


kwani wewe umezuiwa kuandika kuhusu hayo mengine?
au umetuma taarifa zao kwa kubenea na yeye akakataa
kutoa kwenye gazeti?
 
Ni wazi kubenea hana akili ya kutoa mawazo mapya kila siku anaandika yaleyale.gazeti lake lita kosa wasomaji muda si mrefu kutoka sasa.kwa kuwa watu wanapenda mawazo mapya

Weye fisadi waelekea unaota ndoto za mchana kuhusu Mwanahalisi. Unajua watumishi wengi wa serikali(who have sympathy with the li-government) hawapendi magazeti yanayoikosoa serikali.

Lakini hali ni tofauti kwa Mwanahalisi; pamoja na kwamba na lenyewe linaikosoa sana serikali.
 
maane kuwa makini na nchi inavyokwenda.Kubenea kama alikuwa na demu Lowasa akamzidi ujuzi aseme,maana anachosa kama hana habari aseme,wimbo wa lowasa sasa ni zilipendwa zinazopigwa na uncle j radio one,toooooo much lowasa kwenye gazeti lake,kama anapata kitambi mpaka anashindwa kutafuta habari aanzae kufatilia ufisadi wa waganga wa kienyeji wanaomaliza maalbino!ndio ufisadi ulioshika chati kwa sasa,Lowasa alikuibia mfukoni kwako????????????????????????ufisadi anaoufanya Mkapa na Mkewe wakisaidiwa na Mramba yeye kubenea hauoni??????????au wamempa fungu lake lowasa akamnyima???au ndio CHUKI BINAFSI???

Ukiwa na MAshetani wawili, chagua lile lililochovu kufanalo.
 
Its like this jamani,Kubenea katika kazi zake aliibua kashfa ya mkataba wa jengo la UVCCM NA Lowassa kuhusika kwa kiasi kikubwa.Lowassa alikataa juu ya kuhusika kwake na hivyo kutishia kumburuza Kubenea Mahakamani kwa kumuandika hovyo na uongo. ili kuprove ukweli kubenea akaendeleza kazi kwa kuwahoji wahusika mbalimbali kama akina Masilingi na Nagu na wote walikana kuhusika na mkataba.Katika kuprove zaidi ametuletea mkataba wenyewe kwenye front page.So Whats Wrong here?Amekusudia Kuclarify everything kuondoa unnecessary doubts.
 
Back
Top Bottom