Mkuu tindo tatizo lako dogo tu. Ilikuwa mara ya kwanza kulima ulipaswa uanze kidogo ili ujifunze kwa gharama kidogo. Biashara yoyote unapoianza mara ya kkwanza mieleka ni kawaida, kama unapojifunza kuendesha baiskeli.

Mtu asitarajie anapoanza jambo kwa mara ya kwanza apige bingo haiko hivyo. Pia ukae ukijua kuwa kunapokuwa na mafuriko ya zao sokoni wanunuzi wote na si madalali peke yao hunyanyasa sana wakulima. Hali hiyo ipo katika kilimo cha nyanya pia.

Mkoa wa Morogoro ukilima nyanya za kiangazi mwezi wa nane hadi wa kumi na moja huwa kuna mafuriko ya nyanya. anaevuna miezi hiyo na kkama ni mara yake ya kwanza ataapa kwamba nyanya si biashara. Kuna msemo huku NYANYA NINYANYUE NYANYA NINYANYASE. Soko zuri la vitunguu ni mwwezi March hadi June. Ukiweza kuwa na kitunguu majira hayo huna maumivu. wateja wanakutafuta na unaweza kuuza kwa utaratibu unaotaka wewe. wakati huo wewe mwenye mali ndio mjanja. suala la madalali linakuwa halina umuhimu na wala si lazima upeleke sokoni na hata ukipeleka sokoni mzigo wako utagombaniwa.

Tumia utaallam uweze kuhifadhi kitunguu uweze kulifikia soko la Mwezi March, au lima vitunguu uvune February au uvune kuanzia mwezi May hadi July. Ukilima kitunguu cha msimu ambacho kila mtu analima maumivu yake ndiyo hayo.

Kwenye suala la soko kunapokuwa na mafuriko hakuna serikali itakayokusaidia hapo utakuwa umeumia tu. wewe mkulima ndiyo unatakiwa uchemshe bongo kuona utalifikia vipi soko la mwezi March hadi July. Hii miezi hakuna dalali atakae kunyanyasa. Na pia sio lazima upeleke mzigo sokoni kunawanunuzi wazuri tu hufuata mazao mashambani. watu wengi wanafanikiwa sana kwa kuuzia mashambani. kama huna uzoefu afadhari ukauzia shamba ukapata bei utakayoridhika nayo kuliko kwenda mjini ukakutana na madalali wajanja ukarudi kijijini na story tu huna pesa mfukoni.

Kwa hiyo Mkuu kila biashara inachangamoto zake. Tumia muda mwingi kujifunza kwa wazoefu badala ya kulalamika hivyo. Ulikosea kuanza kwa kulima pakubwa ukapata hasara ukarudia makosa yaleyale kwa kulima pakubwa zaidi huku hujarekebisha kilichokutia hasara ulipo anza. Ushauri wangu msimu wa kwanza jifunze mbinu za kilimo cha vitunguu uzijue changamoto zake.

Msimu unaofuata boresha uzalishaji kwa kutatua changamoto, pata ushauri kwa wazoefu. Panua eneo kadri unavyopata uzoefu. Hata kama unauwezo mkubwakifedha usianze kuwekeza eneo kubwa kama huna uzoefu. Usivutiwe na takwimu tamu unazosikia nyingi hufikiwa na wazoefu na nyingi ni exagerated.

Ukizalisha eneo dogo inakupa picha halisi itakayokufanya uamue iwapo kilimo hicho kinalipa au la. Na hapo ndiyo utaamua kupanua eneo la shamba kwa kutokana na picha halisi uliyoiona na changamoto zake.
 
Milioni moja?
Inategemea unalimia wapi?
Inategemea umwagiliaji kwa pampu au mifereji au mvua
Uzoefu wangu huku Kilosa huu:
Mbegu lita 7 kwa ekari @ 25,000/= jumla 175,000/=
Kuandaa kitalu 20,000/=
Kusia mbegu 10,000/=
kutunza kitalu 30,000/=
kukodi shamba 100,000/=
kufyeka shamba 48,000/=
kukatua udongo 64,000/=
kulainisha udongo 48,000/=
kutengeneza majaruba 25,000/=
kupandikiza 160,000/=
dawa ya kuua magugu 40,000/=
palizi mara mbili 100,000/=
Mbolea mifuko mitatu 210,000/=
Mtu wa kuweka mbolea mara mbili 10,000/=
madawa kuua wadudu na magonjwa 50,000/=
mpiga dawa wiki kumi 50,000/=
kung'oa 50,000/=
kukata vitunguu gunia mia 200,000/=
usafiri 100,000/=
chanja kukodi 100,0000
umwagiliaji petrol 2500 x lita 5 x wiki 10 = 125,000/=
mtu wa kumwagilia 5000 x wiki 10 = 50,000
JUMLA KUU = 1,855,000/=

Kwa wastani ni mil 2

Asante mkuu. Hii inamaanisha heka 1 naweza pata magunia 100. Je vipi bei ya vitunguu sokoni?
 
Wadau thid year nililima na nimevuna hivi punde nitarudi kuwapa experience ndogo niliyojifunza.
1447347051088.jpg
1447347071735.jpg
 
Binafsi nalima kitunguu maeneo ya Kware Ruaha Mbuyuni hapa ni potential kw maana ya irrigation na ardhi ni nzur kw kitunguu. Hili zao linahitaj ujikamilishe kifedha unapoanza kulima ni muhimu ukaitenga pesa yake pemben kbsa kw heka inayohudumiwa vzur kila kitu inagarim million 3 ukiweka na lak 5 ya miscellaneous inakua vzur incase kuna mlipuko wa magonjwa km n'gonyo ambao wana athar kubwa na hugarim dawa kila baada ya siku kadhaa. Kware heka moja inakodishwa kw laki na nusu na pamp ya kumwagilia ni elf 50 jumla lak 2 mbegu huuzwa kw lita yale makopo yanayo nywewa mbege vilabuni ambapo kw kila lita ni elf 25 na heka moja inahitaj lita 10 ukiongeza mbili sio mbaya Kulima kw trekta ni sh elf 50 kw heka na ngombe ni 30 ila kw trekta ni nzur zaid cz inachimbua udongo vzur na hupunguza majan meng kuota halaf kuna kupengelenga hii ni kutengeneza majaruba kw ajili ya vitalu vya mbegu na yale ya kupandia shamban kw yale jaruba za mbegu hufanyaga sh 300 kw jaruba kw lita 10 unaweza pata jaruba 35 na zikizid bas kidgo sna halaf kw zile za shamban uwa wana charge kw heka ambapo kw heka wana pelenga laki na 20 hapo inabidi wasawazishe ardhi mana trekta linatifua sna ambapo kw heka wanafanya chini kbsa elf 10 ila wanaanzia elf 20.. Then kuna kupanda mbegu (Kuombeka) hapa ni sh 400 mpka 500 kw jaruba heka moja huwa na jaruba maxmum 400 halaf unapiga dawa ya kuzuia magugu weed stop na ile ya kuua majan yaliyo ota galgan au oxfan hizi ni elf 22 kw lita kw weed stop na unahitaj lita 4 kw heka kuna zile za kuua na kuzuia wadudu km DuDuba 13 kw ml 500 na unahitaj lita 1 kw heka na profercon elf 17 kw lita na unahitaj lita 2 kw heka na ile ya kuzuia ukungu kwenye majan ya kitunguu Amezeb elf 8 kw gram 500 na unahitaj kilo 1 kw heka then kuna mbolea apply after 2 wks urea elf 60 sehem nyngne mpka 66 kw mfuko na heka huitaj mifuko 4 then baadae CAN hii ni kw kukuzia mfuko elf 50-55 weka tena 4 ila dawa zinaweza kua constant kutokana na uwepo wa magonjwa pia gharama constant ni ya kumwagilia ambapo eka moja huitaj diesel lita 10-15 kutegemea na umbali wa shamba toka mtoni pia gharama za kijana atayemwagilia ambapo hudai elf 10-15 kw heka na pia wapiga dawa hudai elf 15 kw heka close supervision ni muhim sna inacse bajet inabana unaweza mwaga urea once then after 3-4 weeks ukapiga booster inaitwa super grow hii ni nzur sna kw kukikuza kitunguu jus elf 22 unapata lita nzima na inatosha kw heka nzima ukishapanda maji ni mara moja kw wiki kumwagilia na wakat wa kuvuna wanacharg 100-200 kw jaruba halaf kuna kukata majan ya kitunguu sh 2000 kw gunia. Eka moja iliyohufymiwa vzur hutoa gunia 70-80 na kila gunia ni elf 80 uwa inapanda mpka lak na 10 kikiwa adim na pia huweza kusguka mara chache mpka elf 70-75 ila average ni 80 kw shamban Vitunguu vya Ruaha Mbuyuni vinalimwa kiustad tofaut na singida au dodoma ivyo bei yake iko juu na huweza kulipa mara 3 mpka 4 zaid kw faida ila uhudumie vzur shamba.. Karibuni

Mkuu...asante sana kwa maelezo yako. Hii mimi naichukulia kama ndiyo notisi "desa" la kilimo cha vitunguu, especially kwa hapo Ruaha Mbuyuni.
 
Zao la vitunguu swaumu ni zao ambalo linaonekana limesahaulika japo linalipa sana,
Nilikua manyara mwaka jana nilipata jifunza haya yafuatayo:
/zao hili haliitaji maji meng kama ilivo vitunguu maji huitaji maji mengi mara moja kwa mwezi
/ zao hili huchukua mieZ 4 hadi 5 kuweza kua tayari kuingia sokoni
/ zao hili haliuzwi kimagunia wala kimadebe ni bei sana hivo linauzwa kwa neti ( net moja ni sawa na beseni moja na nusu) ambayo bei ya neti moja n shillingi elfu 56.
/ bei ya mbegu mara nyingi huwa wakulima wazao hili wananunua kwa mabeseni ambapo beseni moja la mbegu ni shillingi elfu 35
/ zao hili huna haja ya kubeba na kupeleka sokoni wanunuzi wanakufata wenyewe na mafuso yao japo ukienda navyo mombasa au sudani pia uganda ni ghari sana huuzwa huko.
/ mahali ambapo zao hili hustawi n katika udongo wa pemben mwa mabonde udongo ambao sio mgumu sana mtanisamehe aina ya udongo sijui ila mabonden lakn maji yawe yanazuiwa na kuruhusiwa mara moja kwa mwezi au hata mara mbili cio mbaya ila yawe kwa wingi yaende chini,
/ mikoa ya manyara , singida morogoro na baadh ya mikoa ya kusimi yanasupport sana

Thanks... very useful information.
 
Safi sna mkuu,

Haya ndio mawazo tunataka hapa JF,

Kuna technolojia mpya na rahisi mno nimeinyaka sehemu juu ya huu ulimaji bado naimalizia resecrh yake nafikiri baada ya miezi sita itakua imekamilika nitaimwaga hapa jamvini.

Kifupi inawezekana kabisa kuchagua ukubwa wa kitunguu chako, kukuza ndani ya miezi miwili tu na kuchangua shape ya kitunguu.

Hii nikiikamilisha nitaileta hapa maana nafikiria kuteka soko lote la Comorro, Kenya na Zanzibar kwa vitunguu bora kabisa na vya bei nafuu na hakuna atakaye shindana na mie.

Mkuu...miezi 6 ishapita, vipi mrejesho wa hiyo research yako?
 
Hongera Mkuu Kwa Kufikia Hapo Maana Najua Haikuwa Kazi Rahisi
Sio kazi rahisi kweli, lakini there should always be a starting point. Na hapa ndio nilipoanzia na nimejifunza kwa kweli na nitawashirikisha nanyi wenzangu najua kipo cha kujifunza.
 
Habari zenu wadau.
Kama nilivyowaeleza hapo awali nita share experience ndogo niliyoipata katika kilimo cha kitunguu nilichoingia kufanya mwaka huu katika kijiji cha Igawa Mbalali.

Kwanza kabisa shamba langu lilikuwa na ukubwa wa 0.6 eka(Nililipima kwa kutumia GPS) hapa kitu nilichopata ni kwamba kwa ukubwa huu ambao kabla sijalipima niliambiwa ni eka moja, bahati mbaya nilipima wakati nimeshalilipia na kupanda tayari.

Katika shamba hili nilifanikiwa kukata vijaruba 202, na nilipanda mwezi wa saba mwanzoni na nimevuna mwezi huu wa 11 mwanzoni, gharama za kuendesha shamba hili ambapo kwangu ni kama shamba darasa ilifika 2.9m

Lesson learnt
1. Kitunguu ambacho wenyeji wanasadiki kuwa ni chenye faida mara nyingi ni kile kinacholimwa kuanzia mwezi wa 3 au 4 na kutolewa mwezi wa 6 au 7. Au kinacholimwa mwezi 7 au 8 na kutolewa wa 11 au 12 kwa ajili ya kuhifadhi kwenye Ghala.

2. Upandaji, kutokana na ugeni na kutofahamu mambo mengi, upandaji haukufuata utaratibu kwa baadhi ya jaluba na hivyo kubananisha vitunguu. Upandaji unaotakiwa ni ule maarufu wanasema upandaji wa umbali wa kiberiti.

3. Kitunguu nilichopanda mimi ni cha umwagiliaji, hapa napo kuna changamoto lukuki, ukimpata kijana mwaminifu gharama huwa chini kwani mara nyingi wanachakachua sana mafuta. Kijana aliyesimamia shamba langu alikuwa ni majanga tu.

4. Utunzaji wa shamba unahitaji ukaribu sana hasa kipindi chs kupiga dawa na kupiga mbolea. Usipoangalia utakuwa unanunulia wengine mbolea. Pia dawa, kwa kipindi ambacho nilipanda mimi huhitajika dawa nyingi kwa kuwa ni kipindi ambacho kunakuwa na wadudu wengi. Pia nilishambuliwa na wadudu wanaitwa kantangaze hawa wadudu kwa kweli ni balaa ila niliwatuliza kwa dawa moja inaitwa Belt.

5. Uvunaji, kwa kweli kama walivyochangia wadau wengine kipindi cha uvunaji hutakiwi kuingiza maji mengi kwenye jaluba, pia ukivuna omba mungu mvua isikukute maana vikinyeshewa na vikiwa vimesha katwa basi hapo ndio mwisho wa hadithi.

6. Uuzaji, ndugu zangu kama nilivyosema hapo juu kuhusu mvua, vitunguu vyangu vilinyeshewa, ila nashkuru ilikuwa bado havijakatwa ndio kwanza vimetoka kung'olewa. Hapo kwa kweli thamani ya kitunguu changu ilishuka, hata hivyo niliuza gunia kwa 50,000 na vile vilivyopasuka gunia 30,000. Ukweli ni kwamba kipindi hiki ambacho nimevuna vitunguu ni vingi sokoni, hivyo baadhi kipindi hiki vitunguu vyao huhifadhi gharani hadi Januari ambapo bei huwa juu kidogo na ya kuridhisha.

7. Mwisho ningependa kuwashirikisha wenzangu na kuwaambia ya kwamba vitunguu vina pesa ila ukilima kwa wakati sahihi, sehemu sahihi, kilimo na usimamizi sahihi.

Kwa kipindi hiki kitunguu kimenikata, sijapata faida ila kwa niliyojifunza katika awamu hii naamini ni silaha muhimu katika msimu ujao na lazima nifanikishe endapo Mungu akipenda nikawa hai, nitatoboa tu. Nitajitahidi mwezi wa tatu nitakuwa nishapanda Mungu akipenda.

Kwa wale wanaolima maeneo haya hasa kilimo cha umwagiliaji nasema nimeshakaribia tuendeleze mapambano.

Aluta kontinua, daima mbele nyuma mwiko.
davidson689@hotmail.com
1447491768533.jpg
 
Habari zenu wadau.
Kama nilivyowaeleza hapo awali nita share experience ndogo niliyoipata katika kilimo cha kitunguu nilichoingia kufanya mwaka huu katika kijiji cha Igawa Mbalali.
Kwanza kabisa shamba langu lilikuwa na ukubwa wa 0.6 eka(Nililipima kwa kutumia GPS) hapa kitu nilichopata ni kwamba kwa ukubwa huu ambao kabla sijalipima niliambiwa ni eka moja, bahati mbaya nilipima wakati nimeshalilipia na kupanda tayari.
Katika shamba hili nilifanikiwa kukata vijaruba 202, na nilipanda mwezi wa saba mwanzoni na nimevuna mwezi huu wa 11 mwanzoni, gharama za kuendesha shamba hili ambapo kwangu ni kama shamba darasa ilifika 2.9m
Lesson learnt
1. Kitunguu ambacho wenyeji wanasadiki kuwa ni chenye faida mara nyingi ni kile kinacholimwa kuanzia mwezi wa 3 au 4 na kutolewa mwezi wa 6 au 7. Au kinacholimwa mwezi 7 au 8 na kutolewa wa 11 au 12 kwa ajili ya kuhifadhi kwenye Ghala.
2. Upandaji, kutokana na ugeni na kutofahamu mambo mengi, upandaji haukufuata utaratibu kwa baadhi ya jaluba na hivyo kubananisha vitunguu. Upandaji unaotakiwa ni ule maarufu wanasema upandaji wa umbali wa kiberiti.
3. Kitunguu nilichopanda mimi ni cha umwagiliaji, hapa napo kuna changamoto lukuki, ukimpata kijana mwaminifu gharama huwa chini kwani mara nyingi wanachakachua sana mafuta. Kijana aliyesimamia shamba langu alikuwa ni majanga tu.
4. Utunzaji wa shamba unahitaji ukaribu sana hasa kipindi chs kupiga dawa na kupiga mbolea. Usipoangalia utakuwa unanunulia wengine mbolea. Pia dawa, kwa kipindi ambacho nilipanda mimi huhitajika dawa nyingi kwa kuwa ni kipindi ambacho kunakuwa na wadudu wengi. Pia nilishambuliwa na wadudu wanaitwa kantangaze hawa wadudu kwa kweli ni balaa ila niliwatuliza kwa dawa moja inaitwa Belt.
5. Uvunaji, kwa kweli kama walivyochangia wadau wengine kipindi cha uvunaji hutakiwi kuingiza maji mengi kwenye jaluba, pia ukivuna omba mungu mvua isikukute maana vikinyeshewa na vikiwa vimesha katwa basi hapo ndio mwisho wa hadithi.
6. Uuzaji, ndugu zangu kama nilivyosema hapo juu kuhusu mvua, vitunguu vyangu vilinyeshewa, ila nashkuru ilikuwa bado havijakatwa ndio kwanza vimetoka kung'olewa. Hapo kwa kweli thamani ya kitunguu changu ilishuka, hata hivyo niliuza gunia kwa 50,000 na vile vilivyopasuka gunia 30,000. Ukweli ni kwamba kipindi hiki ambacho nimevuna vitunguu ni vingi sokoni, hivyo baadhi kipindi hiki vitunguu vyao huhifadhi gharani hadi Januari ambapo bei huwa juu kidogo na ya kuridhisha.
7. Mwisho ningependa kuwashirikisha wenzangu na kuwaambia ya kwamba vitunguu vina pesa ila ukilima kwa wakati sahihi, sehemu sahihi, kilimo na usimamizi sahihi.
Kwa kipindi hiki kitunguu kimenikata, sijapata faida ila kwa niliyojifunza katika awamu hii naamini ni silaha muhimu katika msimu ujao na lazima nifanikishe endapo Mungu akipenda nikawa hai, nitatoboa tu. Nitajitahidi mwezi wa tatu nitakuwa nishapanda Mungu akipenda.
Kwa wale wanaolima maeneo haya hasa kilimo cha umwagiliaji nasema nimeshakaribia tuendeleze mapambano.
Aluta kontinua, daima mbele nyuma mwiko.
davidson689@hotmail.com
Hongera sana. Hiyo sasa ndio nature ya biashara. Baada ya hapo utafanikiwa. Ushauri wangu uangalie hayo uliyojifunza na ubashiri changamoto nyinginezo ambazo zinaweza kutokea na jinsi ya kuzikabili. Kila lakheri
 
Kilimo cha vitunguu kinaweza kukutoa kama kutakuwa na usimamizi mzuri, binafsi nililima hekari 3 maeneo ya Mtandika lakini wenyeji walichonifanya sitaki hata kukumbuka, mimi natuma hela kama wanavyotaka kwa ajili ya dawa, mbolea na matunzo mengine kumbe jamaa hawana habar na shamba, siku nimeenda nikakuta kwanza hekar moja ilishakufa nilitamani niite trekta lisafishe mpaka vile vilivyopo.

Kama unataka hiki kilimo tafuta vijana waaminifu na sio wenyeji halafu ujitahid kutembelea hata mara moja kwa wiki ila ukilima kwa simu utajuta.
 
Binafsi nina plan ya kuanza kilimo hiki maeneo ya Butuja, mkoani Mwanza. Ila ningependa kufahamu kama kuna mtu ana uzoefu na eneo hilo ama alishawahi fanya zoezi hilo katika kijiji hiko! Msaada wenu nitaendelea kushukuru sana.

Maana tangu mwanzo mwa thread hii hadi hapa kuna mengi mno ya kujifunza.

Kilimo niinue.
 
Habari zenu wadau.
Kama nilivyowaeleza hapo awali nita share experience ndogo niliyoipata katika kilimo cha kitunguu nilichoingia kufanya mwaka huu katika kijiji cha Igawa Mbalali.
Kwanza kabisa shamba langu lilikuwa na ukubwa wa 0.6 eka(Nililipima kwa kutumia GPS) hapa kitu nilichopata ni kwamba kwa ukubwa huu ambao kabla sijalipima niliambiwa ni eka moja, bahati mbaya nilipima wakati nimeshalilipia na kupanda tayari.
Katika shamba hili nilifanikiwa kukata vijaruba 202, na nilipanda mwezi wa saba mwanzoni na nimevuna mwezi huu wa 11 mwanzoni, gharama za kuendesha shamba hili ambapo kwangu ni kama shamba darasa ilifika 2.9m
Lesson learnt
1. Kitunguu ambacho wenyeji wanasadiki kuwa ni chenye faida mara nyingi ni kile kinacholimwa kuanzia mwezi wa 3 au 4 na kutolewa mwezi wa 6 au 7. Au kinacholimwa mwezi 7 au 8 na kutolewa wa 11 au 12 kwa ajili ya kuhifadhi kwenye Ghala.
2. Upandaji, kutokana na ugeni na kutofahamu mambo mengi, upandaji haukufuata utaratibu kwa baadhi ya jaluba na hivyo kubananisha vitunguu. Upandaji unaotakiwa ni ule maarufu wanasema upandaji wa umbali wa kiberiti.
3. Kitunguu nilichopanda mimi ni cha umwagiliaji, hapa napo kuna changamoto lukuki, ukimpata kijana mwaminifu gharama huwa chini kwani mara nyingi wanachakachua sana mafuta. Kijana aliyesimamia shamba langu alikuwa ni majanga tu.
4. Utunzaji wa shamba unahitaji ukaribu sana hasa kipindi chs kupiga dawa na kupiga mbolea. Usipoangalia utakuwa unanunulia wengine mbolea. Pia dawa, kwa kipindi ambacho nilipanda mimi huhitajika dawa nyingi kwa kuwa ni kipindi ambacho kunakuwa na wadudu wengi. Pia nilishambuliwa na wadudu wanaitwa kantangaze hawa wadudu kwa kweli ni balaa ila niliwatuliza kwa dawa moja inaitwa Belt.
5. Uvunaji, kwa kweli kama walivyochangia wadau wengine kipindi cha uvunaji hutakiwi kuingiza maji mengi kwenye jaluba, pia ukivuna omba mungu mvua isikukute maana vikinyeshewa na vikiwa vimesha katwa basi hapo ndio mwisho wa hadithi.
6. Uuzaji, ndugu zangu kama nilivyosema hapo juu kuhusu mvua, vitunguu vyangu vilinyeshewa, ila nashkuru ilikuwa bado havijakatwa ndio kwanza vimetoka kung'olewa. Hapo kwa kweli thamani ya kitunguu changu ilishuka, hata hivyo niliuza gunia kwa 50,000 na vile vilivyopasuka gunia 30,000. Ukweli ni kwamba kipindi hiki ambacho nimevuna vitunguu ni vingi sokoni, hivyo baadhi kipindi hiki vitunguu vyao huhifadhi gharani hadi Januari ambapo bei huwa juu kidogo na ya kuridhisha.
7. Mwisho ningependa kuwashirikisha wenzangu na kuwaambia ya kwamba vitunguu vina pesa ila ukilima kwa wakati sahihi, sehemu sahihi, kilimo na usimamizi sahihi.
Kwa kipindi hiki kitunguu kimenikata, sijapata faida ila kwa niliyojifunza katika awamu hii naamini ni silaha muhimu katika msimu ujao na lazima nifanikishe endapo Mungu akipenda nikawa hai, nitatoboa tu. Nitajitahidi mwezi wa tatu nitakuwa nishapanda Mungu akipenda.
Kwa wale wanaolima maeneo haya hasa kilimo cha umwagiliaji nasema nimeshakaribia tuendeleze mapambano.
Aluta kontinua, daima mbele nyuma mwiko.
davidson689@hotmail.com

Pole kwa changamoto mkuu. Naamin mrejesho wako ujao panapo uhai utakuwa ni wa mikakati ya jinsi gani uliliendea soko na faida lukuki. Kaza buti mkuu wengine tupo nyuma yenu.
 
Naomba lifunguliwe group la whatsapp, tujadili vizuri na kubadilishana mawazo kwa urahisi zaidi, wenye kujifanya ni ma-admin halafu kumbe matapeli haipendezi tunarudishana nyuma kimaendeleo na sio ungwana
 
Naomba lifunguliwe group la whatsapp, tujadili vizuri na kubadilishana mawazo kwa urahisi zaidi, wenye kujifanya ni ma-admin halafu kumbe matapeli haipendezi tunarudishana nyuma kimaendeleo na sio ungwana
Umeongea point toxic
 
wadau naomba mdau anayefaham kilimo hiki aniambie mbegu ikashatoka kwenye kitalu kwenda shambani ni wakati gani wa kuweka mbolea na aina gani kwa eneo la mkoa wa Dodoma na mpangalio wa dawa ni ipi inaanza na kias gani mpaka kuvuna.
 
Mkuu wiki ya pili au ya tatu inafaa kutia mbolea lakini pia inategemeana na mtiririko wa mvua,kwa mpangilio wa dawa pia utaangalia kama kuna mashambuliza ya wadudu ambao mara nyingi husababishwa na uotaji wa majan shambani so ili kuAvoid inabid shamba liwe safi mda wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom