Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Anachosema Mzee Kitine kuhusu nchi kuongozwa kienyeji ni kweli kabisa. Viongozi wengi wamekuwa wababaishaji mno na sijui wamepata vipi huo uongozi. Wanapenda mno uongo kwa sisi wadanganyika!!! Hivi hatuna namna ya kujua watu kabla ya kupewa nyazifa za juu za uongozi? Ama ndio urafiki na undugu wa kugawana nafasi za umma.
Kweli tunahitaji mabadiliko na We need strong leaders when it comes to bold changes...we should never allow things to take us by chance!!! Sasa leo hii we spend more time dealing with petty issues and forget about development.
Nafikiri tufikirie kuwa na mfumo wenye nia ya makusudi ya kuawaandaa vijana wenye uwezo wa kuwa leaders right from the scratch kuwa viongozi wa baadae
Tusiwaachie mafisadi wakaendelea kutuchagulia wapendwa wao. Watayaendeleza matatizo tuliyo nayo leo mpaka yatumalize mana yanafanana fanana Cancer

Mkuu Ndahani, unachosema ni kweli kabisa. Utaratibu uliopo umeshindwa kukindhi mahitaji ya nchi kwa sasa. Huko tuendako, hali inaweza kuwa mbaya zaidi.

Kitine anajua anachosema. Amekuwa kwenye system kwa muda mrfu kuliko Chiligati. In fact, Chiligati amezunguka kauli za Kitine kwa kuanza kuzungumzia amani na utulivu. Ila inashangaza sana kusikia kauli kama hiyo wakati kama huu. Ukiniuliza kama kweli kuna utulivu, nitakataa kwa kiapo. Utulivu umekosekana na ndio maana Kitine anasema mambo yanakwenda kienyeji. Watendaji na viongozi wetu hawajui nini cha kufanya ili tuendelee.

Mkuu, kubadili hali iliyopo sasa, inabidi kubadili Katiba ya nchi. Ni kweli kwamba inawezekana viongozi wa kisiasa wanaoteuliwa wakachambuliwa kabla ya kushika nyadhifa wanazopewa. Ila Katiba inampa madaraka Rais kuteua viongozi wa juu kabisa wa nchi kwa vigezo hafifu sana. Kwa mfano, Waziri Mkuu anatokana na Wabunge wa kuchaguliwa wenye viti vingi Bungeni. Mtu yeyote mwenye hadhi hiyo anaweza kuwa Waziri Mkuu kwa kuteuliwa na Rais na waBunge kusema "ndio" au "hapana". Madaraka makubwa ya Rais, huwafanya waBunge kusema ndio hata kama wana sababu za kusema hapana (ili wasiudhi utawala).

Lingekuwa jambo muhimu pia kwa Mawaziri wote kuteuliwa kutoka popote (kati ya Raia wa Tanzania) bila kujali kama ni waBunge (in fact wangekuwa sio waBunge ingekuwa vyema zaidi). Na wapitishwe na Bunge kwa kujadiliwa kama Baraza zima la Mawaziri ili mchakato huo uwe wa haraka na wa moja kwa moja. Hii yote inategemea mabadiliko ya Katiba. La sivyo haitadumu sana.
 
Ina maana wazee wa hili baraza mnajifanya hamjui undani wa so called Kitine scandal? Ina maana wote hapa hamjui aina ya mahusiano ya huyo anayeitwa mke wa Kitine na Kitine wakati ule kiasi cha kufikia kumbebesha Mzee Kitine Msalaba wote wa huo wizi? Ina maana wote tumesahau mchakato mzima wa scandal ya Kitine wakati ule wa harakati za safisha njia mtandao upite?

Hivi kama kila kinachosemwa mtaani ama magazetini kitachukuliwa kama kipimo cha nani ana uhalali wa kusemea maslahi ya taifa na nani hana ni kweli tutakuwa na mtu wa kusema pale nchi inapoelekea kuzimu?

Naomba mmoja kati yetu hapa ambaye hajawahi kushutumiwa kwa kosa lolote lile?

Hivi humu ndani hatuna watu waliotumia fedha za serikali isivyo halali, ama katika kulipiwa masomo yao wakati wanakosa vigizo ama wakati mwengine hata kutokuwa wanafunzi, ama kutumia bank statements fake kupata visa na wakati mwengine kutumia statements za hao hao tunaowaita mafisadi, ama kuishi ughaibuni kinyume cha sheria kwa wakati fulani, ama kudanganya uhalisia wao ama hata uraia wao halisi ili kuweza kuishi ughaibuni, ama kukiuka kulipa kodi na madai mengine halali ama ughaibuni au nyumbani?

Hivi ni wangapi humu ndani ambao wanaishi ughaibuni na kuhodhi akaunti za benki na wamefanya wajibu wao wa kutoa taarifa Benki Kuu na kulipa kodi wanazopaswa kama raia wengine nchi kama ambavyp taratibu na sheria za nchi zinavyoelekeza?.

Je wote waliofanya haya na mengine hawapaswi kusema kuwa nyumba yetu Tanzania ina ufa unao ongezeka kwa kasi?

Naamini tunahitaji watu kama Kitine kuongea ingawa kuna hatari zake? Tutakuwa tunajidanganya kama tunadhani kuwa aliyesema pale ni Kitine pekee. Kuna wengi nyuma yake, watu binafsi na makundi nyeti. Kitine anawakilisha wengi na mengi. Hali ni mbaya ndugu zangu....

Na hili la nyang'au Lyumba ndio limekoroga mambo kabisa.......

Two wrongs can not make a right!!!!!!!
 
Tunayoyasema yanamake sense kwa kiasi kikubwa. Ni ukweli usiofichika kwamba nchi yetu inaendeshwa kwa auto-pilot wakati ikiwa kwenye hali mbaya, ni wakati ambao rubani alihitajika kuwa makini hasa. Viongozi wetu ni wale wenye majibu rahisi kwa maswali magumu. Ni wakati ambao tungelihitaji major overhaul ktk safu yote ya uongozi. Wasiwasi wangu ni kwamba kama safari hiyo imeanza bado kasi yake ni ya kinyonga, ninamaanisha come 2010, hawahawa jamaa wanaotuhumiwa kwa kashfa kibao wataenda kwa wananchi na kanga na kofia zao, chumvi, na wengine hata underwear(serious), na wananchi watashabikia hivyo walivyopewa na kuwarudisha madarakani. Ukweli huu unajionyesha hata ktk vyuo vikuu, tulikodhani kungekuwa chanzo cha mabadiliko, bahati mbaya mambo si hivyo. Wakati wa uchaguzi wa 2005, viongozi wa ccm walitembelea vyuo vikuu na kugawa fedha, fulana, skafu, u name them, wanafunzi walifanya nini? walivipokea na wakaipa ushindi.
Ninaamini huenda mambo yamebadilika kwa miaka hii michache, lakini hii hainipi raha kwamba tutakuwa na mabadiliko makubwa,nadhani ccm waliliandaa hili kwa siku nyingi kuharibu uwezo wa watu kufikiri na kujua haki zao, na kuwafundisha kuwa kuiba mali ya umma ni sawa tu, na ndio maana watu mtaani watamsifu mtu aliyeiba na kujenga au kufanya jambo la kihistoria mtaani kuliko aliyetumikia nchi kwa uadilifu na kustaafu kwa pensheni kiduchu, hawa wanachekwa mtaani.
Ni dhamira ya viongozi wetu kutawala watu masikini kwa sababu gharama ya kuwahonga ni ndogo, kanga tu na kofia kuliko watu wanaojua haki zao kama raia. Kila mmoja wetu ajiulize anafanya nini kuhakikisha anabadili fikra hizi za wananchi? Sisi tunaweza kuona haya mambo, lakini unadhani mwananchi wa kawaida anajali? Kama kweli tunataka kubadili mfumo huu, ni lazima tujaribu si tu kujadiliana hapa, kujaribu kuelimisha jamii zetu juu ya hali inayotukabili kama taifa. Kwani kuna mtu ni mtanzania zaidi ya mwingine hapa nchini? alipata wapi haki ya yeye kujiona bora kuliko watu wengine? uongozi ni dhamana ambayo wale wanaopewa wanapaswa kuitumia kwa manufaa ya wengine wote, na kuacha ubinafsi huu.
Kama tunataka mabadiliko ya kweli na tuanze kuwa wakweli na kuukemea wizi na ubinafsi kwa stahili zinazofaa, sio kuupaka mafuta.
 
Lingekuwa jambo muhimu pia kwa Mawaziri wote kuteuliwa kutoka popote (kati ya Raia wa Tanzania) bila kujali kama ni waBunge (in fact wangekuwa sio waBunge ingekuwa vyema zaidi). Na wapitishwe na Bunge kwa kujadiliwa kama Baraza zima la Mawaziri ili mchakato huo uwe wa haraka na wa moja kwa moja. Hii yote inategemea mabadiliko ya Katiba. La sivyo haitadumu sana.

- Mkuu Recta, tungekua na hii system, bado Kitine asingekua kiongozi kwa sababu venting system ingemtema, kutakana na wizi alioufanya akiwa uwt in the 80s, na kufukuzwa na Mwalimu.
 
- Kitine hakuadhibiwa kama sheria inavyosema, baada ya kamati ya bunge kugundua kua yeye na mkewe wameliibia taifa, walitakiwa kwenda kwenye sheria kama kina Mramba na Yona, lakini ukafanywa ujanja ujanja ulioishia kumrudisha Kaburu CCM, na Kitine akaishia kulipa only nusu kama alilipa kweli, ya zile pesa, Kitine hakuadhibiwa mkuu ila kwa aibu alijuzulu na kuendelea kuwa mbunge, mpaka alipokimbizwa na wananchi wa Makete.

- kitu ambacho yeye sasa hakitaki anasema kiongozi akishajulikana kuwa ni fisadi atolewe nafasi zote, yeye ufisadi wake ulithibitishwa hata na sheria, lakini hakuachia ngazi zote wala kwenda kwenye sheria, lakini sasa anataka wengine waondolewe na kufikishwa kwenye sheria na kuachia ngazi zote, tunasema hivi hana huo ubavu, aweke mfano wa uongozi usio wa kienyeji kwa kutangulia yeye kwanza kwenye sheria!

- Anachosema sio sahihi, ila kuna yasiyo sahihi hajayasema na anayajua sana kwa sababu ya nafasi alizowahi kuzishika katika taifa, kwa mtizamo wangu serikali yetu iemkua ikiendeshwa kienyeji hata yeye akiwa kiongozi, maana kama isingekua yeye na Mbilinyi, walitakiwa kutoa hizi interview wakiwa jela kama wezi wengine wa kuku na mbuzi.

Maadili na sheria, ni vitu viwili tofauti Kitine na mkewe wamevunja sheria za jamhuri, sasa kwa taifa lisiloendeshwa kienyeji kama anavyotaka, alitakiwa kuwa jela sio kutupa empty lectures kwenye majukwaa ya siasa.

Mkuu FMES, nadhani unajua kuwa kushitaki ama kutoshitaki ni uamuzi wa alietendewa. Kukukumbusha tu, Kitine hakuiba pesa aliyokabidhiwa madaraka ya kuitunza. Ila alitumia mwanya uliokuwepo kumpeleka mkewe kutibiwa nje bila kukamilisha taratibu (kitu kama hicho). Serikali hufanya maamuzi ambayo huwa yana utata mara kwa mara. Mifano ni mingi, ila sio nia yangu kuiweka hapa. Wakati mwingine inapotokea mtu akalalamikia utaratibu na hasa vyombo vya habari kuicharukia serikali, huamua kusitisha taratibu hizo (ambazo nyingi sio mbaya) na kuwafanya waliofaidika nazo waonekane wamekosea. Labda ndio maana Serikali ikaona alipe nusu tu ya gharama.

Mkuu sioni lolote lisilo sahihi katika maelezo ya Kitine. Kama yapo naomba utumie utaratibu wako wa kawaida wa hoja kuyabainisha ili tuelewe zaidi.
 
Mkuu FMES, nadhani unajua kuwa kushitaki ama kutoshitaki ni uamuzi wa alietendewa.

- Tulitendewa wananchi wa Tanzania, hakimu akiwa Kaburu aliyeahidiwa ubunge wa EAC na CCM, hivyo kumuachia Kitine na mkewe, sasa hapa wananchi tungefanya nini zaidi?.

Kukukumbusha tu, Kitine hakuiba pesa aliyokabidhiwa madaraka ya kuitunza.

- Kitine alikula kiapo cha kuilinda jamhuri ikiwa ni pamoja na mali zake, yes aliiba kwa sababu alijua mke wake sio mgonjwa, sasa anachukuaje hela za wagonjwa na huku mume aliyekula kiapo cha kulinda jamhuri na mali zake anajua kuwa sio mgonjwa? Asingekwu mke wa Kitine kiongozi unafikiri asingepewa hizo hela? Sasa kwa nini Kitine alijiuzulu uwaziri wakati aliyechuiba hela mkewe mkuu na sio yeye?

Ila alitumia mwanya uliokuwepo kumpeleka mkewe kutibiwa nje bila kukamilisha taratibu (kitu kama hicho). Serikali hufanya maamuzi ambayo huwa yana utata mara kwa mara. Mifano ni mingi, ila sio nia yangu kuiweka hapa. Wakati mwingine inapotokea mtu akalalamikia utaratibu na hasa vyombo vya habari kuicharukia serikali, huamua kusitisha taratibu hizo (ambazo nyingi sio mbaya) na kuwafanya waliofaidika nazo waonekane wamekosea. Labda ndio maana Serikali ikaona alipe nusu tu ya gharama.

- Serikali haikuona, ila ni Kaburu aliyekwua anataka nafasi ya ubunge wa EAC kupitia CCM kwa kushinikizwa na wenye nguvu ndani ya CCM, ndio waliamoamua kwa ujanja ujanja, lakini ukiifufua hii kesi leo Kitine na mkewe wanatakwia kwenda kwenye sheria na hasa kuishia jela, sio kwenye majukwaa ya siasa kama anavyofanya.

Mkuu sioni lolote lisilo sahihi katika maelezo ya Kitine. Kama yapo naomba utumie utaratibu wako wa kawaida wa hoja kuyabainisha ili tuelewe zaidi

- Hata mimi mkuu sioni lolote la sahihi katika ishu nzima ya Kitine, na hawa waandishi ndio kabisa sielewi wanachofanya, maana nilitegemea wamuulize maswali kama haya tunayouliza hapa!,

- Mkuu ninachukizwa snaa na watu kama huyu Kitine, kwa sababu hawa ndio waliokuwa the trusted wa Mwalimu, kutuongoza akiwa hayupo, sasa tizama waliyotufanyia!
 
Mr Kitine.... You are doing the right thing for a wrong reason!

... We only appriciate tha right componet on it!
 
- Hata mimi mkuu sioni lolote la sahihi katika ishu nzima ya Kitine, na hawa waandishi ndio kabisa sielewi wanachofanya, maana nilitegemea wamuulize maswali kama haya tunayouliza hapa!

Waandishi wetu ni waajabu sana....wanaandika kile ambacho viongozi wanapenda kukisoma, I am afraid uwezom wao wakuwa critical bila kuwa offensive haupo labda hawawezi kufikiria kutengeneza the so called news, stereotype kind of mind....Siamini chochote Tanzania kuanzia Polisi, Mahakama, magazeti, wanasiasa hovyo hovyo kila kitu.
 
Kama ndiyo hivyo basi hakuna kiongozi yeyote mstaafu ambaye ana sifa ya kuongea kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu maana wote ambao wako hai wana tatizo moja au jingine. Mzee Rukhsa tunajua ufisadi wa Mama Siti na yeye mwenyewe kugawa viwanja kwa ndugu, jamaa na marafiki. Cleopa Msuya aliwahi kutwambia kwamba kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe, Malecela tunajua matatizo yake mbali mbali hata Mwalimu alishamuona hastahili kuwa Rais wa nchi yetu. Salim Ahmed ataambiwa ni Mwarabu alikaa nje ya nchi miaka mingi hajui lolote kuhusu Tanzania hivyo hana wajibu wa kutia neno lolote kuhusu uongozi mbovu ndani ya nchi yetu. Sumaye naye ni fisadi alitumia nafasi yake kama PM kujikusanyia utajiri wa hali ya juu ambao hakuwa nao kabla ya kuwa Waziri Mkuu, Kawawa naye ni mwasherati alikuwa na wake zaidi ya mmoja.

Wote wakae kimya tu na kuiacha Tanzania ikiendelea kuangamia kutokana na kuongozwa na watu wasiokuwa na hata chembe ya maadili ya uongozi, wasio na ujasiri na waliojaa woga wa hali ya juu na siku zote wataweka mbele maslahi yao, ya marafiki zao ambao ni mafisadi na chama chao cha kifisadi badala ya yale ya nchi.

Mungu inusuru Tanzania maana badala ya kupima uzito wa maneno yaliyosemwa sasa tunaangalia nani kayasema na kama aliyesema si mtu safi basi hayana sifa ya kujadiliwa na kuyatafakari maana ni upupu tu!!!! 😕😕

Si ajabu viongozi wengi wastaafu wameamua kukaa kimya huku nchi ikiendelea kuangamia maana wakiamua kukemea hali ya uongozi ndani ya nchi yetu basi mafisadi, watetezi wao na hata baadhi ya Watanzania wataamua kuwachafua tena na kuwaambia kaa kimya wewe hustahili kusema lolote wewe na matokeo yake nchi inaendelea kuangamia na matokeo yake mafisadi wanaendelea kupata nguvu na kushamiri kila kukicha!!!!

Oh! Tanzania unaelekea wapi nchi yangu!!!!! 🙁 🙁

I live to disagree. Kiongozi anapostaafu anatakiwa awe kisima cha wisdom cha uongozi uliopo madarakani. Wisdom yake itatokana na performance ya uongozi wake uliopita. Leo hii tutakuwa wapumbavu endapo tutachota wisdom ya viongozi wastaafu wanaonuka rushwa na waliosababisha umaskini wetu kwa namna moja au nyingine.

Kiongozi aliyeliibia taifa wakati wa uongozi wake na kutufanya tuwe maskini anatakiwa ashitakiwe kwanza kabla ya yeye kukemea matendo mabaya.

Inasikitisha; wezi wa taifa letu wa miaka nenda rudi wako mitaani na kibaya zaidi sasa wana nguvu za kukemea wenzao. Wanachofanya ni kutonesha damu kwenye donda ndugu walizotuachia. This only happens in Tz.
 
Hivi wakuu sasa hayo maovu ndani ya chama aachiwe nai kuyasema ? maana kila anyesema ana matope.
Katika viongozi wa Tanzania wa leo hakuna aliye safi, Mr Clean hayupo tena.
Ukweli unatabia moja ,haupingiki hata ukisemwa na shetani!
Bado aliyosema mzee Kitine yana ukweli ambao ni changamoto kwa utawala uliopo.
Ni bora tujisahihishe na tugange yajayo


Tupo pamoja Gwakisa

Nchi mojawapo ya Amerika Kusini iliwahi kukumbwa na janga la rushwa (ufisadi) uliokithiri kiasi kwamba kama ingeamriwa kuweka jela watu wote ambao wanajihusisha na ufisadi, makomeo ya magereza ya nchi hiyo yasingebakiwa na mtu wa kuyafunga!.

Achilia mbali Mzee Mwinyi na Mkapa, hata aliyepo madarakani nina imani akishaachia ngazi naye yataanikwa mengi tu. Wasaidizi wake hali kadhalika. Mfumo tulionao unatuandalia viongozi wabovu.

Tukishafikia hapo hatuwezi kusema mifumo ya utawala basi.Lazima watajitokeza watu miongoni mwenu kusema na kuanika wapi mmepotea njia na nini kifanyike.

Tanzania yetu ya leo ni viongozi wangapi walio madarakani na wastaafu wakianika historia zao watakuwa clean? Yawezekana asipatikane hata mmoja!!

Kitine, Mwinyi,Mkapa,Kawawa,Sumaye,Msuya,Lowasa nk jitokezeni mseme mlipokosea na mkosoe kwa uwazi utawala wa sasa ili kwa pamoja tuweze ku revamp Tanzania yetu. Vyema mnapotambua machungu ya tawala mbovu.


Si dhambi tukijisahihisha,tukakosoana na kusonga mbele.Tukimnyamazisha kila anayetaka kukosoa kwa sababu ya historia yake hatutofika.
 
Kwanini Mr. Kitine analipenda taifa wakati uchaguzi unakaribia?? Issue zake mara nyingi zinakuja mwaka mmoja kabla ya uchaguzi.
 
U turn ndugu zangu!

Asamehewe makosa..hatuna malaika..hata Clinton kwa Monica alichemsha!
 
- Tizama kwenye mbio zangu za ubaharia, mwaka 1987 niliwahi kusihi miji ya Montreal na Ottawa, nikamkuta huyu jamaa Kitine, hivi unakumbuka nchi yetu ilivyokuwa na matatizo ya uchumi wakati huo? Jamaaa alikuwa anapasua kuku tena bila huruma, kisa mtu wa Mwalimu analetewa tu michuzi na serikali huku wananchi masikini wanahangaika, wanafunzi hawana hela shuleni hawa wako majuu wanatesa na hela za wananchi,

- Amerudi bado tu anataka njia za short cut, thanxs wananchi wa Makete kwa kumtupa kwenye ubunge, hawa kina Kitine ingekua u-China dawa yao huwa ni ndogo sana, hivi majuzi rais wao si alikuwepo hakuna aliyemuomba wataalamu wa nyanja za kuondoa ufisadi, watufundihe what to do na watu kama huyu Kitine?
 
Wakuu, katiba yetu pamoja na mapungufu yake haimkatazi Mtanzania yeyote yule kutoa maoni yake kuhusiana na mwenendo katika nchi yetu, hata akiwa fisadi. Tunachotakiwa kufanya sisi kama Watanzania ni kuyatafakari hayo yaliyozungumzwa na Mtanzania mwenzetu je yanaingia akilini? je, yana uzito unaostahili? je, yana ukweli wowote? je, yanastahili kujadiliwa na Watanzania kama yana maslahi makubwa kwa nchi yetu kwa sasa, siku za usoni na vizazi vyetu vijavyo? Kwa maoni yangu aliyoyazungumza Kitine majibu ya mswali niliyoyaweka hapo juu yote ni ndiyo.

Tukianza kuwakejeli Watanzania wenzetu hasa waliowahi kushika nafasi mbali mbali za uongozi wanaotoa maoni yao dhidi ya hali ya nchi yetu basi itafika wakati hakuna Mtanzania yeyote yule atakayethubutu kutoa maoni maana hatuna malaika ndani ya Tanzania. Hakuna muda muafaka wa Watanzania kutoa maoni yao. Hata kama ni karibu na uchaguzi tuna haki ya kufanya hivyo tena huo ndiyo wakati mzuri sana ili kuhakikisha uchaguzi ujao tunakuwa makini mno katika maamuzi yetu ya nani wa kumchagua.

Alichofanya Kitine akiwa madarakani alistahili kabisa kufukuzwa kazi na kufunguliwa mashtaka lakini boss wake wa wakati huo Mkapa hakuona umuhimu wa kufanya hivyo maana naye alikuwa busy akifanya madudu yake (hivi Mkapa wakati wa awamu yake ya tatu aliwahi kumfukuza kazi yeyote yule aliyemteua?) na labda madudu hayo Kitine alikuwa anayajua hivyo aliamua kuyafumbia macho ili Kitine naye ayafumbie macho madudu ya Mkapa.

Tukiamua kunyamaza na pia kuwakejeli wale wanaotoa maoni dhidi ya nchi yetu basi tusishangae miaka michache ijayo nchi yetu kuwa kama Zimbabwe na tukifika huko hakuna wa kumlaumu bali ni sisi wenyewe Watanzania.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Last edited:
Alichofanya Kitine akiwa madarakani alistahili kabisa kufukuzwa kazi na kufunguliwa mashtaka lakini boss wake wa wakati huo Mkapa hakuona umuhimu wa kufanya hivyo maana naye alikuwa busy akifanya madudu yake (hivi Mkapa wakati wa awamu yake ya tatu aliwahi kumfukuza kazi yeyote yule aliyemteua?) na labda madudu hayo Kitine alikuwa anayajua hivyo aliamua kuyafumbia macho ili Kitine naye ayafumbie macho madudu ya Mkapa.

- Mkuu BAK, marekebisho tu Mkapa aliwahi kumfukuzwa wazriri wake mdogo wa pesa Mporogomyi,

- tena kwa hasira sana kama mbwa kwa sababu ndiye aliyemchongea rafiki yake Mkapa, yaani Mbilinyi na zile hela za samaki.
 
- Mkuu BAK, marekebisho tu Mkapa aliwahi kumfukuzwa wazriri wake mdogo wa pesa Mporogomyi,

- tena kwa hasira sana kama mbwa kwa sababu ndiye aliyemchongea rafiki yake Mkapa, yaani Mbilinyi na zile hela za samaki.

Thanks Mkuu, katika miaka yote 10 aliyokaa madarakani alifukuza Waziri mmoja tu pamoja na kashfa zote za Rada, ndege ya Rais, net group n.k.? Hivi yule Simba aliyeweka mbele sera za uzawa naye alifukuzwa au hakuteuliwa tena?
 
-

- Mkuu ninachukizwa snaa na watu kama huyu Kitine, kwa sababu hawa ndio waliokuwa the trusted wa Mwalimu, kutuongoza akiwa hayupo, sasa tizama waliyotufanyia!

Mkuu FMES, sioni sababu ya wewe kuchukizwa na mtu aliyeamua kuurudia ukweli na kuuona kwa rangi zake, hata kama amechelewa kuusema lakini amethubutu kufanya ambacho wengi hawawezi kwa kuchelea kupatwa na yasiyosemeka. Yasiposema na watu wanaoyajua, nani atayasema. Ukweli kwamba nchi inaendeshwa kienyeji na kisanii unajulikana siku nyingi na wengi wetu, lakini yeyote yule ambaye hayupo kwenye hizo system akisema inaonekana ni kelele za chura ambazo hazimzuii tembo ku... kunywa maji. Anaposema mtu ambaye amewahi kuwa kwenye inteligence for such a long time, it makes alot of sense. Hata kama scandal yake ilifunikwa labda kwa uzembe wa utawala, hiyo isiwe sababu ya yeye kutosema ukweli, wakitaka wanaweza pia kumfungulia mashtaka. Lakini usitake tuache kusifia ukweli unaposemwa, hata kama anayeusema ni mwovu, ukweli daima utabaki ukweli hata ukiusiriba kwa lami. Tabia kama hii ndio inayofanya watu kuanzisha magazeti ya kupakana matope, ili kujaribu kutafuta skandali zozote za wale ambao wanaonekana kuuzimamia ukweli. Kama alitenda kosa anastahili kuwajibishwa, lakini kwa hili halina chembe ya unafiki
 
"Simple minds discuss people, ordinary minds discuss events and great minds discuss ideas". I believe we have a choice here - to discuss Kitine, to discuss what he did or to discuss the ideas he put forward. For some the choice will be simple, for others it will be hard and for the rest it wont matter. We are in dire need for help for we are stuck in the mud and are sinking fast - do we grab any rope thrown to us or do we sink and die ? Kitine was once part of the Mafia and for breaking the code of silence, they have but two choices - silence him or ignore and discredit him. Fortunately for those who have the interest of the country at heart, what matters is not what Kitine did but what he said - again the choice is simple.
 
Mkuu BAK, marekebisho tu Mkapa aliwahi kumfukuzwa wazriri wake mdogo wa pesa Mporogomyi,

Mkapa hakuwahi kufukuza waziri wake hata mmoja. Kilichotokea ni kwamba wakati Prof. Mbilinyi akiwa Waziri wa Fedha, Mpologomyi alikuwa Naibu Waziri wa Fedha. Hivyo, ile kasha ilipotokea, Profesa Mbilinyi na Mpologomyi wote wakajiuzu. Kama hawakujiuzulu, tumese basi Mkapa aliwafukuza wote wawili Mbilinyi na Mpologomyi.
 
“Hatuwezi kuwavua watu uanachama au nyadhifa zao ndani ya chama kwa sababu hiyo tu. Yeye aliyesema hivyo atutajie ni kiongozi gani wa serikali ambaye pia ni kiongozi wa chama, ameshathibitika kuwa hana maadili halafu kama chama tumeendelea kumwacha. Atuambie…..hakuna,” alisema Chiligati.

[/COLOR][/font][/size]


Mmmhhhh!!! Viongozi wengine inabidi wapimwe akili kabla ya kupewa madaraka. Haya si maneno ya mtu mwenye akili timamu.
 
Back
Top Bottom