Kuazima gari ni ustaarabu?

Kuazima gari ni ustaarabu?

Kumuazimisha Mtu Gari, Ni sawa na kumuazimisha Mtu Mkeo, Kwani hasara ni Nyingi kuliko Faida.Ni kweli huwezi kujua shughuli Maalumu ya Huyo rafikio,anaweza kwenda kupakilia Meno ya Tembo au akaenda kufanyia tukio Mtaani, au hata akamgonga Mtu Bahat mbaya.na kama ilivyo,Vitu vya kuazima sijui kwa nn watu wanakuwa na mbwembwe navyo. Mara nyingi huendesha kwa Maspeed ya mbwembwe na kufukia Mashimo bila ya kujua gharama ya Vipuli.

Jirani yangu aliwahi kuniazima gari aende kwenye dili lake Mara Moja. Kumbe alikuwa na Mtoko na demu wake.akalala na Gari yangu Night Club, asubuh ilipofika ananirudishia gari saa mbili asubuh huku mm nkiwa nshachelewa kwenda kazini. Na gari alikuwa ameigonga Nyuma. Nilisikitika sana. Tangia hapo ukawa ndio Mwisho wa kumuazima yoyote Gari. Ni afadhali umpatie 10,000 ya Taksi kuliko kmuazimisha mtu Gari yako.

Kitu Muhimu hawa wanaozima wasichokijua ni:

Gari sio Mafuta.Gari ikiwa inatembea Barabarani inakuwa na Mlolongo wa vitu vingi hadi unaiona inatembea Barabarani. Gari sio Mafuta tu. Hivyo unapoenda kuazima gari ya Mtu usifikirie kwamba Gari ni Mafuta Tu. Huwezi amini,kuna jamaangu eti ananipigia Simu kutaka kuazima gari ili akaangalie Mpira Eti Masaki. Inashangaza kwa Kweli. Kama Starehe unazipenda kwa nn usitafute na hela kwa ajili ya mambo yako ya Starehe Pia!????
 
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria

mimi huwa namsaidia RAFIKI YANGU/NDUGU YANGU gari na wao huwa wananiazima kwasababu gari zao/yangu inaweza kupata matatizo. hadi nampa mtu gari nazingatia haya
1. namfahamu vizuri
2.ana gari,hii itanisaidia kujua anajua kundesha na anajua kuhandle gari.
3.muda huo sina shughuli nalo

kinyume na hivi simpi gari.
 
Kwani gari ina nini usiazime mwenzio? Kama kitu cha maana sana mbona ukifa huzikwi nayo?
Cha msingi
1.mufahamiane,
2.Ajue kuendesha,
3.ujue shughuli anayoenda kufanyia.
Tuache ulimbukeni ukiwa na gari ndo kujiona umemaliza.

Sio kumaliza mkuu, mtoa mada kajieleza vizuri tu Kuwa jirani mwenyewe hawafahamiani hata majina ina maana hana mazoea naye sana. Sasa mtu wa hivyo anawezaje kwenda kuazima gari? Inawezekana hujui hata Kazi anayofanya.
Akienda kulifanyia ujambazi je? Mimi simpi. Kama niko vizuri nampa ya tax. Kama Niko ovyo namwambia nina kazi nalo.
 
Sio kumaliza mkuu, mtoa mada kajieleza vizuri tu Kuwa jirani mwenyewe hawafahamiani hata majina ina maana hana mazoea naye sana. Sasa mtu wa hivyo anawezaje kwenda kuazima gari? Inawezekana hujui hata Kazi anayofanya.
Akienda kulifanyia ujambazi je? Mimi simpi. Kama niko vizuri nampa ya tax. Kama Niko ovyo namwambia nina kazi nalo.

na ole waje ampe
alafu aje hapa kuomba ushauri
 
hata kama ni rafiki yako wa karibu, gari sio kitu cha kuazima, nasema hivi kwa sababu nimeshuhudia watu wakikamatwa kisa gari lake lilihusika kwenye tukio fulani,,,,mtu anaweza akaazima gari kumbe anaenda nalo kwenye tukio la unyang'anyi/ujambazi kinachofuata ni msako na anayeyekamatwa ni mwenye gari mbaya zaidi unakuwa huelewi kilichotokea,,,hahahaa! na polisi nao wasio na dogo mbona utajuta
 
mi nilikuwa mtu simple sana kwenye vitu vidogo vidogo mfano kumwachia gari mtu ndo nn bna....yan mtu alikuwa akiomba nampa tu...duh last year nikaifunza kitu.....kijana wa jiran kachukua gari afu sikuwepo nilikuwa mkoa....bahati mbaya akapinduka nayo ila hakuumia bahati alifunga mkanda....ila gari haikutamanika yan inaonekana iligalagala kama mpira.....sasa bwana hapo tu trafic wameizingira wanataka details...trafic case n.k.....dogo hakuwa na leseni kakimbia kujificha.....mungu si athuman najuana na baadhi ya trafics nikawapigia sim wasiifatilie wakaachia hapo.....kimbembe kikabak huyu dogo ndg zake walinipigia sim ndani ya dk 30 hadi ikazma chaji....angekufa ningemezwa naona....so plz usiazimishe gari ovyo ovyo utakuwa mhanga wewe tu
 
Jamaa yangu aliniazima gari wakati naenda kuoa toka Dar kwenda mkoani, Landcruiser Prado, akaniwekea na mafuta full tank na gari nilikaa nayo wiki nzima ndio nikamrudishia. Tena ilikuwa ndio gari yake ya thamani kuliko nyingine na wakati nimesafiri akawa anashea na mkewe gari kwenda kazini. Inategemea mnahusiana vipi na uwezo wako kiuchumi. Una kagari kamoja, tena ka mkopo then unamuazima "mtu baki" hata Mimi nisingetoa.
 
Jamaa yangu aliniazima gari wakati naenda kuoa toka Dar kwenda mkoani, Landcruiser Prado, akaniwekea na mafuta full tank na gari nilikaa nayo wiki nzima ndio nikamrudishia. Tena ilikuwa ndio gari yake ya thamani kuliko nyingine na wakati nimesafiri akawa anashea na mkewe gari kwenda kazini. Inategemea mnahusiana vipi na uwezo wako kiuchumi. Una kagari kamoja, tena ka mkopo then unamuazima "mtu baki" hata Mimi nisingetoa.

Mkuu, inategemea na urafiki ulokuwa nao na huyo mtu.

Hapo inaelekea mlikuwa mabest hasa, ila kwa case kama hiyo hapo juu, sidhani kama ni sawa aisee
 
Duuuuuuuuu! Khaaaaaaaa! Tutauana kwa presha gari lenyewe ndio kwaanza hata marejesho yenyewe bado!
 
Jamaa yangu aliniazima gari wakati naenda kuoa toka Dar kwenda mkoani, Landcruiser Prado, akaniwekea na mafuta full tank na gari nilikaa nayo wiki nzima ndio nikamrudishia. Tena ilikuwa ndio gari yake ya thamani kuliko nyingine na wakati nimesafiri akawa anashea na mkewe gari kwenda kazini. Inategemea mnahusiana vipi na uwezo wako kiuchumi. Una kagari kamoja, tena ka mkopo then unamuazima "mtu baki" hata Mimi nisingetoa.
Kweli mkuu!!
 
Vigari vya mikopo ndo kawaida mmiliki wake kua mchoyo.
Acha kukuazima hata lifti tu hatoi.
 
Tukizoea haya mambo hata post za hivi haziwezi kuandikwa! Umaskini mbaya huu
 
Naona jinsi watanzania walivyo wachoyo.
 
Hii mambo kweli ni shida, ukute mtu anataka kuazima kwa ajili ya misele ya kawaida kabisa. Mi namuazima mtu kwa kweli kama kuna dharula iliyo serious, like kumpeleka mtu mgonjwa n.k. Kuna mshkaji wangu aliniomba gari akapige misele na demu wake, bahati mbaya nilikuwa na misele yangu siku hiyo, duu jamaa hadi leo amekata mawasiliano.


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
gari anaazima hadi ridhiwani kikwete sembuse wewe mlalahoi? au hamkusikia ridhiwani akisema msione anabadilisha magari tu hayo ni mambo ya kimjinimjini tu, yeye anamiliki toyota Camry moja tu.

wazungu walishapita kote huku ambako sisi leo mishipa ya shingo inatutoka na ndio maana walibuni rent car self driving, ili kuondokana na kumtukuza mtu kwa sababu ya makopo haya.
 
Kumuazimisha Mtu Gari, Ni sawa na kumuazimisha Mtu Mkeo, Kwani hasara ni Nyingi kuliko Faida.Ni kweli huwezi kujua shughuli Maalumu ya Huyo rafikio,anaweza kwenda kupakilia Meno ya Tembo au akaenda kufanyia tukio Mtaani, au hata akamgonga Mtu Bahat mbaya.na kama ilivyo,Vitu vya kuazima sijui kwa nn watu wanakuwa na mbwembwe navyo. Mara nyingi huendesha kwa Maspeed ya mbwembwe na kufukia Mashimo bila ya kujua gharama ya Vipuli.

Jirani yangu aliwahi kuniazima gari aende kwenye dili lake Mara Moja. Kumbe alikuwa na Mtoko na demu wake.akalala na Gari yangu Night Club, asubuh ilipofika ananirudishia gari saa mbili asubuh huku mm nkiwa nshachelewa kwenda kazini. Na gari alikuwa ameigonga Nyuma. Nilisikitika sana. Tangia hapo ukawa ndio Mwisho wa kumuazima yoyote Gari. Ni afadhali umpatie 10,000 ya Taksi kuliko kmuazimisha mtu Gari yako.

Kitu Muhimu hawa wanaozima wasichokijua ni:

Gari sio Mafuta.Gari ikiwa inatembea Barabarani inakuwa na Mlolongo wa vitu vingi hadi unaiona inatembea Barabarani. Gari sio Mafuta tu. Hivyo unapoenda kuazima gari ya Mtu usifikirie kwamba Gari ni Mafuta Tu. Huwezi amini,kuna jamaangu eti ananipigia Simu kutaka kuazima gari ili akaangalie Mpira Eti Masaki. Inashangaza kwa Kweli. Kama Starehe unazipenda kwa nn usitafute na hela kwa ajili ya mambo yako ya Starehe Pia!????
Kabisaaa!
 
Mkuu jigili, use your common sense..
Mimi nina gari lakini ni mtu mmoja tuu kati ya marafiki zangu naweza kumpa gari langu japo nina marafiki wengi.
Sababu za msingi ni kama ifuatavyo;
  • Hata kama ni rafiki yako, usimpe gari, badala yake kama unaweza na una nafasi, mpeleke mwenyewe. Unapoendesha gari lako unajua how to take care.
  • Hebu fikiria una rafiki unampa gari. Inatokea inapata ajali alafu mtu mwenyewe hana hata hela ya matengenezo unapigiwa simu gari iko mtaroni utafanyaje? kumdai huwezi, ukimwacha roho itakuuma.
 
Last edited by a moderator:
gari anaazima hadi ridhiwani kikwete sembuse wewe mlalahoi? au hamkusikia ridhiwani akisema msione anabadilisha magari tu hayo ni mambo ya kimjinimjini tu, yeye anamiliki toyota Camry moja tu.

wazungu walishapita kote huku ambako sisi leo mishipa ya shingo inatutoka na ndio maana walibuni rent car self driving, ili kuondokana na kumtukuza mtu kwa sababu ya makopo haya.
Si unaazima kwa unaye mfahamu? Huwezi kurupuka tu! Kisa mshikaji huwa namuona kitaa hata kufahamiana vizuri hamfamiani!!!
 
njoo uazime ikiwa tuko karibu tena nikijua udereva na .si vinginevyo, ila mafuta yangu uyaweke....
 
Back
Top Bottom