johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,979
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Kunenge amesema Jumatano hii ndio siku ya mwisho kwa kituo cha Ubungo kutumika na kuanzia Alhamis kituo kipya cha Mbezi kitaanza kutumika.
Naye kamanda Mambosasa amesema wapiga debe wa Ubungo hawatakiwi kuonekana stendi mpya ya Mbezi na kwamba stendi hiyo haitakuwa na wapiga debe.
Maendeleo hayana vyama
--
RC Kunenge amesema hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa miundombinu yote muhimu ikiwemo majengo, maegesho, barabara na ofisi za kutoa huduma.
Aidha, RC Kunenge amesema tayari Serikali imekutana na wadau wote husika ikiwemo chama Cha Wamiliki wa Mabasi TABOA na wote wamejiridhisha kuwa kituo kimekamilika na kipo katika hali nzuri ya kutoa huduma hivyo wapo tayari kutoa huduma.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Sporah Liana amesema ifikapo siku ya Jumanne watafanya kikao na Wafanyabiashara wote watakaokuwa wakitoa huduma ndani ya jengo na siku ya Jumatano watakutana na Wamachinga, Baba lishe na Mama lishe kwa ajili ya kuwekeana mikakati ya biashara.
Naye Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha abiria wote wanaosafiri au kuingia kituoni hapo hawapati usumbufu wa aina yoyote.
Naye kamanda Mambosasa amesema wapiga debe wa Ubungo hawatakiwi kuonekana stendi mpya ya Mbezi na kwamba stendi hiyo haitakuwa na wapiga debe.
Maendeleo hayana vyama
--
RC Kunenge amesema hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa miundombinu yote muhimu ikiwemo majengo, maegesho, barabara na ofisi za kutoa huduma.
Aidha, RC Kunenge amesema tayari Serikali imekutana na wadau wote husika ikiwemo chama Cha Wamiliki wa Mabasi TABOA na wote wamejiridhisha kuwa kituo kimekamilika na kipo katika hali nzuri ya kutoa huduma hivyo wapo tayari kutoa huduma.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Sporah Liana amesema ifikapo siku ya Jumanne watafanya kikao na Wafanyabiashara wote watakaokuwa wakitoa huduma ndani ya jengo na siku ya Jumatano watakutana na Wamachinga, Baba lishe na Mama lishe kwa ajili ya kuwekeana mikakati ya biashara.
Naye Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha abiria wote wanaosafiri au kuingia kituoni hapo hawapati usumbufu wa aina yoyote.