Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Kitine ni kweli alikuwa na scandle za ufisadi na kwa kweli ufisadi wa wakati wao ndio uliofungua milango ya ufisadi wa sasa.
Hata hivyo inaelekea hata yeye ameona kuwa kumbe ukiwa kwenye system ufisadi si sawa na ameamua kukolomea chama na serikali yake. Ni haki yake na anayoyasema ni kweli tupu hakuna uongo.
Na nadhani kwa kuwa alikuwa fisadi pia hii haimpi haki ya kutozungumza mawazo yake. Tutayasikiliza na bado tutamwambia hata wewe ulikuwa fisadi, na ni mmoja wa waliofungulia milango ya ufisadi chi hii.
Mi naona ufisadi wa enzi za BWM na wa sasa hivi hauna tofauti maana wizi ni wizi tu. Sina jina la kuuita ili niupambe.
 
Isitoshe kwenye AA, Gambling Anonymous e.t.c ktk zile 12-steps towards recovery, ya kwanza ni kukubali kuwa wewe (muhusika) una tatizo, yaani lazima uwe na insight ya tatizo lako na sio kuwa kwenye denial.

...only you would know about eeh....kwikwikwiiiiiii
 
"Simple minds discuss people, ordinary minds discuss events and great minds discuss ideas". I believe we have a choice here - to discuss Kitine, to discuss what he did or to discuss the ideas he put forward. For some the choice will be simple, for others it will be hard and for the rest it wont matter. We are in dire need for help for we are stuck in the mud and are sinking fast - do we grab any rope thrown to us or do we sink and die ? Kitine was once part of the Mafia and for breaking the code of silence, they have but two choices - silence him or ignore and discredit him. Fortunately for those who have the interest of the country at heart, what matters is not what Kitine did but what he said - again the choice is simple.


WOW!!! Thanks a lot Mkuu for your wisdom. You just made my weekend 🙂 Have a great weekend!
 
Amazing grace how sweet the sound that saved a wrench like me.
I once was lost but now I'm found, was blind but now I see.

This gospel song was written by a former slave owner who saw the evil of his ways
and sought salvation. The Black church in America sings this song because they
believe in redemption. Tukifuata kanuni za wengi ukumbini hapa Kitine hana haki ya
kuzungumzia hatma ya nchi yetu. Na kwa mtaji huu hatutafika.
 
Amazing grace how sweet the sound that saved a wrench like me.
I once was lost but now I'm found, was blind but now I see.

This gospel song was written by a former slave owner who saw the evil of his ways
and sought salvation. The Black church in America sings this song because they
believe in redemption. Tukifuata kanuni za wengi ukumbini hapa Kitine hana haki ya
kuzungumzia hatma ya nchi yetu. Na kwa mtaji huu hatutafika.

Miye hapa nakenua tu gego mpaka gego kwa jinsi nilivyojaa na furaha ya kuwa na watu makini hapa ukumbini kama wewe. Ahsante sana Mkuu Jasusi.
 
Kwa mara ya kwanza in a longtime nakubaliana na Kuhani Mkuu, bila ubishi!...... Isitoshe kwenye AA, Gambling Anonymous e.t.c ktk zile 12-steps towards recovery, ya kwanza ni kukubali kuwa wewe (muhusika) una tatizo, yaani lazima uwe na insight ya tatizo lako na sio kuwa kwenye denial......swali rahisi kwa Kitine na wale wanaomshabikia, je huyu bwana kuna mahali popote kakubali kuwa yeye aliwahi kuwa fisadi (assuming kuwa sasa kesha pona 'ako kau-gonjwa) au bado ni fisadi anayetafuta tiba? Vinginevyo hana mamlaka ya upayukaji dhidi ya wenzake na kwa mtaji huo basi Bwa' Kitine ni publicity opportunist.......! Hafai, bado ni fisadi tena ni hatari kabisa kwa afya zetu mmoja mmoja na taifa zima kwa ujumla.

Ijumaa njema na wkend njema.

Mkuu YNM,
Cheo ni dhamana, Kitine alipewa dhamana aka abuse, sasa anataka atupige changa la macho kwamba baada ya uongozi wake kwisha na kukosa ulaji kwenye serikali mpya, yuko tayari apewe tena dhamana, kana kwamba Tz hatuna watu wengine wanaoweza kuongoza.

Ni jambo rahisi sana. Kitine anatakiwa aidha akae kimya ama aite press conference na kushukuru umbumbumbu wa wananchi kwa kutomsweka jela pale alipotuibia.

Kinachonisikitisha ni kwamba njaa za waandishi wetu zinafanya wanaandike habari za majasusi walioiba miaka nenda rudi. Habali za watu kama Kitine na wengine wote walio na scandal za rushwa au wizi zilitakiwa zisiandikwe. Hapa waandishi wangesaidia katika vita vya ufisadi....vinginevyo waliotuibia watatutukana pia, na mfano wa Kitine ni tusi dhahiri.

Tangu lini mwizi wa benki akawa mshauri wa benki aliyeiibia? Kama tunaweza kutofautisha matumizi ya kikombe na umbo lake, basi tunaweza kutofautisha alichosema Kitine na Kitine mwenyewe.
 
Tangu lini mwizi wa benki akawa mshauri wa benki aliyeiibia? Kama tunaweza kutofautisha matumizi ya kikombe na umbo lake, basi tunaweza kutofautisha alichosema Kitine na Kitine mwenyewe.

Hakuna aliyesema Kitine awe mshauri. Bali tunachosema ni hiki je aliyoyasema Kitine kuhusu uongozi wa nchi yetu yana ukweli? je, yanaingia akilini? je yanastahili kujadiliwa na Watanzania ili kurekebisha hali ya uongozi ilivyo hivi sasa nchini mwetu?. Baadhi yetu tunasema NDIYO!!! Na hii haina maana Kitine atakuwa mshauri na Katiba ya nchi yetu haimnyimi uhuru Kitine wa kutoa maoni yake pamoja na kuwa fisadi
 
Last edited:
Right, kwa hiyo Kitine inabidi asimame aseme "ninachoweza ku share na nyinyi kuhusu experiences zangu za ufisadi ni kwamba unaweza kupoteza kazi kaa mimi, unaweza kufungwa jela, ingawa mimi niliponea chupuchupu, unaweza kupoteza credibility maisha, na kila unachosema kinaonekana ni cha kinafiki tu, etc. etc. kwa hiyo tujaribu kuepuka haya yaliyonikuta mimi."

Ndivyo wanavyofanya wenzake recovered alcoholic anonymous wakiongea kwenye teenage community centers.

Hawahamaki "...COMMUNITY IMEJAA WALEVI! ENZI ZETU KULIKUWA HAKUNA ULEVI! VIONGOZI WA COMMUNITY HAWAPIGI VITA DRUNK DRIVERS...."

No, no, no, taratibu Mr. Recovered Fisadi Kitine.

We tueleze kwa unyenyekevu tu, tunaweza kujifunza nini kutoka katika experiences za ufisadi wako, sio ku lambast mafisadi wenzio. Huna moral authority.

.....kwi kwi kwi kwi kwi kwi......ama kweli TGIF.....Kuhani hiyo yako ni kali aisee........kwi kwi kwi kwi
 
Kwa mara ya kwanza in a longtime nakubaliana na Kuhani Mkuu, bila ubishi!...... Isitoshe kwenye AA, Gambling Anonymous e.t.c ktk zile 12-steps towards recovery, ya kwanza ni kukubali kuwa wewe (muhusika) una tatizo, yaani lazima uwe na insight ya tatizo lako na sio kuwa kwenye denial......swali rahisi kwa Kitine na wale wanaomshabikia, je huyu bwana kuna mahali popote kakubali kuwa yeye aliwahi kuwa fisadi (assuming kuwa sasa kesha pona 'ako kau-gonjwa) au bado ni fisadi anayetafuta tiba? Vinginevyo hana mamlaka ya upayukaji dhidi ya wenzake na kwa mtaji huo basi Bwa' Kitine ni publicity opportunist.......! Hafai, bado ni fisadi tena ni hatari kabisa kwa afya zetu mmoja mmoja na taifa zima kwa ujumla.

Ijumaa njema na wkend njema.

- Mkulu YRSMN tuko pamoja sana hapa, hakuna nyongeza.

Respect!
 
YNMIS
Unachosema ni sahihi kama tunalenga mjumbe na si ujumbe. Mimi sijui Kitine ana mipango gani katika politics za nyumbani. Ninachomulika zaidi ni ujumbe wake. Is it relevant? Anasema kweli? Kwa kuwa tu alifanya madhambi huko nyuma haimwondolei haki yake ya kuchambua hali ya nchi yetu. Tumulike ujumbe zaidi badala ya mjumbe ama sivyo mapambano dhidi ya mafisadi yatatushinda tukijiwekea kigezo kuwa only those who are clean ought to engage in the fight. We need the Kitines because they know much of what has been going on behind the scene. That's all.
 
Bila kuingilia uhuru wa mtu yeyote yule,ningependekeza turudi kwenye mada(content).Naona ni kama wachangiaji wamebase kwa mtoa hoja na sio hoja yake.Kama kuna wanaotaka kumjadili Kitine as Kitine then they better start a new thread.Ni hayo tu.



Kweli mimi naona ww umenena tunatakiwa kuijadili hoja yake maana naona watu wanamjadili yeye,na cha kushangaza hata kama yeye fisadi kama anapiga vita mafisadi wezange mbaya iko wape! Kama ni kwa manufaa yake au mnafiki sisi anatusaidia .
 
Kwanini Mr. Kitine analipenda taifa wakati uchaguzi unakaribia?? Issue zake mara nyingi zinakuja mwaka mmoja kabla ya uchaguzi.

Ahaaaaaaaaaaaaa so anajijenga kisisa !?lakini anachosema si sahihi ?
 
Tukubaliane just for the sake of argument:

a. Mke wa Kitina aliwahi kuhusishwa na vitendo vya kifisadi never prosecuted.
b. Kitine alitaka kuwa Waziri sana hakupewa nafasi
c. Kitine bado ana machungu ya kuwekwa pembeni
d. Kitine naye ni fisadi (I'll go to that extreme).

Sasa:

a. Hoja zake juu ya tatizo la uongozi uliopo sasa hivi zina nguvu yoyote?
b. Je mtazamo wake kuhusu wajibu wa Usalam wa Taifa ni sahihi?
c. Assessment yake ya siasa za makundi ndani ya chama zina mantiki yoyote?
d. Je, kuna jambo lolote ambalo amelisema ambalo lina chembe ya ukweli au yote ni fabrication of his bitter mind?



a.Hoja zake zina nguvu ,
b.mtizamo wake sahihi kuhusu Usalama wa taifa
c.Assessment yake kuhusu siaisa za makundi ndani ya chama zina mantiki
d.Aliyosema ni kweli tupu.

ANGALIZO:alichosema ni sahihi na ndio ukweli wenyewe iwe amesema kwa ajili ya uchungu na nchi yake ,ama anajijenga kisiasa au kutokana na yeye kutengwa ama vyoyote haibadilishi alichosema kuwa kweli kwenda kwenye uongo (Reality never change)

Kwa hiyo kujitia smart kuangalia kwa nini anasema hivyo na kukumbia hoja na kuanza kumjadili yeye it is low minded.
 
Hakuna aliyesema Kitine awe mshauri. Bali tunachosema ni hiki je aliyoyasema Kitine kuhusu uongozi wa nchi yetu kina ukweli? je, kinaingia akilini? je kinastahili kujadiliwa na Watanzania ili kurekebisha hali ya uongoz ilivyo hivi sasa. Baadhi yetu tunasema NDIYO!!! Na hii haina maana Kitine atakuwa mshauri na Katiba ya nchi yetu haimnyimi uhuru Kitine wa kutoa maoni yake pamoja na kuwa fisadi

Asante BAK, sidhani hapa kuna anayemtetea FISADI Kitine hata moja - la hasha. Kitine hata akikamatwa leo wala sitakosa usingizi na nitakuwa miongoni mwa wale watakaopaza sauti kutaka asulubiwe. Kwa hasira ningeweza hata kumzaba kibao......

Lakini gari tulilolipanda linakaribia milima ya Kitonga na anatokea Kitine anatupa tahadhari kuwa dereva wetu anaonekana kalewa na uwezo wake wa kutufikisha salama uko mashakani. Na kweli tukiangalia anavyolikokota gari roho zetu ziko mikononi......

.....the choice is simple.
 
- Kitine na Mkapa, Mwalimu's people tena damu damu, Mwalimu alipokuwa ana-retire akapelekwa Canada kula nchi, akilipiwa kila kitu na serikali yaani hela zetu walipa kodi anachokifanya hakieleweki, Mkapa kuwa rais tu akamuomba kurudi great friends akarudi, Mkapa akatumia ubabe na nguvu za ajabu within a month Kitine ni mbunge na waziri ofisi ya Mkapa, all this time hajaona ubovu wa uongozi wetu wala tatizo la integrity,

- The next thing Kitine anaota urais, ghafla kaanza kuvaa kanzu na barakashia bungeni, nini kaambiwa rais anayefuata Mkapa lazima awe Muisilamu, mara oooh mawaziri ni wala rushwa, haya Kitine tuambie majina yao, akadai oooh no waandishi wamekosea sikusema vile, next mke wake amechukua maelfu ya dola za walipa kodi kwenda kutibiwa nje, kumbe ameenda kuzifanyia shopping bila kwenda Hospital wala kwa Daktari yoyote huko Canada na wala haumwi chochote, sasa all this time Kitine haoni ubovu wala tatizo la integrity na uongozI wetu,

- The next thing Kitine amehonga honga na kujaribu kuzuia uchunguzi wa kamati ya bunge kuhusiana na wizi wa mkewe wa hela zetu walipa kodi alizotumia nje tena kwa uharibifu sana, wabunge kuja juu sana ndio Kitine baada ya kubanwa sana na wabunge kukubali kujiuzulu na kulazimishwa kulipa nusu ya zile pesa tena katika mazingara yaliyojaa uhuni uhuni, badala ya mkewe kwenda jela kwa wizi wa mchana wa hela zetu walipa kodi, all this time Kitine haoni matatizo ya uongozi wetu na integrity yake kua hovyo!

Sasa leo he is supposed to be a hero kwa sababu amesema maneno ya kuponda serikali ya CCM, akitukana ubovu ule ule uliomponya yeye na mkewe, sometimes huwa ninajiuliza hivi vita tunavyopigana na mafisadi, kwa mfano tukiwatoa mafisadi wote leo, eti ni kweli tutaweza kuweka viongozi wapya ambao hawatakuwa mafisadi? Ningeelewa kwamba Kitine sasa ameamua kwamba wananchi wa Tanzania wameonewa vya kutosha na kuweka mfano anataka mkewe afunguliwe mashitaka kwanza ya kuiba hela zetu walipa kodi huko nyuma maana sasa anataka to come clean, no sasa yeye na Mbilinyi ni mashujaa against uozo wa uongozi wetu uliowaponya.

Tuangalie sana ndugu zangu tusije kua kama wenzetu weusi huko US, kabla ya Obama kukosekana kwa real heros kuliwafanya kuanza kuamini hata yule Ferguson aliyeuwa wazungu kwenye LIIR Train bila sababu kuwa shujaa, badala ya a murdereeer!

Mungu Aibariki Tanzania!

FMES, Pania zana Baba mapambano ndio kwanzaaa! yanaanza wengi watakuja CHUI katika sura ya MWANAKONDOO hatujamaliza hoja za mzee MBILINYI (Profesa) amezuku KITINE (Dr) hawa wazee nenda rudi wao walikua watu wa chama na serekali CCM was father to them and SEREKALI was mother WAKIISHI kwa kuvitegemea, WAKITUMWA NA KUTUMIKA, WAKAJENGA,WAKILA,WAKINYWA,WAKINYA,WAKIVAA,WAKISTAREHE,WAKIRUKA na MADEGE HUKU na KULE zaidi ya yote wakilipwa MISHAHARA na MARUPURUPU kwa PESA ya WAVUJA JASHO wa TANZANIA isitoshe heshima tukawapa kwa kutegemea watachukua DHAMANA WALIOAPA kuipokea kwa moyo wa uaminifu.matokeo ni kuwa WAMETUSALITI na sasa wanonyesha UNAFIKI WAO kwa Watanzania. wana JF naomba tuelewane tuwe makini katika kusoma mistari na kuifasiri (read my lips) tusome midomo ya hawa JAMAA kumbuka heshima uliyokuwa ukiwapa, hadhi na daraja ulilowaweka,hawakujali yote hayo WAKATUIBIA WAKAACHA WENZAO WAIBE na wao wako pale as PART and PARCEL ya uongozi wa CHAMA TAWALA na SEREKALI na hawa wazee wetu si wazungu wa reli kama Majuto na Kingwendu ni wasomi PROFESA mzima na DAKTARI mzima. Ni kweli kabisa wanayosema yanaweza kuwa na ukweli sipingi wala sikatai kuwa umo ukweli, lakini MLIKUWA WAPI WAKATI TAIFA LINAWAHITAJI KIKWELIKWELI na wakati mna MENO ya UWAZIRI na UKUU WA USALAMA wa TAIFA?????? Na namna ya kuwasilisha hoja zenu nayo ni potofu, kwanza MNGETOA BORITI KWENYE MACHO YENU, mngetupa angalau Muktahsari wa DHAMBI zenu na kuonyesha HUZUNI juu ya USALITI mliotufanyia,Hapo MNGEKIONA VEMA VIBANZI KATIKA MACHO YA WENZENU!! Na ukweli ni kuwa katika hali hii si RAHISI usimzungumzie MTU au MATUKIO bali uzungumzie MAWAZO ni vigumu sana kwa sababu hawa jamaa wamehusika na hayo MATUKIO kinachoweza kuwatenganisha nayo ni MAHAKAMA ya Sheria tu na mawazo ndio hayo pia tunayajadli kwa MAONI yangu mawazo haya yakichukuliwa kama USHAHIDI wa MUHALIFU dhidi ya MUHALIFU mwanzie yatasaidia sana upande wa MASHTAKA Pengine nayo ikawasaidia wao mbele ya HAKIMU kupata ADHABU AFUENI kidogo.Lakini sikubaliani na maoni ya kuwavalisha watu kama hawa KOFIA ya USHUJAA. Kama kuna KIZEE GAGULA Kingine kianze kuonyesha MIKOBA YAKE kwanza ndipo kifichue wengine.
 
.....wakati Kitine anatoa hiyo tahadhari, yeye mwenyewe kalewa chakari!! LOL.....sasa sijui bado utaendelea kumsikiliza au utaona mlevi mwingine tu huyu! kaaaaazi kweli!

Yeye kalewa lakini hakukamata usukani na gari lazidi kuyumba na milima ya Kitonga inaanza kuonekana..............

.
............the choice is simple
 
Back
Top Bottom