KUBENEA Vs LOWASSA

KUBENEA Vs LOWASSA

huo ndio unaitwa uandishi, you continue to write the news even if it looses the heat.
Ripota anaandika ripoti anaishia hapo.
mwandishi wa uchambuzi, kama huyu anaandikia wale wenye kutaka ukweli wa mambo, kwa kila upande, kupata picha halisi.
Najua hatupo wengi ila sasa habati ya jengo la umoja wa vijana ndio inaeleweka.
Kumbuka lengo si lowasa tu, lengo kuu ni kufichua wote walioshiriki kama kweli kuna tatizo lionekane, kama hakuna ijulikane.
Hawa huitwa jounalists.
habari itaisha pale ambapo utata utaisha na kupatikana solution na mwafaka, na yeye alieinanzisha habari hii kuifunga rasmi.
Wenye kupenda udaku publishers saa hizi wanasubiri tena hot news zingine.
Kazi anayoifanya Kubenea ni ngumu na inahitaji persistence ambayo wanahabari wengi hawana.
 
ukweli unabaki pale pale tu, kuwa ili kuua mti ni lazima ung'oe mizizi mikubwa sasa huyu lowasa yeye ndiye mzizi mkubwa kabisa wa ufisadi.Hongera sana kubenea
 
Washkaji wa jf naomba mnielekeze namna ya kulipata gazeti la mwanahalisi ktk mtandao nikiwa huku ugaibuni maana mara ya mwisho nilikuwa nalipata ktk KICHEKO lakini tangu wakati huo naona limeganda tu pale na habari ile ile ya dr slaa. i need help pls
 
Siamini kama Lowasa ni kichwa cha ufisadi nchi hii. Kama ni suala la kichwa cha ufisadi nadhani tumtaje JAKAYA. Binafsi huwa nina shangaa na nadhani sitakoma kushangaa hadi pale hali itakapo badilika. Haiwezekani katika nchi hii tukitaja mafisadi tunataja LOWASA, RA, KARAMAGI, CHENGE nk. Inapokuja kwa upande wa JAKAYA tunamsifiia tu eti anapambana na ufisadi wakati wote hawa tunaowataja kama mafisadi ni maswahiba wake sana, hivyo, hakuna doubt kwamba yeye pia JAKAYA ni fisadi ila sijui kwa nini tunamremba kiasi hiki. Tumsemeni naye, au tunasubiri hadi astaafu kama MKAPA ndo tuanze kuchonga? Muda ndo huu bwana Jakaya naye tumwambie ukweli wake.

Jana mwanahalisi wameandika kuwa JAKAYA ALIDANGANYA. Lakina nina uhakika stori hii haitakuwa na muendelezo wowote tofauti na kama ingemhusu Lowasa.
 
Lakina nina uhakika stori hii haitakuwa na muendelezo wowote tofauti na kama ingemhusu Lowasa[/B].

ndugu yangu tangu lini umekuwa mpiga ramli!!??

manake huu sio unabii!!

au wewe ndio mchapishaji wa gazeti????
 
Binafsi ninamheshimu sana Said Kubenea kwani ni miongoni mwa waandishi wenye misimamo hasa kwa yale wanayoamini kuwa ni kweli, lakini wasiwasi wangu unakuja baada ya kusoma makala zake nyingi nimegundua zinamhusu Lowassa, kitu kilichonifanya nidhani kuwa kuna tatizo kati ya wawili hawa na si ufisadi kama anavyochukulia Kubenea kama mwanvuli.

Maana kila toleo, tena kwenye ''front page'', utakuta mara Lowasa hivi, mara Lowasa vile, ilimradi tu amseme Lowasa.

Sio kama ninamsemea Lowasa, hapana. Ila tu kama kweli Kubenea unania ya dhati ya kupambana na ufisadi, basi sema juu ya ufisadi na sio Lowasa tu kila siku, mbona kuna mafisadi wengi tu nji hii.

Leo ni Jumanne, kesho Mwanahalisi litakuwa mtaani, habari kuhusu Lowassa ninatarajia kuikuta tena kwenye front page.

Hata watu wa haki za bina damu wanasema "hate the the vice and not the person".

Nakushauri bwana Kubenea utafute namna nyingine ya kukemea ufisadi la sivyo watu wataanza kupoteza imani na wewe.


Mi nafikiri wewe sio msomaji wa mwanaalisi kama umepotoka ni wewe lakininsio sie waomaji makini wa mwanalisi
 
lazima amwandike EL kwa kuwa jina lake linajitokeza mara nyingi sana kwenye mambo ya ufisadi, punde si punde tusubiri tutassikia ameumbuka kwenye mojawapo ya madili yake na hawa jamaa wa kkkt, kumbukeni EL hana tabia ya kuenda mahali bila ya kuwa na maslahi yoyote. Huyu jamaa ni kiboko na ndio maana mzee wa kuchonga alishamtosa mapema sana.
 
Wednesday, September 10, 2008
Mwandishi: haki Tarehe: Wednesday, September 10, 2008 | kiungo mahususi
Uzinduzi wa Tawi la CCM nchini
Marekani Jumamosi...


CHAMA CHA MAPINDUZI TAWI LA MAREKANI AMBALO MAKAO YAKE MAKUU YAPO MJINI HOUSTON TEXAS KWA KUSHIRIKIANA NA CHAMA CHA MAPINDUZI SHINA LA MISSOURI KITAFUNGUA RASMI SHINA LAKE LA KWANZA NCHINI MAREKANI KATIKA JIMBO LA MISSOURI HAPO SIKU YA JUMAMOSI YA TAREHE 13/9/2008.


WANACHAMA WOTE WA CHAMA CHA MAPINDUZI,WAKEREKETWA,PAMOJA NA WANAMAPINDUZI WOTE POPOTE HAPA MAREKANI NA NJE YA MAREKANI MNAALIKWA RASMI KATIKA SHUGHULI ZA UZINDUZI HUO.


SHUGHULI YA UZINDUZI ITAONGOZWA NA MWENYEKITI WA TAWI LA CCM MAREKANI NDUGU MICHAEL NDEJEMBI AMBAYE ATAAMBATANA NA VIONGOZI WENGINE WA TAWI NA WANACHAMA KUTOKA HOUSTON TEXAS PAMOJA NA MWENYEKITI WA SHINA LA MISSOURI NDUGU DEOGRATIS RUTABANA VIONGOZI WENGINE WA SHINA LA MISSOURI.SIKU YA UZINDUZI:
TAREHE 13/09/2008
MAHALI:JIMBO LA MISSOURI
UKUMBI:COVES CLUB HOUSE 5417 NW.85TH
MTAA:KANSAS CITY MO 64154.


KADI ZA CHAMA CHA MAPINDUZI ZITAKUWEPO UKUMBINI TAFADHALI WANACHAMA MJE NA PICHA(PASSPORT SIZE).


KWA MASWALI YOYOTE KUHUSU UZINDUZI HUO,TAFADHALI WASILIANA NA MWENYEKITI WA CCM MISSOURI NDUGU DEOGRATIS RUTABANA SIMU 816-812-5495 AU KENNEDY MALLYA SIMU 816-255-4944.
KUMBUKA: KIINGILIO KITAKUWA BURE NA KUTAKUWA NA VINYWAJI
 
Ni wazi kubenea hana akili ya kutoa mawazo mapya kila siku anaandika yaleyale.gazeti lake lita kosa wasomaji muda si mrefu kutoka sasa.kwa kuwa watu wanapenda mawazo mapya

Enyi kizazi cha kifisadi siku zenu zinahesabika.
kawaulize wauza magazeti watakuambia miongoni mwa magazeti yenye wasomaji wengi na huisha mapema kwenye vichanja na hata kwa wanaotembeza, basi watakuambia mwanahalisi ni moja wapo.
we unadhani kubenea haitaji faida pamoja na kuelimisha umma na kupambana na mafisadi!!
Magazeti mangapi yanadoda hadi kufa kutokana na kukosa mvuto!!??tena hata ambayo yameanzishwa na mafisadi, wanayapa ruzuku ya kutosha bado yamekosa mvuto kwa watanzania.
watanzania sasahivi wako kwenye mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi kwahiyo kubenea anatumia nafsi yake kumshughulikia key player wa ufisadi.
 
Na kweli hayakuhusu sasa unahamaki nini? We siyo Mtanzania? Je huna uchungu na nchi hii? Jengo la UVCCM ni mali yangu na yako. Tulichangia tangu tulipokuwa shule. Labda wewe hukusoma Tanzania ndo maana unasema hivyo. Inawezekana!!!!!!
I might you have personal interest to special person. Inawezekana kaka zilikupitia maana magari yenu ya kifahari hatuyaoni sasa.
Jamani tuache njaa ya kushabikia yasiyoshabikiwa. Na mkuu labda uelewe sina ligi hapa,,, ni kwa msaada wako tu na siyo wa kubenea.
 
Na kweli hayakuhusu sasa unahamaki nini? We siyo Mtanzania? Je huna uchungu na nchi hii? Jengo la UVCCM ni mali yangu na yako. Tulichangia tangu tulipokuwa shule. Labda wewe hukusoma Tanzania ndo maana unasema hivyo. Inawezekana!!!!!!
I might you have personal interest to special person. Inawezekana kaka zilikupitia maana magari yenu ya kifahari hatuyaoni sasa.
Jamani tuache njaa ya kushabikia yasiyoshabikiwa. Na mkuu labda uelewe sina ligi hapa,,, ni kwa msaada wako tu na siyo wa kubenea.

Eeka Mangi has no status.
Junior Member
 
Washkaji wa jf naomba mnielekeze namna ya kulipata gazeti la mwanahalisi ktk mtandao nikiwa huku ugaibuni maana mara ya mwisho nilikuwa nalipata ktk KICHEKO lakini tangu wakati huo naona limeganda tu pale na habari ile ile ya dr slaa. i need help pls

Mimi nilisema mapema mkalisome kwanza ndio mjadili kma anakosea au la! Kumbe mnaongelea ushabiki tu kusoma kwenyewe hamjasoma makala za kujirudia!!
 
Ndugu yangu Mwita haihitaji elimu kubwa kujua hilo! Huyu ana bifu EL sio JK.

Hata kama ana bifu nae, lakini unakubali kuwa EL ni kamanda wa genge la ufisadi???
vile vile hata kama kuna mafisadi wengine, yeye anayemjua na ambaye ana ushahidi nae ni EL, sasa aache kumuandika kwa kuwa mtasema eti ana bifu nae?Hivi huoni kuwa hizo habari za ufisadi wa EL hata wewe unazipenda na kuzishabikia ndio maana kila wiki hukosi kulisoma mwanahalisi, iwe kwenye mtandao hao vibandani.
Hao mafisadi wengine kubenea kawaachieni nyie, yeye kaamua kufa na mnyonge wake EL!tehe...tehe...teheeee!!!
 
Aah...! Kumbe mwisho wa siku, EL ni mnyonge wa Kubenea....

Unajua mtu anakua mnyonge kwa makosa yake. Kabla ya sakata la Rich.... kutinga bungeni na mambo kuwa kama yalivyokuwa, EL alikuwa haguswi na atakayemgusa atakiona cha mtemakuni hata kama unafanya kazi chombo binafsi. LAkini hebu fuatilia kesi zote za wezi wanaochomwa moto, vibaka wanaopigwa, wanaofumaniwa, utabaini kwamba kibaka akikamatwa anayemkamata au kumpiga ni mtu ambaye hana hata nguvu ya kushindana naye kama wangekutana mahali ambapo huyo kibaka hajafanya kosa. Mhalifu anakosa nguvu anapokamatwa tena LIVE na hata kama una nguvu kama tembo ukifumaniwa unachanganyikiwa na unaweza kupigwa na sisimizi. Habari ndio hiyo kwa Lowassa v/s Kubenea (KUbenea vs Lowassa) kwani hata muandikaji amatanguliza jina la Kubenea kwa kuwa anaonekana ndiye anayeng'aa kwa sasa na si LOWASSA tena, zama zake zimekwisha, asubiri kusafishwa na mahakama kama ZUMA maana nasikia anajiita Zuma wa Monduli (tehe tehe tehe).
 
UKITAKA KUMPIGA NYOKA ANZA KICHWA KWANZA. LOWASSA ni kichwa cha ufisadi Tanzania. MENGINE NI BLAH BLAH.

Hata magazeti yote yakiandika kila siku, habari za ufisadi wa Lowassa hazitakwisha maana hata leo kuna ufisadi mwingine unafanyika, ndio maana wakati kina mwanyika wanaanza kuchunguza EPA, kina Lukanza na wenzake walikuwa wanachoma nyama kule Monduli na walichangia katika harambee hadharani pale Arusha. Kumbukeni.

Suala la Nape ni ufisadi mwingine wa Lowassa ambao uko katika chati, sasa unategemea nini? Gazeti linalotaka kuandika ukweli kuhusu ufisadi haliwezi kumkwepa Lowassa hata kwa mawe.

Kama una uhusiano na Lowassa, nenda kamsalimie binti kutoka Handeni anayeitwa Mwajabu Ibrahim, anayefanya kazi nyumbani kwake na ambaye alipojiuzulu 'aka-mjiuzulisha' mtoto wa watu ili ahame naye. Mwambie akupa kadi zake za benki ukaone ana fedha kiasi gani ukilinganisha na za kwako unayehangaika na kazi usiku na mchana. Hiyo ni ili mujue tunajua mengi.

Habari mkuu wangu....
 
Kubenea na kingunge sawa maana kingunge anasema ccm hakuna haki ya nafasi wakati hata huko cdm hali haikuwepo watu wenye pesa walinunua saccoss tu,
 
Kubenea na kingunge sawa maana kingunge anasema ccm hakuna haki ya nafasi wakati hata huko cdm hali haikuwepo watu wenye pesa walinunua saccoss tu,

Kwanza sidhani kama kubenea ni mwanasiasa, nunavyomjua mimi ni mwandishi wa habari tena habari za upande mmoja, ok, hilo ni la kwake na uwezo wake ndipo ulipofikia. Lakini hili la kujiunga na Lowassa ni la kawaida maana hawezi kupigana naye tena. He failed to fight him, so he has decided to join him
 
Back
Top Bottom