Daaaa!, nimecheka sana mpaka watu ofisini wakashangaa, Mkuu vipi tena, jamaa kajitahidi kutoa mchanganuo, wewe umemmiminia matusi kibao....
Kazi kweli kweli!
Mi mwenyewe bado nacheka kaka, yaani acha tu. Halafu tunasema nchi hii itaendelea. Ndo maana watu wana chuki za BINAFSI na wenye hela.
Tatizo sio wenye hela tatizo ni serikali kutotekeleza sera zake.
Mfano ngoja nimsaidie huyu Mtanzania asinichukie mimi na Lowassa, Hapa Town kila unachouliza madukani ni USD based price, computer USD, hotelini USD, Rentals USD. Sasa ndugu yangu inahitaji hata darasa la nne kuona kuwa mnaongeza demand ya USD hapo na kuiuwa TSHS?
Tukiwaambia mnasema sisi ni Kenge. Jamani Tanzania bila umasikini inawezekana.