Adventure c
Member
- Jan 18, 2014
- 28
- 49
Kama habari inavyoeleza hapo juu,
Mimi ni mkulima mzuri wa nyanya, nimelima zao hili kwa zaidi ya miaka kadhaa kutokana na changamoto za hapa na pale zilinifanya kuwa mzoefu na mtaalamu sana wa kilimo hiki, hivyo ilikuwa nikiweka mbegu shambani.
Ililazimu jirani angalie nitaivisha wakati gani Ili tusikutane naye hii ni kutokana tu na kutengeneza Jina la uzalishaji wa bidhaa bora,kama wahenga walivyosema "Mwenye nguvu mpishe "kauli hii ilinipa kujiamini kutokana na kile tulichokuwa tunakizalisha, zama huwa zinabadilika.
Mabadiliko ya Kila Leo ya soko la nyanya na vijana wengi kuhisi tunapiga pesa nyingi basi kulianza kunifikirisha kulihana zao hilo, baada ya kuona vijana wengi wakiiga pasi na ujuzi juu ya uzalishaji wa zao hili,kulileta mafuriko katika soko letu kiasi kwamba kwa mtu unayezalisha kwa kutumia gharama kubwa.
Huwezi kushindana na mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo na anauza anavyojisikia, ukizingatia walaki wetu wa mwisho Wana angalia quantity na si quality, hivyo mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo atapima mfuko ule unaouzwa kwa Shilingi mia tatu(Magufuli)Wasukuma Wa Meatu Mwandoya Simiyu.
Huwa wanaita hivyo, mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo atauuza Shilingi 500,huku Mimi na rafiki yangu Makoye kibarua wangu tukiuza nyanya 5 kwa Shilingi mia 500, Tuliona kabisa kuwa tunakoelekea tutakwenda kukwama.tuliamua kulihana zao hilo na kuamua kuhamia kwenye vitunguu.
Hamasa ya kutiana mioyo ilikuwa kubwa tulikuwa tukipiga stori za kupata mamilioni ya pesa kwani wakati huo gunia lilikuwa likinunuliwa 350k, tulijipa matumaini makubwa kuwa hata kama tutakuta bei imeshuka basi tutakuta angalau ngunia linanunuliwa 150k.
Haiwezekani bei iporomoke kutoka 350k mpaka liivuke 150k, mjadala juu ya Nini tufanye uliishia Mwanaume nikajitosa kwenda kununua mbegu,nilikwenda maduka kadhaa kufanya ulinganifu wa bei na upelelezi wa Kila walaka unaozungumuzia kilimo hiki nilisoma kwa makini huku nikiulizia Kila uzoefu na changamoto za hapa na pale juu ya zao hili.
Nilibahatika kupata mzoefu wa zao hili kwa kuuza mbegu,kulima na mrejesho wa wakulima mbali mbali aliokuwa anaupata kwa wakulima walikuwa wakichukua mbegu kwake.
ITAENDELEA...
Mimi ni mkulima mzuri wa nyanya, nimelima zao hili kwa zaidi ya miaka kadhaa kutokana na changamoto za hapa na pale zilinifanya kuwa mzoefu na mtaalamu sana wa kilimo hiki, hivyo ilikuwa nikiweka mbegu shambani.
Ililazimu jirani angalie nitaivisha wakati gani Ili tusikutane naye hii ni kutokana tu na kutengeneza Jina la uzalishaji wa bidhaa bora,kama wahenga walivyosema "Mwenye nguvu mpishe "kauli hii ilinipa kujiamini kutokana na kile tulichokuwa tunakizalisha, zama huwa zinabadilika.
Mabadiliko ya Kila Leo ya soko la nyanya na vijana wengi kuhisi tunapiga pesa nyingi basi kulianza kunifikirisha kulihana zao hilo, baada ya kuona vijana wengi wakiiga pasi na ujuzi juu ya uzalishaji wa zao hili,kulileta mafuriko katika soko letu kiasi kwamba kwa mtu unayezalisha kwa kutumia gharama kubwa.
Huwezi kushindana na mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo na anauza anavyojisikia, ukizingatia walaki wetu wa mwisho Wana angalia quantity na si quality, hivyo mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo atapima mfuko ule unaouzwa kwa Shilingi mia tatu(Magufuli)Wasukuma Wa Meatu Mwandoya Simiyu.
Huwa wanaita hivyo, mtu aliyezalisha kwa gharama ndogo atauuza Shilingi 500,huku Mimi na rafiki yangu Makoye kibarua wangu tukiuza nyanya 5 kwa Shilingi mia 500, Tuliona kabisa kuwa tunakoelekea tutakwenda kukwama.tuliamua kulihana zao hilo na kuamua kuhamia kwenye vitunguu.
Hamasa ya kutiana mioyo ilikuwa kubwa tulikuwa tukipiga stori za kupata mamilioni ya pesa kwani wakati huo gunia lilikuwa likinunuliwa 350k, tulijipa matumaini makubwa kuwa hata kama tutakuta bei imeshuka basi tutakuta angalau ngunia linanunuliwa 150k.
Haiwezekani bei iporomoke kutoka 350k mpaka liivuke 150k, mjadala juu ya Nini tufanye uliishia Mwanaume nikajitosa kwenda kununua mbegu,nilikwenda maduka kadhaa kufanya ulinganifu wa bei na upelelezi wa Kila walaka unaozungumuzia kilimo hiki nilisoma kwa makini huku nikiulizia Kila uzoefu na changamoto za hapa na pale juu ya zao hili.
Nilibahatika kupata mzoefu wa zao hili kwa kuuza mbegu,kulima na mrejesho wa wakulima mbali mbali aliokuwa anaupata kwa wakulima walikuwa wakichukua mbegu kwake.
ITAENDELEA...