Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Tukubaliane just for the sake of argument:

a. Mke wa Kitina aliwahi kuhusishwa na vitendo vya kifisadi never prosecuted.
b. Kitine alitaka kuwa Waziri sana hakupewa nafasi
c. Kitine bado ana machungu ya kuwekwa pembeni
d. Kitine naye ni fisadi (I'll go to that extreme).

Sasa:

a. Hoja zake juu ya tatizo la uongozi uliopo sasa hivi zina nguvu yoyote?
b. Je mtazamo wake kuhusu wajibu wa Usalam wa Taifa ni sahihi?
c. Assessment yake ya siasa za makundi ndani ya chama zina mantiki yoyote?
d. Je, kuna jambo lolote ambalo amelisema ambalo lina chembe ya ukweli au yote ni fabrication of his bitter mind?

im with you on this one! so far zaidi ya upinzani hakuna aliyesema kuusu uozo wa UWT. Whether kitine analake jambo au la its a win win for those who want change.
 
Vipi kuhusu bosi wake Mkapa? What does he have to say about him?

NN:

Ndio siasa ya bongo. Mtu akiboronga anaingia mitini miaka kumi na baadaye anaibuka.

Mkapa anajichimbia baada ya miaka kumi utamsikia anarudi kutupa shule kama Mzee Rukhsa na sasa Kitine.
 
Tukubaliane just for the sake of argument:

a. Mke wa Kitina aliwahi kuhusishwa na vitendo vya kifisadi never prosecuted.
b. Kitine alitaka kuwa Waziri sana hakupewa nafasi
c. Kitine bado ana machungu ya kuwekwa pembeni
d. Kitine naye ni fisadi (I'll go to that extreme).

Sasa:

a. Hoja zake juu ya tatizo la uongozi uliopo sasa hivi zina nguvu yoyote?
b. Je mtazamo wake kuhusu wajibu wa Usalam wa Taifa ni sahihi?
c. Assessment yake ya siasa za makundi ndani ya chama zina mantiki yoyote?
d. Je, kuna jambo lolote ambalo amelisema ambalo lina chembe ya ukweli au yote ni fabrication of his bitter mind?

Mkuu MM Villager,Hivi ni nani alikuwa akiseme alichokisema ili kieleweke na watanzania na wakielewe.
Mwalimu ndo hayupo hivo.
Mtu akiwa ndani , akicheza na uchafu hajioni kuwa ni mchafu.
Watu wadogo wadogo wakirusha maneno kuwa we mchafu , kama wengi wanavyofanya sasa si rahisi waloi ndani , wachafu kuwaelewa.Hata mtu ukiandika makala zenye urefu wa kitabu.
Hawa watu waliokuwa ndani, wana chembe za uchafu, wanaona uchafu wao na wenzao wakiwa nje, hata vyombo vya habari vinaupa kipaumbele ujumbe huu, people litsen.
Ndio maana tunasema our best chance ni kujisahihisha sisi wenyewe na kusonga mbele.
Hivi aje mzungu ndo akuambie kuna uchafu ndo mtu utaridhika kwamba kweli kuna uchafu?
 
ndio tuseme keshaokoka au ndio ufisadi umezidi mno hadi aliyewahi kuwa fisadi anaona uchungu nchi inavyotafunwa na mapapa wakubwa? duh kaaazi kwelikweli
 
Huyu wakati wake ndio rushwa imechipuka na kuota mizizi sasa anataka kuchonga, yeye mwenyewe inatakiwa achunguzwe, mali alizojilimbikizia zimetokana na mshahara na marupurupu yake tu? aueleze uma, mali zake kazitowa wapi?

Dar Es Salaam!
Mzuri kwako ni yupi? anayewatetea mafisadi?
 
"If you dont know where you are going, any road will take you there"..., kuna mantiki sana kwenye msemo huu. Watanzania nahisi hatujui tunachotaka zaidi ya kulalamika. May be it makes us feel better katikati ya lundo letu la umaskini. Ukitazama, mtu anayetetea uozo anashambuliwa, na anayekemea uozo nae anashambuliwa.

Alikuja mzee Warioba siku za nyuma, akataka watu wasiiongelea vibaya taasisi ya urais(wakati kelele za Mkapa kushtakiwa) sababu nchi itayumba. Watu wakapiga kelele wee hapahapa, kwamba huyu mzee anataka kuficha mabaya ya viongozi, analinda uozo n.k...

Sasa hivi anatokea huyu ambaye ni heavy weight mwingine, au insider anatoa a critical assesment ili tujisahihishe moving forward, then naye tunamrukia kuwa yeye ni mchafu, kwanini hakufanya alipokua waziri n.k...

Ukitazama ni kama tumeamua kuwa bitter tu kwa yeyote aliyewahi kuwa na power zamani. Ni kweli wanamakosa yao, lakini kwa vita hii ya kulirudisha taifa kwenye mstari, ni muhimu kuyafanyia kazi mawazo mazuri yeyote, hasa yanayotoka kwa such heavyweights, maana yana leverage kubwa. Kauli moja critical ya hawa heavyweights inaweza kuwa na effect kubwa kuliko post 10,000 za mtu mmojammoja hapa jamvini.

Im sure kama JMK ameziona headlines za leo na picha ya Kitine, atapata something to think about, a food for thought, whether positively au defensively na kuichukulia negatively. Na hilo ndio tunalotaka, Mkuu lazma kichwa kimuume kwa kujua watanzania wanampima vipi.

Kwa tunavyoenda hapa, hata akija CD Msuya, JS Malecela, K Ngombalemwiru, AH Mwinyi, RM Kawawa, FT Sumaye n.k... maana yeyote yule kati ya former heavyweights akiinua mdomo kukemea uozo kama tukiamua tunaweza kum bring down na mapungufu yake...in the end taifa ndio linalolose as tunaangalia personalities badala ya agenda za taifa..
 
- Kitine na Mkapa, Mwalimu's people tena damu damu, Mwalimu alipokuwa ana-retire akapelekwa Canada kula nchi, akilipiwa kila kitu na serikali yaani hela zetu walipa kodi anachokifanya hakieleweki, Mkapa kuwa rais tu akamuomba kurudi great friends akarudi, Mkapa akatumia ubabe na nguvu za ajabu within a month Kitine ni mbunge na waziri ofisi ya Mkapa, all this time hajaona ubovu wa uongozi wetu wala tatizo la integrity,

- The next thing Kitine anaota urais, ghafla kaanza kuvaa kanzu na barakashia bungeni, nini kaambiwa rais anayefuata Mkapa lazima awe Muisilamu, mara oooh mawaziri ni wala rushwa, haya Kitine tuambie majina yao, akadai oooh no waandishi wamekosea sikusema vile, next mke wake amechukua maelfu ya dola za walipa kodi kwenda kutibiwa nje, kumbe ameenda kuzifanyia shopping bila kwenda Hospital wala kwa Daktari yoyote huko Canada na wala haumwi chochote, sasa all this time Kitine haoni ubovu wala tatizo la integrity na uongozI wetu,
- The next thing Kitine amehonga honga na kujaribu kuzuia uchunguzi wa kamati ya bunge kuhusiana na wizi wa mkewe wa hela zetu walipa kodi alizotumia nje tena kwa uharibifu sana, wabunge kuja juu sana ndio Kitine baada ya kubanwa sana na wabunge kukubali kujiuzulu na kulazimishwa kulipa nusu ya zile pesa tena katika mazingara yaliyojaa uhuni uhuni, badala ya mkewe kwenda jela kwa wizi wa mchana wa hela zetu walipa kodi, all this time Kitine haoni matatizo ya uongozi wetu na integrity yake kua hovyo!

Sasa leo he is supposed to be a hero kwa sababu amesema maneno ya kuponda serikali ya CCM, akitukana ubovu ule ule uliomponya yeye na mkewe, sometimes huwa ninajiuliza hivi vita tunavyopigana na mafisadi, kwa mfano tukiwatoa mafisadi wote leo, eti ni kweli tutaweza kuweka viongozi wapya ambao hawatakuwa mafisadi? Ningeelewa kwamba Kitine sasa ameamua kwamba wananchi wa Tanzania wameonewa vya kutosha na kuweka mfano anataka mkewe afunguliwe mashitaka kwanza ya kuiba hela zetu walipa kodi huko nyuma maana sasa anataka to come clean, no sasa yeye na Mbilinyi ni mashujaa against uozo wa uongozi wetu uliowaponya.

Tuangalie sana ndugu zangu tusije kua kama wenzetu weusi huko US, kabla ya Obama kukosekana kwa real heros kuliwafanya kuanza kuamini hata yule Ferguson aliyeuwa wazungu kwenye LIIR Train bila sababu kuwa shujaa, badala ya a murdereeer!

Mungu Aibariki Tanzania!

Ukweli unatabia moja ,haupingiki hata ukisemwa na shetani! -Lole Gwagisa
 
Wanaompinga Kitine ni wale tu wasioitakia mema tanzania hasa mafisadi, marafiki zao na familiya zao.

- Mkuu wangu mimi ninampinga sana tena sana Kitine na sio kwa sababu ulizozitoa hapo juu ambazo ni nothing but name calling, meaning kwamba huna hoja,

- Kumuunga mkono Kitine na haya maneno, eti ni kuitakia mema Tanzania? Hapana Kitine amewahi kukurupuka na maneno kama haya ndio kwa mara ya kwanza wanaomfahamu vizuri wakamtolea ya kwake na mkewe, Mkewe amewahi kuwa convicted na kamati ya bunge na akalazimishwa kulipa hela back.

- Kitine alidai mawaziri ndio wanaongoza kwa rushwa, alipoambiwa awaseme kwa majina akadai hakusema hivyo waandishi wamem-quote vibaya, sasa kwa nini unataka niamini kwamba this time he is for real? Kwa kujali uozo wake wananchi wa jimbo lake wakamtosa nje hatukusikia kwenye kampeni za kura za maoni akisema haya ya uozo wa serikali kwa nini? Ni kwa sababu alidhani mtandao watamuonea huruma na kumpa mlo, sasa ni clear kuwa hawana mpango wa kumpa mlo ameanza na yalke yale, akikabwa koo atasema sikusema, sasa with all the past history ya huyu mkuu na wizi wake mkubwa sana toka hata enzi za mwalimu mpaka akafukuzwa uwt, ninatakiwa kumuamini this time na kwamba eti nisipomuamini na kumuunga mkono basi siitakii mema Tanzania? Hapana mkuu sio kweli kabisaa! Huyu ni kiongozi mwizi tu kama wengine sina sababu hata moja ya kumsikiliza lakini unaweza kumsikiliza ukitaka,

-Majuzi Msekwa alipokuwa kwenye sidelines, ameponda sana serikali leo amerudishwa kwenye mlo hebu niambie amefanya nini kuhusiana na malalamiko yake akiwa nje? Sasa after all this eti kukataa maneno ya Kitine ni kutoitakia mema Tanzania?

- In one way or another, karibu wote hapa tunajuana na mafisadi lakini kinachotutofautisha ni tabia zetu kuanzia kwenye maisha yetu ya kila siku, na mpaka maneno tunayoyasema hapa, Kitine ni fisadi period ndio maana alifukuzwa kazi na Mwalimu, na mkewe pia ni fisadi period ndio maana Kitine alijizulu uwaziri infact mkewe hata alikuwa convicted na kamati ya bunge, lakini Kaburu akai-fisadi process akapona kwenda jela,

Sasa mkuu kama umeamua kwamba huyu Kitine ni shujaa wako good for you, lakini naomba tukubaliane kutokubaliana, mimi siwezi kusikiliza neno hata moja la Kitine kuhusu ufisadi, kwa sababu ni fisadi aliyewekwa nje ya mlo sasa ana njaaa! Huyu aliyetaka kutafuta urais kwa njia za udini na kuanza kuvaa kanzu na kibaraghashia kwa sababu eti next rais ni lazima awe Muisilam ndio leo nimsikilize kwa sababu eti sasa anakemea ufisadi hapan mimi simo mkuu na I have nothing to do na ufisadi!

Thanxs!
 
Kwenye kitabu kitakatifu hakuna mtu aliyekuwa mchafu kama Saulo. Lakini leo hii Wakristo wote tunajitahidi kufuata maagizo ya Saulo ambaye baada ya kuona mwanga akiwa njiani kuelekea Damascus aligeuka na kuwa Mtakatifu Paulo. Kitine naye huenda ana madhambi yake, lakini tusikilize ujumbe wake. Je,anayoyasema ni kweli? Tukianza kutafuta watakatifu peke yake katika vita vya ufisadi hatutafika mbali.
 
Jamani kama kuna aliye msafi ajitokeze kumpiga Kitine mawe.

Kila mtu ana mapungufu yake, ila kupinga rushwa na ku challenge status quo ni muhimu hata kwa aliye mchafu!

Sasa kama yeye si msafi wka nini ananyooshea vidole wenzake?
 
- Mkulu wangu with all due respect mimi ni msafi na clean na sina ufisadi wa anything na ninaamini tupo wabongo wengi sana kama mimi ambao tunaweza kulisaidia hili taifa kwa kuanza na one, na kufuta mafisadi wote!

- Kama mfano wako ungekua kweli, basi Mungu asingewamaliza Sodoma na Gomora kwa ufisadi wao, msiwe mnainginza mifano ya dini na ufisadi wa bongo wka sababu huwa haifanani kabisaa, fisadi wa bongo hana mfano dunia nzima na wala kwenye vitabu vya dini, pleaseee huyu Kitine ni pure fisadi!.

Respect Mkuu!
 
Kitine aliwahi kumpeleka mke wake Canada na Japan kutibiwa chunusi kwa dola 100,000 za walipa kodi wa Tanzania!!! Watu wa aina hii wanaitwaje vile... let me think..mmhhhh.. freakin` FISADI.
 
Mkuu FMES,
Nimekusikia. Nakubaliana na mengi unayosema lakini ujumbe wangu umelenga zaidi
aliyoyasema Kitine. Unajua hapa Marekani kuna benki ilimwajiri mwizi aliyekubuhu katika bank robbery awasaidie kupambana na wizi huo. Sasa kama Kitine ni fisadi naye ameona kuwa mambo nchini hayaendi vizuri, tusikilize ujumbe wake. He may have some inside information, no?
 
Mkuu FMES,
Nimekusikia. Nakubaliana na mengi unayosema lakini ujumbe wangu umelenga zaidi
aliyoyasema Kitine. Unajua hapa Marekani kuna benki ilimwajiri mwizi aliyekubuhu katika bank robbery awasaidie kupambana na wizi huo. Sasa kama Kitine ni fisadi naye ameona kuwa mambo nchini hayaendi vizuri, tusikilize ujumbe wake. He may have some inside information, no?

- Huyu amekua usalama under Mwalimu, na amekua waziri wa usalama under Mkapa, sasa akiamua ksuema kweli huyu anakwenda na majina tu na ufisadi wao, lakini as long as anaruka ruka viunzi hana lolote anataka mlo tu kama Msekwa, Dr. Slaa milango yake iko wazi siku zote kama ana dataz lakini anaogopa basi ampe tuone ushujaa wa Kitine,

- Hatuwezi kulegeza the bar na high profiles kama Kitine, kama hawezi sema solution na majina ya mafisadi, please akae pembeni we can figure this out yaani ya mafisadi on our own.

Thanxs!
 
Mkuu FMES,
Nimekusikia. Nakubaliana na mengi unayosema lakini ujumbe wangu umelenga zaidi
aliyoyasema Kitine.

Mkuu Jasusi, hata anayoyasema Kitine hakuna jipya hata moja, ni kama amerudia yaliyowahi kusemwa huko nyuma. kwa nafasi aliyozowahi kushika nilitarajia asema mengine ya ndani zaidi kuliko haya, aje na kitu ambacho kitawalazimisha watawala kufanya mabadiliko yanayhitajika, si kuendeleza hizi politic
 
Mkuu Jasusi, hata anayoyasema Kitine hakuna jipya hata moja, ni kama amerudia yaliyowahi kusemwa huko nyuma. kwa nafasi aliyozowahi kushika nilitarajia asema mengine ya ndani zaidi kuliko haya, aje na kitu ambacho kitawalazimisha watawala kufanya mabadiliko yanayhitajika, si kuendeleza hizi politic

- Ahsante mkuu, tupo pamoja sana hapa!
 
Hii ni Black propaganda tu, ajue faili lake takukuru laweza pelekwa kwa DPP pia.
 
Bila kuingilia uhuru wa mtu yeyote yule,ningependekeza turudi kwenye mada(content).Naona ni kama wachangiaji wamebase kwa mtoa hoja na sio hoja yake.Kama kuna wanaotaka kumjadili Kitine as Kitine then they better start a new thread.Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom