KLH News On Saturday...

KWA HIYO UNASEMA MWANAKIJIJI KAOLEWA ?? mi nauliza tu. unajua wazungu/weusi hata kama mwanamme anakwambia am married !
 
Halafu huu ujeuri wa kusema kama mnaona tumekosea NENDENI mahakamani.......haya nimatusi kwa wanachi wa tanzania wanaotaka kuelewa YANAYOJIRI

...si wanajua chaguzi bado!,

...siku za kampeni zikifika 'lugha' inabadilika, na hata shikamoo wanazitoa!

...Mkjj na BongoRadio endeleeni kuhifadhi haya mahojiano tuje kukumbushana panapo majaaliwa,

...wakati huo wa kumwaga "dataz"

...2010 sio mbali..
 
Mbona mna kiherehere? chuki nyingine za ajabu sana watu badala ya kujadili anachosema mnajadili lahaja na lafidhi ya waziri. Naona mnashindana nani mpondaji zaidi... JF usanii tu

Masatu, 'chuki' neno kubwa sana bwana, sidhani kama kuna mtu anachuki na Mh. Khatib. Sikatai wanaweza kuwepo ila si mimi. Kejeli si chuki.

SteveD.
 
Gamba la nyoka
usalama wa nchi unauchukuliaje ndg yangu......................TRUST ME, pamoja na kazi zingine za ulinzi, classified information zozote ambazo zaweza kuleta utata ndani ya jamii kama ilivyo sasa...........ni moja ya kazi zao kuhakikisha hizi classified inf hazi-leak.
Maan nenda ktk Intelligence Unit yeyote ulimwenguni kuprotect nyaraka za serikali ni moja ya kazi muhimu kwao

Ila wakati mwingine hao hao wana Intelijensia huwa wanavujisha siri, mfano mzuri ni wa zile picha za Abu Ghraib.
 
yaani mbaya sana unawaambia watu wasikilize radio saa 7 mchana saa za marekani halafu wee mwenyewe huonekani ! mie nilizidisha sauti ya computer hadi mwisho, sikusikia kitu, kuna mtu akanipigia simu nikawa simsikii vizuri akauliza wee maskio yako mazuri kweli, nikasema labda nimekuwa kiziwi maana radio ya mwanakijiji sisikii kitu ukizingatia sauti maxima halafu mtu mwingine ananiuliza kama maskio yangu mazuri, i was wild ! kumbe kosa lako wee bana wa shambani !

Ina maana umemiss Usanii wa Selfish Katibu?
 
Wanachotakiwa ni kuwahusisha wabunge, kwenye hii mikataba, sioni tatizo liko wapi mbona ishu nyingi huwa wanawa-consult bunge? Kwenye masuala yote ya ubinafsishaji walikuwa wakiwa-consult kamati ya bunge ya uwekezaji, sasa kinachowashinda sasa ni nini?

Ni vigumu kwa mkataba kupitiwa na sisi wananchi wote wa taifa zima, lakini wabunge wetu wa CCM na upinzani, ambao kwa kawaida huwa wana-make kamati hizi za bunge wanatosha sana kuipitia hii mikataba kwa niaba ya siss wananchi wote at latge,

Kwa hiyo hakuna kisingizio chochote cha mikataba kusainiwa ikiwa mibovu namna hii ya Buzwagi, ni suala la uwajibikaji kwa taifa ndio linalo-lack kwenye ishu nzima na kukosekana kwa a balanced power between three branches of government, yaani Judicial, Executive, na Parliament, tungekuwa nazo hiii sasa hivi ya mkataba wa Buzwagi, ilitakiwa kuwa ni ishu ya bunge, wwaliohusika wote wangeitwa mbele ya bunge na kuhojiwa under oath ili kupata ukweli uko wapi,

Geeeque you got it right, hii interview ilikuwa shame maana huyu waziri ni msanii!

Mungu Aibariki Bongo!
 
Siku ya Jumamosi kwenye matangazo yetu ya moja kwa moja (live) nilipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB).

<p> Makubwa tuliyozungumza ni suala zima la tuhuma zilizotolewa na ushirika wa wapinzani tarehe 15 Septemba pale Jijini Dar. Pamoja na hayo tulizungumzia kuhusu suala la Buzwagi na jinsi mwitikio wa wananchi ulivyokuwa na hasa ziara ambazo zimefanywa wiki iliyopita na Mawaziri na Manaibu wao kwenye mikoa mbalimbali.</b>

<p>Je, hoja za wapinzani zina msingi? Je serikali ina msimamo gani kuhusu kuvuja kwa mkataba wa Buzwagi na kama ina mpango wa kuwachukulia hatua za kisheria wale watakaokutwa nao? </b>

Hayo na maswali mengine mengi yanajibiwa na Mhe. Khatib. Lakini majibu yake yanajibu maswali niliyomuuliza? Sikiliza uamue... Kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kusikiliza mahojiano yangu na Mhe. Khatib, unaweza kusikiliza kupitia KLH News...
 
hii thread kweli ilikuwepo hapa muda wote or am i tripping ? niliitafuta kichizi lakini sikuiona ndio sasa hivi naiona ! duh, ama kweli sioni vizuri siku hizi !
 
Siku ya Jumamosi kwenye matangazo yetu ya moja kwa moja (live) nilipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB).

<p> Makubwa tuliyozungumza ni suala zima la tuhuma zilizotolewa na ushirika wa wapinzani tarehe 15 Septemba pale Jijini Dar. Pamoja na hayo tulizungumzia kuhusu suala la Buzwagi na jinsi mwitikio wa wananchi ulivyokuwa na hasa ziara ambazo zimefanywa wiki iliyopita na Mawaziri na Manaibu wao kwenye mikoa mbalimbali.</b>

<p>Je, hoja za wapinzani zina msingi? Je serikali ina msimamo gani kuhusu kuvuja kwa mkataba wa Buzwagi na kama ina mpango wa kuwachukulia hatua za kisheria wale watakaokutwa nao? </b>

Hayo na maswali mengine mengi yanajibiwa na Mhe. Khatib. Lakini majibu yake yanajibu maswali niliyomuuliza? Sikiliza uamue... Kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kusikiliza mahojiano yangu na Mhe. Khatib, unaweza kusikiliza kupitia KLH News...


Mzee mwana wa kijiji asante sana kwa haya mahojiano nilikuwa bado kuyasikiliza.
 
Mzee Mkjj heshima mbele mkuu.

Ahsante sana mkuu umembana vizuri sana huyu muheshimiwa. Kuna wakati nilijisahahu nikadhani Bill O'Reilly anambana Rev Al Sharpton...(Nuf jokes!).

Huyu muheshimiwa hakujibu maswali aliyoulizwa...kwa kifupi he was just arguing in a circle. Ndiyo maana hata wakati wa uchaguzi mkuu hawa jamaa hukimbia mdahalo kwasababu hawana hoja.
 
Katika Mahojiano yake na Mwanakijiji Jumamosi Waziri wa Habari na Utamaduni,Seif khatib alidai kuwa si kweli kwamba Viongozi wanazomewa huko Mikoani,naomba mumuonyeshe article hii ya kuzomewa kwa Dr. Ngasongwa na kule Mbeya Bwana Tyson(Waziri Wasira) alipozomewa!!!,Kitendo cha kuzomea kinaonyesha kuchoshwa.

ZIARA ZA MAWAZIRI MIKOANI NI BALAA.

2007-10-08 09:27:14
Na Waandishi Wetu


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Henry Daffa Shekifu, amelazimika kuingilia kati na kuwasihi wananchi wa wilaya ya Hanang wasimzomee Waziri wa Mipango Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa, anaripoti Zillipa Joseph wa PST kutoka Hanang.

Bw. Shekifu aliwataka wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya soko mjini Katesh kutoa nafasi kwa viongozi kujieleza badala ya kuzomea.

Hali hiyo ilijitokeza baada ya Dk. Ngasongwa kujibu maswali ya baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.

`Tufautishe mikutano. Mkutano huu sio wa kampeni ni wa serikali, tutoe nafasi kwa viongozi, tusitunishiane misuli tukapoteza amani, na amani ikivunjika kuirudisha ni kazi. Kama kuna mwananchi anataka kubadilisha mkutano huu uwe wa kampeni nitamdhibiti kwa nguvu za serikali,` alionya Bw. Shekifu.

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi hao ni kutaka kufahamu ni kwa sababu? gani serikali inawasambaza mawaziri na manaibu wao mikoani kuelezea bajeti, na kudai kuwa huo ni ubadhirifu wa fedha za walipa kodi, wakati wananchi wanataabika na bei za bidhaa kupanda.

Swali lingine lilihoji uhalali wa kumsimamisha mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe, kuhudhuria vikao vya Bunge huku wananchi hao wakidai kuwa ziara hiyo ni sehemu ya kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Akijibu maswali hayo, Dk. Ngasongwa alisema Bw. Zitto, anajitafutia umaarufu na kuongeza kuwa alitoa lugha ya matusi bungeni ndio sababu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao.
 
Katika Mahojiano yake na Mwanakijiji Jumamosi Waziri wa Habari na Utamaduni,Seif khatib alidai kuwa si kweli kwamba Viongozi wanazomewa huko Mikoani,naomba mumuonyeshe article hii ya kuzomewa kwa Dr. Ngasongwa na kule Mbeya Bwana Tyson(Waziri Wasira) alipozomewa!!!,Kitendo cha kuzomea kinaonyesha kuchoshwa.

ZIARA ZA MAWAZIRI MIKOANI NI BALAA.

2007-10-08 09:27:14
Na Waandishi Wetu


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Henry Daffa Shekifu, amelazimika kuingilia kati na kuwasihi wananchi wa wilaya ya Hanang wasimzomee Waziri wa Mipango Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa, anaripoti Zillipa Joseph wa PST kutoka Hanang.

Bw. Shekifu aliwataka wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya soko mjini Katesh kutoa nafasi kwa viongozi kujieleza badala ya kuzomea.

Hali hiyo ilijitokeza baada ya Dk. Ngasongwa kujibu maswali ya baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.

`Tufautishe mikutano. Mkutano huu sio wa kampeni ni wa serikali, tutoe nafasi kwa viongozi, tusitunishiane misuli tukapoteza amani, na amani ikivunjika kuirudisha ni kazi. Kama kuna mwananchi anataka kubadilisha mkutano huu uwe wa kampeni nitamdhibiti kwa nguvu za serikali,` alionya Bw. Shekifu.

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi hao ni kutaka kufahamu ni kwa sababu? gani serikali inawasambaza mawaziri na manaibu wao mikoani kuelezea bajeti, na kudai kuwa huo ni ubadhirifu wa fedha za walipa kodi, wakati wananchi wanataabika na bei za bidhaa kupanda.

Swali lingine lilihoji uhalali wa kumsimamisha mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe, kuhudhuria vikao vya Bunge huku wananchi hao wakidai kuwa ziara hiyo ni sehemu ya kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Akijibu maswali hayo, Dk. Ngasongwa alisema Bw. Zitto, anajitafutia umaarufu na kuongeza kuwa alitoa lugha ya matusi bungeni ndio sababu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao.


Mwaka huu utaingia katika historia ya WTZ kudai haki zao za kikatiba ambazo CCM walifikiri hawangeweza kuja kuulizwa. Jambo ambalo CCM wanaweza kufanya ni kuondoa mafisadi wote katika system kabla ya mwaka ujao na kuweka mikakati mipya, kufuta mikataba yote ya madini ambayo hailifaidii taifa na wananchi wake. Kuweka kipaumbele kwa wawekezaji wazawa badala ya kutegemea wageni,
 
Kwamara nyingine CCM wamezihilisha udikteta wao. Waziri alikuwa anajibu kama mmiliki(owner) wa Tanzania. Ni sawa na lile jibu la Iran hakuna magay. Non sense answers
 
Hawajui kuwa nguvu ya umma ni kubwa kuliko hata nguvu za polisi na majeshi, nguvu za katiba mbovu na utawala usioheshimu sheria hauna nafasi kwenye peoples power.

Wiki ijayo atafutwe Nimrod Mkono pamoja na mambo mengie aje aeleze ni kwa nini bodi ya mikopo inachochea wanafunzi wa vyuo vikuu kugoma hapa nchini?

Aeleze pia tuhuma zake , ili kutusaidia kisheria wale ambao hatukuwahi kuwa learned brothers,.

Zomeazomea hii kuna siku Makamba ataamua kutoka jukwaani na kumkimbiza mwananchi halafu amdunde live.... hoohooo?
 
Zomeazomea hii kuna siku Makamba ataamua kutoka jukwaani na kumkimbiza mwananchi halafu amdunde live....hoohoo?
Tehe tehe ! patamu hapo,maana hiyo mechi itaitwa CCM vs Wananchi. Kwa kujikomba,Tambwe na Akwilombe watataka kumuonyesha bosi wao walivyo jasiri kwa kusaidia kumshushia kipigo mwananchi huyo.
 
Back
Top Bottom