Poa basi itume kwa mpesa
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria
Kwani gari ina nini usiazime mwenzio? Kama kitu cha maana sana mbona ukifa huzikwi nayo?
Cha msingi
1.mufahamiane,
2.Ajue kuendesha,
3.ujue shughuli anayoenda kufanyia.
Tuache ulimbukeni ukiwa na gari ndo kujiona umemaliza.
Katika watu wenye hoja za kitoto basi Makamee unaongoza.
Uchumi wako ni wa kiwango fulani, ndiyo maana huoni tabu kumwazima fyekeo. Uchumi wako ungekuwa wa kiwango fulani kingine usingeona tabu kumwazima gari. Nakublina nawe kwamba jamaa anakosea kujaribu kwenda kinyume na hali zenu za uchumi.
thats brilliant mzee.......cha mtu mavi.sasa mimi nina jamaa yangu ana gari yake na akisafiri huipaki kwangu kwa sababu kwake hana parking ili kuokoa gharama za ulazaji magari na ufunguo uniachia pia.
lakini mpaka anarudi gari yake huikuta iko vilevile ninachokifanya uwa namsaidia kuiwasha injini asubuhi iungurume na kuizima. that's it.
amefanya la maana sana kushare, faida kubwa imepatikana kutokana na komenti za wachangiaji.Sasa hiyo personal issue ya jirani yako kutaka kukuazima gari, nayo unaileta humu janvini?
Sasa kama wewe mwenyewe kama ulivyosema huyo jirani yako humjui hata jina lake!
Sasa ulishindwa nini kumpasulia LIVE kuwa pamoja na kuwa nyinyi ni majirani, lakini ujirani huo una mipaka yake, vipo vitu vya kushare, lakini vingine siyo vya kushare, vikiwemo hilo gari lako plus your wife/husband!!
huyo mtu wa karibu nilishawahi kumuazima gari masaa matano badae kapata nalo ajari tena akiwa amelewa...garama matengenezo ilikuwa 1.2m , wala nusu ya gharama hakuweza kuto.Heshimu gari baba .gari siyo kiungo mtu anazaliwa nacho.